Nape: Kukosoa na kujikosoa ni silaha ya mapinduzi na kujiimarisha na si dalili ya udhaifu

Nape: Kukosoa na kujikosoa ni silaha ya mapinduzi na kujiimarisha na si dalili ya udhaifu

Hapo ndo napowakubali CCM,ni wepesi kumaliza tofauti zao. vizavizabina watabaki wanaumbuka mchana kweupe.
 
Kumkosoa marehemu siku ya tatu akiwa kaburini baada ya ripoti ya CAG kuweka hadharani? Lazima baadhi ya walio fanya hivyo watalipia gharama ya kisiasa ni suala la majira na nyakati tu.

Kanuni hiyo ya CCM ya kujikosoa na kujisahihisha haikuweka hapo ili wengine wajivue utu na kujivika uhayawani.
 
Huyu mjinga naye hana lolote.
Si vizuri kum label mtu mjinga...

Lakini chamsingi hapa ni kuwa wanasiasa waelewe kwamba hii ni experience ya kwanza kufiwa na Rais madarakani.

Naamini wanaelewa nini maana ya ilani ya chama na kwamba hatukuingia kwenye uchaguzi mpya....Sasa kuanza kulinganisha moja kwa moja awamu zote as if zinafanana na hizi hapana si sawa!

Hii awamu inaendeleza kazi iliyokuwa imeanza lakini haikukamilika. Kwahiyo kama ni kuitafsiri katiba aawasawa kwa minajili hiyo ya mgombea mwenza kuchukua nafasi ni ili kutopoteza mwelekeo wa ile ilani iliyopigiwa kura na wananchi ambayo ndiyo mkataba wa raia na chama kilichounda serikali.

Hili tusilikwepe...Na mgombea mwenza aliinadi ilani hii, kwahiyo 2025 raia watakihukumu chama kwa kuangalia ilani ya uchaguzi na siyo kiongozi aliyeiongoza...Huu ni mtego wapinzani wana utega ili wapate agenda ya kukishinda chama kwenye uchaguzi ujao.

Mh. Rais ametumia akili sana kuzima hizi njama kwakuanzisha salamu yake ya "kazi iendelee" very intelligent mama Keep it up!
 
Hapo ndo napowakubali CCM,ni wepesi kumaliza tofauti zao. vizavizabina watabaki wanaumbuka mchana kweupe.
Naona umesalimu amri kwa kichaka cha 'kuzika tofauti'. Ulikuwa unapigana na njemba ukakomaa, lilipoanza kukuelemea ukaanza kuhimiza maridhiano
 
Tunaelekea kuelewa yupi ni yupi yuleeee. Sidhani kuna mstaarabu anayekataa kukosoa kwa lengo la kusonga mbele. Issue ni namna ya ukosoaji na wakati wake. Mlikuwepo kwenye chama mlikwama wapi kukosoa?
Acting smart, kumbe wana ulterior motives...Hawa watu ni kuwa nao makini sana...Watu ambao wapo kama popo usiku mnyama mchana ndege hawafai kabisa...Hawa sidhani kama wataweza ku withstand temptations wakiaminiwa kwenye mambo ambayo ni mazito na yanahitaji kujitoa kwaajili ya taifa...Ni mbegu mbaya kwa vizazi vyetu, hawa hata kwenye dunia ya walioendelea are not trusted ndiyo maana utakuta tunapewa masharti magumu kwakua hatuna misimamo!
 



Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amesema kwa mujibu wa nyaraka za chama hicho tawala, kukosoa na kujikosoa ni silaha ya mapinduzi na kujiimarisha na si dalili ya udhaifu.

Nape ameyasema hayo leo Alhamisi Aprili 15, 2021 wakati akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya ofisi ya waziri mkuu na taasisi zake kwa mwaka 2021/22.

Amesema Rais wa awamu ya sita, Samia Suluhu Hassan ameanza vizuri na kutaka wananchi kumpa ushirikiano, “mzee Mwinyi (Ali Hassan- rais wa awamu ya pili) alituambia kila zama na kitabu chake.”

Amebainisha kuwa wamekuwa na vitabu vitano akirejea marais watano Julius Nyerere, Mwinyi, Benjamin Mkapa, Jakaya Kikwete na John Magufuli akisisitiza kuwa wito wake kwa viongozi, wabunge wenzake, wanachama wa CCM pamoja na Watanzania kumsaidia Samia kwa kumuunga mkono aandike kitabu cha awamu ya sita.

“Tusigombane bila sababu Tanzania ni yetu sote tumsaidie mama naye aandike kitabu chake tusimshike mkono kumwandikia kitabu tumwache aandike kitabu chake na ndugu zangu legacy (alama) haitetewi inajitetea yenyewe.”

“Hasa ile inayofanywa na mtu kama Magufuli itajitetea na kujisimamia miaka labda kama mtu ana mashaka na legacy yake lakini kama hamna mashaka na legacy yake itasikilizwa, itaongewa sisi watoto wajukuu na vitukuu kwa sababu haya waliyoyafanya watayakuta,” amesema.

Amesema sasa hivi hawana sababu ya kugombana na hawana sababu ya kutoana macho.

“Mimi nimekuwa kiongozi katika chama, nimesimamia idara ya maktaba na nyaraka duniani hakuna chama bora kilicho document vya kutosha CCM ni karibia namba moja kwa kila kitu,” amesema.

Amesema kwenye nyaraka zao wamesema kukosoa na kujikosoa ni silaha ya mapinduzi na kujiimarisha na sio dalili ya udhaifu.


Chanzo: Mwananchi

......ndugu zangu legacy (alama) haitetewi inajitetea yenyewe.

Maneno muhimu
 
Hivi huyu sio yule Nape aliyepewa msamaha?



Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amesema kwa mujibu wa nyaraka za chama hicho tawala, kukosoa na kujikosoa ni silaha ya mapinduzi na kujiimarisha na si dalili ya udhaifu.

Nape ameyasema hayo leo Alhamisi Aprili 15, 2021 wakati akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya ofisi ya waziri mkuu na taasisi zake kwa mwaka 2021/22.

Amesema Rais wa awamu ya sita, Samia Suluhu Hassan ameanza vizuri na kutaka wananchi kumpa ushirikiano, “mzee Mwinyi (Ali Hassan- rais wa awamu ya pili) alituambia kila zama na kitabu chake.”

Amebainisha kuwa wamekuwa na vitabu vitano akirejea marais watano Julius Nyerere, Mwinyi, Benjamin Mkapa, Jakaya Kikwete na John Magufuli akisisitiza kuwa wito wake kwa viongozi, wabunge wenzake, wanachama wa CCM pamoja na Watanzania kumsaidia Samia kwa kumuunga mkono aandike kitabu cha awamu ya sita.

“Tusigombane bila sababu Tanzania ni yetu sote tumsaidie mama naye aandike kitabu chake tusimshike mkono kumwandikia kitabu tumwache aandike kitabu chake na ndugu zangu legacy (alama) haitetewi inajitetea yenyewe.”

“Hasa ile inayofanywa na mtu kama Magufuli itajitetea na kujisimamia miaka labda kama mtu ana mashaka na legacy yake lakini kama hamna mashaka na legacy yake itasikilizwa, itaongewa sisi watoto wajukuu na vitukuu kwa sababu haya waliyoyafanya watayakuta,” amesema.

Amesema sasa hivi hawana sababu ya kugombana na hawana sababu ya kutoana macho.

“Mimi nimekuwa kiongozi katika chama, nimesimamia idara ya maktaba na nyaraka duniani hakuna chama bora kilicho document vya kutosha CCM ni karibia namba moja kwa kila kitu,” amesema.

Amesema kwenye nyaraka zao wamesema kukosoa na kujikosoa ni silaha ya mapinduzi na kujiimarisha na sio dalili ya udhaifu.


Chanzo: Mwananchi
 
Back
Top Bottom