Nape alichoongea ni ukweli mchungu; atabaki kuwa shujaa daima

Nape alichoongea ni ukweli mchungu; atabaki kuwa shujaa daima

Sio sahihi kusema Nape ni shujaa kwa Yale aliyoyasema kwa Byabato ile ilikuwa siasa tu.Angesema rasmi kama Waziri,au kwenye vikao rasmi tungejua kamaanisha.tujifunze !"ukiwa unaongea ongea sana Kuna siku utaongea Kila ambacho hakisemwi"
Lakini kaongea ukweli tupu. Sasa kwanini atumbuliwe kwa kusema ukweli? Wewe unadhani adhabu aliyopewa inastahili?
 
Unapozungumzia Tanganyika kumbuka Rwanda na Burundi zilikuwa sehemu ya Tanganyika,lakini pia 50km kutoka Pwani ya Bahari ya Hindi ilikuwa chini ya utawala wa Sultan.
Je tukubali Tanganyika irudi ili Rwanda na Burundi ziwe sehemu yake..na wakati huo huo hizo 50Km kutoka Pwani ya Bahari ya Hindi ziwe ni sehemu ya Zanzibar...?
Rudi shuleni ukasome vizuri historia ya Tanganyika mkuu
 
Nape kutolewa uwaziri sababu ya kauli yake ya kweli ya"mbinu za ushindi" si haki, maana hata aliyemtoa uwaziri naye basi ilitakiwa awe amefutwa kazi ( na sisi tukiomuajiri) kwa ile kauli yake kwamba "hata ukipiga kura kwingine, CCM ndiyo itakayounda serikali", maana kauli zote zinafanana.

Nimeamini kuwa Tanzania kuongea ukweli ni dhambi na kosa kubwa sana.

Nape hana uwezo wa kiuongozi kama ambavyo wengi wa mawaziri wasivyokuwa na uwezo, lakini hili la kuongea ukweli lazima apongezwe sana na sisi wapenda ukweli.
Kweli kabisa mkuu. Tatizo maCCM yanapenda kuficha mambo.
 
Rudi shuleni ukasome vizuri historia ya Tanganyika mkuu
1721852952333.png
 
Hii nchi inaongozwa na mijitu mbumbumbu sana
 
Back
Top Bottom