Naomba ushauri tafadhali

Naomba ushauri tafadhali

Nijuacho mimi hapo ni nguvu za giza na maagano ya ufalme wa giza,maisha yetu tunayo ishi huwa yana anzia rohoni.ninakushauri OKOKA mkuu,wokovu sio dini mpya ni kumkiri YESU kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako.ww ndio unajua namna gani unaumia na hayo maumivu humu ndani hayupo wa kukusaidia kwa kiasi ambacho utapata raha nafsini mwako zaidi ya Damu ya Yesu inenayo mema na iliyo lipa gharama ya hayo yote.karibu kwenye ulimwengu wa nuru
 
Shekh, nimeangaika mnoo kwa maustadha bado shida inaendelea.
Nasikiza saaana Quran na kuswali pia.
Nimeenda miskiti kuomba dua, kilichotokea, narudi tu nalopokewa na mke kwamba namswalia kabla hajafa misikitini
Huko unateseka mwamini Yesu mwana wa Mungu ,utaokoka.
 
Pole sana kwa changamoto,
Kua karibu na Mola wako kuliko ulivyowahi kua hapo mwanzo. Amini kabisa hakuna mtu au kitu chchote kinachoweza kukusaidia isipoku Allah
Jitahidi kukaa na udhu, dhikri zifanye nyakati zote ( subhanAllah, Allahu Akbar, la ilaha illa llah, la hawla wala quwata ila billah, nk, ayaat kursiyu baqara 255, suraht falaq, nas na ikhlas) ziwe zinapita moyoni mwako) swali rakaa mbili kisha mwombe Allah akuondolee hii mitihani, lia nae sema kama unamuona hakika atakusikia. Jifunze majina ya mwenyezi Mungu na maana yake yeye anajibu , anasikia , na anafanya jambo kua jepesi akitaka.
Ila hakikisha mfumo wako wa maisha unabadilika kbisa. Fanya aliyoamrisha mola wako na acha aliyokataza.
Pia usianze kuruka ruka mara kwa shekh mara kwa mganga mara kwa wachungaji, simama wewe pekee Allah atasikia
Ukisoma pia al fatha imaanishe utapata wepesi
(Mfno pale unaposema iyyak naabudu wa iyyaka nastaghiin hakikisha kwel ni yeye unamuuabudu pekee na kumtaka msaad yeye tu na si mwingin)
Kisha naapa kwa Allah kua kila kitu kitakaa sawa.
Ukiweza pia simama visimamo vya usiku
Shukran Sana umemuwaidhi ipasavyo ...
Asichanganye dua na shirki ...usiruke ruke ndugu tawakal kwa Allaah..
 
Kama ni muslim fanya dua sana either mwenyewe au kushirikisha watu wanaoweza kufanya dua...zoezi hili liendane sambamba na kutoa sadaka kwenye vituo vya watoto yatima au nyumba za ibada..

Kama ni christian, fanya maombi toa sadaka...jpili nenda kanisani...

Dunia ina mambo sana magumu na mepesi pia..chukulia huo ni mtihani kama wengine unavyowaona wana mitihani..

InshaAllah Mungu ni mwema atakufanyia wepesi..
 
Mkuu pole Sana sana mpk nmeogopa sana. Na nmejaribu kuvaa viatu vyako hakika vmenipwaya Sana uwenda ningekimbia familia.
Sasa hapo kuna maagano ya kiukoo yanakufatilia paspo ww kujua kuna viapo viliapwa huko zamani na kafala kutolewa uwenda ww umekiuka baadhi ya Mambo
Utateseka Sana bro hayo maagano ya ukoo lazma ujitenge nayo haraka sana.
Raia humu huwa wanambeza Sana mwamposa bt hakika kuptia jina la Yesu amesaidia wengi Sana.
Ungekuwa upo kanda ya ziwa huku ningekuja huko na rafiki yangu tuchape maombi hapo tuvunje hayo maagano hakuna kingebaki kukusumbua usje sema twataka hela au sadaka hapana yaani ni nauli Tu basi. Tungekuonyesha uwezo WA Jina na Damu ya Yesu hayo madude yangesema yanatoka wapi Amini usiamini
 
Mkuu pole Sana sana mpk nmeogopa sana. Na nmejaribu kuvaa viatu vyako hakika vmenipwaya Sana uwenda ningekimbia familia.
Sasa hapo kuna maagano ya kiukoo yanakufatilia paspo ww kujua kuna viapo viliapwa huko zamani na kafala kutolewa uwenda ww umekiuka baadhi ya Mambo
Utateseka Sana bro hayo maagano ya ukoo lazma ujitenge nayo haraka sana.
Raia humu huwa wanambeza Sana mwamposa bt hakika kuptia jina la Yesu amesaidia wengi Sana.
Ungekuwa upo kanda ya ziwa huku ningekuja huko na rafiki yangu tuchape maombi hapo tuvunje hayo maagano hakuna kingebaki kukusumbua usje sema twataka hela au sadaka hapana yaani ni nauli Tu basi. Tungekuonyesha uwezo WA Jina na Damu ya Yesu hayo madude yangesema yanatoka wapi Amini usiamini
Nashukuru saaana, nimezingatia
 
Pole sana mkuu,

Upo mkoa gani?
Wake zako wote wanaonyesha dalili za magonjwa ya akili, usipokuwa makini hata huyo wa sasa naye siku si nyingi atachizika,


Jaribu kwenda Muhimbili au Mirembe ukawaome wataalam.
 
Shekh, nimeangaika mnoo kwa maustadha bado shida inaendelea.
Nasikiza saaana Quran na kuswali pia.
Nimeenda miskiti kuomba dua, kilichotokea, narudi tu nalopokewa na mke kwamba namswalia kabla hajafa misikitini
tatizo unaswali kwasababu ya matatizo ndo shida..
 
Salaaam.
Nimekuwa na changamoto katika maisha yangu na familia yangu.
1. Nilikuwa nimeowa mke wa kwanza 1996 na kubahati kuishi kwa miaka 9 ivi na kupata watoto 3. Lakini, ikaja changamoto mke akawa ananishutumu kuwa nawatuma watu wamzalilishe, akawa anakosa amani aliamini kuwa nawatuma watu wamchungulie Hadi chooni/bafuni na hata tunapolala. Nikamuacha kwa kuamini alikuwa analengo lake. Lakini baada ya kuachiwa Hali yake ikawa mbaya zaidi na kuwa mtu aliechanganyikiwa.

2. Nikaowa Tena 2003, lakini baada ya miaka Kama Saba Hali ya yule mke wa kwanza ikajitokeza kwa huyu na kupelekea kukosa Furaha ya ndoa. Amekuwa anasikia na kusema Mambo ambayo wengine tunashangaa tu na ngumu kuamini. Anaweza kuwa ndani lakini akakuambia watu wanamzomea au wanamtuka nje bila wengine kusikia
Mbaya zaidi kunasiku akaamka na kuniambia kuwa ameota kuwa na jitu kubwa na lilimwambia yeye ni mkubwa na aniambie nimwaache. Baada ya mwezi, anadai kuachwa. Naogopa kumwacha kwakuhofia lile la mke wa awali.
3. Wakati napambana na Hilo, mwaka juzi mtotowangu alitoka nyumbani nilikozaliwa na kuanguka na pikipiki na lakini hakuumia sehemu yoyote ile lakini alisema alishangaaa tu ameanguka na hakuwa anajielewa na kujikuta tu anaburuza pikipiki kwa mda mrefu na baada ya kupata fahamu akawasha na kurudi nyumbani anakoishi. Toka siku hiyo akawa anaongea Mambo ambayo ni ngumu kuelewa, atoki ndani mchana na kuchukia kuwa karibu na watu.
Naomba Allah akuongoze kunishauri Hilo maana linanikosesha amani. Naomba saana kwa Allah Ila nakosa maarifa ya kutafakari ndoto zangu.
1996+9=2005, wewe uliongeza mke 2003.

Pole sana, muombe Mungu atakusaidia hakika.
 
Back
Top Bottom