Naomba ushauri wenu wana JF

Naomba ushauri wenu wana JF

Nashukuru sana wote kwa ushauri wenu, ila mimi wasiwasi wangu ni kuwa je ni kweli anamaanisha anachokisema?
Maana kwa jinsi ninavyomuelewa anaweza kusema hivyo lakini bado hajawa na maamuzi kamili. Na wasiwasi wangu umenidhihirishia baada ya sasa kuanza vituko,
Mfano jumamosi nilimuuliza kama ataenda na watoto kumuona babu yao anaeumwa akasema hajajua, baada ya mimi kuondoka kwenda kazini alikwenda nao na akawaacha walale huko bila kunitaarifu, na hapo yule mtoto wa kwetu wote naumwa na kuna dawa anatumia na ameziacha nyumbani, baada ya mimi kurudi nyumbani na kugundua kuwa mtoto hatarudi na dawa ameziacha nikampigia kumuuliza sasa tunafanyaje maana dose itaharibika, akasema subiri nakuja tena kwa hasira, na aliporudi alikuwa kimya wala hakulizungumzia na likuwa amelewa, asubuhi pia akawa kimya, sasa ni visa tu na juzi amempeleka mtoto kwa aunt yake bila mimi kujua pia mpaka leo hajarudi, yaani kama mtu mwenye bifu fulani hivi na maelewano hakuna, na jana amelala kwenye chumba cha watoto.

Hio ndioo hali halisi ndugu zangu haya naendelea kusikiliza ushauri wenu.

Mpendwa baraka , kama wadau walivyoshauri jana , mwende mkapime wote mjue status zenu mpokee majibu kwa pamoja.Kutoka hapo mnaweza kufanya maamuzi.Kama ameshaanza kukunyanyasa mapema hivyo sijui huko mbeleni itakuwaje .Naamini hamaanishi anachokisema muendelee kuishi.Baraka unahitaji upendo na faraja sio hayo anayoyafanya hata kama ni kweli yu negative. Pole sana mlilie Mungu atakusaidia.
 
Dnt take me worng but i nid to know wewe ulipata wapi hiyo ugonjwa? Nikijua hiyo naweza nikakushauri!
 
Mpendwa nimecheka kweli asubuhi ya leo eti sijui ataniconvisi vipi nikapime. Kama anavyosema dena jamani kupima kwataka moyo lol, na sio rahisi mume ajue we unao ye hana akubali kirahisi rahisi hivyo, hawa wenzetu akikufumania tu ni kasheshe haya asikie umeukwaa huko si balaa.

Dena kama ndio wapimaga watu nyie watu wa ushauri nasaha mnajua kututisha, Mi nikienda kupima nawaambiaga naomba msinipe ushauri nasaha nipimeni na nipeni tu majibu. pengine umekutwa positive lakini mshauri ataanza bwana ooh unajua ukimwi this, ukimwi that mpaka jasho linakuchuruzika akimaliza ndio anakwambia hongera uko positive kha! hapo moyo karibu uachane na mwili.

Ha ha ha ha Maty bana tutaongea kwenye PM maana naona hapa si mahala pake
 
Dnt take me worng but i nid to know wewe ulipata wapi hiyo ugonjwa? Nikijua hiyo naweza nikakushauri!

Hilo ndo nililosema mimi huyo mumeo huyo shika mkono nenda nae mkapime wote uone matokeo....................kiukweli mimi kwa uzoefu wangu simuamini kabisa
 
Ahasante (Pihu)
Mimi kama sijapata kwake basi nitakuwa nilipata kabla ya kuolewa
Huo ndio ukweli wangu ndugu yangu.

Hilo ndo nililosema mimi huyo mumeo huyo shika mkono nenda nae mkapime wote uone matokeo....................kiukweli mimi kwa uzoefu wangu simuamini kabisa
 
Mimi kwa mtazamo wangu naona huyo mwanaume bado anakupenda whether ameasirika na hataki kuwa wazi au hajaathirika, kwani mfano akiwa ameathirika na umesema unatumia kinga kuna athari gani kwako? Endelea kukaa naye huna haja ya kumuacha maadam anajua hali yako na amekiri mwenyewe kwamba yupo tayari kuendele kuishi na wewe. Ni vizuri ukajua hali yake inagwa si muhimu sana kwa kuwa wewe umeshajua yako na yeye analijua hilo. Unachopaswa kufanya ni kumuomba Mungu tu ili muwe na amani na anaweza kuwaponya pia kwani hakuna lisilowezekana kwake
 
mmh..inawezekana hii?? kwa ufahamu wangu naona kama mwanaume akiathirika mwanamke pia anakuwa kwenye hatari kubwa ya kuathirika..
Ila kwa tukio la huyu dada yetu mpendwa ni kwamba yeye ameathirika lakini mumewe hajaathirika,.. ndo nilikuwa nataka kujua kumetokea nini??
Any way, vyanzo viko vingi, na cha msingi ni kusahau yaliyotokea na kuendelea na maisha..

Hiyo inawezekana kabisa kuwa mmoja wa wanandoa ameathirika na mwengine hana virus, wenyewe huita 'DISCORDANT' partner.

Dada Mhusika, Pole sana!, lakini kama ulivyo pewa ushauri na wapimaji(Counselling), huu sio mwisho wa maisha, watu wengi wameathirika lakini ukiwaona wako sawa tu. Cha kufanya ni kuwa na Positive attitude, na pia unahitaji kwenda na mumeo kwenye CLINIKI, ili mupewe ushauri wa pamoja, kwani ni hatari kuishi hivyo, kwa mumeo na wewe pia bila ya ushauri mzuri.
 
Ahasante (Pihu)
Mimi kama sijapata kwake basi nitakuwa nilipata kabla ya kuolewa
Huo ndio ukweli wangu ndugu yangu.

tunashukuru kwa taarifa hii, maana maswali yalikuwa mengi..Mungu ni mwaminifu. Hawezi kumtupa mja wake. Ningeshauri utafute watu ambao mnawaheshimu wakusaidie ukae na mume wako chini muone mtaishi kwa namna gani.. Huwezi kuugua moyo kila siku juu ya mume wako ambaye haeleweki sasa.. Na kwa vile mko nyumba moja ataendelea kukusumbua akili. Ni vyema ukafanya hima ili utulie, usije ukaruhusu stress ambazo zi za lazima
 
Huyo mumeo ni muongo sana tena wa kutupwa..........................iko siku utakuja kusema hapa.................wanaume walivyo wakali eti akubali hali uliyonayo ha ha ha ha ha wewe unacheza na kusikia kwenye redio akubali eti yeye mzima sio kweli nikwambie..........................

Nakubaliana na wewe. Huyu mwanaume ni muhongo. As long as alienda kupima peke yake jua na yeye ni muhathirika ila si muwazi kama wewe. Na watu kama wao (nisamehe lakini) ukute ndo wanaleta magonjwa ndani. Na hapo amekudanganya ni mzima na utakuta na nje anaendelea kuambukiza wadada wasiojali kutembea na wame za watu.
 
Dada pole sana. Nakuelewa kwani ili si janga la mmoja. Kama si wewe basi ndugu yako yamemkuta. Kwa tabia ya wanaume dada nakwambia wewe wala hukuolewa na huo ugonjwa. Jamaa amekuletea na ndio maana amekuwa mpole na kujifanya understanding. Anyway inabidi umfanyie counselling ili mtulie kwani akiendelea natabia yake ya kutoka nje basi atapunguza muda wa kuishi kwani ukifuata masharti waweza kuishi muda mrefu kuliko mtu ambaye si positive. Kwa kuwa kwako muwazi Mungu anakuongezea muda wa kuishi kwani umejikubali.


Ahasante (Pihu)
Mimi kama sijapata kwake basi nitakuwa nilipata kabla ya kuolewa
Huo ndio ukweli wangu ndugu yangu.
 
Umesema upo kwenye ndoa kwa miaka 13, ila kwa miaka 3 ya hivi karibuni hali yako imezidi kuzorota..
Nilitaka kufahamu ni nani aliyekuambikiza?..Maana kama mume amesema kapima na hajaonekana nao, ninapata wasiwasi na uaminifu kwenye ndoa.

Swali la muhimu sana linaloweza kutoa majibu.
Nendeni pamoja mkapime uthibitishe ukweli. Kwa hali ya sasa kama hajaathirika nadhani angeshakufukuza.
Kama ameathirika ikathibitika endeleeni na maisha kulingana na hali ilivyo.
Kwa vile uligundua hali hiyo na kukaa kimya nadhani maambukizo ni mahusiano nje ya ndoa,na endapo hajaathirika unapaswa kujiuliza je kuendelea kuishi naye katika 'risk' ya nanma hiyo ni kumtendea haki? ukizingatia kuwa tayari kuna dalili za usaliti.
 
Hilo ndo nililosema mimi huyo mumeo huyo shika mkono nenda nae mkapime wote uone matokeo....................kiukweli mimi kwa uzoefu wangu simuamini kabisa

Mhhh! DA wapo wenye mioyo kama ya huyu bwana (kama ni kweli yuko negative) ingawaje ni wachache sana, ila kwa waume/wake wengi uamuzi kama huu ni mgumu sana unapogundua mwenzio ameathirika na wewe mambo yako bado yako safi. Pamoja na kujua kwamba hupati maambukizo kwa kushare nyumba, kitanda, vyombo n.k. lakini mhhhhh! inahitaji moyo sana.

 
Huyo mumeo ni muongo sana tena wa kutupwa..........................iko siku utakuja kusema hapa.................wanaume walivyo wakali eti akubali hali uliyonayo ha ha ha ha ha wewe unacheza na kusikia kwenye redio akubali eti yeye mzima sio kweli nikwambie..........................
Too general DA, wa2 wa namna hiyo wapo na huko CTC anako chukua dawa huyo dada huduma ya ushauri wa namna ya kuishi wenza wenye HIV status walonazo ipo, hivo wai2mie, kizuri zaidi ni kuwa hata mwenzie kaacha kujinyanyapaa amini wakizingatia wataish maisha ya amani!.KUNA IMPROVEMENT KUBWA MNO KTK HIV MANAGEMENT TOFAUTI NA HAPO AWALI SEMA TU JAMII NDO HAIJAELIMIKA VYA KUTOSHA NDO MAANA INAKUWA NGUMU KU2MIA HIZO HUDUMA ZILIZO TAYARI. Kwakifupi waende wote ctc kuna msaada mkubwa tu.
 
Dnt take me worng but i nid to know wewe ulipata wapi hiyo ugonjwa? Nikijua hiyo naweza nikakushauri!
Historia hiyo Haitasaidia chochote hapo,.....wote wawili waende kwa mnasihi mwenye taaluma ambao wengi hupatikana ctc na huduma hiyo haina malipo
 
Hi,

Mshike mkono mumeo makpime wote; i am sure na yeye pia anao...not possible kwamba asiwe nao keeping in mind that u might have got it from him or from the beginning you had this.......

Ushauri wangu: Nenda mguu kwa mguu nae akapime yeye; and then if he has or has not STAY WITH HIM....Kumbuka u had sworn to be together for HAPPINESS AND SORROW..........
 
Habari wana jamii wote,ni mara yangu ya kwanza kuingia huku kwenye forum hii
Naomba sana mnipe ushauri wenu kwa haya nitakayoyaeleza hapa

Mimi nimeolewa nina miaka 13 katika ndoa, nina mtoto mmoja wa kiume mwenye miaka 12, mume wangu ana mtoto wa kike mwenye miaka 10 aliezaa na mwanamke mwingine.

tatizo langu ni kuwa miaka mitatu iliyopita niligundua kuwa nimeathirika na sasa natumia dawa za kupunguza makali(ARV)
Nilishindwa kumweleza mume wangu kuhusu hali yangu kwa kuwa kila nilipomshauri kuhusu kupima afya alikuwa hataki akidai kuwa siku akigundua kuwa ameathirika atakufa. Ila mimi nilipogundua kuwa nimeathirika nikawa sikubali kufanya mapenzi bila kutumia kinga, ingawa wakati mwingine alikuwa analazimisha lakini sikuwa tayari.

Hivi karibuni akanieleza kuwa amegundua kuhusu hali yangu baada ya kuona kadi yangu ya clinic, na yeye ameenda kupima na amesema yeye hajaathirika, hivyo kasema tuendelee kuishi bila watu kujua.

Mimi nikampa option kuwa kwa kuwa yeye ni mzima basi nisimbane kama atahitaji awe na mwenza mwingine basi tunaweza kuachana na yeye akaanza maisha mapya, lakini kasema kuwa haiwezekani tuachane kwa kuwa tumeishi muda mrefu na tumesaidiana mengi.

sasa naomba ushauri wenu je hili linawezekana? Au mna ushauri gani?

Ahasanteni
Dada, kwanza mm nakukaribisha sn ktk mtandao wetu wa sema usikike ktk jamii yetu, ila usivunje sheri, kwa mtu yeyote aliyeko humu kwenye mtandao au nje ya mtandao kwa kudhalilisha kwa namn yoyote ile, ili uwanja na carpet let au jamvi letu liweze kuwahabarish maelfu ya watu,
kuhusu jambo hili, dada nakupa pole kidogo tu, kwa hili lililotokea kwani hata mm limenikuta japo sijawahi kusema kuwa limenikuta llkn kwa ujasiri wako namm napenda kuwa wazi kwa hili, mm nilisafiri nje ya nchi nikiwa huku, nikasikia mke wangu anaumwa sn, tulikuwa tumeachana kama miezi mitano hivi alipopima akagundua kaathirika, lkn hakusema, niliporudi hakuwa wazi lkn alijikinga ili nisiambukizwe, lkn namshukuru sn Mungu nilipopimwa nikwa mzima, lkn mbele ya nesi mke wangu akawa analia, nikamwambia usihofu mke wangu, nitakuwa na ww kwa kila hali wala sifikirii kukuacha naposema mpaka ss niponae tunaishi maisha mazuri tu, watoto wetu wapo sekondari wengine wako primary school, napendakusema kuwa si lazima unisikilize mm au dada anaesema wanaume waongo sn atakubwaga sikumoja, c kweli sn mbona mm sijambwaga mke wangu tunakula tunda kivingine ci lazima liwe kama mwanzo,
jipe moyo mkuu sn, usiwaze wala kumfikiria sn mumeo kuwa ss anakula tunda kwa kumenya maganda wakati kwako ala kwa maganda, jitulize sn, ondoa gubu kabisa mbembeleze sn umlee zaidi ya mwanzo ili akupende zaidi ya mwanzo, usisikie la mtu maadam akubali kuwa atakuwa na ww kama mm nilipokubali mpende sn, leo toka alipoumwa mke wangu ni mwaka wanne, tupo woe na watoto wetu hawajui km mama aanumwa hiv.
Ubarikiwe sn.
 
pole mwaya..mwenyezi Mungu akupe subira:hat:
 
Mhhh! DA wapo wenye mioyo kama ya huyu bwana (kama ni kweli yuko negative) ingawaje ni wachache sana, ila kwa waume/wake wengi uamuzi kama huu ni mgumu sana unapogundua mwenzio ameathirika na wewe mambo yako bado yako safi. Pamoja na kujua kwamba hupati maambukizo kwa kushare nyumba, kitanda, vyombo n.k. lakini mhhhhh! inahitaji moyo sana.


Wapo watu wa hivyo lakini kukubali kiulaini hivyo hata kudiskasi kusiwepo?? BAK mmmhhhh

Wapo wanaishi hivyo wengie lakini lazima mlizungumze mpewe ushauri jinsi ya kuishi na kukubaliana mtakavyoishi.

Swala langu ni kukubali kiulaini hapo ndo pamenishangaza mie hakuna kingine ndoa za negative na positive zipo nyingi tu
 
Back
Top Bottom