Naomba Ushauri, Mpangaji wangu 'kaniblock'

Naomba Ushauri, Mpangaji wangu 'kaniblock'

Ndugu yangu DeepPond kusimamia wapangaji lazima uwe katili, hutakiwi kucheka na kima, hao ni watu ambao hawapendi kutimiza majukumu yao, ukiendelea na roho ya kondoo watakupaka mavi funga mkataba akuachie chumba chako weka mtu mwingine aliye serios na maisha lasivyo utapakwa sana mavi
Kama kuna jambo sipendi na anogopa ni kudaiwa kodi. Mimi huwa nina tabia ya kulipa kodi mwezi mmoja kabla ya kuisha. Napoishi kodi hulipwa january tarehe 1 na july tarehe moja kwa wapangaji wote.
Hapa kabla ya christmas nishamalizana na mwenye nyumba tutakutana tena july napo nitajitahidi nimalizane naye mapema.
Ukiwa waishi kwenye nyumba ya mtu kuwa mstaarabu kama kujenga ni rahisi mtu angejenga yake.
 
Kama kuna jambo sipendi na anogopa ni kudaiwa kodi. Mimi huwa nina tabia ya kulipa kodi mwezi mmoja kabla ya kuisha. Napoishi kodi hulipwa january tarehe 1 na july tarehe moja kwa wapangaji wote.
Hapa kabla ya christmas nishamalizana na mwenye nyumba tutakutana tena july napo nitajitahidi nimalizane naye mapema.
Ukiwa waishi kwenye nyumba ya mtu kuwa mstaarabu kama kujenga ni rahisi mtu angejenga yake.
Nikweli mkuu
 
Wakuu,

Kama Kuna sehemu nmekosea labda mnambie ninyi.

Kuna sehemu nna kibanda Cha wapangaji wanne huwa nakipangisha, Sasa Kutokana na mkataba.

Kila mpangaji ananilipa Kodi yake kutokana na tarehe aliyoingia kwangu, na Kodi huwa napokea kuanzia miezi 6.

Huyu mpangaji alihamia kwangu mwaka JANA mwezi Novemba mwanzoni, Hivyo Kodi yake Kwa miezi 6 ikaisha mwezi APRIL mwanzoni. Hivyo mwezi MEI mwanzoni alipaswa kunilipa tena Kodi Inayofuata. Na nilimtumia sms ya kumkubushia.

Tatizo la huyu mpangaji,
sms yangu ya kumkubushia aliiona Ila akanyamaza kimya, na mwezi MEI Ukaisha bila kupokea hata Senti Moja Wala taarifa yoyote ya dharula toka kwake. Nikanyamaza Kimya.

Ukaanza mwezi JUNI, nikampigia simu, akajifanya kasahau Kama Kodi imeisha na sms zangu hakuziona, Ila akaahidi kua atanilipa mwisho wa mwezi juni.
Nikasema sawa, nisubiri Kodi Yake mwisho WA mwezi juni

Mwisho WA mwezi JUNI ukaisha wote, jamaa Yuko kimya, nikampigia simu zangu hapokei, nilipobadili namba akapokea na akadai shule zimefunga, kwaiyo kwa Sasa amesafiri mkoani ila atanilipa akisharudi JULAI, nikasema sawa.

Jamaa amekuja kurudi mwezi JULAI mwishoni na Kodi yangu akanilipa mwezi AGOSTI mwanzoni. Nami nikienda kwenye daftari langu, nikaandika kua "Leo tarehe 03 AGOSTI, nmepokea Kodi ya mwezi MEI-OKTOBA"

Sasa Baada ya miezi 2 (yaani mwezi OKTOBA) nikamdai tena Kodi ya miezi 6, jamaa akalalamika mbona mapema Sana, mbona katoka kulipia juzi TU Kodi yake ya miezi 6. Namkumbusha kua ile Kodi yake ilipaswa kulipwa mwezi MEI, yeye kaivuta na kuja kuilipa mwezi AGOSTI, ndo maana imekua hivyo.

Basi Jamaa Akadai amenielewa, akasema atanilipa Kodi yangu mwisho WA mwezi oktoba akishapokea mshahara , nikasema sawa. Nikaenda zangu.

Mwisho WA mwezi umefika, jamaa Kimya.Nikajua labda katingwa, na kumkubushia ovyo kodi sio vizuri, nikakaa Kimya mpk mwezi NOVEMBA.

Katikati ya mwezi Novemba ikabidi nimpigie, akawa hapokei simu zangu, nilipobadili namba akapokea na kudai anaelewa, Ila Atalipa mwisho WA mwezi huu huu, zimebaki wiki 2 anaomba nimvumilie. Nikasema sawa.

Mpaka mwezi Novemba umeisha, sijapokea pesa Wala simu yoyote ya jamaa. Ulipoanza mwezi DISEMBA ikabidi nimpigie, Kama kawaida yake hakupokea simu zangu. Ila nilipobadili laini, akapokea na kudai amesafiri mkoani kula sikukuu,kurudi dar Ni Hadi January.

Nikaulizia khs Kodi yangu,akadai ataituma tar. 15 kwenye account yangu ya benki. Nikasema sawa,jitahidi.

Tar 15 imefika, Kimya.
Nikavumilia Hadi tar 20 Nako Kimya. Nimempigia simu zangu hapokei, nilipobadili laini akapokea na kudai tar 22 jioni anaituma, uhakika 100%. Nikasema sawa.

Tar 22 ikapita Kimya, mpaka Jana tar 24 ikabidi nimpigie, nikastuka Kila mara simu yake inadai inatumika Kisha inajikata. Nilipobadili laini, ikaita vizuri TU.Nikagundua kaniblock.

Nilivojitambulisha kua Ni Mimi mwenye nyumba wake, akakata simu ghafla na nilipojaribu kumpigia Tena, ikawa inadai anatumika Kisha inajikata. Nikagundua Hii namba nayo jamaa kaamua kuiblock.

HAPA KIUKWELI WAKUU NMEGHAFIRIKA SANA,

NAWAZA HUYU MPANGAJI SIJAJUA ANANICHUKULIAJE YAANI.

KAMA HAYUKO VZUR NI BORA ASEME MAPEMA AELEWEKE NA SIO KULETA UBABAISHAJI USIO NA KICHWA WALA MIGUU.

KUNIBLOCK NI UTOTO,UJEURI NA UPUUZI ULIOPITILIZA, PIA NI KUNIVUNJIA HESHIMA ILHALI KESHAVUNJA MASHARTI YA MKATABA.

Hapa nafikiria kumuandalia NOTISI Yake, ili January akirudi akatafute pa kuishi. Ila mama watoto kanishauri nisifanye hivo maana huenda Kuna magumu anapitia.

Wazo lake linanipa ukakasi sn maana Kama anapitia magumu, Kuna Sababu gani mpk aniblock zaidi ya kuhisi ananifanyia UJEURI TU.

Plz MNISHAURI pia wakuu🙏.
Notice ya pango ni miezi mitatu (3) tu yaani mpangaji kukaa bure akijiandaa kuhama, kwa hiyo huyo tayari keshajipa notice.

Akirudi mburuze kwa mwenyekiti S/M kudai haki yako aliyokaa ziada ya miezi mitatu ya notice na kumtaka ahame bila wewe kutoa visingizio.

Hapo kubali hasara ndogo kuliko kuendelea kufuga hicho kirusi.

Mpangaji yeyote mwenye mkwamo, hufunguka mwenyewe mapema kwa mwenye nyumba akiwa tayari kapiga hesabu zake ni mwezi gani atakuwa tayari kulipa na ukifika mwezi huo lazima alipe na siyo kusongesha blah blah zake tena.

Wapangaji aina hiyo siyo wazuri, umesoma kwenye mitandao issue ya Kawe, hadi Mbunge Gwajima kulivalia njuga?

Nyumba ya mamillioni imeuzwa na mpangaji, kisa kilo 38 za nyama na mwenye nyumba kubaki analalamika asijue aanzie wapi.

Baadaye akiisha kukuzoea sawasawa, mtaingia naye kwenye migogoro ya kupotezeana muda mahakamani na ukimhurumia lazima itakula kwako tu, mimi nina uzoefu sana na mambo hayo, kubali hasara hiyo ya kodi ya miezi mitatu kisha fukuza.
 
Ukiwa na roho nzuri sana na huruma zikizidi binadamu watakupanda kichwani hatimae kukung'ofoa nywele mpaka ubaki kipara.

Timua huyo mpangaji mkuu, umeonesha uungwana wako na ustaarabu ila kwa bahati mbaya mtendewa yeye hahitaji kufanyiwa hizo taratibu ulizo jaribu kumfanyia kiubinadamu.

Huruma sio malezi kqbisa timua huyo tapeli hapo kwako aisee! Haina haja ya kusubiri january mpigie simu aje atoe vitu vyake fasta usifanye makosa kabisa kumbakiza huyo mtu hapo kwako.

Hallelujah!!!
 
Na January inavyokuwa kavu, unasubirishwa mpaka mwisho wa February. Sasa hapo utajikuta mshavuruga mpangilio wa miezi ya kulipa. Kama vipi badili kitasa ila awepo Mwenyekiti wa Mtaa
Hapana asifanye hilo zoezi bila ya mwenye chumba kuwepo.

Amsubiri mpangaji wake arejee kisha ampeleke kwa mwenyekiti, kudai pesa ya pango iliyozidi miezi mitatu ya notice, kisha ampe masaa 24 kuondoka, kwa sababu alishajipa notice mwenyewe kwa kushindwa kulipa kodi zaidi ya miezi mitatu kwa makusudi.

Akishindwa kulipa hiyo hela pamoja na kuhama, ndiyo achukue hatua zaidi atakazoona zinafaa.
 
Ukiwa na huruma watakaa bure we siku waibukie ukiwa na watu wawil waambie nyumba ndo hii chumba kipo huyu anahama mwez ujao walipie kodi
 
Kuna mmoja kang’ang’ania nyumba ya upangaji kesharipotiwa lakin hatoki kuna watu wana roho ngumu
 
Kuna mmoja kang’ang’ania nyumba ya upangaji kesharipotiwa lakin hatoki kuna watu wana roho ngumu
Yaani mwenye nyumba anakosa mbinu za kumfukuza kisheria, hiii imekaaje hii!

Akishakaa bure miezi mitatu ni notice hiyo kajipa, anafukuzwa hata kwa fujo ya kutupiwa mizigo yake nje.

Kikubwa kila hatua ni lazima awepo kiongozi wa serikali ya mtaa.
 
Wapangaji ni changamoto jamaniii tena wengi wakorofi kulipa kodi huwa wanafanya makusudi wakitegemea Notisi,Hapo pesa ya kuhama kwako anayo si ya kukulipa deni.
Ww hujawahi kupanga au ndio maskin akipata
 
Wakuu,

Kama Kuna sehemu nmekosea labda mnambie ninyi.

Kuna sehemu nna kibanda Cha wapangaji wanne huwa nakipangisha, Sasa Kutokana na mkataba.

Kila mpangaji ananilipa Kodi yake kutokana na tarehe aliyoingia kwangu, na Kodi huwa napokea kuanzia miezi 6.

Huyu mpangaji alihamia kwangu mwaka JANA mwezi Novemba mwanzoni, Hivyo Kodi yake Kwa miezi 6 ikaisha mwezi APRIL mwanzoni. Hivyo mwezi MEI mwanzoni alipaswa kunilipa tena Kodi Inayofuata. Na nilimtumia sms ya kumkubushia.

Tatizo la huyu mpangaji,
sms yangu ya kumkubushia aliiona Ila akanyamaza kimya, na mwezi MEI Ukaisha bila kupokea hata Senti Moja Wala taarifa yoyote ya dharula toka kwake. Nikanyamaza Kimya.

Ukaanza mwezi JUNI, nikampigia simu, akajifanya kasahau Kama Kodi imeisha na sms zangu hakuziona, Ila akaahidi kua atanilipa mwisho wa mwezi juni.
Nikasema sawa, nisubiri Kodi Yake mwisho WA mwezi juni

Mwisho WA mwezi JUNI ukaisha wote, jamaa Yuko kimya, nikampigia simu zangu hapokei, nilipobadili namba akapokea na akadai shule zimefunga, kwaiyo kwa Sasa amesafiri mkoani ila atanilipa akisharudi JULAI, nikasema sawa.

Jamaa amekuja kurudi mwezi JULAI mwishoni na Kodi yangu akanilipa mwezi AGOSTI mwanzoni. Nami nikienda kwenye daftari langu, nikaandika kua "Leo tarehe 03 AGOSTI, nmepokea Kodi ya mwezi MEI-OKTOBA"

Sasa Baada ya miezi 2 (yaani mwezi OKTOBA) nikamdai tena Kodi ya miezi 6, jamaa akalalamika mbona mapema Sana, mbona katoka kulipia juzi TU Kodi yake ya miezi 6. Namkumbusha kua ile Kodi yake ilipaswa kulipwa mwezi MEI, yeye kaivuta na kuja kuilipa mwezi AGOSTI, ndo maana imekua hivyo.

Basi Jamaa Akadai amenielewa, akasema atanilipa Kodi yangu mwisho WA mwezi oktoba akishapokea mshahara , nikasema sawa. Nikaenda zangu.

Mwisho WA mwezi umefika, jamaa Kimya.Nikajua labda katingwa, na kumkubushia ovyo kodi sio vizuri, nikakaa Kimya mpk mwezi NOVEMBA.

Katikati ya mwezi Novemba ikabidi nimpigie, akawa hapokei simu zangu, nilipobadili namba akapokea na kudai anaelewa, Ila Atalipa mwisho WA mwezi huu huu, zimebaki wiki 2 anaomba nimvumilie. Nikasema sawa.

Mpaka mwezi Novemba umeisha, sijapokea pesa Wala simu yoyote ya jamaa. Ulipoanza mwezi DISEMBA ikabidi nimpigie, Kama kawaida yake hakupokea simu zangu. Ila nilipobadili laini, akapokea na kudai amesafiri mkoani kula sikukuu,kurudi dar Ni Hadi January.

Nikaulizia khs Kodi yangu,akadai ataituma tar. 15 kwenye account yangu ya benki. Nikasema sawa,jitahidi.

Tar 15 imefika, Kimya.
Nikavumilia Hadi tar 20 Nako Kimya. Nimempigia simu zangu hapokei, nilipobadili laini akapokea na kudai tar 22 jioni anaituma, uhakika 100%. Nikasema sawa.

Tar 22 ikapita Kimya, mpaka Jana tar 24 ikabidi nimpigie, nikastuka Kila mara simu yake inadai inatumika Kisha inajikata. Nilipobadili laini, ikaita vizuri TU.Nikagundua kaniblock.

Nilivojitambulisha kua Ni Mimi mwenye nyumba wake, akakata simu ghafla na nilipojaribu kumpigia Tena, ikawa inadai anatumika Kisha inajikata. Nikagundua Hii namba nayo jamaa kaamua kuiblock.

HAPA KIUKWELI WAKUU NMEGHAFIRIKA SANA,

NAWAZA HUYU MPANGAJI SIJAJUA ANANICHUKULIAJE YAANI.

KAMA HAYUKO VZUR NI BORA ASEME MAPEMA AELEWEKE NA SIO KULETA UBABAISHAJI USIO NA KICHWA WALA MIGUU.

KUNIBLOCK NI UTOTO,UJEURI NA UPUUZI ULIOPITILIZA, PIA NI KUNIVUNJIA HESHIMA ILHALI KESHAVUNJA MASHARTI YA MKATABA.

Hapa nafikiria kumuandalia NOTISI Yake, ili January akirudi akatafute pa kuishi. Ila mama watoto kanishauri nisifanye hivo maana huenda Kuna magumu anapitia.

Wazo lake linanipa ukakasi sn maana Kama anapitia magumu, Kuna Sababu gani mpk aniblock zaidi ya kuhisi ananifanyia UJEURI TU.

Plz MNISHAURI pia wakuu🙏.
Vumilia yote lakini sio dharau. Huyo analeta dharau sasa. Wife anafanya maamuzi kwa hisia wee fanya kwa kutumia akili
 
Pole sana mkuu. Mimi wapangaji wangu wakizingua tu kulipa kodi nampa notice ya siku saba awe tayari amenikabidhi funguo za nyumba, na pia nyumba aiache ikiwa na hali ya usafi kama siku anaingia.

Pili bill ya maji ni shared kwa kila apartment block, hivyo ikitokea mpangaji anazingua tu kulipa bill ya maji na yeye notice inamhusu kwa sababu siwezi sababisha usumbufu kwa wapangaji wengine kwa ajili ya mzembe mmoja.

Kwa wapangaji huwa sitaki mzahaa na FEDHA yangu
 
Back
Top Bottom