Napata harufu ya matumizi ya Nyuklia Ukraine baada ya Kursk kuanguka

Napata harufu ya matumizi ya Nyuklia Ukraine baada ya Kursk kuanguka

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Wengi watakumbuka katika vita vya uvamizi vinavyoendelea huko Ukraine wakati vinaanza ilikuwa Ukraine akijibu mashambulizi kwa kushambulia eneo lolote ndani ya Russia au maeneo ya Ukraine yaliyotekwa na Urusi kama vile Crimea basi jeshi Urusi litajibu maradufu kwa kuvurumisha mvua ya makombora hadi ya supersonic kila mahali ndani ya Ukraine, Kyiv na miji mingine ilikuwa inashambuliwa sana kuanzia hospitali hadi shule za nursery za watoto.

Nimeshangaa kuona kuona kuna uvamizi au SMO ya wiki mbili sasa ndani ya mipaka ya Urusi katika eneo la Kursk majeshi ya Ukraine yakijivinjari ndani ya mipaka ya Urusi na kupelekea wakimbizi wa ndani wa Urusi zaidi ya 20,000 huku tukiwa hatujaona majibu ya majeshi ya Urusi mpaka sasa! Hii sio kawaida ya Putin kabisa ukizingatia mbele kidogo ya eneo hili kuna bomba la gesi linalopitisha 50% ya gesi kupeleka nje ya nchi.

Labda Putin ameisha amekuwa mdebwedo kabisa baada ya mipango yote ya uvamizi kuvurugika na kwenda mrama. Vinginevyo kuna uwezekano mkubwa anaandaa shambulizi "barbaric" la nuclear.
 
Ukraine ana halalisha uvamizi wa Urusi katika mipaka yake.

Ukraine alipaswa kumfukuza Urusi katika mipaka yake na sio kuvamia mipaka ya Urusi kama Urusi alivyofanya kwake.

Sina hakika sana juu ya silaha hizo za maangamizi ila ninachoona ni Urusi kupata support zaidi ya kuingamiza Ukraine kupitia uvamizi huu.

Support ya ndani na ya nje kwa washirika wake na hata wasio washirika wake.

Urusi atasema najilinda dhidi ya uvamizi wa Ukraine atautumia udhaifu huu kuleta maafa sijajua ni kipi makamanda na majeshi ya Ukraine wanacho fikiri.
 
Putin anapukuchuliwa taratibu mpaka ataisha.

West wanampukuchua Putin kwa akili sana.

Angalia walianza kumpa Ukrain silaha ndogo ndogo ila kadiri siku zinavyozidi kwenda wanaongeza uzito wa silaha, ni kama vile mtoto unaanza kumpa Uji baadae ugali.

Mwanzo Marekani ilikuwa inawambia Ukrain marufuku kushambulia ndani ya Rusia, ila sasa hivi Ukrain ruksa kushambulia Rusia.

Mwishowe tutaanza kuona makombora yakitua Moscow hapo ndio Putin atashtuka kwamba kumbe kapukuchuliwa kweli.

Nmeshangaa sana Putin kaishiwa makombora hadi anaomba kutoka Iran.

Vita ni gharama, lakin wafuasi wa Putin ukiwambia hili kwamba Urusi baadae itakuwa hohehae wana bisha ila muda utaongea
 
Kursk kuanguka una maanisha imeanguka au kama itatokea ikaanguka.. For my information Ukraine army wana retreat back due to heavy fight from Wagner na Russian army and within this week mtapata habari kamili.

Ila mass of Nato weapons, air defense and tanks vimekuwa destroyed kwa wingi sana in Kursk so it seems like Nato this time wameamua kweli kweli kumfanya mbaya bwana Putin.

Kama Putin na Russia kwa ujumla watashindwa kutoa adhabu kali kwa Ukraine na ikawa funzo kwa Nato nzima basi naamini Russia ijiandae kuvamiwa zaidi hapo mbeleni na kupoteza Mikoa yake mengine.
 
Kursk kuanguka una maanisha imeanguka au kama itatokea ikaanguka.. For my information Ukraine army wana retreat back due to heavy fight from Wagner na Russian army and within this week mtapata habari kamili.
Imeanguka tayari mikononi mwa Ukraine na raia zaidi ya 20,000 wamehamishwa kama wakimbizi wa ndani, Inachofanya sasa hivi Urusi ni kupambana kuirudisha katika himaya yake.
 
Kursk kuanguka una maanisha imeanguka au kama itatokea ikaanguka.. For my information Ukraine army wana retreat back due to heavy fight from Wagner na Russian army and within this week mtapata habari kamili...
Katibu mkuu wa NATO alisema vita hii itaamua usalama na mstakabali wa nchi za ulaya siku zijazo.

Kwa kauli hiyo utaelewa nini kinaendelea hapo Ukrain na Rusia
 
Back
Top Bottom