Nape atofautiana na Jaji Warioba Bunge la Katiba

Nape atofautiana na Jaji Warioba Bunge la Katiba

Kitu pekee kinachonipa faraja ni kwamba Nape ana umri mdogo,atazeeka na majuto na masikitiko kwa kusimamia uongo na uovu..malipo ya unafiki hapahapa duniani.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Hski ya Mungu sikujua kama Nape ana akili ndogo hivyo! Yaani MABORESHO NI KUONGEZA CHUMBA- kwa mfano wake aliotoa! Ni mtu wa kufikiria uwingi na sio viwango (yaani Quantity na sio Quality) Bure kabisa. KUBORESHA KAMWE SIO KUBADILI na hili halina utata katika lugha zetu mbili kiingereza na kiswahili. Unaweza kubadili mtaala kwa maana ya kufanya kitu kipya kabisa lakini unaboresha kwa kuongeza au kupunguza baadhi ya masomo au muundo wa kufundisha! Huyu ni aibu kwa Chama Cha Mapinduzi! CCM wamekosa watu wenye akili zaidi ya huyo? puuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu
 
Dar es Salaam. Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, amesema Bunge Maalumu la Katiba,litatekeleza majukumu yake kwa kufuata Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na si mawazo ya mtu yeyote.

Kauli hiyo ya Nape imekuja siku moja baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba kusema kuwa litakuwa jambo lisilo la kawaida kwa Bunge hilo kubadili hoja ya msingi iliyopo kwenye Rasimu ya Katiba, akisisitiza kuwa jukumu lake ni kuifanyia marekebisho.

Warioba alisema hayo juzi alipokuwa akizungumza katika mkutano ulioandaliwa na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD),kuhusu tafakuri na maridhiano kuelekea katika Katiba Mpya.

Alisema kama Bunge Maalumu la Katiba likipewa jukumu la kuandika Katiba linaweza kubadili mambo mengi, lakini kama Katiba itakuwa imeandaliwa na
chombo kingine, Bunge hilo linatakiwa kutobadili hoja za msingi.

Akizungumza na gazeti hili jana, Nape alisema: "Mchakato wote wa Katiba Mpya unasimamiwa na sheria na sio maneno ya Warioba. Sheria inazungumzia haki, wajibu na mamlaka ya Bunge hilo, hivyo inawezekana kabisa kuboreshwa na hata kubadilishwa kwa hoja."

Nape alisema kulingana na sheria hiyo,Bunge hilo lina mamlaka ya kufanya jambo lolote katika Rasimu hiyo, ikiwa ni pamoja na kuifanyia maboresho kadri itakavyoonekana kuwa inafaa.

"Bunge haliwezi kutishwa na mtu yeyote kwa sababu lipo kwa ajili ya kuwawakilisha wananchi. Ndiyo maana baada ya Bunge hilo kwisha wananchi watapiga kura yamaoni," alisema.

Akitolea ufafanuzi kauli ya Jaji Warioba kwamba Bunge hilo lifanye maboresho na si kubadili hoja za msingi, Nape alisema:"Maboresho maana yake ni kubadili.

Ukiwa na nyumba ya vyumba vinne na kuiboresha kwa kuweka chumba kimoja si umeibadili?"


Alisema Bunge hilo linatakiwa lisiingiliwe katika uamuzi wake.

Source: Mwananchi.

Si umeona pumba zake hapo!
 
Waache wapige kura zao, ikipigwa kura ya maoni na Wananchi tutaikataa tutoke bila bila waanze upya.
Sidhani kama CCM hawalijui hilo, inaelekea kuwa hata huko kwenye kura ya wananchi wamejiandaa kisawasawa ikiwemo wizi wa kura.

Sasa hivi aidha kwa kujua au kutojua kivyovyote vile CCM wanampiga vita ya kisaikolojia Warioba (na wenye mawazo yake) ili wamshinde kisaikolojia kabla ya kuanza kwa bunge la katiba.

Wakifanikiwa kumshinda sasa hivi kabla ya bunge basi kazi itakayobakia itakuwa ni ndogo.

Ilitegemewa viongozi wanaotaka serikali tatu nao wakajitupa ulingoni sasa hivi na kuzitetea hoja za Warioba kabla ya bunge kuanza lakini wapi..
 
umbo la mwili la huyu mtoto na akili yake vitu viwili tofauti. maana yake kimo chake na hekima ni kama chumvi na mchanga!
 
Kama kutakuwepo na suala la kupiga kura kwa wabunge basi watakuwa wamejipanga.Ndio maana kuna makada wengi humo achilia mbali wale watakaonunuliwa
Hilo sahau, labda kura kama hazitakuwa za siri... Wana CCM wengi chama ndo kinawabana..... Kwani Nimrodi Mkono na wenzie hawakupiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu..?? kama ni mimi, hela nachukuwa na kura hupati...
 
Aliyo ongea Jaji Warioba juzi

"Kazi ya Bunge la katiba sio kubadili Rasimu" Joseph Sinde Warioba aliongea juzi haya

Majibu ya Nape jana


Nape Nnauye “Mchakato wa Katiba unasimamiwa na sheria na sio maneno ya Warioba; Bunge linaweza kuboresha na hata kubadilisha Rasimu.”

WE REPORT, YOU DECIDE
 
Kama Bunge linaweza kufanya yote hayo (Ikiwa ni pamoja na kutunga KATIBA kwa maana ya kutozingatia mawazo ya Wananchi); kamati ya Rasimu ya Katiba iliundwa kufanya nini????
 
Kama Bunge linaweza kufanya yote hayo (Ikiwa ni pamoja na kutunga KATIBA kwa maana ya kutozingatia mawazo ya Wananchi); kamati ya Rasimu ya Katiba iliundwa kufanya nini????
Nape ni vuvuzela, unategemea mtu aliye pata div four awe na mchango wa maana kwenye hili taifa??
 
Mwisho wa nape utakuwa wa aibu sana! Hicho "cheo cha msimu" kimempa kiburi sana, sasa anafikia hadi hatua ya kutukana wazalendo wa kweli wa taifa hili.!
 
Aliyo ongea Jaji Warioba juzi

"Kazi ya Bunge la katiba sio kubadili Rasimu" Joseph Sinde Warioba aliongea juzi haya

Majibu ya Nape jana


Nape Nnauye "Mchakato wa Katiba unasimamiwa na sheria na sio maneno ya Warioba; Bunge linaweza kuboresha na hata kubadilisha Rasimu."

WE REPORT, YOU DECIDE

Aliyosema NAPE ni kweli, kama bunge lisingekuwa na mamalaka ya kubadili Rasimu kusingekuwa na haja ya kutumia pesa za walipakodi kwenda kupoteza muda wa miezi mitatu kujadili kitu ambacho hakiwezi kubadilika. Waryoba amemaliza kazi yake atulie sasa na bunge lifanye kazi yake.
 
Sasa jamani tulitegemea aseme nini wakati chama chake kinaamini kwenye serikali mbili na ufisadi?Tumsamehe bure ila tumuelimishe tu.
 
Mwisho wa nape utakuwa wa aibu sana! Hicho "cheo cha msimu" kimempa kiburi sana, sasa anafikia hadi hatua ya kutukana wazalendo wa kweli wa taifa hili.!

kwa hiyo wewe uko pamoja na yule mvuta sigara namba moja Tanzania(WARYOBA). Yule kalewa pesa za walipa kodi na kujiona yeye ndiyo kila kitu kwenye Katiba.
 
Back
Top Bottom