Nape atofautiana na Jaji Warioba Bunge la Katiba

Nape atofautiana na Jaji Warioba Bunge la Katiba

Nape ndio tank thinker wa C.c.m?inasikitisha sana!rasimu ya katiba ni mawazo ya wananchi,bunge halina uhalali wa kubadili maoni na matakwa ya wananchi,bali ni kuboresha
 
wamekula kodi zetu bure walichotoa hakina maana!!

ila wenyewe wanadai kamati ya rasimu kazi yake ilikuwa ni kutoa tu mwanga wa kianzio, eti bunge hilo ndo litatunga katiba
ndiyo swali la kujiuliza, kama Tume ya Waryoba ndiyo kila kitu , kwa nini Bunge la Katiba? tuache mbwembwe, Bunge la Katiba inaweza kukubaliana/ kubadili na hata kukataa kabisa kilichomo kwenye rasimu zote mbili. Kile ndicho chombo cha kutunga sheria na hakiwezi kupitisha kila kitu ambacho wananchi wengine walitoa maoni yao waliandaliwa kwa maslahi ya baadhi ya watu wachache. BIG NO.
 
Safi sana Mkuu, na warejee miswada ya serikali ambayo imekuwa ikiwasilishwa bungeni , siyo yote inayopita kama ilivyowasilishwa na wakati mwingine hukataliwa kabisa na kurudishwa. Nawashangaa sana wanaoabudu rasimu wakati ile ni sawa na mswada tu.

Ni kweli kabisa, lakini kutulazimisha serikali2 na sisi wananchi tuna uhuru wa kukataa serikali2, sawa na wale wanaokataa 3, sawa na wale wanaokataa 1. Kura ya maoni itaamua.! Hatutaki kuhubiri kulinda Muungano kwa viini macho na hadaa, tunataka dhati kutoka moyoni. Dhati halali kuliko zote ni Serikali1, 3 zenyewe nazo ni mashaka, 2 ndo kelele nyingi sana kama wote tunavyofahamu.
 
Nape ndio tank thinker wa C.c.m?inasikitisha sana!rasimu ya katiba ni mawazo ya wananchi,bunge halina uhalali wa kubadili maoni na matakwa ya wananchi,bali ni kuboresha

Hahaaa, sasa wanakwenda kufanya nini DODOMA? safari hii mtalia sana , MBOWE hana nafasi tena ya kugoma bungeni akiondoka tu bado kuna takribani wabune zaidi ya 500 watafanya vizuri sana hiyo kazi.
 
Umeipenda kwa kutoju kasema nini. Na kama Kamati ya WARYOBA ndiyo kila kitu, kwa nini Bunge la Katiba kimeundwa?

Binafsi tangu mwanzo sikuona umuhimu wa hilo Bunge, ni ufujaji wa kodi zetu bure. Ilitakiwa maoni ya kamati ya warioba yaletwe kwa wananchi moja kwa moja kwa ajili ya kura ya maoni, period!
 
Ni kweli kabisa, lakini kutulazimisha serikali2 na sisi wananchi tuna uhuru wa kukataa serikali2, sawa na wale wanaokataa 3, sawa na wale wanaokataa 1. Kura ya maoni itaamua.! Hatutaki kuhubiri kulinda Muungano kwa viini macho na hadaa, tunataka dhati kutoka moyoni. Dhati halali kuliko zote ni Serikali1, 3 zenyewe nazo ni mashaka, 2 ndo kelele nyingi sana kama wote tunavyofahamu.

Habri yote iko bungeni tupende tusipende, hizi zingine kelele tu.
 
Ni kweli kabisa, lakini kutulazimisha serikali2 na sisi wananchi tuna uhuru wa kukataa serikali2, sawa na wale wanaokataa 3, sawa na wale wanaokataa 1. Kura ya maoni itaamua.! Hatutaki kuhubiri kulinda Muungano kwa viini macho na hadaa, tunataka dhati kutoka moyoni. Dhati halali kuliko zote ni Serikali1, 3 zenyewe nazo ni mashaka, 2 ndo kelele nyingi sana kama wote tunavyofahamu.

una mawazo kama yangu mku hapo kwa red
 
Ni akili ya matope sana kuamini kuwa mabadiliko ya Kipengele kimoja cha Katiba tena kwa personal interests za watu eti ndiyo mabadiliko. Pole sana Dada yangu.

Kwangu mimi ukiangalia maneno yako yanakutafsiri tabia uliyonayo,so kubishana na wewe au kuendelea kukujibu nitapoteza muda wangu.Ni bora kuitwa nina akili ya matope lakini mwisho wa siku nina kubali mabadiliko na pia nina uzalendo na utaifa,kwangu mie utaifa kwanza ubabaishaji baadaye,tunachohitaji ni KATIBA ya watanzania na si KATIBA ya CCM.
 
Binafsi tangu mwanzo sikuona umuhimu wa hilo Bunge, ni ufujaji wa kodi zetu bure. Ilitakiwa maoni ya kamati ya warioba yaletwe kwa wananchi moja kwa moja kwa ajili ya kura ya maoni, period!

ndiyo ujue sasa kwamba Bunge la Katiba ndiyo kila kitu.
 
Hahaaa, sasa wanakwenda kufanya nini DODOMA? safari hii mtalia sana , MBOWE hana nafasi tena ya kugoma bungeni akiondoka tu bado kuna takribani wabune zaidi ya 500 watafanya vizuri sana hiyo kazi.

Me sizungumzii unachowaza wewe,nazungumzia maoni waliyotoa Watanzania juu ya katiba waitakayo,na sheria iliyowekwa juu kuongoza rasimu ya katiba!hizo porojo unazoleta mimi sipo huko
 
ndiyo swali la kujiuliza, kama Tume ya Waryoba ndiyo kila kitu , kwa nini Bunge la Katiba? tuache mbwembwe, Bunge la Katiba inaweza kukubaliana/ kubadili na hata kukataa kabisa kilichomo kwenye rasimu zote mbili. Kile ndicho chombo cha kutunga sheria na hakiwezi kupitisha kila kitu ambacho wananchi wengine walitoa maoni yao waliandaliwa kwa maslahi ya baadhi ya watu wachache. BIG NO.

Binafsi tangu mwanzo sikuona umuhimu wa hilo Bunge, ni ufujaji wa kodi zetu bure. Ilitakiwa maoni ya kamati ya warioba yaletwe kwa wananchi moja kwa moja kwa ajili ya kura ya maoni, period!
 
Ni kweli kabisa, lakini kutulazimisha serikali2 na sisi wananchi tuna uhuru wa kukataa serikali2, sawa na wale wanaokataa 3, sawa na wale wanaokataa 1. Kura ya maoni itaamua.! Hatutaki kuhubiri kulinda Muungano kwa viini macho na hadaa, tunataka dhati kutoka moyoni. Dhati halali kuliko zote ni Serikali1, 3 zenyewe nazo ni mashaka, 2 ndo kelele nyingi sana kama wote tunavyofahamu.

Kwa jinsi watanzania tulio wengi tulivyo (shule ndogo, hatufuatilii kinachoendelea katika siasa, hatujitokezi kupiga kura, etc), hata hilo la serikali mbili litapita tena kwa kura nyingi tu.
 
Kwangu mimi ukiangalia maneno yako yanakutafsiri tabia uliyonayo,so kubishana na wewe au kuendelea kukujibu nitapoteza muda wangu.Ni bora kuitwa nina akili ya matope lakini mwisho wa siku nina kubali mabadiliko na pia nina uzalendo na utaifa,kwangu mie utaifa kwanza ubabaishaji baadaye,tunachohitaji ni KATIBA ya watanzania na si KATIBA ya CCM.

naona kama unajitukana mwenyewe kwa vile sasa unaona hauna hoja. Hivi kwa akili yako unaweza kutafsiri neno mabadiliko kuwa ni kuwa na serikali tatu? na je zile nchi ambazo hazijaundwa na muungano wa nchi mbili au zaidi haziwezi kufanya mabadiliko? Halafu nakushangaa sana unaposema huna sababu ya kubishana na mimi wakati kila ninapojaribu kukuelewesha unaendelea kutoa mapovu badala ya kuishia kabisa na usijibizane na mimi.
 
Kwa jinsi watanzania tulio wengi tulivyo (shule ndogo, hatufuatilii kinachoendelea katika siasa, hatujitokezi kupiga kura, etc), hata hilo la serikali mbili litapita tena kwa kura nyingi tu.

Na kwa mtanzania yeyote anayeutakia mema muungano, lazima aikubali serikali mbili. Wale wenye malengo binafsi na ambao hawautaki muungano lazima watajitumbukiza kwenye janga la serikali tatu.
 
Me sizungumzii unachowaza wewe,nazungumzia maoni waliyotoa Watanzania juu ya katiba waitakayo,na sheria iliyowekwa juu kuongoza rasimu ya katiba!hizo porojo unazoleta mimi sipo huko

Watanzania wapi mkuu, wale waliokuwa wnanunuliwa kwenda kusema hivyo kwa nguvu bila kujua wanaowatuma wana malengo gani? Subiri vichwa vimekwenda DODOMA na vitakuja majibu mazuri tu.
 
Uelewa wa Nape na akili yake kwa ujumla hana uwezo hata kidogo wa kubishana na Mhe. Jaji Warioba. Anachoweza Nape ni kuongea pumba majukwaani, kupiga ngoma ama gitaa na kukoleza maharage kwa wali pekee. Hayo mambo ya kitaalam na yanayohitaji weledi na akili iliyotulia awaachie wahusika wenyewe.
 
Dar es Salaam. Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, amesema Bunge Maalumu la Katiba,litatekeleza majukumu yake kwa kufuata Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na si mawazo ya mtu yeyote.

Kauli hiyo ya Nape imekuja siku moja baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba kusema kuwa litakuwa jambo lisilo la kawaida kwa Bunge hilo kubadili hoja ya msingi iliyopo kwenye Rasimu ya Katiba, akisisitiza kuwa jukumu lake ni kuifanyia marekebisho.

Warioba alisema hayo juzi alipokuwa akizungumza katika mkutano ulioandaliwa na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD),kuhusu tafakuri na maridhiano kuelekea katika Katiba Mpya.

Alisema kama Bunge Maalumu la Katiba likipewa jukumu la kuandika Katiba linaweza kubadili mambo mengi, lakini kama Katiba itakuwa imeandaliwa na
chombo kingine, Bunge hilo linatakiwa kutobadili hoja za msingi.

Akizungumza na gazeti hili jana, Nape alisema: “Mchakato wote wa Katiba Mpya unasimamiwa na sheria na sio maneno ya Warioba. Sheria inazungumzia haki, wajibu na mamlaka ya Bunge hilo, hivyo inawezekana kabisa kuboreshwa na hata kubadilishwa kwa hoja.”

Nape alisema kulingana na sheria hiyo,Bunge hilo lina mamlaka ya kufanya jambo lolote katika Rasimu hiyo, ikiwa ni pamoja na kuifanyia maboresho kadri itakavyoonekana kuwa inafaa.

“Bunge haliwezi kutishwa na mtu yeyote kwa sababu lipo kwa ajili ya kuwawakilisha wananchi. Ndiyo maana baada ya Bunge hilo kwisha wananchi watapiga kura yamaoni,” alisema.

Akitolea ufafanuzi kauli ya Jaji Warioba kwamba Bunge hilo lifanye maboresho na si kubadili hoja za msingi, Nape alisema:“Maboresho maana yake ni kubadili.

Ukiwa na nyumba ya vyumba vinne na kuiboresha kwa kuweka chumba kimoja si umeibadili?”

Alisema Bunge hilo linatakiwa lisiingiliwe katika uamuzi wake.

Source: Mwananchi.

Bunge litaingiliwa tu ktk maamuzi yake kwa kura ya maoni.
 
Ukumbuke kuwa hata serikali imekuwa ikiwasilisha miswada ya sheria mbalimbali bungueni na siyo yote inayopitishwa, ipo inayofanyiwa marekebisho na ipo inayokataliwa kabisa. Usijifanye kuwa haujui uhusiano uliopo kati bunge na mihimili mingine mkuu. Unajitengenezea upofu usio wa lazima kawa sbabu tu una-personal interest fulani.

kuna tofauti kubwa kati ya uandaaji wa miswada ya serikali na hili la katiba mpya! kumbuka kuwa bunge huwakilisha maoni ya wananchi na hii huwa pale wananchi wenyewe hawawezi kupata fursa ya kutoa maoni yao,tofauti na sasa ambapo tayari wananchi wenyewe wametoa maoni yao kupitia tume ya mabadiliko!!!! Hivi wabunge watawezaje kutuwakilisha ili hali sisi wenyewe tumetoa maoni yetu?????
Bunge la katiba ni kwa ajili ya kurekebisha dosari ndogondogo tu na si kubadili maudhui ya rasimu ambayo kimsingi ndiyo maoni ya watz!
 
Back
Top Bottom