Wakati miezi sita ya mama samia kakopa trillioni 2.4 na mpaka sasa hakuna mradi wowote..maana madarasa na vituo vya afya tumeambiwa ni tozo. Ina maa ndani ya miaka 5 atakopa zaidi ya trillioni 20 huku kukiwa hakuna mradi wowote wa maana.Usitoke nje ya mada
Tunazungumzia miaka mitano ya Magufuli amekopa trillion 20
Zimetumikaje...????
Legacy ya Mwendawazimu wamefura humu leo, Sukuma GANG wamesahau kabisa hata wao walimtukana na kumdharirisha sana Kikwete na serikali yake, na hawa kina Nape wake."Tembeeni vifua mberee, Tanzania ni dona kantri"
Rudia kusomaKama nakuelewa ila sasa kama Mkapa alikuta deni hilo la 7.4 na madeni mengi yakafutwa kwa ule mpango wa HIPC ilikuwaje ikabaki 8.4? Tusaidie kwenye mahesabu hapo manake naona hakuna usuluhisho?
Nimeeza hapo hadi sasa Mama Samia kakopa trillion 4, wewe unasema trillion 2.4.Wakati miezi sita ya mama samia kakopa trillioni 2.4 na mpaka sasa hakuna mradi wowote..maana madarasa na vituo vya afya tumeambiwa ni tozo. Ina maa ndani ya miaka 5 atakopa zaidi ya trillioni 20 huku kukiwa hakuna mradi wowote wa maana.
Hakuna miradi iliyoanzishwa tu. Kila mradi ulikuwa na malengo. Yawezekana sio sasa ila kesho. Hiyo ni vision ya tanzania ijayo kama sio sasa. Ndio maana hata uzinduzi wa miradi ya maji unaambiwa una uwezo wa kuhudumia watu mill 1 ila kwa wakati huu unahudumia watu laki 4.Mkuu wa sitoki nje ya mada, Bali haya madeni yote yametumika ndivyo sivyo.
Kujianzishia miradi bila kufuata utaratibu ni upigaji na hili jiwe analo la kujibu.
Mada yangu nimelenga kumsahihisha nape kuhusu Deni alilokopa mkapa na kikwete. mkapa alikola dola bilion 1 na sio 9, kikwete alikopa dola bilion 11 na sio 7.
Nape ameamua kwa makusudi au kwa bahati mbaya kudanganya.Mkuu nashukuru sana kwa analysis nzuri uliyofanya.Nape sijui hata kama anajua maths.Hivi vitu ni vya wataalam wa model za econometrics. Nape anaamini kuwa kupiga kelele sana ataonekana anafahamu.Nape sijui hata kujumlisha na kutoa anafahamu.Na hajui kuwa anajenga uadui na watu wengi zaidi.
Mnamatatizo sana nyie, hivi unadhani Nape hajui kwamba JPM hajakopa hizo pesa? JPM hakukopa na hakulipa, alitaka kujenga nchi kwanza, deni lenye riba linakua kama hulipi.Usitoke nje ya mada
Tunazungumzia miaka mitano ya Magufuli amekopa trillion 20
Zimetumikaje...????
hatukuwa tuna export sana lakini tulishindwa kumaintain balance baada ya kukua kwa wigo wa biashara ikiwemo uuzaji wa bidhaa zetu na uagizaji wa bidhaa za nje.mkuu kwa hiyo kipindi shilingi yetu ilipokua sawa na kenya tulikua tunaexport sana?
Hata magufuli amekopa bilion 7 dollar mpaka mauti yanamkuta. Nape nimuongo.Nimezisikia na kuzisoma hoja za Nape ila, ukweli kuwa Nape kwa kujua au kutokujua amemuonea mzee mkapa(apumzike salama).
Nape akiwa na confidence ya Hali ya juu amesema mkapa kwa miaka 10 alikopa dola Bilioni 9.
Hii si kweli kabisa, na sijajua kwa nini mh.Nape aliamua kusema hivi.
Mkapa aliingia madarakani 1995 Deni lilikuwa ni dola bilion 7.37. na hadi anaondoka madarakani kwa mwaka wa fedha alioishia nao Deni lilikuwa ni dola Bilioni 8.4
Hivyo kwa miaka 10 mkapa alikopa dola bilion 1 tu ambayo ni sawa na trillion 2.3 ya sasa na sio bilion 9 ambayo ni sawa na trillion 20 Kama alivyosema mh.Nape.
Kutokana na mpango wa kufutiwa madeni Deni lilifutwa na kufikia dola bilion 4 mwaka 2006 mwanzoni, ila likatoka hapo na kufikia dola bilion 15 Hadi kikwete anaondoka.
Hivyo kikwete alikopa dola bilion 11 na sio Bilioni 7 Kama alivyosema Nape
Mh.Nape kwa hesabu ulizopiga unaenda kumhukumu mama Samia bila kujua, maana kwa kipindi chake Cha miezi 6 tu ameshakopa zaidi ya Trillion 4 ( 2.7 za world Bank na 1.3 za IMF).
Mh.Nape umesifia mikopo hii kwa mama, lakini jua kwa kipindi Cha miezi 6 mkopo kwa mama samia umezidi mkopo wa mkapa kwa kipindi chake cha miaka 10.
Lakini mimi sitamhukumu jiwe mwendazake, mama Samia na atayekuja. Kwa sababu;
Kipindi cha mkapa na mwanzoni mwa kikwete mfumuko wa bei ulikua mdogo sana na pesa yetu ilikuwa na thamani kwenye dola 1.
Mfano: kipindi Cha mkapa ili kujenga darasa 1 ilihitaji si zaidi ya mil 5. Hivyo akienda kukopa atakopa pesa kidogo na deni kwa sasa litaonekana dogo kipindi chake.
Sasa hivi kujenga darasa moja si chini ya mil 20, bati kipindi cha mkapa liliuzwa sh.5,000 Ila leo bati ni sh.25,000 hivyo mama Samia akienda kukopa ni lazima atakopa kingi.
Mfano mwingine rahisi tu, Kuna kipindi Cha mkapa bajeti ya nchi ilikuwa Trillion 4 tu.
Lakini sasa hivi hizi trillion 4 ukiweka kwenye barabara tu zote zimeisha kutokana na thamani ya pesa kwa sasa.
Hivyo kwa hesabu rahisi tu kwa kipindi Cha miaka 5 inayokuja mama samia atakopa hadi trillion 30(huu ni ukweli). Na atayekuja baada ya mama Samia nae atakopa zaidi ya hizo 30.
Nini kifanyike ili deni lisikue;
Hayo yote yanawezekana Ila kwa serikali ambayo itakuwa na vision na watu wenye akili
- kupandisha thamani ya shilingi dhidi ya dola. mfano dola moja iwe sh.1200. na hapo Deni letu litakuwa limeshuka kwa nusu. Badala ya trillion 64 litakuwa trillion 32.
- kupunguza mfumuko wa bei, mfano bati liwe sh.8000, cement sh.7000, nondo sh.9000.
Kumbuka hiyo miradi yote jiwe alikuwa akituambia inatekelezwa kwa fedha za ndani.Wewe huoni? Hizo interchange mnazopita mnadhani zimetolewa bure? Huoni SGR,huoni NHPP,kweli hutuoni au tunajitoa ufahamu tu Magufuli kafanya parefu Sana na panaonekana hakuna aliyekuwa na huo uthubutu,hili Deni la Magufuli nalipokea kwa mikono miwili na ninafurahi kulipa na wajukuu zangu watamalizia kwa amani maana alikopa kwa faida yetu na kizazi chetu.
Sawa mkuu kwa kunirekebisha. Kama miezi sita ni trillioni 4 basi miaka mitano sawa na trillioni 30 na ushee..Nimeeza hapo hadi sasa Mama Samia kakopa trillion 4, wewe unasema trillion 2.4.
Muwe mnafatilia.
Trillion 2.7 zilikuwa za world Bank na trillion 1.3 ni ya IMF
Kwa kiasi kikubwa pesa ya ndani imehusika pia tambua mradi NHPP hakuna taasisi ilikuwa tayari kutukopesha.Kumbuka hiyo miradi yote jiwe alikuwa akituambia inatekelezwa kwa fedha za ndani.
Sahihi kabjsaSawa mkuu kwa kunirekebisha. Kama miezi sita ni trillioni 4 basi miaka mitano sawa na trillioni 30 na ushee..
It was through a consortium of many International banks!! I am sure of this, Mustapha Mkullo was finance Minister.
Na hapa ndio pale unaposema Nape anaibua mijadala ambayo badala ya kumsaidia huyu mama atamletea shida.Sahihi kabjsa