Naomba ushauri wa namna ya kutatua tatizo la kushindwa kujiamini

Naomba ushauri wa namna ya kutatua tatizo la kushindwa kujiamini

Habari wana JF, mimi ni kijana umri miaka 30. nina familia mtoto mmoja na nimeajiriwa kazi nzuri tu. Kwa haraka haraka naweza kusema maisha yangu ni mazuri kwa hilo nashukuru Mungu. Kilichonifanya kuandika uzi huu ni tatizo langu ambalo nimekua nalo muda mrefu naweza kusema toka nimezaliwa, tatizo la kushindwa kujiamini (wazungu wanasema social anxiety).

Labada nielezee historia yangu kwa kifupi inaweza kusaidia. Mimi nilizaliwa kwenye familia ya kawaida tu na nimelelewa tu vizuri. ilitokea nlikua namuogopa sana mzee wangu sijui kwanini. nilikua nashindwa kuongea nae freely na nikisikia amerudi kutoka kazini nilikua naingia hofu kwelikweli. Shuleni pia pamoja kua nilikua mwanafunzi bora, nilikua siwezi kusimama kuuliza maswali au kuchangia kitu chochote darasani kutokana na hofu. kipindi cha presentations nlikua natetemeka sana na kutoka jasho hali ambayo ilinifanya kuchekwa na kutaniwa na wenzangu.

Mpaka leo nimeajiriwa nina miaka sita kazini bado hali hii ipo. Naona aibu sana kuongea na watu wapya, siwezi kuangalia mtu machoni, ikitokea mabishano mimi hua ni mtu tu wakukubali hata kama naona si sawa, kwenye social events naogopa kuudhuria nahisi naweza itwa mbele labda kutoa speech kidogo.

Kazini nadhani walishaona mapungufu yangu haya. Mara nyingi wakihitaji mawazo kutoka kwangu hua hawaniulizi tukiwa wengi manake wanajua ntaogopa kuongea, badala yake hua wananiambia niwapatie riport iliyoandikwa nikishauri nini cha kufanyika.

Japokua naonekana kama mfanyakazi bora na anayejituma, nakiri kua hali hii imeniruidisha sana nyuma katika carrier growth. uwezo wangu mdogo wa kushawishi mambo kufanyika, kuongoza wenzangu na kujiamini umesababisha viongozi wangu kutonipatia majukumu makubwa zaidi japokua wanafahamu wazi kua nayaweza ila ndo ivo yanaitaji social skills ya hali ya juu.

Mimi ni mzuri sana nikipewa kalamu na karatasi, lakini likija swala la kuongea siwezi kabisa. kuna baadhi ya wenzangu ambao nilikua nao nafasi moja, walizitumia kazi zangu kwa sababu mimi sikuweza kuzipresent kwenye vikao vikubwa na ziliwawezesha wao kupandishwa vyeo na mishahara.

Hili kwakweli liliniumiza sana na sasa nimeona nitoke out of my comfort zone na kujaribu kukabiliana na tatizo hili. kwa utafiti niliofanya mtandaoni wanasema suala hili linatibika kwa dawa pamoja na ushauri na saha. Kwa hapa Tanzania kwa sijajua kama kuna taasisi ambazo zinahusika na masuala haya. Kama ipo tafadhali naomba lkufahamishwa. Kama kuna mtu ana ushauri wowote naupokea pia. Asante
Tafuta hela mkuu ukitembea na maburungutu mfukoni utajiamin sana
 
Habari wana JF, mimi ni kijana umri miaka 30. nina familia mtoto mmoja na nimeajiriwa kazi nzuri tu. Kwa haraka haraka naweza kusema maisha yangu ni mazuri kwa hilo nashukuru Mungu. Kilichonifanya kuandika uzi huu ni tatizo langu ambalo nimekua nalo muda mrefu naweza kusema toka nimezaliwa, tatizo la kushindwa kujiamini (wazungu wanasema social anxiety).

Labada nielezee historia yangu kwa kifupi inaweza kusaidia. Mimi nilizaliwa kwenye familia ya kawaida tu na nimelelewa tu vizuri. ilitokea nlikua namuogopa sana mzee wangu sijui kwanini. nilikua nashindwa kuongea nae freely na nikisikia amerudi kutoka kazini nilikua naingia hofu kwelikweli. Shuleni pia pamoja kua nilikua mwanafunzi bora, nilikua siwezi kusimama kuuliza maswali au kuchangia kitu chochote darasani kutokana na hofu. kipindi cha presentations nlikua natetemeka sana na kutoka jasho hali ambayo ilinifanya kuchekwa na kutaniwa na wenzangu.

Mpaka leo nimeajiriwa nina miaka sita kazini bado hali hii ipo. Naona aibu sana kuongea na watu wapya, siwezi kuangalia mtu machoni, ikitokea mabishano mimi hua ni mtu tu wakukubali hata kama naona si sawa, kwenye social events naogopa kuudhuria nahisi naweza itwa mbele labda kutoa speech kidogo.

Kazini nadhani walishaona mapungufu yangu haya. Mara nyingi wakihitaji mawazo kutoka kwangu hua hawaniulizi tukiwa wengi manake wanajua ntaogopa kuongea, badala yake hua wananiambia niwapatie riport iliyoandikwa nikishauri nini cha kufanyika.

Japokua naonekana kama mfanyakazi bora na anayejituma, nakiri kua hali hii imeniruidisha sana nyuma katika carrier growth. uwezo wangu mdogo wa kushawishi mambo kufanyika, kuongoza wenzangu na kujiamini umesababisha viongozi wangu kutonipatia majukumu makubwa zaidi japokua wanafahamu wazi kua nayaweza ila ndo ivo yanaitaji social skills ya hali ya juu.

Mimi ni mzuri sana nikipewa kalamu na karatasi, lakini likija swala la kuongea siwezi kabisa. kuna baadhi ya wenzangu ambao nilikua nao nafasi moja, walizitumia kazi zangu kwa sababu mimi sikuweza kuzipresent kwenye vikao vikubwa na ziliwawezesha wao kupandishwa vyeo na mishahara.

Hili kwakweli liliniumiza sana na sasa nimeona nitoke out of my comfort zone na kujaribu kukabiliana na tatizo hili. kwa utafiti niliofanya mtandaoni wanasema suala hili linatibika kwa dawa pamoja na ushauri na saha. Kwa hapa Tanzania kwa sijajua kama kuna taasisi ambazo zinahusika na masuala haya. Kama ipo tafadhali naomba lkufahamishwa. Kama kuna mtu ana ushauri wowote naupokea pia. Asante
Yaani kama vile umetoa historia yangu kabisa.
Hata mimi nilikua hivyo. Nakumbuka niliwahi kusanabisha darasa nzima likachapwa viboko kwa kutoweza kujibu swali moja. Swali ambalo nilikua najua jibu lake lakini kwa vile nilikua siwezi kuongea mbele za watu sikujibu.
Mimi pia ni mzuri wa kuandika, ninaweza kuandika mada hadi watu wakiisoma hawaamini imetoka kwangu, aibu ukimia na upweke ndio shida yangu.
Yaani hukuacha kitu vyote ulivyosema labda ninaweza kukuzidi maana pia nilikua napenda kukaa peke yangu zaidi na si rahisi kuzoeana na watu.

Ila sasa hivi nimebadilika sana.
1. Naweza kuanzisha story na kuisimamia kijiweni
2. Naweza kuongoza watu na nimekua kuongozi
3. Siogopi tena kuhojiwa kwwnye T.V au public ila inabidi nijikamue kisawasawa
4 Aibu haijaisha lakini imepungua sana
5 Nimekuwa mhubiri wa injili kanisani jambo ambalo sikutarania
6 Eti kuna wakati hata mimi ninakuwa mchekeshaji na watu wakacheka.
7. Jambo ambalo bado najitahid ni kuongea mbele za watu haswa nikishtukizwa, wakati mwungine tunakua kwenye semina za kikazi sasa kutoa point inakua mbinde japo nikijikakamua nawezaga.

Sasa nilifanyaje?
1. Nilimuomba Mungu
2. Niliikataa ile hali hapo najua nilirithi kwa mzazi
3 Elimu ilinisaidia maana nilikutana na watu wengi
4. Nilifanya practise sana. Wakari mwingine nilikua najifungua ndani naongea na kalamu makaratasi najihubiria kana kwamba niko na watu.
5 ambayo ni muhimu sana nilisoma vitabu, kuna vitabu vingi sana vinafundisha namna ya kuongea.
6 Nilijikubali na nilijua hatuwezi kufanana na wote.

Hakuna dawa, usijaribu kulewa wala kwwnda kwa waganga watakuharibia. Kama lazma upate tiba basi soma neno kama ww ni mkrsto kama sio mkrsro piga dua zako za kutosha
 
Habari wana JF, mimi ni kijana umri miaka 30. nina familia mtoto mmoja na nimeajiriwa kazi nzuri tu. Kwa haraka haraka naweza kusema maisha yangu ni mazuri kwa hilo nashukuru Mungu. Kilichonifanya kuandika uzi huu ni tatizo langu ambalo nimekua nalo muda mrefu naweza kusema toka nimezaliwa, tatizo la kushindwa kujiamini (wazungu wanasema social anxiety).

Labada nielezee historia yangu kwa kifupi inaweza kusaidia. Mimi nilizaliwa kwenye familia ya kawaida tu na nimelelewa tu vizuri. ilitokea nlikua namuogopa sana mzee wangu sijui kwanini. nilikua nashindwa kuongea nae freely na nikisikia amerudi kutoka kazini nilikua naingia hofu kwelikweli. Shuleni pia pamoja kua nilikua mwanafunzi bora, nilikua siwezi kusimama kuuliza maswali au kuchangia kitu chochote darasani kutokana na hofu. kipindi cha presentations nlikua natetemeka sana na kutoka jasho hali ambayo ilinifanya kuchekwa na kutaniwa na wenzangu.

Mpaka leo nimeajiriwa nina miaka sita kazini bado hali hii ipo. Naona aibu sana kuongea na watu wapya, siwezi kuangalia mtu machoni, ikitokea mabishano mimi hua ni mtu tu wakukubali hata kama naona si sawa, kwenye social events naogopa kuudhuria nahisi naweza itwa mbele labda kutoa speech kidogo.

Kazini nadhani walishaona mapungufu yangu haya. Mara nyingi wakihitaji mawazo kutoka kwangu hua hawaniulizi tukiwa wengi manake wanajua ntaogopa kuongea, badala yake hua wananiambia niwapatie riport iliyoandikwa nikishauri nini cha kufanyika.

Japokua naonekana kama mfanyakazi bora na anayejituma, nakiri kua hali hii imeniruidisha sana nyuma katika carrier growth. uwezo wangu mdogo wa kushawishi mambo kufanyika, kuongoza wenzangu na kujiamini umesababisha viongozi wangu kutonipatia majukumu makubwa zaidi japokua wanafahamu wazi kua nayaweza ila ndo ivo yanaitaji social skills ya hali ya juu.

Mimi ni mzuri sana nikipewa kalamu na karatasi, lakini likija swala la kuongea siwezi kabisa. kuna baadhi ya wenzangu ambao nilikua nao nafasi moja, walizitumia kazi zangu kwa sababu mimi sikuweza kuzipresent kwenye vikao vikubwa na ziliwawezesha wao kupandishwa vyeo na mishahara.

Hili kwakweli liliniumiza sana na sasa nimeona nitoke out of my comfort zone na kujaribu kukabiliana na tatizo hili. kwa utafiti niliofanya mtandaoni wanasema suala hili linatibika kwa dawa pamoja na ushauri na saha. Kwa hapa Tanzania kwa sijajua kama kuna taasisi ambazo zinahusika na masuala haya. Kama ipo tafadhali naomba lkufahamishwa. Kama kuna mtu ana ushauri wowote naupokea pia. Asante

Kwanza nikupe hongera Kwa kushare hii changamoto yako hapa na pole Sana Kwa matatizo ambayo umeyapata na kufanya ukose fursa nzuri kazini.

Kwanza nitashare ya kwangu ili tubadilishane uzoefu na baadae nitachangia nini kifanyike.

Mimi ni tofauti kidogo na wewe lkn changamoto ni zile zile, tatizo langu lilikuwa kushindwa kuandika mbele za watu,yaani mkono unatetemeka hatar,nakumbuka iIitokea ghafla Tu ndani ya chumba cha mtihani,mkono ikawa unatetemeka lkn baadae Hali ikaisha nikaendelea na mitihani,sasa Ile kumbu kumbu ya lile tukio ndo Lilazaa huo ugonjwa na kibaya Zaidi nikaenda Kwa daktar kutaka ushauri,daah nae anasema haelewi nini cha kufanya,naona hapo sasa ndo Ile Hali ikazidi,just imagine unaenda Kwa dokta Kwa kutaraji akupe nafuu nae anakuacha njia panda.

Haikuishia hapo likaja tatizo lingine,nikawa naogopa kwenda kunywa chai kantini chuoni,kwasababu ikawa nikishika kikombe mikono inatetemeka,nikajikuta nachukia kabisa kunywa chai,kwakweli hii Hali ilinikosesha furaha,hata Kula chakula mbele za watu ikawa mtihani,daah we Acha hii Hali isikie Kwa mwenzako,lakini nashukuru tatizo la kutetemeka wakati wa Kula au kunywa likaisha lenyewe Bila hata Mimi mwenyewe kugundua nikajikuta Tu nipo normal,ishu ikabakia kuandika mbele za watu,na hii tatizo nimekaa nao Kwa miaka kama Saba au nane,na mpaka Leo huwa mara chache chache Sana hujitokeza pale nikikumbuka Ile Hali ya zamani
 
Nilichokuja kujifunza baada ya kusoma vitabu mbalimbali vya namna ya kuondoa hofu,ni kuwa haya matatizo yanawakumba watu wengi Sana duniani,na inafikia mpaka wengine kushindwa kutoka nje kabisa,wengine inafikia mpaka wanawaogopa watu na kadhalika,na mara nyingi linaanza tatizo moja na yanakuja mengine.

Kwanini tunaendelea kuwa na haya matatizo? Ni hivi haya matatizo yanapata nguvu zaidi na kutuathiri mara pale tunapo yakimbia,Yana unavyoyakwepa ndo jinsi yanavyozidi kututawala katika Maisha yetu,na kibaya ukishakuwa na haya matatizo kitu cha Kwanza ni kutaka kujiepusha na mazingira yote ambayo yanakufanya usiwe na Amani,ndio maana wewe hapo unajikuta hutaki kuongea mbele za watu,unaogopa kujumuika mbele za watu na kadhalika,basi ujue Kwa kufanya hivyo ndo unayafanya yashike mizizi na kushinda nguvu.

Kwa mtu yoyote mwenye matatizo Aina hizi basi ajue jinsi anavyojiweka mbali na hofu inayomsumbua basi ajue hiyo hofu ndo inazidi marudufu,kile kitendo cha wewe kuiogopa Ile basi ubongo wako unatuma taarifa ambayo inafanywa kazi mara Ile Ile kuwa hii hofu ni hatari na mwisho unajikuta unashindwa na hofu Ile .

Kwa uelewa zaidi ni hvi,Kwa kawaida katika ubongo wetu kuna sehemu mbili,moja ni conscious mind na subconscious mind,hii conscious Mind inadili na matukio ambayo tunaweza kuyatawala ,Kwa unaweza kuamua kuwaja Jambo Fulani au kufanya Jambo Fulani au kuongea kitu Fulani,na baadae hizi taarifa hupelekwa ktk subconscious mind,ambayo hii kazi yake ni kupokea matokeo yote yalitokea ktk Maisha yako Kwa siku hiyo na kuyahifadhi na kuwa ktk faili la kumbukumbu,iwe maneno,mawazo au matendo yote huifadhiwa huko.
 
Na kibaya Zaidi hii subconscious mind haijui hili ni tatizo au hili si tatizo,taarifa zote zinakuwa ni Sawa Tu tayar Kwa kufanyiwa kazi.

Kwahiyo mfano wake ni kama Google vile,ukiandika habari za mpira zitakuja zote ktk screen yako,ukiandika kuhusu tennis zitakuja taarifa zote zinazo husu tennis,sasa ktk Maisha yetu ni hivyo hivyo,ukiliwaza Tu lile Jambo linalo kupa hofu basi taarifa na kumbukumbu zote za hofu zitakujia,utakumbuka jinsi mara ya mwisho ulivyoshindwa kuongea mbele za watu,utakumbuka jinsi wenzako walivyo kucheka na kadhalika,na hapo ndo utajikuta hofu imekujia tena na kuogopa kuzungumza tena mbele za watu na kukwepa kabisa kuzungumza.


Nami hivyo hivyo jinsi nilivyokumbuka mara ya mwisho kutetemeka mbele za watu,basi najikuta naanza kutetemeka tena,hapo ubongo wako unaona kama vile hii ni taarifa sahihi ya kufanyiwa kazi kumbe kwako ni majanga,kumbuka subconscious mind haijui zuri na Baya.

Nitaendelea.....
 
Sasa namna pekee ya kubadilisha records za sub mind ni wewe kurekodi matukio mapya,ima yawe ni matendo au maneno au mawazo,jinsi utakavyoulisha ubongo wako na mambo mapya basi yale ya zamani ambayo ni hasi yatapotea taratibu,muhimu ni kujua kuwa Hili si Jambo la siku moja,litachukua Mda mrefu pia,kama tatizo lilivyokaa Mda mrefu na kuondoka pia itachukua Mda.

Anza kuyaface Yale yote ambayo yanakupa hofu,Anza kuongea mbele za watu kidogo kidogo,mwanzo inaweza kuwa ngumu lakini usijali kumbuka unajifunza,Ile sauti inayokwambia '' we Acha kuongea mbele za watu utajitia aibu au Acha utashindwq" ipuuzie kabisa Yani usiisikilize,halafu kubwa kuliko yote usijali watu watachukulia vipi pale ukajitahidi kuongea na kusitasita yaani Achana nao kabisa usiwajali ,Anza kidogo kujiingiza katika maongezi na watu wageni,trust me brother hiyo Hali utaishinda kabisa na Maisha yako yatakuja kuwa ya Amani na furaha kabisa.

Jiambie maneno yatakayo kufanya ujiamini,wanaita positive affirmations,jiambie Kwa mfano " am okay" na hii jiambie pale Tu mawazo ya kutojiamini yakikujia,ukifanya hivi Kwa Mda mrefu yatakuwa sehemu ya Maisha yako na subconscious mind yako itayarekodi na kukupa kujiamini tena,huo ni mfano Tu,Mimi hutumia Hilo neno AM OKAY, unaweza tafuta neno lako ambalo utakuwa unalitumia mara Kwa mara,laweza kuwa la Kiswahili ni wewe Tu na uchaguzi wako,jiambie maneno mazuri yatakayoongeza kujiamini kwako.

BUT usijiambie kuwa Mimi sitaki kuogopa kuongea tena,au sitaki kuogopa kuangalia watu usoni ninapoongea,unajua kwanini ukijiambia hivyo ubongo wako utaleta tafsiri Ile Ile kuwa unaogopa kuongea na kuangalia watu usoni, nimepitia haya najua Sana,kwahiyo jipe maneno mengine kabisa kama vile,Nina Amani,Nina furaha,ninaweza na mambo kama hayo,Ila nakumbusha it takes time USIKATE TAMAA endelea kupambana.

Anza kuangalia watu unapozungumza nao kidogo kidogo japo Kwa sekunde kadhaa,kidogo kidogo utajenga confidence na baada ya Mda utakuwa Sawa,habar nzur ni kuwa hicho sio kilema kuwa hakitapona,utapona broo,we jiamini utafanikiwa na utashinda hayo mapungufu.

Kama utakuwa na maswali waeza uliza tukasaidiana kutatua changamoto zetu.

Nami nilipambana,nashukuru Kwa asilimia 99 nipo Sawa,naamini nitafikisha Mia hivi karibuni inshallah.
 
Habari wana JF, mimi ni kijana umri miaka 30. nina familia mtoto mmoja na nimeajiriwa kazi nzuri tu. Kwa haraka haraka naweza kusema maisha yangu ni mazuri kwa hilo nashukuru Mungu. Kilichonifanya kuandika uzi huu ni tatizo langu ambalo nimekua nalo muda mrefu naweza kusema toka nimezaliwa, tatizo la kushindwa kujiamini (wazungu wanasema social anxiety).

Labada nielezee historia yangu kwa kifupi inaweza kusaidia. Mimi nilizaliwa kwenye familia ya kawaida tu na nimelelewa tu vizuri. ilitokea nlikua namuogopa sana mzee wangu sijui kwanini. nilikua nashindwa kuongea nae freely na nikisikia amerudi kutoka kazini nilikua naingia hofu kwelikweli. Shuleni pia pamoja kua nilikua mwanafunzi bora, nilikua siwezi kusimama kuuliza maswali au kuchangia kitu chochote darasani kutokana na hofu. kipindi cha presentations nlikua natetemeka sana na kutoka jasho hali ambayo ilinifanya kuchekwa na kutaniwa na wenzangu.

Mpaka leo nimeajiriwa nina miaka sita kazini bado hali hii ipo. Naona aibu sana kuongea na watu wapya, siwezi kuangalia mtu machoni, ikitokea mabishano mimi hua ni mtu tu wakukubali hata kama naona si sawa, kwenye social events naogopa kuudhuria nahisi naweza itwa mbele labda kutoa speech kidogo.

Kazini nadhani walishaona mapungufu yangu haya. Mara nyingi wakihitaji mawazo kutoka kwangu hua hawaniulizi tukiwa wengi manake wanajua ntaogopa kuongea, badala yake hua wananiambia niwapatie riport iliyoandikwa nikishauri nini cha kufanyika.

Japokua naonekana kama mfanyakazi bora na anayejituma, nakiri kua hali hii imeniruidisha sana nyuma katika carrier growth. uwezo wangu mdogo wa kushawishi mambo kufanyika, kuongoza wenzangu na kujiamini umesababisha viongozi wangu kutonipatia majukumu makubwa zaidi japokua wanafahamu wazi kua nayaweza ila ndo ivo yanaitaji social skills ya hali ya juu.

Mimi ni mzuri sana nikipewa kalamu na karatasi, lakini likija swala la kuongea siwezi kabisa. kuna baadhi ya wenzangu ambao nilikua nao nafasi moja, walizitumia kazi zangu kwa sababu mimi sikuweza kuzipresent kwenye vikao vikubwa na ziliwawezesha wao kupandishwa vyeo na mishahara.

Hili kwakweli liliniumiza sana na sasa nimeona nitoke out of my comfort zone na kujaribu kukabiliana na tatizo hili. kwa utafiti niliofanya mtandaoni wanasema suala hili linatibika kwa dawa pamoja na ushauri na saha. Kwa hapa Tanzania kwa sijajua kama kuna taasisi ambazo zinahusika na masuala haya. Kama ipo tafadhali naomba lkufahamishwa. Kama kuna mtu ana ushauri wowote naupokea pia. Asante
Yaani hii story kama unanisema mimi kila kitu siwezi kuongea mbele za watu lakini ukinipa kalamu Mara nyingi ninachoandika huweziamini kuwa ni mimi nimeandika
 
Back
Top Bottom