BADILI TABIA
JF-Expert Member
- Jun 13, 2011
- 32,767
- 23,198
Leo michepuko sio dili sio🤣Nimejifunza kitu. Michepulo sio dili. Heri mara mia machangudoa
vyote vipo kwa jina langu na sijamwoa,na mke anafahamuKwani wakati Unamjengea Jina la Hati ya nyumba uliandika ya nani??? Hati ya kiwanja je??? Huyo mwanamke unaweza mfukuza hapo kama hivi vyotr vipo kwa jina lako na hamjawahi kuishi pamoja at least kwa mwaka pia ufanye mpango ukamzunguke polisi kulee hilo tuu otherwise nyumba itauzwa hiyo mgawane au wewe utaambiwa Umuache hapo aishi na mwanao na Kingine kama Umeoa huyo mwanamke hana chake kabisa hapo ila Tu ishu ni Kwa mkeo vitaumana.
So jiandae kupigania mali zako lakini kwa mkeo hizi habari kufika ni lazima.
naona huja ielewa mada,kama nyumba nimejenga ,watoto wamesoma academy, kuna la zaidi ya upendo huo?Shida kubwa ya wanaume ni kuishi kwa kutaka kuficha ficha mambo...
Mtu unamletea mke mdogo ulimuandaa kisaikolojia kwamba utamuolea mke wa pili?.
Mapenzi una maintain ama umehamishia nyumba ndogo?
kweli Mungu hachelewi
Kaka Mwitore kaa tulia jiulize kwa nini ulihitaji/unahitaji wanawake wawili?jiulize sana
WHY?
Js because u can?
Wewe ni mwanaume una hitaji hilo?
Mkeo mkubwa hakukutosheleza?
Unawapenda wote wawili?
Ulipenda watoto wengi?
pata sababu
Kama ni genuine need ambayo Mungu kaweka moyoni mwako waeleze wote wawili..
Rasimisha...jamii ikutambue hivyo na familia nzima...
Wape uhakika wa mapenzi yako kwao...
Short of that...endelea kuomboleza
Ulitegemea mke mdogo aishi kificho miaka yote bila ndoa rasmi?
Polygamy is not for the faint hearted...
Its double trouble but on the positive side its double blessings na faraja na attention na kila kitu
issue ni mwanaume umejipanga kufurahia na kukabiliana nayo ama mnaingiaga kichwa kichwa kama huyu mtoa mada?. Hehe
Ujue binadamu nje ya mahitaji hayo uliyotaja,naona huja ielewa mada,kama nyumba nimejenga ,watoto wamesoma academy, kuna la zaidi ya upendo huo?
Bhasi huyo unaweza mfukuzaa mchana kweupe yaniivyote vipo kwa jina langu na sijamwoa,na mke anafahamu
Miezi 9 imetosha sana kusema mmeachana mkuu nasema Nenda kamfukukuzee beba watu wakambebee juu juu...!! Hana chake hapoo hawezi kwenda kufanya umalaya huko alafu anarudi hapo anavyotaka....huyu mwanamke amerudi ili kuja kutaka nyumba iuzwe , ameondoka huu ni mwezi wa tisa na si mala moja anaondoka na kuludi tumshapelekana mpaka mahakamani ameshanilaza polisi kwa mambo kusingizia, kiufupi story nzima nlishaieleza nuymba nimejenga mimi na hati au karatasi ninazo,
kwa ufupi naombeni ushauri wa namna ya kumwondoa ili niepuke mambo ya polisi,
rbya polisi nilichukua toka alipoondoka mwezi wa january,
je hiyo rb itanisaidia nikimwondoa kwa nguvu ?
Hapo ndo unapokoseavyote vipo kwa jina langu na sijamwoa,na mke anafahamu
Njoo inbox tuyajenge chief,,nina imani yatakwishajamani msikae kimya naomba ushaur kwa wajuzi wa mambo haya, najuta kama nini kumfahamu mtu huyu
Napata ugumu wa kuingia inbox,Njoo inbox tuyajenge chief,,nina imani yatakwisha
Unapoatelekeza kichwa cha juu ukaendekeza cha chini matokeo ndiyo haya. Hivyo, jilaumu tu mwanangu au ubadilikeUshauri wenu ni muhimu sana.
Umri wangu ni miaka 50, nimeoa mke kanisani huu ni mwaka wa 25 naishi naye na tumejaliwa watoto wanne, wa kwanza na wapili wamemaliza tayari chuo kikuu na wa tatu yupo chuo kikuu mwaka wa pili. Wa nne kamaliza kidato cha 4 mwaka jana, katikati hapo miaka 18 iliyopita bahati mbaya nikajiingiza kwenye mahusiano na binti wa miaka 20 wakati huo na akapata ujauzito, nilipomwambia nimeoa ili aitoe mimba ile na kwa kuwa bado ni binti mdogo anaweza kupata wa kumwoa, alikataa katakata. Na mimi kwa kuogopa maana alinitamkia kuwa atajiua kama nitamlazimisha kutoa mimba na kuwa yupo tayari kuishi na mimi kama mke wa pili na ujauzito ule hawezi kutoa kamwe.
Niliendelea kumshawishi atoe, matokeo yake akakimbia akaenda kwao mpaka akajifungua huko.
Lakini kiufupi zaidi, alirudi tena na kunitafuta na kunitishia kumwambia mke wangu, hivi ninavyoandika ilibidi nirudishe nyuma majeshi na kuanza kuishi naye kama mke wa pili.
Nilimpangishia chumba na maisha yakaendelea, baada ya muda alipata mtoto wa pili, wote ni wa kike, baada ya muda nilianza kuwasomesha kuanzia chekechea mpaka sasa hivi wa kwanza anafanya mtihani wa form Six mwaka huu na wa pili anafanya wa form 4 mwaka huu na wote wamesoma shule za Private toka chekechea mpaka sasa hivi na kwa wastani kila mmoja alikuwa ananigharibu 2.5m hasa shule za msingi mpaka secondary. Hapo bado michango mbalimbali na usafiri, kwa maana walikuwa wanasoma mikoani.
Baada ya kumpata mtoto wa kwanza akiwa kwenye chumba cha kupanga, niliona sina budi watoto wangu na mimi binafsi niwe na uhuru maana maisha ndio yalishaanza hivyo, na mimi upendo tayari ulishaingia na kuona ni maisha kama maisha mengine.
Ndipo nilipoamua kununua viwanja, kama unakumbuka miaka ile ya 2000 nadhani kuanzia 2006 serikali ilipima viwanja 20,000 maeneo mbalimbali ya DSM, mimi nilichukua viwanja viwili, wakati ule nakumbuka kimoja nilinua 1,800,000 na kingine 1,300,000 ml. Ukubwa ni sq m 1200 na 1000. Kimoja kikubwa nikamjengea nyumba ya mgongo wa tembo, vyumba 2 na sebule katikati na choo kizuri cha nje, nikaacha eneo kubwa tu kwa ajili ya kujipanga na kujenga nyumba kubwa baadaye, kumbuka huo ni mwaka 2007 alipohamia hapo au tulipohamia hapo.
Baadaye nimfungulia biashara ya saloon, akafanya kama miaka 2 vibaka wakaingia nakuiba kila kiatu, nikaona isiwe shida nikamfungulia mghahawa ambao ulikuwa na vitu 16 na meza nne kubwa, bado na wenyewe haukufanya kazi vizuri, nikamfungulia grocery ya bia na kuweka kila aina ya kinywaji kwa kutumia viti na meza za mghahawa.
Nayo haikufanya kazi vizuri, nikamnunulia Hiace iliyotumika tayari kama dala dala.
Na yenyewe usimamizi ukawa mgumu.
DA NITAENDELEA, MAANA DA SIPO VIZURI KABISA KIAKILI NI NIMECHANGANYIKIWA SASA HIVI.
SEHEMU YA 2
MUENDELEZO WA TUKIO HILI SOMA HAPA CHINI:
SEHEMU YA 3
SEHEMU YA 4
SEHEMU YA 5
SEHEMU YA 6
SEHEMU YA 7
SEHEMU YA 8
SEHEMU YA 9
SEHEMU YA 10
SEHEMU YA 11
SEHEMU YA 12
SEHEMU YA 13
SEHEMU YA 14
SEHEMU YA 15
SEHEMU YA 16
SEHEMU YA 17
SEHEMU YA 18
SEHEMU YA 19
SEHEMU YA 20
SEHEMU YA 21
Daa , sawa ukimaliza niulize,Huu uzi ntaumalizia kesho
Sasa hivi unaendeleaje lakini?Daa , sawa ukimaliza niulize,
Vipi lakini na wewe imeku touch nini,
Lakini ndio maisha
Kesi ipo mahakamani toka mwezi wa 10 mwaka jana na inaendelea mwezi wa pili,Sasa hivi unaendeleaje lakini?
Naomba sehemu ya 21 na kuendelea mkuu...Kesi ipo mahakamani toka mwezi wa 10 mwaka jana na inaendelea mwezi wa pili,
Sasa hivi nimeshamwacha na yupo mwenyewe pale