Naona 99.9% Yanga anashinda dhidi ya Morrison

Naona 99.9% Yanga anashinda dhidi ya Morrison

Kiukwel simba imejishushia heshima kweny swala la Morrison wamefanya ujinga na ujinga huo unaweza kuwagarimu
Ujinga gan? Inawezekana ww ndo ume comment ujinga kitu usichofaham..kesi ipo TFF ni yanga vs morison, hakuna mkataba wa simba vs morison..kama upo tumbie.

Simba hajamsajil morison. Tumia ubongo kuchanganua mambo
 
Ujinga gan? Inawezekana ww ndo ume comment ujinga kitu usichofaham..kesi ipo TFF ni yanga vs morison, hakuna mkataba wa simba vs morison..kama upo tumbie..
Simba hajamsajil morison..
Tumia ubongo kuchanganua mambo
Picha alizopiga za wapi?
 
Hili sakata yanga waachane nalo hivi akirudi yanga atakuwa na moyo wa kucheza tafuteni mchezaji mwingine
 
Kwa kauli hii ya msemaji wa serekali kuna kitu wanajua.
status_me_status_IMG-20200812-WA0011.jpeg
 
Hiyo ngoma ngumu,hakuna atakayeshinda hapa ila inaweza kula kwa mchezaji mtani,huyu mchezaji tunaweza kumkosa wote
Hata na mie nimeifikiria hiyo Mtani hii inaeza kula kwake Mchezaji mwisho wa siku wote tukakosa.

Ila liishe bana tushachoka kusubiri.
 
Hata na mie nimeifikiria hiyo Mtani hii inaeza kula kwake Mchezaji mwisho wa siku wote tukakosa.

Ila liishe bana tushachoka kusubiri.
Ila navyoona wanaweza wasimalize kesi leo pia ,maana TFF nao wana madudu kibao
 
Kwanza kabisa mimi ni mshabiki wa Simba nakiri hili lakini hapa sitachambua kama mshabiki wa Simba bali Kama mshabiki wa Soka.Kwa Hili sakata linaloendelea naona kabisa BM hatachomoka kwenye Hili sakata ukiangalia kwa makini utaona hili.

BM Amejitia kitanzi mwenyewe

Wakati BM alikuwa akihojiwa kwa njia ya simu na Wasafi FM kupitia kipindi Cha sports Arena hapo ikiwa hajaingia mgogoro na Yanga alikiri kabisa amesaini mkataba na Yanga na akasema kabla ya kusaini Yanga alikuwa anatakiwa na team 3 za South Africa ikiwemo team ya Ajax Capetown. Huu Ni mkataba ule wa miezi 6 baada ya Yanga kuridhika na huduma Yake wakataka kumuongezea mkataba ndipo BM akasaini kwa miaka miwili baada ya kusaini BM akaongezea akasema baada ya yeye kusaini akawa anapewa maneno kwamba team ya Yanga hailipi mishahara wachezaji wake kwa wakati,haiendeshwi kiprofessionalism ndipo akaona Bora awaombe kuvunja mkataba nao huku Kuna baadhi ya offer akawa amepokea ikiwemo ya Simba.

Ukiachana na hapo tukaona email ya BM mtandaoni akiomba Yanga kucancel extension ya mkataba.kwenye Hili unajiuliza Kama ajasaini mkataba na Yanga inakuaje kwenye email yake anaomba acancel extension ya mkataba wake?

So ukitazama kwa ujumla wake bila ushabiki unaona kabisa jamaa anajifunga mwenyewe kwa Hali kama hii unaanzaje kumuamini BM?

Kwa upande wa Simba
Uongozi wangu wa Simba ulifanya kosa kubwa Sana kumtambulisha kumsajili Morrison mapema wangesubiri kwanza kesi ya Yanga na BM iishe Kama walivyoshauriwa na "Senzo" lakini kwa akili ya uswahili wa viongozi wakaenda against. Kwa maana hii Kama Yanga itashinda lazima watafungua kesi dhidi ya Simba kumsajili mchezaji wao mwenye "mkataba".
hata shishimbi alitamka amesaini

Sent from my M4 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom