Naomba ushauri: Miaka 18 iliyopita niliingia kwenye uhusiano na ‘Bi Mdogo’ na kuzaa naye watoto 2

Naomba ushauri: Miaka 18 iliyopita niliingia kwenye uhusiano na ‘Bi Mdogo’ na kuzaa naye watoto 2

Wenye upendo, heshima au hekima na wake zao, wana michepuko, ila hawana ulimbukeni huo wa mapenzi,

Hutosikia anapigana na mchepuko, au wanatoana ngeo, au wamepelekana polisi sijui ustawi wa jamii au wanashinda kutwa kujaza watu wa mtaa wakigombana,
Hiyo nyumba wangeiacha wangesonga mbele, hakuna mwenye busara anayejijua ana mali za 500M na atapokea pension 250M, atakubali ajidhalilishe katika mazingira hayo.
Especially kama watoto wa mke mkubwa wapo tiyari vizuri, NEVER!
Ni zaidi ya kurogwa!

Everyday is Saturday.............................. [emoji41]
Jamaa anakuambia akiuza assets zake una uhakika wa 700M - 1B[emoji38]

Halafu eti anang'ang'ania kieneo cha 50M
 
Lakini unanichamba bure kabisa, tena kwa kuziamini hisia zako,
Umekasirika sana kwa kitu ambacho sio kweli kabisa

1,mimi sikuwahi kumuacha mke wangu hata kidogo,
2. Mimi sijawahi kugombana na mke wangu kiasi hata cha kukataliana tendo la ndoa
3.haya amekuja kuyajua kwa uhakika zaidi watoto wakiwa form na std 7
4 ukiangalia miaka hiyo ndio kipindi nimeanza kusumbuliwa huko nje,kwa hiyo ndio upendo ulizidi sana kwa bi mkubwa
5. Watoto kunitumia hiyo laki, kwanza huwa najiuliza wanitumie zaidi ili nifanyie nini
Mimi nina pesa yangu, viwanja natoka na mama, na anachangia kununua kinywaji ingawa mimi sio mywaji sana, bia mbili tu chali,

Najua wanamtumia mama yao, na uzuri wakati mwingine akitumiwa ananiambia,

Na akisha tumiwa nitaona nguo mpya hapo
Na mwenyewe anafurahi na mimi natafurahi kumwona mke wangu kapendeza na anakuwa kijana zaidi

Sijawahi kununua boxer wala fulana za ndani, vyote nashtukia zipo kabatini, na zile za zamani anatupa, tena wakati nakasirika anatupa zikiwa bado nzuri kabisa

Kiujumla hajawahi nichukia wala sijawahi mchukia
Turudi kwa watoto kutonitumia pesa, walishaona sizishobokei pesa zao, kwa sababu hawajui wanitumie kiasi gani ili nilizika, mimi nina pesa yangu ya kunitosha
Lakini wakati mwingine wadogo wanawapiga mizinga huko, unaona tu dogo karudi nyumbani na shati jipya , hapo si wanakuwa wamesaidia,

Mimi ninachohitaji kwao ni usafiri tu, na wameshaniahidi kunako majaliwa kama hawajajenga wanisuprise na usafiri,

Kwa hayo machache kuwa na amani tu

Mkuu una familia nzuri sana zaidi ya watu wanavyofikiri. Uzuri umejitoa sana kwao,Mungu akusaidie umalizana na huyo Bi mdogo salama,kitu ambacho kiko wazi utashinda hiyo vita kwani umeshikilia mpini
 
Mkuu kwa nini unajiumiza sana,hati ina majina yako,bi mdogo siyo mke halali,yaani kwa nini ujiuzie? Tafuta mteja kabisa akupe hela nzuri kama utahamua kumpa robo ya pesa its okay akafie mbele huko,si ameamua kuishi kama shetani

Mwitoro atakua na moyo sawa na mfalme Daudi
Mfalme Daudi @Mwitoro
 
Siku ambayo hao watoto wangenitamkia hivyo mimi haijalishi ni wangu au sio wangu wangepata adhabu inayokwenda sambamba na mama yao na kutokea hapo ningewatuma wakatafute baba yao
Hata ningefanya hivyo
 
  • Thanks
Reactions: T11
Upo sahihi kabisa mkuu.

Lakini vipi kuhusu watoto wawili waliopatikana hapo. Nadhani ni busara ingetumika kuwawaza pia, tusiangalie tu matendo na hitimisho la hayo mapenzi ya baba na Mama yaliyopelekea kupatikana hao watoto.
Unajua Luv iko hivi,

Tayari mahusiano hayo ya wawili yameshakuwa shubiri. Kisheria hiyo mali ni yao hao wawili ambao wamekuwa wote katika mahusiano yasiyokuwa rasmi lakini kisheria yapo rasmi.

Na ndio maana nimeshauri kuwa ni bora akamalizane na mke wake halali na kumweleza kila kitu juu ya hilo. Natumaini atamwelewa vizuri na watoto pia awasogeze karibu na wenzie ili waweze kuwa pamoja kama familia, vinginevyo atapata shida sana.

Nyumba wauze, wagawane nuvu aelekeze kwa mkewe halali
 
  • Thanks
Reactions: Luv
Jamaa anakuambia akiuza assets zake una uhakika wa 700M - 1B[emoji38]

Halafu eti anang'ang'ania kieneo cha 50M

Nakumbka alisema viwanja sita hapo alinnua kimoja ndio akajenga hiyo nyumba hivo nyumba na eneo nafkir zinapita jamani khaaa 50M eneo lote hilo[emoji16]
 
Lakini unanichamba bure kabisa, tena kwa kuziamini hisia zako,
Umekasirika sana kwa kitu ambacho sio kweli kabisa

1,mimi sikuwahi kumuacha mke wangu hata kidogo,
2. Mimi sijawahi kugombana na mke wangu kiasi hata cha kukataliana tendo la ndoa
3.haya amekuja kuyajua kwa uhakika zaidi watoto wakiwa form na std 7
4 ukiangalia miaka hiyo ndio kipindi nimeanza kusumbuliwa huko nje,kwa hiyo ndio upendo ulizidi sana kwa bi mkubwa
5. Watoto kunitumia hiyo laki, kwanza huwa najiuliza wanitumie zaidi ili nifanyie nini
Mimi nina pesa yangu, viwanja natoka na mama, na anachangia kununua kinywaji ingawa mimi sio mywaji sana, bia mbili tu chali,

Najua wanamtumia mama yao, na uzuri wakati mwingine akitumiwa ananiambia,

Na akisha tumiwa nitaona nguo mpya hapo
Na mwenyewe anafurahi na mimi natafurahi kumwona mke wangu kapendeza na anakuwa kijana zaidi

Sijawahi kununua boxer wala fulana za ndani, vyote nashtukia zipo kabatini, na zile za zamani anatupa, tena wakati nakasirika anatupa zikiwa bado nzuri kabisa

Kiujumla hajawahi nichukia wala sijawahi mchukia
Turudi kwa watoto kutonitumia pesa, walishaona sizishobokei pesa zao, kwa sababu hawajui wanitumie kiasi gani ili nilizika, mimi nina pesa yangu ya kunitosha
Lakini wakati mwingine wadogo wanawapiga mizinga huko, unaona tu dogo karudi nyumbani na shati jipya , hapo si wanakuwa wamesaidia,

Mimi ninachohitaji kwao ni usafiri tu, na wameshaniahidi kunako majaliwa kama hawajajenga wanisuprise na usafiri,

Kwa hayo machache kuwa na amani tu
Kuchambwa lazima. Muhimu mnooo... maana unafanywa zoba.

Naomba nikuambie... acha kbs kujisemea eti una hela nyingi... hakuna kitu kitamu kama cha kupewa mzee wangu. Baba yangu ana jimudu vyema. Lakini vile vidogo nampatiaaa.... heheheeee yaanii anaona rahaaa. Usituongopee hapa. Yaan hakuna kitu raha kama kutunzwa. Yaan mashati alonunua babangu ameyatelekeza anavaa yangu. Na anasema malaika wangu ameninunulia haya ili nivae. Na yamepauka anayapenda balaa. Wewe hutaki hizo raha? Hakuna kitu kibaya kama kutengwa na familia. We rudi tu kwa mkeo ndo la msingi. Yaan rudi. Mwanao hata akakupa elf 10 ni tamu sana. Hela yako mwenyewe haina mzuka kama ya wale ambao wanakijali wewe na unawajali... rudi kundini.
 
Kufikia hapa mzee wangu nikupe tu moyo kuwa, umefanya maamuzi sahihi kuja kuomba ushauri hapa kabla hujachelewa ukapoteza kila kitu.

Wasamehe walio toa lugha chafu kukutukana ama kukufedhehesha, hawajui kesho yao,

Chukua ushauri unaoona unakufaa anza kuufanyia kazi tangu sasa, pesa juhudi ulizo poteza kwa huyo mwanamama chukulia tu ni kama ulikuwa unamsaidia mtu mwenye shida au mtoto yatima, hivyo Mungu atakukumbuka kwenye ufalme wake, amka asubuhi moja iliyo njema, Anza maisha mapya ukaipate jioni njema ya maisha yako.
 
Huyu mzee kuna vitu vingi sana katuficha na atapata ushauri ambao hautamsaidia sababu anafichaficha mambo.
King,
Nimeshazungumza kuhusu bi mkubwa, ni kweli baadaye sana alifahamu,
Tokea mwanzo nilisema huu uzi sitaki sana kumzungumzia,
Shabaha ya uzi ni bi mdogo, sasa nimejikuta nalazimishwa mpaka kufahamu mambo ya bi mkubwa,

Kiufupi hana tatizo na mimi, sasa kama ananichekea mdomoni tu mimi sijui
Kama ananitegea kunifanyia kitu mbaya, vile vile sijui, siwezi kuingia kwenye moyo wake

Nachoona tupo happy tu
Ameshakubali hali halisi tunaishi,
Hakuna anachokosa yetu uzima I mwake

Kama mnataka nifunguke zaidi kuhusu bi mdogo nitaendelea kadri nitakapokuwa nakumbuka mambo ya ovyozaidi

Kwa taarifa bado sijafunguka kuhusu vikao zaidi ya 8 tulivyokuwa tunaitisha, alikuwa anazungumza nini

Kwa nini alianza kuniita huyu hataki wageni

Majirani na marafiki zake walikuwa na tabia gani, na nini kiliwapa

Polisi.ustawi wa jamii, mahakama, ofisi za kata

Pote huko walikuwa Na mchango gani kuokoa huu uhusiano Na nini udhaifu mkubwa kabisa upo huko hapana nikashangaa hivi kweli wapo serious kabisa na matatizo ya watu au wapo kwa ajili ya kupiga soga tu, na kutaka kujua matatizo ya watu kiumbea

Mama ni mengi,
Na mwisho kwa ajili ya kumbukumbu zangu za baadaye, haya ni maandishi ambayo itabidi niyahifadhi kitaalaam ili niweze kutumia baadaye

Hasa tukifikia kipindi cha kupelekana mbele zaidi,

Ninachoshukuru kila tunapoendelea na michango na maswali, nashangaa nakumbuka mambo ambayo nilishayapotezea, Ahsante sana

Ila kumbukeni tu,

HII NI TRUE STORY
SIO TAMTHILIA

hata mimi kuna kipindi ninapokuwa mwenyewe nikifikiria haya matukio, iwe kwenye usafiri, ofisini, chooni, naoga, huwa nacheka sana,

Maana huo siamini kama haya mambo yanaweza kunitokea mimi na nikaendelea kuishi

Watu wengi sana wameshajiua kwa maana kama kama haya
 
Jamaa anakuambia akiuza assets zake una uhakika wa 700M - 1B[emoji38]

Halafu eti anang'ang'ania kieneo cha 50M
JF kisima cha burudani nimeamini😂😀

Wenye busara zao kimya kimya wasingetumia hilo eneo kama silaha dhidi ya huyo mchepuko.
Wangemuachia wakajitunzia heshima zao.
Jamaa kajivunjia heshima sana, hao watoto wa bi mdogo kwa wanayoyashuhudia, asijidanganye, eti kuna BOND, wanayashuhudia na mama yao anawaambia yote, baba yao anawafukuza anawadhulumu!

Miaka 100, hawezi kuwa na amani! Sababu kubwa haamini hapendwi na yule aliyempenda kwa kumhonga kila kitu!

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Mi hapo ndo nabaki na maswali inawezekanaje yani

Mimi mfano ndio bimkubwa bac hata iwe Mwitore ana ratiba za kutoka ucku kwenda kazin mara asafiri haijalishi bac mm kama bimkubwa nagundua ndani ya mwezi mmoja tu kuwa una hali sio ya kawaida Yani hamna mwanamke pia atakaejua una mtoto nje halafu situation ikawa poa hata iwe ni mtakatifu kiac gani wachilia kuzaa nje mko kwenye ndoa iwe ana mtoto tu na akaoa bila kusema ana mtoto bac siri ikitoka bac ugomv unaibuka je azae nje watoto wawil halafu mke aseme tu wajengee tu huko waishi yani wanawake sisi wa karne hii? Ugomv usiibuke? Anyway hatufanani wanawake Labda hawajagombana na bimkubwa Ila kwa ushaur tu bado ana nafac me nawajua watu wametengana kwa miaka zaidi ya 20 na ni wanandoa na wakarudiana na mambo safi tu nayy arekebishe sakata la nyumba then arudi kwa bimkubwa aitwe mchungaji ndoa ibarikiwe upya waanze maisha yao wasubir matunda ya pensheni
 
Connection aliyonayo na mchepuko ni hiyo nyumba, akiiuza, anajua ndiyo kampoteza mchepuko kimoja, hatomuona tena! Na hatamani hili litokee, thin line between love & hate!

Wala watoto hawajawaunganisha, kilichowaunganisha ni hela na nyumba.

Everyday is Saturday............................... [emoji41]
Halafu anazuga eti hamtaki huku roho inauma
 
Wenye upendo, heshima au hekima na wake zao, wana michepuko, ila hawana ulimbukeni huo wa mapenzi,

Hutosikia anapigana na mchepuko, au wanatoana ngeo, au wamepelekana polisi sijui ustawi wa jamii au wanashinda kutwa kujaza watu wa mtaa wakigombana,
Hiyo nyumba wangeiacha wangesonga mbele, hakuna mwenye busara anayejijua ana mali za 500M na atapokea pension 250M, atakubali ajidhalilishe katika mazingira hayo.
Especially kama watoto wa mke mkubwa wapo tiyari vizuri, NEVER!
Ni zaidi ya kurogwa!

Everyday is Saturday.............................. [emoji41]
Mwanzo nilisema aseme ukweli upande wa bi mkubwa baadae akaja kukiri bi mkubwa alikuja kujua huu mchepuko
Bado kuna kitu hajasema baada ya kujua nini kilifuata, asiseme mambo yaliisha kwa amani
 
27- namwomba yule rafiki ajaribu amwambie nina maongezi naye lakini, anajibu sisi tumekuja kwa shughuli ya mtoto, nikamwomba basi naomba niongee na wewe,
Akasema lakini nikupe simu ya mzee ili alinipe ruhusu ya kuongea na wewe,

Yule rafiki yangu alinivuta shati kwa ghafla bila kutegemea,
Akaniambia tuondoke, ‘kumbe mwanamke mwenyewe ndio huyu, mbona yupo,(primitive sana) mmm yaani mke wangu Primitive, aliishia tu kuniambia yule sio mwanamke wa kunisumbua mimi, yaani sio hadhi yangu kabisa, kwamba ana mwonekano wa kishamba hasa, acha tabia yake.
Mapenzi upofu
 
Exactly. Kuna heshima ipi na upendo gani mtu kwenda kuvunja agano lake la ndoa na mchepuko? Labda kama kuna definition mpya ya upendo na heshima
Mimi amenishangaza alivyo na ujasiri wa kujivika mizigo, wamejuana kidogo tu kurupu amempangia chumba, mara amemnunulia kiwanja, mara amemuweka miradi eti vya watoto[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]kajitesa sana maisha yake
 
Asaiv watangazie wapambe kuwa migogoro imeisha, [emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Ahsante,
Tatizo nalo wapambe, maana ukishatangaza tu
Nauza wapambe hawa hapa, mala nyumba ina mgogoro mala nini, maana uuzaji wa nyumba ni mgumu, bora uuze gari
images(6).jpg

Mzee ukitukana inaelekea una mabomu mazito haswa
 
Back
Top Bottom