DAVID PALMER
JF-Expert Member
- Jan 19, 2020
- 318
- 1,597
Achana na hiyo biashara!
Kama utaziweza hizi changamoto try!
1-Ale dereva!
2-Ale msaidizi!
3-Ile gari!
4-Ile serekali!
5-Ale dalali!
6-Ale Trafic
Kitakacho fika kwako sound!....
Wekeza kwenye kilimo cha Kitaalamu!
Ahsante Mkuu kwa maneno ya kutia Moyo.Kila mtu mwenye semi angekua na mawazo kama yako hakuna semi ambayo ingekua inatembea barabarani ssahv. Watu wengi tu wanaanza na semi moja au mbili baada ya miaka kadhaa unakuta kafikisha adi 7 huko au zaidi. Mtoa mada naomba usikatishwe tamaa na mawazo finyu ya huyu jamaa.
Mkuu kabla hujajiingiza kwenye kilimo Lazima upate Ushauri wa Kitaalamu kuanzia Ardhi, Mazao,/Mifugo na Soko...!Kilimo gani?? Au matikiti??
"Kila unachokiona mbele yako kilishawahi kuwa kwenye truck"Wakuu nawasalimu kwa Jina la JMT.
Kama kichwa cha Habari kinavyojieleza. Nimekuja humu ndani kupata ushauri wa Biashara ya Malori haya ya kubeba mizigo iwe ya Local ama Transit.
Kutokana na Connection nilizonazo nadhani suala zima la kupata Mizigo ya Kusafirisha halitokuwa la kuumiza kichwa.
Changamoto inayonikabili ni funding pamoja na aina ya truck ambayo inapaswa ni nunue.
Kabla ya kuja humu ndani nilishaomba ushauri kwa watu kadhaa ambao wapo kwenye hii industry na wamenijuza truck nzuri ya kununua ni Mtumba SCANIA 124 420 iliyotumika Europe. Hawakunishauri kabisa kununua Truck Mpya ama Refurbished za Mchina, DAF na Volvo wakaniambia zitanitesa maana ndio kwanza naingia kwenye game. Hata nilipouliza SCANIA zilizotumika south Africa wakaniambia ni bora nichukue za europe zinakuwa bado zipo Bora na hazijatembea sana kwenye rough road kwa hizo za SOUTH japo hizo za south walikiri kwa gharama ya manunuzi zipo chini kiasi.
FUNDING
Kama nilivyoeleza awali mimi ni new comer kwenye hii industry hivyo nategemea kujichanga kama 50-60Mil then the rest nichukue mkopo maana nakopesheka vizuri sana. Baada ya kufanya window shopping nimegundua horse scania mtumba inaweza kunicost kati ya 75Mil - 85Mil hapa nitapata gari nzuri tu, Trailer nimeshauri kununua ya Mkononi ambayo imetumika hapa nchini ambapo zina range 25Mil - 30Mil kutokana na hali yake. Nimejaribu kuulizia. Mpya lakini naona bei imechangamka sana USD 28,500.00 flatbed Double tire
TECHNICAL
Nimeshauriwa hapo kwenye trailer kununua super single kwa maana inabeba Mzigo Mkubwa kulinganisha na trailer yenye double tire.
Kwenye Horse kama nilivyoeleza awali nimeshauriwa SCANIA 6x2 124L 420 Mtumba kutoka EUROPE
BUDGET
Ukiangalia makisio ya gharama zote Horse na Trailer budget yake inacheka kati ya 100Mil - 115Mil. 60% Nategemea kuitoa Mfukoni na 40% nichukue Mkopo. Nategemea kulipa Mkopo kwa kutumia Mshahara wangu pamoja na Mapato yatakayokuwa yanapatikana baada ya Truck kuanza kuoperate. Nimekuja kuomba ushauri kwa yeyote mwenye kuielewa biashara hii kwa undani, nimeweka mchanganuo wote hapa ili niweze kupata ushauri mzuri kulingana na information nilizopokea pamoja na uwezo wangu wa kifedha. Nategemea kuna wajuzi wengi humu na nitambulia ushauri mzuri katika kukamilisha hili. Ahsanteni na niwakaribishe kwa Ushauri. Kejeli na dharau hapa si mahala pake.
Ahsante kwa muongozo lakini huko nimepita na ninaendelea kupita. Kama nilivyoeleza awali nipo na connection fulani inayoniwezesha kuongea na madereva na wamiliki ama wasimamizi wa magari. hivyo hilo pia la kuongea na madereva nalifanya sana katika research yangu.Mkuu hongera, nimeandika kiasi kuhusiana na haya maduala ila nikupe assignment maana najua huo utafiti ama uchunguzi wako umeufanya kwa mmmilikimsimamizi wa magari, hakikisha unawapata hata madereva wako watatu nao uwafanyie usaili wa uhalisia wa sekta halafu tukae sasa hapa tukushauri. Utanishukuru baadae
"Kila unachokiona mbele yako kilishawahi kuwa kwenye truck"
Umeamua vyema kuwaza biashara hii.
Niongeze kidogo
Kuliko kununua gari used budget yako inatosha kuwapa TATA wakakupa gari mpya kwa 35m na trailer ukiunga unga utapata kwa 30m double tyres.
Super single ina changamoto nyingi sana kuliko unavyoweza kudhan!
Transcargo, Dangote hawana trailer za super single.
Ukiamua kuchukua gari used jitahidi kuipitia kila sehemu ikiingia barabaran usipate changamoto. Maghari yanayotoka Poland usichukue mengi yametumika sana.
Gari kutoka South Africa ukipata muungwana akakurekebishia kabla ya kulisafirisha ni gari bora kuliko mtumba wa Uingereza.
Ukiamua kuchukua Uingereza hakikisha MOT iko active hii gar imejaribiwa kwao na inafanya kazi katika barabara za Uk.
Scani 124 420, kuwa makina kuanzia 2002 hadi 2004 nying ni HPI ama red dot zinasumbua sana katika mazingira yetu.
6x2 chagua tag axle yaan teriaz nyuma ili uweze kubeba mzigo mkubwa.
Biashara ni nzuri ngumu, jitahidi ujibanze kwenye kampuni yenye kazi za uhakika. Kazi za dalali zitakufanya uchukie kazi.
Usimamizi jitahid mda mwigini uone gari nanufanye service.
Hayo machache kwa nilivyojionea barabaran.
Ahsante sana Kamanda. Umenipa wazo zuri. Nikweli kabisa naweza kuanza kwa kuwa na horse yangu na nikatumia trailer ya kukodi. Nalifanyia kazi Kamanda. AhsanteChukua hio gari mkuu tela usichukue supersingle pia waweza kukodi kwa kuanza usiingie mazima Sana jaribu kuminimize initial costs..chonde chonde KUA KARIBU NA GARI NA UIFUATILIE HASWA NASEMA HASWA MPAKA DEREVA WAKUONE MNOKO FLANI Kama Hilo huwez achana na hio biznes maana hapo ndio uchawi wake ulipo,,, welcome to the industry
124 , 420 mwaka 1999 hadi 2001 cummis engine , utafurahi, unaweza jaribu na V8 164 ama R500 kwa kazi za kiume zina fanya vyema sana.Mkuu ahsante sana kwa ushauri. Naomba niongezee hapo kwenye 124 420 nichukue ya mwaka gani hasa.. Naomba nishauri range ya miaka ambayo imeonekana ni bora zaidi. Pia hiyo ya TATA Naifanyia kazi Mkuu.
Mkuu biashara nyingine iniingizie faida ya laki tano kwa siku yaani 15mil kwa mwezi? hahahaa Acha utaniKabla hajaingia huko hakikisha una njia zingine zinazo kuingizia mapato japo kima cha chini uingize laki5 kwa siku tofauti na hapo endelea kujiwekeza,sikukatishi tamaa ila naielewa vizuri hiyi biashara mwaka wa tano sasa ukiweza hilo karibu ni bonge la biashara
Ahsante Mkuu, ila Wadau waliniambia niachane na R Series zitanisumbua ni Mayai sana special for European Roads.124 , 420 mwaka 1999 hadi 2001 cummis engine , utafurahi, unaweza jaribu na V8 164 ama R500 kwa kazi za kiume zina fanya vyema sana.
164 haina umeme mwingi, shida kubwa huwez para right hand , nyingi zinatoka ylaya ya kati wanatumia left hand.Ahsante Mkuu, ila Wadau waliniambia niachane na R Series zitanisumbua ni Mayai sana special for European Roads.
Point taken for consideration, Vp hizi 114 kuna kadhaa nimekutana nazo za 1999-2001. Ama unaweza kunipa series zote za scania zenye kufanya vizuri katika barabara zetu164 haina umeme mwingi, shida kubwa huwez para right hand , nyingi zinatoka ylaya ya kati wanatumia left hand.
Kwamba haiwezekani au?Mkuu biashara nyingine iniingizie faida ya laki tano kwa siku yaani 15mil kwa mwezi? hahahaa Acha utani
So mkuu unataka kuanza biashara na semi1 umeweka add-ons maana naona unaelezea as if tayari una yard, mafundi ikizingua njiani, hela ya risk in case ikizingua kwa ajali kama unanunua na upo familia na hio biashara basi nunua semi1 halafu ji-attach na tajiri mmoja ili mwende sawa ukiongeza la2 unajiachia and fly soloMkuu nimedhamiria kuzikabiri changamoto ulizotaja. Ahsante kwa ushauri
Hakuna haja ya kujiattach kwa mtu. Mm Sio mgeni kwenye biashara mzee, nafahamu risk zilizopo. Niko na biashara nyingine na kazi pia. Nina uhakika wa kipato hvyo sitegemei kutetereka sana kama unavyodhania.So mkuu unataka kuanza biashara na semi1 umeweka add-ons maana naona unaelezea as if tayari una yard, mafundi ikizingua njiani, hela ya risk in case ikizingua kwa ajali kama unanunua na upo familia na hio biashara basi nunua semi1 halafu ji-attach na tajiri mmoja ili mwende sawa ukiongeza la2 unajiachia and fly solo