Naomba watanzania tumsaidie Ray C tumchangie

Naomba watanzania tumsaidie Ray C tumchangie

haina haja ya kumchangia mtu kama huyu...wacha avune alichopanda...........
 
Kuna kitu kimoja wasanii wa Kitanzania haswa wale ambao ni maarufu na waliofanikiwa katika kazi zao za sanaa huwa hawakifanyi, nacho ni KUTOA kwa jamii (CHARITY). Huwaza sana maisha yao binafsi pale wanapopata breakthrough na kusahau kuwa pasipo VIINGILIO vya Watanzania, wao wasingekua hapo walipo kifedha.

Sasa kwa dhana hiyo leo hii mimi ukiniambia nimchangie RAY C sikuelewi, huyu mtu nimchangie mara ngapi?? Kama ni viingilio vya show zake nilitoa sana, Tapes, CD, DVD zake ninazo kila album(kumbuka hapa huwa tunanunua pia)...
Mwisho wa siku hivi ndivyo anavyowalipa wapenzi, mashabiki na maswaiba wake...

...........................................Hii haikubaliki, hii haiwezekani..............................
 
agent wake mama yake mzazi tigo pesa 0655 999 700 kwa mujibu wa Michuzi Blog
 
Nilimsikia mama yake akitaja no za cmu clouds fm bt ckuwezazinote,sielewi kwann wasanii hawafanyi fundraising kumchangia pesa za matibabu,huu ubaguzi unachangia kurudisha maendeleo nyuma hapa tz! Imagine mtu anatoa 10 mil kama rambirambi kwa sm1 ambaye ni marehemu ila aliye hai hachangiwi, ama kwasababu ray c hawezi wapa political fame and capital? so sad

Wengine tupo mbali na redio, mtusaidie mliosikia, kwani ray C anashida gani? Na hizo hela achangiwe za shughuli gani? Nae anahitajika kupelekwa india for matibabu au inakuaje?
 
sometimes nawaza kumchangia lakini moyo unasita kutokana na sababu zifuatazo.
1. Unga kala mwenyewe baada ya kuwa limbukeni wa ela anazopata. Kawa hashauriki na mtu kama kawaida ya watanzania akishapata kila anayemshauri asipotee basi machoni pake uwa ni mwenye wivu au snitch.
2. Kuna watanzania wana matatizo makubwa tena ambayo siyo ya kujitaftia lakini sijaona watu mkijitolea kuwasaidia. Nenda muhimbili kuna watanzania wana magonjwa ya ajabu wanahitaji pesa japo mil 1 wameshindwa kupata matibabu wanateseka lakini hawajasaidiwa na mtu. Nenda mtaani kuna watoto yatima, kuna wajane waliodhurumiwa wanahitaji japo msaada wa kisheria lakini hawajasaidiwa hapo mimi ndipo nashindwa kumsaidia ray c.
3. Akisaidiwa ray c kesho atakuja lord eyes naye teja jamani tumsaidie, atafuata TID ambaye ni wazi naye ni mla unga lakini leo hii ukimsema utaishia kuporomoshewa matusi yasiyo andikika na utaitwa snitch. Hapo huja mtaja Ngwair na wengine wengi ambao bila shaka leo hii wanaona effects na matatizo wanayo pata wenzao lakini wao wamekaa kwa kujiona wajanja.
Si muda mrefu TID atafuata maana ukikaa naye mazungumzo yake ni illusions anaongea vitu kama mtoto mdogo.

Mwisho watakao mchangia mchangieni na Mungu atawalipa kwa wema wenu ila mimi ni afadhali ela yangu nkanunue kiroba cha unga nipeleke kwa watoto yatima kuliko kumchangia mtu ambaye leo hii anaomba mchango kisa alitumia ela nyingi kununua hayo matatizo.

........kweli mkuu u have a point
 
Hivi yeye ana umuhimu sana kuliko wale wengine wanaotumia?

kwanini tusihamasishe vijana wasitumie madawa ili haya yasijetokea?
Tutachangia wangapi maana watumiaji ni wengi sana au kisa msanii?

Mbona Langa aliacha mwenyewe hakuhitaji mchango wetu?

Mi naona wamuache ili iwe fundisho
 
Watu wengine bwana!! Ukiangalia profile zao wana miaka JF lakini post zao kama wamejiunga jana!!

Twambie Ray C amekuwaje, msaada wa nini, ilkuwaje, sio wote tuko Tz ama wanaelewa kila kitu!!
 
she deserves wat she already get kwani alikuwa hajui side effects zake.
 
Jamani, na Ray c nae tumchangie, kwa lipi? Matatizo ya kujitafutia mwenyewe uje uchangiwe, alitumwa na nani kutumia unga?

Lol! bora mnichangie mimi alfajiri ya leo kaka yangu kwa mama mkubwa amefariki dunia, R.I.P my bro Daud
 
Mimi personal nipo tayari kumchangia Ray c .Agent wake ni nani?.mtu anaeaminika afungue account tumchangia.She needs help .mimi personal nipo tayari

unataka kurusha stimu zake wakati stimu amezilipia?. mia
 
Namna ya kumsaidia Ray C ni kama mahakama itakubali akabidhiwe kesi ya Lulu, Akae jela weee akitoka ashakua mtu safi na Arosto yote imeisha
 
Jamani, na Ray c nae tumchangie, kwa lipi? Matatizo ya kujitafutia mwenyewe uje uchangiwe, alitumwa na nani kutumia unga?

Lol! bora mnichangie mimi alfajiri ya leo kaka yangu kwa mama mkubwa amefariki dunia, R.I.P my bro Daud

Pole kwa msiba!
 
jamani ,mimi naona asaidiwe but Natalia muke ya muzungu tajiri hilo jukumu si dogo tu kwako
izo dolari elfu kumi za breakfast kwa wiki zinatosha kabisa matibabu
 
Last edited by a moderator:
Mimi personal nipo tayari kumchangia Ray c .Agent wake ni nani?.mtu anaeaminika afungue account tumchangia.She needs help .mimi personal nipo tayari

Agent wa yaliyomsababishia madhara au agent wa nini?

Aende alikokuwa anasali waumini wenzake wamsaidie
 
Mimi personal nipo tayari kumchangia Ray c .Agent wake ni nani?.mtu anaeaminika afungue account tumchangia.She needs help .mimi personal nipo tayari
Hahitaji msaada huyu,hayo madawa si anayapata kwa kununua?hiyo pesa si anayo huyu!.katorokea Kenya ili apate muda mzuri wa kuburudika mwache aburudike tu,kama ni kifo anakikaribisha mwenyewe,hata hivyo uamuzi wa kuacha uko mikononi mwake mwenyewe akimrudia mungu wake na kujutia makosa yake ni dawa tosha tena haihitaji michango ya wasamaria wema.
 
JF kuna watu wana roho.mbaya astaghafiruAllah ....

Hatuna roho mbaya, tunasema ukweli. Kuna mitoto mijinga inaishi kwa illusions na hii ndio hatma. Kama kuchanga kuna watu wangapi wanatangazwa ITV kwa shida mbali mbali tusiwachangie tuje kumchangia mtu aliyekula miunga kwa starehe na kiburi cha vijihela vya kuonesha maungo yake.

Nawaacha wafu muwazike wafu wenu, mimi nijaliwapo nitamchangia mwenye mahitaji na sio mwenye kujitakia. Huyu aliyeanzisha hii topic sina shaka na yeye ni wa trend hiyo hiyo. Endeleeni kuweka mapaja nje mkijiona mmefika bila kujua hatma ya maisha yenu mnayojiwekea.

Kama michango, kachukueni kwa wanaowauzia hiyo midawa, au mnajifanya hamuwajui?
 
Back
Top Bottom