Naomba ushauri wa biashara ya malori

Naomba ushauri wa biashara ya malori

Ahsante sana Kwa mchango wako kaka.
Kuhusu Mafundi wa Kibongo ni kweli aiseeee. Yaani gari ikienda garage Kwa ajili ya Corrective maintenance ni ngumu kurudi kwenye Hali yake ya mwanzo. Nimeshaexperience hili jambo.
Nilitaka ni quote kipande kipande matokeo yake technology ikanipiga chenga nikakuta nime edit post yako badala ya ku'comment

Si shauri kabisa na siamini kwenye kubadili mfumo wa gari haswa kwenye steering!
 
Nilitaka ni quote kipande kipande matokeo yake technology ikanipiga chenga nikakuta nime edit post yako badala ya ku'comment

Si shauri kabisa na siamini kwenye kubadili mfumo wa gari haswa kwenye steering!
Vp kwenye kubadili mguu wa jini yaani unanunua truck ambayo kiuhalisia ni 4X2 then unaibadili kuwa 6X2. Nayo hii imekaaje Mkuu?
 
Mkuu, kwahyo unachoshauri ni kutozibadili kuwa RHS? Je, hazitowasumbua madereva hususani kwenye suala zima la kuovertake?

Kuna mdau huko juu alisema ni muhimu dereva wa RHS kupata somo jinsi ya kuendesha LHS. Je, wewe ulipata hilo somo? Je, ni kweli Kuna huo umuhimu?

Raha uliyojisikia ni Ipi hasa, unaweza kuelezea japo kidogo?
Kama umenunua gari ya Lhd ,ambayo kwa sasa ni cheap kuliko Rhd , bora libaki hivyo hivyo.
Kama unapenda au ni muhimu kuwa na gari ya Rhd , kwa sababu kadha wa kadha kama madereva n.k, ni bora ununue original ikiwa Rhd.
Nitazungumzia Scania ,maana nimeishi nazo, by default Design ya Scania ni Lhd , Scania za uk, ireland ,n.k ambazo ni Rhd, zimefanyiwa add on. Ie kuna parts zinaongezewa kuja upande wa kulia , mf gear link , hii huwa inatoka hapo kushoto ambapo gearstick ya Lhd huwepo kuelekea kulia , kuna air pipes za brake valve , pia huwa llinked kutoka kushoto kwenda kulia , kwa sababu hii procedure inafanywa kiwandani huwa ni salama , maana wanatumia designed parts. Hata hivyo bado scania za Rhd zina gear stick nzito kuliko za Lhd .
Nyingi nilizoziona zimefanyiwa conversion ,zinasumbua sana gear , zinasumbua sana short circuit kwa sababu ya kuhamisha fuse box , na nyingi vitu vizuri kama retarder huwa hazirudi haya kama ilikuja nayo , maana wanaofanya ile wiring uswahilini hawana uwezo wa kuirudishia kila kitu,
 
Vp kwenye kubadili mguu wa jini yaani unanunua truck ambayo kiuhalisia ni 4X2 then unaibadili kuwa 6X2. Nayo hii imekaaje Mkuu?
Hiyo haina shida sana japo hua kuna makosa yanatokea! Vipimo vikikosewa jiandae kubadili matairi mara kwa mara, kuna ulaji mbaya ambao utalazimika kurudia marekebisho na kuna ambao utaweza vumilia, hapo ni kwenye vipimo!

Kuna ile teriazi ya super single ambayo ina katakona na tairi za mbele, ile ni janga bora ikae nyuma au hata hapo mbele ila isikate kona, unaweza kukuta mbele kuzima tu ila hapo ndio panakua na shida na mara nyingi ndipo pana peleka uharibifu mbele

Kuna setup ya booster pale katikati kwa ajili ya kunyanyulia terias wengine wanafunga vi booster namba8 like structure na wengine wanaweka airbags, pale napo pasipo nyooka ni mtihati jiandae kubadili busta hiyo mara kwa mara

Kuna mzani pale wa booster za diff, huwa nazo hawaset vizuri na mara nyingi unakutana na valve badala ya magnetor, sio mbaya ila magnetor ndio nzuri zaidi! Maana unakuta zile booster za teriazi zinajaa zaidi kuliko za diff hivyo kufanya diff kushindwa kugandamiza vizuri chini, ndio maana unakuta gari za namna hii haswa scania unakuta imekwama mahala pakijinga kama kirikuu

Napenda ile teriazi iwe inakaa nyuma yaani badala ya kusukumwa na diff iwe inavutwa! Ikikaa mbele kuna muda inakua kama kigingi, ni mpaka umwage upepo na ikiwa na mzigo hata ukimwaga upepo mda mwingine haisaidii, japo ni sehemu chache unaweza pata usumbufu huo au kwenye rough_road zenye mashimo makubwa ( madimbwi ya maji au yaliyokauka maji )

Teriazi ya double tire ni nzuri zaidi kuliko ya single hata kwenye ubebaji wa mzigo
 
Kama umenunua gari ya Lhd ,ambayo kwa sasa ni cheap kuliko Rhd , bora libaki hivyo hivyo.
Kama unapenda au ni muhimu kuwa na gari ya Rhd , kwa sababu kadha wa kadha kama madereva n.k, ni bora ununue original ikiwa Rhd.
Nitazungumzia Scania ,maana nimeishi nazo, by default Design ya Scania ni Lhd , Scania za uk, ireland ,n.k ambazo ni Rhd, zimefanyiwa add on. Ie kuna parts zinaongezewa kuja upande wa kulia , mf gear link , hii huwa inatoka hapo kushoto ambapo gearstick ya Lhd huwepo kuelekea kulia , kuna air pipes za brake valve , pia huwa llinked kutoka kushoto kwenda kulia , kwa sababu hii procedure inafanywa kiwandani huwa ni salama , maana wanatumia designed parts. Hata hivyo bado scania za Rhd zina gear stick nzito kuliko za Lhd .
Nyingi nilizoziona zimefanyiwa conversion ,zinasumbua sana gear , zinasumbua sana short circuit kwa sababu ya kuhamisha fuse box , na nyingi vitu vizuri kama retarder huwa hazirudi haya kama ilikuja nayo , maana wanaofanya ile wiring uswahilini hawana uwezo wa kuirudishia kila kitu,
Bora umekazia mkuu! Nili sahau hiyo section ya gear hua inakera sana haswa ukikumbana na Fundi Maiko[emoji1787]
Hata dashboard hua havirudi ku fuction kama awali utakuta switch hazifanyikazi baadhi RPM unaweza kuikuta salama ila c speedmeter, mara chahe sana kuikuta salama
 
Tafuta Howo mpya gharama za uendeshaji ni ndogo kuliko European trucks. Biashara ikikuwa ndio uende huko kwa European trucks. Trailer la double tyres ndio linabeba mzigo zaidi kutokana na sheria mpya za Tanroads(mizani) ...hawataki singles kwente barabara zao hivyo wamepunguza uzito unaoruhusiwa kwenye axles za single tyres.
Mkuu umemshauri vizuri sana nakuongezea nyota ya tatu boss
 
Unajua wengi tunawekeza tulicho Fanya utafiti

Mi sijawahi kumiliki roli ila nimeendesha pamoja na kusimamia

Ukiwa umepata gari nzuri Dereva mtunzani Fundi anae jua wajibu wake

Hii biashara utaipenda

Ili uweze kuifanya kwa Uhuru lazima kila Dereva awe na mkataba wa kazi utakao ondoa changamoto zisizo na ulazima kuwepo

Lazima uwe na msimamizi anae jua magari vizr

Hapo lazima utoboe
Amina mkuu ubarikiwe
 
8th Floor, CRDB Building, Azikiwe Street, Dar es Salaam, Tanzania. PO Box 20660
+255 22 2127 398
+255 : 22 2129 891
+255 22 2127 268
info@moassurance.co.tz
Piga hizo simu akuelekeze uende yard Nyerere rd nyuma Pepsi kila mtu eneo hilo anawajua ana horse kama 700 hivi kila mwezi zinaingia...trailers ziko mbagala...kila la kheri
Ubarikiwe mkuu.
 
Leo ndio mara yangu ya kwanza kusoma Uzi wenye wachangiaji zaidi ya 200 na kumalizia .
Nilichojifunza anunue flatbed trailer mpya na iwe springs na lazima iwe double tyre . BPW, wabco , Ukiagiza mwenyewe kutoka China mpaka hapa ni $12000 ushuru ni milioni 12.malipo mengine hapo bandarini hayo sijui utaonge na ajent wako mkuu kama sijakosea haizidi milioni 2.huu ni utafiti wangu niliofanya kwa miezi 6
Screenshot_2023-03-23-18-47-17-786_com.whatsapp.jpg
 
Mkuu nunua Shacman used au Howo utafanya Kazi nalo miaka 6 halafu litakuwa limesharudisha , Scania kwa wewe unayeanza litakuwa na changamoto kidogo. Good Luck mkuu . Ushuru wa schacman TRA 13 Million . Horse ya shacman or Howo ni $ 17000 mpaka Dar .
Screenshot_2023-03-26-16-39-31-466_com.whatsapp.jpg
Screenshot_2023-03-26-16-40-00-730_com.whatsapp.jpg
Screenshot_2023-03-17-11-20-25-584_com.adobe.reader.jpg
 
Mkuu nunua Shacman used au Howo utafanya Kazi nalo miaka 6 halafu litakuwa limesharudisha , Scania kwa wewe unayeanza litakuwa na changamoto kidogo. Good Luck mkuu . Ushuru wa schacman TRA 13 Million . Horse ya shacman or Howo ni $ 17000 mpaka Dar . View attachment 2566702View attachment 2566703View attachment 2566704
Ahsante kaka.

Ila hizo Bei za Shacman labda kama ni used wanaita refurbished. Refurbished mpaka bongo si chini ya Milioni 70. Gari za kichina unashauriwa ununue ikiwa mpya. Hivyo hizo Gharama ulizoweka ni unrealistic. Fanya Tena uchunguzi makini ndugu. Ahsante
 
Ahsante kaka.

Ila hizo Bei za Shacman labda kama ni used wanaita refurbished. Refurbished mpaka bongo si chini ya Milioni 70. Gari za kichina unashauriwa ununue ikiwa mpya. Hivyo hizo Gharama ulizoweka ni unrealistic. Fanya Tena uchunguzi makini ndugu. Ahsante
Ni used mkuu na ni Refurbished. Kweli wewe ni Msomi kama umeweza kuandika hili neno Refurbished basi uko vizuri kielimu mkuu . Hata saw ingine Linanishinda kutamka ila nalielewa vizuri
 
Ahsante kaka.

Ila hizo Bei za Shacman labda kama ni used wanaita refurbished. Refurbished mpaka bongo si chini ya Milioni 70. Gari za kichina unashauriwa ununue ikiwa mpya. Hivyo hizo Gharama ulizoweka ni unrealistic. Fanya Tena uchunguzi makini ndugu. Ahsante
Ushuru wa TRA mkuu
Screenshot_2023-03-26-22-44-11-288_com.android.chrome.jpg
 
Dear james, if we can catch the March vessel, for the tractor head, we can do at CIF USD$17, 200. For the used trailer, we can do at CIF USD$10, 500. That's to say, the total cost for the tractor truck and the trailer is USD$27, 700,the new flatbed trailer springs leaf you will add $2000
 
Kumi na Moja na upuuzi alfajiri gari iliendelea na safari. Baada ya kama dakika 30, niliona kupitia GPS gari imesimama. Ilisimama Kwa Muda Mrefu sana zaidi ya dakika 40. Muda mchache baadae nilipokea simu kutoka Kwa Namba ngeni Kwa njia ya WhatsApp.

Alijitambilisha kama dereva aliyekuwa nyuma ya gari yangu wakiongozana. Alinitaarifu juu ya Ajali iliyohusisha gari yangu. Gari imedondoka kama km 20 kutoka kwenye mizani ya Mpika.

Kiza kikatawala, mapigo ya Moyo yakaongezeka, Miguu ikakosa nguvu. Sikujua kilichoendelea tena. Nilizinduka baada ya kumwagiwa maji. Itaendelea......
POLE SANA MKUU . NIMESIKITIKA SANA MKUU. ULIFANIKIWA KUREJESHA GARI TÀNZANIA? MALIZIA HUU MKASA BHANA.
 
Dear james, if we can catch the March vessel, for the tractor head, we can do at CIF USD$17, 200. For the used trailer, we can do at CIF USD$10, 500. That's to say, the total cost for the tractor truck and the trailer is USD$27, 700,the new flatbed trailer springs leaf you will add $2000
Ahsante. Sasa kununua gari ya kichina iliyotumika si Majanga hayo kaka. Option kama ni kununua ya kichina ni kuchukua brand new yaani zero kilometre. Sishauri kuchukua refurbished ya kichina ni Bora kuchukua mtumba scania.
 
Ahsante. Sasa kununua gari ya kichina iliyotumika si Majanga hayo kaka. Option kama ni kununua ya kichina ni kuchukua brand new yaani zero kilometre. Sishauri kuchukua refurbished ya kichina ni Bora kuchukua mtumba scania.
Mpya ya kichina bei gani?
 
Ahsante. Sasa kununua gari ya kichina iliyotumika si Majanga hayo kaka. Option kama ni kununua ya kichina ni kuchukua brand new yaani zero kilometre. Sishauri kuchukua refurbished ya kichina ni Bora kuchukua mtumba scania.
Thanks man , hiyo bei na ushuru mkuu ndio kitendawili brother.
 
Thanks man , hiyo bei na ushuru mkuu ndio kitendawili brother.
Kaka tofauti ya Mchina Refurbished na Scania Mtumba si kubwa sana kwenye Nia ya dhati ya kuwekeza kwenye reliable trucks.
 
Back
Top Bottom