Nape: Kukosoa na kujikosoa ni silaha ya mapinduzi na kujiimarisha na si dalili ya udhaifu

Nape: Kukosoa na kujikosoa ni silaha ya mapinduzi na kujiimarisha na si dalili ya udhaifu

Kama mtu alikuwa dhalimu, na kufanya mauji, kuwabambikia kesi, kuhujumu shughuli zao wote wanamkosoa, unataka mbwembwe gani za kumkosoa? Anayetawala kidhalimu, anakosolewa bila kubembelezwa.
Shida ya MATAGA, hayataki kuamini kama zama za meko, zimekwisha, wanafikilia kuwa labda ni kama vile anaumwa hivyo mama samia amemshikia tu!!!kwa hiyo hana uwezo wa kufanya anayotaka yeye!ili mwenyewe aje aendelee tena!!!ila yataelewa tu.
 
Hawa watu huwa system ikiwatekeleza ndio akili zinawarudi.Mtu ambaye akili haijawahi kurudi hata akitelekezwa ni Bwana Lameck Madelu tu.Huyu ni bingwa wa kulamba miguu,nafikiri anayo PhD ya kulamba miguu 🤣
Huyu amelaaniwa
 



Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amesema kwa mujibu wa nyaraka za chama hicho tawala, kukosoa na kujikosoa ni silaha ya mapinduzi na kujiimarisha na si dalili ya udhaifu.

Nape ameyasema hayo leo Alhamisi Aprili 15, 2021 wakati akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya ofisi ya waziri mkuu na taasisi zake kwa mwaka 2021/22.

Amesema Rais wa awamu ya sita, Samia Suluhu Hassan ameanza vizuri na kutaka wananchi kumpa ushirikiano, “mzee Mwinyi (Ali Hassan- rais wa awamu ya pili) alituambia kila zama na kitabu chake.”

Amebainisha kuwa wamekuwa na vitabu vitano akirejea marais watano Julius Nyerere, Mwinyi, Benjamin Mkapa, Jakaya Kikwete na John Magufuli akisisitiza kuwa wito wake kwa viongozi, wabunge wenzake, wanachama wa CCM pamoja na Watanzania kumsaidia Samia kwa kumuunga mkono aandike kitabu cha awamu ya sita.

“Tusigombane bila sababu Tanzania ni yetu sote tumsaidie mama naye aandike kitabu chake tusimshike mkono kumwandikia kitabu tumwache aandike kitabu chake na ndugu zangu legacy (alama) haitetewi inajitetea yenyewe.”

“Hasa ile inayofanywa na mtu kama Magufuli itajitetea na kujisimamia miaka labda kama mtu ana mashaka na legacy yake lakini kama hamna mashaka na legacy yake itasikilizwa, itaongewa sisi watoto wajukuu na vitukuu kwa sababu haya waliyoyafanya watayakuta,” amesema.

Amesema sasa hivi hawana sababu ya kugombana na hawana sababu ya kutoana macho.

“Mimi nimekuwa kiongozi katika chama, nimesimamia idara ya maktaba na nyaraka duniani hakuna chama bora kilicho document vya kutosha CCM ni karibia namba moja kwa kila kitu,” amesema.

Amesema kwenye nyaraka zao wamesema kukosoa na kujikosoa ni silaha ya mapinduzi na kujiimarisha na sio dalili ya udhaifu.


Chanzo: Mwananchi


Na kukusolewa
 
citizensindevelopment18 usijifanye uko nje ya Tanzania. Magufuli alikuwa anaua, anateka, na alikuwa anaweza kukutafutia kesi isiyo na dhamana kwa issue ya kumkosoa tu.

Kwa hiyo ulidhani akina Nape hawajui kilichompata Ben Saanane, Tundu Lissu na RomaMkatoliki?
Hata yeye mwenyewe alipojaribu kupinga mambo ya bashite nadhani hakuna asiyejua kilimtokea nini. Kuna watu wanaongea kama vile kipindi cha nyuma walikuwa wamezimia ndo wamezinduka baada ya mwendazake kwenda
 



Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amesema kwa mujibu wa nyaraka za chama hicho tawala, kukosoa na kujikosoa ni silaha ya mapinduzi na kujiimarisha na si dalili ya udhaifu.

Nape ameyasema hayo leo Alhamisi Aprili 15, 2021 wakati akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya ofisi ya waziri mkuu na taasisi zake kwa mwaka 2021/22.

Amesema Rais wa awamu ya sita, Samia Suluhu Hassan ameanza vizuri na kutaka wananchi kumpa ushirikiano, “mzee Mwinyi (Ali Hassan- rais wa awamu ya pili) alituambia kila zama na kitabu chake.”

Amebainisha kuwa wamekuwa na vitabu vitano akirejea marais watano Julius Nyerere, Mwinyi, Benjamin Mkapa, Jakaya Kikwete na John Magufuli akisisitiza kuwa wito wake kwa viongozi, wabunge wenzake, wanachama wa CCM pamoja na Watanzania kumsaidia Samia kwa kumuunga mkono aandike kitabu cha awamu ya sita.

“Tusigombane bila sababu Tanzania ni yetu sote tumsaidie mama naye aandike kitabu chake tusimshike mkono kumwandikia kitabu tumwache aandike kitabu chake na ndugu zangu legacy (alama) haitetewi inajitetea yenyewe.”

“Hasa ile inayofanywa na mtu kama Magufuli itajitetea na kujisimamia miaka labda kama mtu ana mashaka na legacy yake lakini kama hamna mashaka na legacy yake itasikilizwa, itaongewa sisi watoto wajukuu na vitukuu kwa sababu haya waliyoyafanya watayakuta,” amesema.

Amesema sasa hivi hawana sababu ya kugombana na hawana sababu ya kutoana macho.

“Mimi nimekuwa kiongozi katika chama, nimesimamia idara ya maktaba na nyaraka duniani hakuna chama bora kilicho document vya kutosha CCM ni karibia namba moja kwa kila kitu,” amesema.

Amesema kwenye nyaraka zao wamesema kukosoa na kujikosoa ni silaha ya mapinduzi na kujiimarisha na sio dalili ya udhaifu.


Chanzo: Mwananchi

Hivi nani alikuwa anapigia debe bao la mkono? Tuachane na hayo mwambie kama ana namba ya Kigogo2014 anitumie
 
Kama vile ya Nyerere wala haina mjadala lakini hii ya kulazimisha ya Mwendazake inatumia nguvu nyingi sana.

Maana hata shughuli zilizoamzishwa na JK na yeye kumalizia wanazihesabu ni legacy yake
Wala hakuna chochote kipya, labda kuiharibu tu nchi yetu, kitaifa na kimataifa kwa kauli tata!
 
Alianza Makamba kutandika jamvi la ukosoaji au kwa maneno mengine kusafisha njia, leo Nape na wengine watakuja kupita mulemule. Hiki ndo kizazi cha awamu ya 4. Kwa mujibu wa katiba yetu Rais Samia anao uchaguzi, ingawa ni mwembamba, wa kwenda na kizazi cha awamu ya 4 au 5. Ila awamu tano imefanya mambo iliyo yapigia debe vizuri na kuyaona kwa sasa uambiwi tazama la hasha.
 
Wanaojirudi kwa sasa na kukubali ukweli hata Mungu anawasemehe ubaya ni wale wanaoendelea kulazimisha mabaya kua ni mema.

Nimeelewa Legacy inajitetea kwa nini kutumia nguvu nyingi kuitetea ya awamu iliyokomea njiani?
Kila zama na kitabu chake yes.

Tukubali siku tutakua na Ilani ya Taifa na siyo ya chama ndipo tutasonga mbele kama taifa.
 
Back
Top Bottom