Naondoka na Slaa kampeni ya CHADEMA Asilia!

Naondoka na Slaa kampeni ya CHADEMA Asilia!

Dr Slaa akidanganyika kwa kurubuniwa na mkewe ataondoka peke yake, sisi tunaenda na mabadiliko na atapotea kabisa katika historia ya Tanzania pia atakuwa katupa shilingi chooni.
 
Wachochezi tu nyie, hamna lolote, kama viongozi wa CHADEMA akiwemo Slaa wamekubaliana kumpokea LOWASSA nyie mna nini cha kuwaambia wananchi?
CHADEMA wamefanya kitendo cha ki - UNGU kumpokea LOWASSA aliyenyanyaswa vya kutosha na mfumo kandamizi, pia akapokwa haki yake na KITENGO ambacho hakiko kisheria! Sasa ukisema mambo ya kuondoka CHADEMA wakati huu ambapo neema imewazukia kila mtu anakuona wa ajabu! Tulieni LOWASSA achukue Nchi Kwanza!!!

Viwanda vya uongo mnaumbuka mchana kweupe!!


KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
 
Dr Slaa akidanganyika kwa kurubuniwa na mkewe ataondoka peke yake, sisi tunaenda na mabadiliko na atapotea kabisa katika historia ya Tanzania pia atakuwa katupa shilingi chooni.

Mabadiliko ya kurasimisha ufisadi
 
Kwa taarifa tu,Dr Slaa nae alihamia toka CCM kama hivi na nyakati hizi.Zaidi Dr Slaa siyo Chadema asilia,amekikuta kikiwa ni chama sio fukuto
 
Nasubiri tamko la Dr. Slaa ili nijue nn cha kufanya..
 
Kwa taarifa tu,Dr Slaa nae alihamia toka CCM kama hivi na nyakati hizi.Zaidi Dr Slaa siyo Chadema asilia,amekikuta kikiwa ni chama sio fukuto
Kabla ya Slaa kuhamia Chadema ilikuwa na majimbo mangapi?leo hii ina majimbo mangapi?
 
Slaa hawezi ng`olewa na fisadi yeyote.Wakijaribu ana wanachama wanaompenda wengi watatumia ile nguvu ya umma ya wanachama kumrudisha.Ule msemo wa PEOPLE`S POWER sasa unairudia CHADEMA yenyewe.Wanachama watahakikisha wanalikimbiza fisadi mchana kweupe na kumuweka Slaa madarakani.

Taarifa za karibu zinasema kuna fisadi baada ya kuona mambo magumu Ukawa anataka kutimukia ACT kwa ZITTO kabwe CHAMA ambacho hakiko muungano wa UKAWA na Zitto kakubali kuwa akiona magumu aende tu watampokea chap chap awahi muda wa tume kuchukua fomu.
 
Slaa hawezi ng`olewa na fisadi yeyote.Wakijaribu ana wanachama wanaompenda wengi watatumia ile nguvu ya umma ya wanachama kumrudisha.Ule msemo wa PEOPLE`S POWER sasa unairudia CHADEMA yenyewe.Wanachama watahakikisha wanalikimbiza fisadi mchana kweupe na kumuweka Slaa madarakani.

Taarifa za karibu zinasema kuna fisadi baada ya kuona mambo magumu Ukawa anataka kutimukia ACT kwa ZITTO kabwe CHAMA ambacho hakiko muungano wa UKAWA na Zitto kakubali kuwa akiona magumu aende tu watampokea chap chap awahi muda wa tume kuchukua fomu.

Toka lini ukawa msemaji wa CDM
 
Mabadiliko ya kurasimisha ufisadi
Hatogopi tena ufisadi kwani chama kilicho madarakani ndicho kiwanda cha kutengeneza mafisadi. Bora tusiangamize aliyetuonyesha kiwanda cha kufyatulia mafisadi bali tusaidiane naye kukiangamiza kiwanda hicho mkuu ili tuokoe vizazi vijavyo.
 
Hatogopi tena ufisadi kwani chama kilicho madarakani ndicho kiwanda cha kutengeneza mafisadi. Bora tusiangamize aliyetuonyesha kiwanda cha kufyatulia mafisadi bali tusaidiane naye kukiangamiza kiwanda hicho mkuu ili tuokoe vizazi vijavyo.

Ina maana Ugaidi ukiongezeka tutachagua gaidi!

Umasikini ukiongezeka tunachagua masikini!

Ulevi ukiongezeka tunachagua mlevi....
 
ha haha hahaha haha baregu mchaga? tundu lisu mchaga? lwakatare mchaga? silaa mchaga? mnyika mchaga? salumu mwalim mchaga? jusa Mchaga? na sasa lowasa ni mchaga? wachacheni propaganda za kijinga leteni hoja eti chama viongozi ni wachaga toa mfano
 
Nimepita maeneo ya mianzini jijini Arusha kuna kampeni ya chini kwa chini yenye kupeana hamasa kuwa wanachadema asilia waliojitolea kupigwa risasi na mabomu pale Soweto kwa ushawishi wa Ufuasi wa Slaa.

Sasa wameweka nadhiri kuwa watahama na kumfuata kokote mpendwa wao Dr Willy Slaa ambaye ni baba wa vita dhidi ya ufisadi Tanzania.

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA.


wana CHADEMA wenyewe tumetuliaaaa na CHDEMA yetu ila MAGAMBA ndo wamegeuka wasemaji wa chama...haya bwana hongereni kwa kujipa ajira
 
Dr. Slaa, tunakuomba uwatendee haki wananchi kwa kuanzisha chama kipya cha siasa. Sioni chama chochote cha siasa ambacho Dr. Slaa anaweza kujiunga nacho. Siyo CHADEMA ambao wameamua kumsaliti Dr. Slaa ambaye alihatarisha maisha yake na familia yake na wengine kukipa CHADEMA heshima iliyopata kabla ya ujio wa Lowassa. Dr. Slaa pia hatakiwi kujiunga na CCM, wala ACT, wala CUF, wala NCCR mageuzi wala chama chochote cha siasa.

Kitu pekee anachoweza kufanya Dr. Slaa ili kuwatendea haki wananchi watanzania ambao wanadhamira ya kweli ya kupigana na ufisadi kwa dhati kabisa ni kuanzisha chama kipya cha siasa. Hata kama Dr. Slaa ataanzisha chama chake baada ya uchaguzi mkuu itakuwa ni vizuri mno. Ukweli ni kuwa uongozi wa Dr. Slaa akiwa na chama chake cha siasa unahitajika sana ili wananchi waliopondeka moyo kwa unafiki wa CHDEMA na UKAWA wapate pa kujisitili.

Madonda na makovu ambayo CHADEMA kwa kughilibiwa na UKAWA wameyacha kwa wananchi wapenda haki ni makubwa mno. Njia ya pekee ni kwa Slaa kuanzia chama kipya cha siasa. Kiukweli CHADEMA wamemfanyia Dr. Slaa na wapenda haki wote kitu kibaya mno. Binafsi nimesononeshwa sana.
 
Mkuu unataka tuwe na vyama kama vioski? Au vyama kama UPDP ya Dovutwa?
 
Back
Top Bottom