Naomba ushauri: Miaka 18 iliyopita niliingia kwenye uhusiano na ‘Bi Mdogo’ na kuzaa naye watoto 2

Naomba ushauri: Miaka 18 iliyopita niliingia kwenye uhusiano na ‘Bi Mdogo’ na kuzaa naye watoto 2

Du , kusema sikuwa na la kujibu ilibidi nikawa chini kwanza nitafakari, akili haikunipa kabisa,

Suala sio kwa nini kanunua na kuficha hivyo vitu kwa ndugu yake, ila ni kuwa inaonesha sasa haya ni maandalizi ya kunikimbia na pesa zangu,

Sikumuliza chochote, ila baada nilikuwa kama najisemeshakuwa nimeota kama kuna mizigo unaleta hapa nyumbani, akasema ndoto tu hizo,

Baadaye tena nikamwambia mbona nasikia kuna vitu umenunua umehifadhi kwa ndugu yako, kwa nini usilete hapa? Akanijibu nimekuambia sijanunua kitu mimi, na nilishakukataza mmambo ya kusikia sikia huko nje usiwe unaniletea hapa, umesikia wewe,

Nikamwambia basi sio kusikia tu ila niliokotaga risiti hapa ndani ila sikutaka kukuambia, akasema nipe hiyo risiti, nikamwambia niliiacha hapa hapa, nikijua siku moja utaniambia

Akasema mimi sijui una niuliza kitu gani maana na wewe sasa hivi umekuwa mswahili kweli,

Aliendelea sasa kulalamika hasa kuwa namtuhumu kwa mamvo mengi,sasa mala sio mwaminifu mala mwizi, hivi kama hivyo vitu nimenunua, hapa si kwangu kwa nini nisilete hapa nyumbani,

Na wakati unaona hata magodoro hapa sio mazuri, na kitanda chenyewe cha zamani!
 
Sumu yake ni nini?
Hata mke wa mtu ni sumu,

Lakini wewe mwenye mume wa mtu, wewe ni nani zaidi ya hao tunaowaona mitaani hawana waume na wako tayari kutembea na mtu yeyote
Kutokana na hali ya maisha, na bi mdogo ambaye, unapata huduma zote na unajaliwa?

Ila kumbuka hata wewe mwenye ukileta upuuzi kama huo utatimuliwa tu , hakuna excuse kuwa wewe ni mke wa ndoa
😂😂😂😂😂
Dah
 
Siyo kweli, hiyo empire angeitengeneza vipi, nilimchukulia kama mke hasa, na hana tofauti na mke mkubwa, na sasa hivi naye yupo over 40, ukisema mke mkubwa mzito kiuchumi, mimi naona vile vile sio sawa kwani yeye alikosa nini cha kumfanya asiwe mzito, wote wana nyumba na wote watoto wao wameenda shule,kusema mimi nimezeeka nayo sio kweli, kwa taarifa yaani sasa hivi, Mungu apitishie mbali ndio naanza kuona utamu wa maisha, hiyo naisikilizia hasa, nataka nianze sasa kutalii sehemu mbalimbali,

Na kwa taarifa yake nilikuwa nimejipanga kuzeeka naye kwa kuwa nilishaanza kumtafutia kiwanja huko jirani na kijijini kwetu ili kibeneke liendelee, hata gari ningemnunulia,

Halafu mbona namwona naye kama anamabadiliko ya kiutu uzima kulikomimi, kitu gani kinakufanya umwone yeye ni kijana zaidi yangu,
Kumbuka tumeachana miaka minane tu, ujana wote kamaliza akiwa na mimi, leo hii mimi nikienda Club natoka na mtoto wa 25, na wala haoni aibu kukaa na mimi, vipi yeye anaweza kutoka na mtoto wa 25 na akawa happy, au huyo kijana anaweza kuwa happy.

Ila tatizo lingine kubwa ni nalo liona nyinyi wanawake mna chuki na husuda kwa wenzenu wenye maisha mazuri, na hayo maneno yenu ndio chanson cha kuwaingiza chaka na kuharibu kabisa maisha yao
😂😂😂😂😂
Salaleeeh!! We baba wewe
 
SASA NINI CHA KUFANYA:
Kwanza mzee wangu lazima uweke BOUNDARY/LIMIT. Huyo bi mdogo kashasahau nafasi yake, hivyo ni wajibu wako kumkumbusha vividly bila kumuangalia usoni.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣 umenichekesha kingisimani uwiiii

Miaka 18 aweke boundary leo 🤣🤣🤣🤣🤣
 
Mwitore, mimi ni kaka yako mkubwa! Ni retired officer, ninacho takukushauri ni kwamba; mosi, usijilaumu kwa yaliyo kukuta. Hayo siyo mageni katika Dunia hii. Wanaume wote wenye nafuu ya kipato huwa yanawakuta haya. Huyo mwanamke alijilenge umpe mimba kwasababu alijua uwezo wa kumsaidia kulea huyo mtoto unao.

Pili, huyo mwanamke inabidi umwache kwa amani ! Unaachana nae taratibu wala usimwambie unakusudia kumwacha kwa faida ya watoto wako wasiathirike kisaikolojia. Wanawake wengi at 40s huwa very ambitious. Usipokuwa makini yatakukuta makubwa. Kimsingi dalili ya mawingu ni mvua. Alipo kuambia akuage wewe nani, jua kuwa amejiandaa kwa mapambano. Mpangie vyumba viwili kwaajili yake na watoto. Lakini punguza frequency za kwenda. Ikibidi usiende hata miezi miwili mfululizo ila matumizi mtumie kwa kutumia mitandao .

Mwisho, rudi kwa mkeo mkubwa 100%. Hujachelewa.
Nadhani uzi ufungwe tuu, umeshamaliza kila kitu.

He have to be realistic kwamba huyo ni mchepuko tuu na anatakiwa akate connection naye za kimaisha, wabakishe connection kwenye watoto tuu.

Huyu mchepuko wake itafika muda atadai wawe na hadhi 50/50 na mke halali wa ndoa. Na kwa sheria zetu zilivyo tayari huyo mchepuko anatambulika kama mke halali wa jamaa na kimaslahi anatakiwa apate 50/50 na mke mkubwa.

Kaka mkubwa bado hajachelewa,anatakiwa achukue maamuzi magumu.
 
Back
Top Bottom