Naomba ushauri wa gari gani zuri la kutembelea lisilozidi Sh. milioni 10

Kiukweli kabisa mleta mada huwezi kupata gari nzuri yenye kukidhi vigezo vyako vyote vitatu (Economic, Family na Safari).

Jikite zaidi kwenye suala la kiuchumi (uwezo wa kuinunua gari na gharama za kila siku za kuliendesha) kulingana na ukubwa wa familia yako. Suala la kuitumia kusafiri nalo safari za mbali kwa sasa achana nalo kabisa, maana gharama yake ni kubwa sana na hatari kiasi fulani kama hujajipanga vizuri.

Kwa budget ya shilingi milioni 10-12, kipato cha maisha ya kawaida, mizunguko ya mjini, basi fikiri kumiliki gari ya Toyota IST. Ni gari imara, imetulia, inatumia mafuta kidogo na inadumu fresh. Hiyo ndio kama simu ya Nokia ya tochi kabla ya kipindi cha zama za smart phones kuingia. Hapo hutajuta na utafurahia maisha na familia yako. Chaguo la pili ni Raum.

Kwa leo niishie hapo.
 
nimenunua raum mwezi feb ,shida inayonisumbua ni kwamba kila nikiendesha kuna wakat nasikia gari inakwaruza chini.

hili tatizo natatuaje wazee maana spencer wanasema inabadili stability ya gari.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
nimenunua raum mwezi feb ,shida inayonisumbua ni kwamba kila nikiendesha kuna wakat nasikia gari inakwaruza chini.

hili tatizo natatuaje wazee maana spencer wanasema inabadili stability ya gari.

Sent using Jamii Forums mobile app
Weka Spencer usisikilize Maneno ya watu,

Raum bila Spencer huwezi kuenjoy,mie nishawahi kutumia Raum miaka mitatu na niliweka kuanzia Spencer mpaka naiuza ipo Stable

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ushauri wangu ni kati ya haya hapa chini unaweza kuchagua linalokufaa

1. Toyota ist (kuanzia 10.8mil )
2. Toyota sienta( 9.8ml chenchi inabaki )
3. Toyota vitz (kuanzia 8.9 mil chenchi inabaki)
4. Toyota funcargo( 9.8mil chenchi inabaki)
5. Toyota ractis (10mil )
6. Toyota ruminion( ila itabid uongeze pesa kidogo maana nyingi zinaanzia 13m)
7. Subaru impreza( bei kuanzia 13m )
8. Toyota raum ( 10.3m )
9. Toyota runx/allex ( bei kuanzia 13m )
10. Toyota spacio ( bei kuanzia 11.9mil )



Sent from my iPhone using JamiiForums
 
No 1&10 nazfanyia kazi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…