Naomba ushauri na mapendekezo kuhusu Suzuki Escudo old

Naomba ushauri na mapendekezo kuhusu Suzuki Escudo old

Kwanza,haikisha unamtumia fundi mzoefu,ukiogopa gharama,utalia. Japo unatakiwa ujue kinatengemezwa kitu gani.
1. Fuel pump yako ina hali gani?
2. Kwa sasa,ulaji wake umekaaje?
3. Spark plugs unazotumia zikoje?! Unaweza itoa utuonyeshe!
4. Engine yako ina hali nzuri(kama ilibadilishwa)
5. Uliagiza,au ulichukua kwa mtu!
6. Unajua lakini pia kuwa fuel tank yake ina chamber? Kwa maana mafuta yakikata si kwamba yanakuwa yameishamo!
tatizo wengi wanaotumia magari yenye engine ya 3s wanalalamika sana ulaji wake wa mafuta ni mkubwa
 
Duh.yani uifananishe N.Patrol/N.Safari na LR kweli?
Kwa Nissan ataingia gharama sababu ya spea kua ghali na adimu kwa baadhi ya mikoa ila kwa wenzetu kenya wanazo zakutosha maana wanatumia sana nissan.
Offroad zinakata shimo haswa bila kuhitaji matengenezo ya kila mara kama LR yenye ma-leakages zikitokaga rough roads!

spea gharama ila ukifunga umefunga!
Naona wabongo tuna kasumba ya kuziogopa sana Nissan
 
tatizo wengi wanaotumia magari yenye engine ya 3s wanalalamika sana ulaji wake wa mafuta ni mkubwa
Ni kweli. Sasa,hizo engine zinatumiwa na magari aina ya jeep. Utaambiwa mtu hataki kutemea amekalia kigoda,anataka gari yenye nguvu. Ukimwambia ki Toyota baloon anakwambia hataki. Kwenye uwezo mdogo,wanunue BB. Af,unanunua gari imechakaa,kisa bei rafiki. Hujiulizi aneuza sababu ni nini? Na unapoamua kuchukua,basi andaa na gharama za ziada kuweka katika hali unayotaka wewe
 
Ni kweli. Sasa,hizo engine zinatumiwa na magari aina ya jeep. Utaambiwa mtu hataki kutemea amekalia kigoda,anataka gari yenye nguvu. Ukimwambia ki Toyota baloon anakwambia hataki. Kwenye uwezo mdogo,wanunue BB. Af,unanunua gari imechakaa,kisa bei rafiki. Hujiulizi aneuza sababu ni nini? Na unapoamua kuchukua,basi andaa na gharama za ziada kuweka katika hali unayotaka wewe
sawa sawa nakupata vilivyo mkuu, kwahiyo bajeti yangu na kwa mazingira niliyoraja hapo juu unanishaurije mkuu
 
Wakuu habari ya muda huu,

Nimekuja mbele yenu nipate ushauri na mapendekezo zaidi kuhusiana na gari aina ya Suzuki Escudo old model.

Mimi napiga sana mihangaiko ya vijijini mashambani ambako ni 100% rough road. Kulingana na mazingira hayo nilitamani gari yenye spec zifuatazo;



Sasa kulingana na vigezo hivyo nikawaza Suzuki Escudo old model maana naskia zina ulaji mzuri wa mafuta naskia zinafika hadi 12km/l, pia nasikia 4WD yake ni balaa. Japo nasikia zina changamoto ya bodi kuingiza vumbi ndani. Nina mpango wa kuchukua mkononi na bajeti yangu ni 6m max.

Awali niliwaza kuhusu Rav4 old, changamoto ikawa ni ulaji wa mafuta maana naona nyingi zinaenda 7km/l sasa kwa mizunguko yangu nikaona haitanifaa japo sifa nyingine inazo.

Naombeni ushauri wenu kama nipo sahihi kwa chaguo hilo na kama kweli escudo old ina sifa hizo na pia kama kuna mbadala tofauti na hiyo escudo old kwa bajeti hiyo ya 6m mkononi. Asanteni.
Njoo tuyajenge ninayo Suzuki hiyo naona vijana wanichakaza nipigie +255622642620
 
sawa sawa nakupata vilivyo mkuu, kwahiyo bajeti yangu na kwa mazingira niliyoraja hapo juu unanishaurije mkuu
Kwanza kabisa,inategemea na wewe unapenda gari aina gani. Af, kwa nini unanunua gari? Bro,usijichaanganye,gari ni kama malaya unayemhudumia wewe. Pesa unayotumia inaondoka hairudi. Kama huna vyanzo vingine vya kuihudumia,utalia.
Pili,uwezo wako unakuruhusu?
Tatu,kumbuka unachukua gari lililotumika. Ila kwa sababu unataka gari,ukiliona utanunua tu.
Nne, mafundi hawajakuibia. Nawatukana wanisamehe kama humu wamo. Ila wale ndo watoto wa mbwa halisi kama hujui
Tano, Je, bajeti yako inatosha kukava imajensi(ulaji wa mafuta,matengenezo,kuiweka katika hali unayotaka)? Kama unataka la M18, angalau tenga 10 nyingine.

Ni kweli maendeleo ni gharama. Mi nakushauri uanzie kigari cha bei ndogo,kikupe uzoefu,ukitunze,ukishajiweka sawa,utakiuza uongezee uchukue la ndoto yako.
 
Kwanza kabisa,inategemea na wewe unapenda gari aina gani. Af, kwa nini unanunua gari? Bro,usijichaanganye,gari ni kama malaya unayemhudumia wewe. Pesa unayotumia inaondoka hairudi. Kama huna vyanzo vingine vya kuihudumia,utalia.
Pili,uwezo wako unakuruhusu?
Tatu,kumbuka unachukua gari lililotumika. Ila kwa sababu unataka gari,ukiliona utanunua tu.
Nne, mafundi hawajakuibia. Nawatukana wanisamehe kama humu wamo. Ila wale ndo watoto wa mbwa halisi kama hujui
Tano, Je, bajeti yako inatosha kukava imajensi(ulaji wa mafuta,matengenezo,kuiweka katika hali unayotaka)? Kama unataka la M18, angalau tenga 10 nyingine.

Ni kweli maendeleo ni gharama. Mi nakushauri uanzie kigari cha bei ndogo,kikupe uzoefu,ukitunze,ukishajiweka sawa,utakiuza uongezee uchukue la ndoto yako.
kiufupi kulihudumia haitakuwa shida kwangu ila ni na ulazima wa kumiliki gari kulingana na mizunguko yangu ya vijijini mashambani kama nilivyosema hapo awali,

sasa kulingana na changamoto za barabara za mashambani ndio maana niliwaza Escudo ile old pamoja na Rav4

sasa nikapata kigugumizi kwenye Rav4 old kama nilivosema hapo awali kuwa watumiaji wengi wanalalamika ulaji wa mafuta.

isingekuwa ni ruti za mashambani ni kweli ningeangalia kigari kidogo
 
kiufupi kulihudumia haitakuwa shida kwangu ila ni na ulazima wa kumiliki gari kulingana na mizunguko yangu ya vijijini mashambani kama nilivyosema hapo awali,

sasa kulingana na changamoto za barabara za mashambani ndio maana niliwaza Escudo ile old pamoja na Rav4

sasa nikapata kigugumizi kwenye Rav4 old kama nilivosema hapo awali kuwa watumiaji wengi wanalalamika ulaji wa mafuta.

isingekuwa ni ruti za mashambani ni kweli ningeangalia kigari kidogo
Sasa brother,kubaliana na mimi,ukisema ni imara,labda. Lakini kwenye kuhimili,haizidi Rav4
 
kiufupi kulihudumia haitakuwa shida kwangu ila ni na ulazima wa kumiliki gari kulingana na mizunguko yangu ya vijijini mashambani kama nilivyosema hapo awali,

sasa kulingana na changamoto za barabara za mashambani ndio maana niliwaza Escudo ile old pamoja na Rav4

sasa nikapata kigugumizi kwenye Rav4 old kama nilivosema hapo awali kuwa watumiaji wengi wanalalamika ulaji wa mafuta.

isingekuwa ni ruti za mashambani ni kweli ningeangalia kigari kidogo
Kwa bajeti yako nenda kwa escudo au jimny.rav 4 anafeli kwa hao kwenye fuel consumption na 4wd.awd yake haifui dafu kwenye tope kwa hizo gari.
 
ni nyingi sana nadhani with proper maintainance hata 10km/l kufika ni mziki
Unaongelea nyingine tofauti na hii?
We changamsha jukwaa,maana kama nyingi,tafuta pikipiki. Unaelezwa kilichofanyiwa kazi wala siyo stori ya kijiweni,mara hivi,mara vile.
Hiyo achana nayo we nunua BB. Inakufaa sana
 

Attachments

  • Screenshot_20231123-101859.jpg
    Screenshot_20231123-101859.jpg
    116 KB · Views: 35
Back
Top Bottom