Naombeni msaada wenu

Naombeni msaada wenu

Pole sana mkuu.. Jitahidi ukatembelee makaburi japo uone walipopumzishwa wapendwa wetu
 
sawa nitafanya hivo
Usiwaze sana kuhusu ndugu zako afu usijipe sana umuhimu kwao wakati hawaona umuhimu wako, focus na maisha yako jitahidi kufanya kazi kwa bidii pambania maisha yako acha kuwaza watu wasio kuwa na muda na wewe, Undugu kufaana sio kufanana. Ukienda kwenye kaburi la babu na bibi yako nenda kazike maumivu yako yote sijui mama au mdogo wako, ukirudi rudi na swala moja tuu kujiwazia wewe na mtoto usikubali kuishi tena na maumivu yakatae kwa jina la Yesu.
 
Usiwaze sana kuhusu ndugu zako afu usijipe sana umuhimu kwao wakati hawaona umuhimu wako, focus na maisha yako jitahidi kufanya kazi kwa bidii pambania maisha yako acha kuwaza watu wasio kuwa na muda na wewe, Undugu kufaana sio kufanana. Ukienda kwenye kaburi la babu na bibi yako nenda kazike maumivu yako yote sijui mama au mdogo wako, ukirudi rudi na swala moja tuu kujiwazia wewe na mtoto usikubali kuishi tena na maumivu yakatae kwa jina la Yesu.
nimekuelewa sana. asante
 
Tatizo naloona hapa dadaangu Dadakidoti ni upweke wa kukosa mtu wa kukujali, wa kukuskiliza sauti yako ya ndani, wa kukupa faraja mpaka uyasahau uliyopitia. Vilevile hisia mbaya za huzuni huzuni iliyokomaa ikawa sononeko, angepatikanam mtu huyo hakika pengo lililoachwa na bibi,babu pamoja na mama asiekupenda litazibwa.

Kiukweli pekeako itakuwa ngumu kuyashinda unahitaji msaidizi hapa duniani, habari njema ni kwamba msaidizi alieko mbinguni MUNGU anakujali mwamini hajakuacha atakukumbuka very soon na utapona.

-Inasikitisha sana kwa uliyopitia tokea upo mdogo POLE SANA dadaangu, utaimarika zaidi, majaribu humpata kila mwanadamu hauko pekeako, tuko nawe tunakuombea utashinda, utayaweza, utapona, kwa jina la BWANA na MWOKOZI WETU YESU KRISTO, AMEN!
 
Tatizo naloona hapa dadaangu Dadakidoti ni upweke wa kukosa mtu wa kukujali, wa kukuskiliza sauti yako ya ndani, wa kukupa faraja mpaka uyasahau uliyopitia. Vilevile hisia mbaya za huzuni huzuni iliyokomaa ikawa sononeko, angepatikanam mtu huyo hakika pengo lililoachwa na bibi,babu pamoja na mama asiekupenda litazibwa.

Kiukweli pekeako itakuwa ngumu kuyashinda unahitaji msaidizi hapa duniani, habari njema ni kwamba msaidizi alieko mbinguni MUNGU anakujali mwamini hajakuacha atakukumbuka very soon na utapona.

-Inasikitisha sana kwa uliyopitia tokea upo mdogo POLE SANA dadaangu, utaimarika zaidi, majaribu humpata kila mwanadamu hauko pekeako, tuko nawe tunakuombea utashinda, utayaweza, utapona, kwa jina la BWANA na MWOKOZI WETU YESU KRISTO, AMEN!
amen
 
Bila shaka wote mko poa kabisa.
Kidoti wenu nimerudi maji ya shingo nashindwa hata pa kuanzia. Kama familia yangu ya JF naombeni ushauri wenu wenda nikapata hata msaada.

Kama mnakumbuka nilileta uzi huu Kuna wengine hatujui tulipokosea
Sikuweza kuandika kila kitu. wengi mlisoma historia yangu na mnajua wapi nimepitia mpaka nilipo.
niwawachoshe moja kwa moja kwenye mada.

Katika maisha yangu watu ambao ndo walikuwa familia yangu ni babu na bibi zangu sababu wao ndio walikuwa wanasimama kama wazazi ninapopitia changamoto. Hasa hasa babu mzaa baba na bibi mzaa mama. kwa ufupi mwaka jana mwezi wa tatu mwishoni babu yangu alikufa. Kipindi msiba unatokea nilikuwa na wakati mgumu sana sababu sikuwa na kazi ya kueleweka na nilikuwa na mtoto mdogo. Hivyo sikuweza kwenda kanda ya ziwa msibani. wakati huo huo bibi yangu mzaa mama alikuwa Arusha kwa ajili ya matibabu alikuwa anaumwa baada ya kupata taarifa alinipigia simu kunipa pole na kunitia moyo sababu alijua jinsi nilivyokuwa nampenda babu yangu. akanisisitiza nimwangalie mtoto alijua nilivyokuwa nimeumia kutoweza kwenda kumzika babu yangu. alikuwa anasisitiza nisiangalie kitu kingine zaidi ya kumwangalia mtoto. nilitaka kuuza kibanda changu ili nipate nauli lakini bibi alikataa akaniahidi kuwa akirudi nyumbani atanitumia nauli nitaenda kuzuru kaburi.nikaona ni sawa nikamkubalia.

Ilikuwa ni ijumaa bibi alinipigia simu tliongea sana karibia masaa mawili. akinisisitiza akili yangu yote iwe kwa mtoto. Kesho yake ajabu napigiwa simu kuwa bibi yangu nae hayupo tena duniani ndani ya wiki mbili tu nilipoteza watu muhimu sana kwangu. walisafirisha mwili pia sikuweza hata kwenda kuzika. hakuna kipindi kigumu niliwahi kupitia kama kipindi hicho. sina kazi ya kueleweka nilikuwa nafanya kazi kwa mama ntilie nalipwa elfu tano angalau nipate kula na mtoto. Mama angu alikuja kumzika bibi lakini hakunipigia hata simu kujua angalau mimi na mtoto tunaendeleaje. kwa ufupi bibi ndo alikuwa kama mama yangu.

Mungu ni mwema nilifanikiwa kupata kazi ambayo naendelea nayo mpaka sasa namshukuru Mungu nipo vizuri japo si sana nina dhiki za kawaida kama za watu wengine. hatulali njaa na mtoto naweza kulipa ada kodi na kujikimu mahitaji yangu na mtoto. naweza kula nachokitamani. namshukuru sana Mungu kwa hilo.
ila kinachoniumiza toka itokee hiyo misiba sina amani nikiwakumbuka babu na bibi yangu naanza kulia. usiku silali nimekonda nimepungu kutoka 63kg mpaka 55kg.

usiku nikilala naweza kuota nipo kanda ya ziwa yaani naota makaburi naweza ota nimeenda kwa bibi lakini nyumba imejengwa makaburini. naweza kuota nipo mochwari yaani kwa ujumla sioti ndoto za kawaida. najikuta wakati mwingine natamani kufa labda naweza kupumzika lakini akili inaniambia ukifa huwezi kupumzika kwa amani kwa sababu mtoto wako hutakuwa umemuacha katika mazingira magumu sana. nimedhoofika sana kichwa kinaniuma kila siku nameza pain killer lakini kuna muda zinadunda.
samahani naombeni msaada wenu nipo njia panda.
Pole sana. Nenda katembelee makaburi yao haraka na roho yako itapona na furaha kurejea. Mungu akusaidie.
 
Bila shaka wote mko poa kabisa.
Kidoti wenu nimerudi maji ya shingo nashindwa hata pa kuanzia. Kama familia yangu ya JF naombeni ushauri wenu wenda nikapata hata msaada.

Kama mnakumbuka nilileta uzi huu Kuna wengine hatujui tulipokosea
Sikuweza kuandika kila kitu. wengi mlisoma historia yangu na mnajua wapi nimepitia mpaka nilipo.
niwawachoshe moja kwa moja kwenye mada.

Katika maisha yangu watu ambao ndo walikuwa familia yangu ni babu na bibi zangu sababu wao ndio walikuwa wanasimama kama wazazi ninapopitia changamoto. Hasa hasa babu mzaa baba na bibi mzaa mama. kwa ufupi mwaka jana mwezi wa tatu mwishoni babu yangu alikufa. Kipindi msiba unatokea nilikuwa na wakati mgumu sana sababu sikuwa na kazi ya kueleweka na nilikuwa na mtoto mdogo. Hivyo sikuweza kwenda kanda ya ziwa msibani. wakati huo huo bibi yangu mzaa mama alikuwa Arusha kwa ajili ya matibabu alikuwa anaumwa baada ya kupata taarifa alinipigia simu kunipa pole na kunitia moyo sababu alijua jinsi nilivyokuwa nampenda babu yangu. akanisisitiza nimwangalie mtoto alijua nilivyokuwa nimeumia kutoweza kwenda kumzika babu yangu. alikuwa anasisitiza nisiangalie kitu kingine zaidi ya kumwangalia mtoto. nilitaka kuuza kibanda changu ili nipate nauli lakini bibi alikataa akaniahidi kuwa akirudi nyumbani atanitumia nauli nitaenda kuzuru kaburi.nikaona ni sawa nikamkubalia.

Ilikuwa ni ijumaa bibi alinipigia simu tliongea sana karibia masaa mawili. akinisisitiza akili yangu yote iwe kwa mtoto. Kesho yake ajabu napigiwa simu kuwa bibi yangu nae hayupo tena duniani ndani ya wiki mbili tu nilipoteza watu muhimu sana kwangu. walisafirisha mwili pia sikuweza hata kwenda kuzika. hakuna kipindi kigumu niliwahi kupitia kama kipindi hicho. sina kazi ya kueleweka nilikuwa nafanya kazi kwa mama ntilie nalipwa elfu tano angalau nipate kula na mtoto. Mama angu alikuja kumzika bibi lakini hakunipigia hata simu kujua angalau mimi na mtoto tunaendeleaje. kwa ufupi bibi ndo alikuwa kama mama yangu.

Mungu ni mwema nilifanikiwa kupata kazi ambayo naendelea nayo mpaka sasa namshukuru Mungu nipo vizuri japo si sana nina dhiki za kawaida kama za watu wengine. hatulali njaa na mtoto naweza kulipa ada kodi na kujikimu mahitaji yangu na mtoto. naweza kula nachokitamani. namshukuru sana Mungu kwa hilo.
ila kinachoniumiza toka itokee hiyo misiba sina amani nikiwakumbuka babu na bibi yangu naanza kulia. usiku silali nimekonda nimepungu kutoka 63kg mpaka 55kg.

usiku nikilala naweza kuota nipo kanda ya ziwa yaani naota makaburi naweza ota nimeenda kwa bibi lakini nyumba imejengwa makaburini. naweza kuota nipo mochwari yaani kwa ujumla sioti ndoto za kawaida. najikuta wakati mwingine natamani kufa labda naweza kupumzika lakini akili inaniambia ukifa huwezi kupumzika kwa amani kwa sababu mtoto wako hutakuwa umemuacha katika mazingira magumu sana. nimedhoofika sana kichwa kinaniuma kila siku nameza pain killer lakini kuna muda zinadunda.
samahani naombeni msaada wenu nipo njia panda.
Pole sn. Kuwa na subra. Muombe Mungu. Jikaze sn kwa ajili ya mtt. Hio hali itapungua taratibu mwisho itaondoka kabisa. Ni suala la muda tu
 
Basi jitahidi uende kule na huko makaburini utasema shida zako zote,ila nadhani kuna namna umeathirika kisaikolojia.
Kama mtandao huu ungekuwa unaaminika bila shaka ungepata watu wanaoishi huko ulipo wakakusogeza sogeza maana inaonekana shida sio kubwa kiivo ila umejikatia tamaa tu
 
Pole nakushauri pata rafiki,rafiki ambae ataweza kuwasiliana na wewe muda wowote,atakutoa kwa mawazo na ukajiona uko wa thamani

You need some body…
Wewe unataka kumuongezea binti matatizo, hakuna mtu anaiona thamani yako zaidi yako, furaha ipo ndani yako sio mpaka utafute rafiki huyo rafiki yeye hana ishu za kufanya hadi awe anakuangalia wewe na yeye anaangaliwa na nani??
 
Basi jitahidi uende kule na huko makaburini utasema shida zako zote,ila nadhani kuna namna umeathirika kisaikolojia.
Kama mtandao huu ungekuwa unaaminika bila shaka ungepata watu wanaoishi huko ulipo wakakusogeza sogeza maana inaonekana shida sio kubwa kiivo ila umejikatia tamaa tu
sawa shukrani sana
 
Back
Top Bottom