Nape Nnauye: Anaachwaje kichaa mmoja hivi anasema ‘Mama hatukuelewi’?

Nape Nnauye: Anaachwaje kichaa mmoja hivi anasema ‘Mama hatukuelewi’?

I am Groot

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2018
Posts
3,929
Reaction score
10,747
"Tulifungia vyombo vya habari, tumevifungulia bila masharti, je hawamuelewi mama? Wafanyakazi wa Umma walikaa miaka mingapi bila kupandishiwa mshahara? Mama juzi kasema jambo lenu lipo, halafu anakuja mtu anasema mtaani watu hawamwelewi mama?"

~Nape Nnauye

----

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amezungumza kuhusu kauli ya ‘mama hatukuelewi’ ambayo anadai kuna watu wamekuwa wakiitumia wakimaanisha hawamuelewi Rais Samia Suluhu.

Huyu hapa Nape akizungumza katika Ufunguzi wa Kikao cha 17 cha Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano wa Serikali, Mei 9, 2022 Jijini Tanga katika Ukumbi wa Hoteli ya Regal Naivera:

“Mtu mmoja nimeona amerekodi video anasema ‘Mama huku mtaani watu hawakuelewi’, inawezekana wapo kweli ambao hawamuelewi, lakini nikajiuliza wale waliofukuzwa kwa vyeti feki wamerudishwa kazini.

“Watoto waliofukuzwa kwa ujauzito na walioacha shule kwa sababu mbalimbali wameruhusiwa kurudi shule.

“Kuna watu wamefunguliwa akaunti za biashara zilifungwa kwa sababu mbalimbali, bado unasema watu hawamuelewi, lakini kwa sababu hajibiwi inaonekana ni kama kweli watu hawamuelewi.

“Nilikuwa Karatu wakati nakagua mradi wa Anwani za makazi, wakaniambia kuna wakati ulikuwa ukitoka Karatu kwenda Arusha hukutani na magari ya watalii, lakini sasa hivi yanapishana tu magari ya utalii.

“Tumefungua vyombo vya habari bila masharti, wafanyakazi wa Serikalini walikaa miaka mingapi bia kupandishiwa mshahara, mama ameshasema jambo lenu lipo, hao nao hawamuelewi mama?

“Anaachwaje mtu kichaa mmoja hivi anasema ‘unajua huku hawakuelewi’, nawapa changamoto maofisa habari, unapokuwa afisa habari wewe ni katibu Mwenezi wa Serikali, wajibu wako ni kuwafanya wananchi waielewe Serikali.”

Chanzo: Maelezo
 
"Tulifungia vyombo vya habari, tumevifungulia bila masharti, je hawamuelewi mama?,
wafanyakazi wa Umma walikaa miaka mingapi bila kupandishiwa mshahara?,mama juzi kasema jambo lenu lipo, halafu anakuja mtu anasema mtaani watu hawamwelewi mama?"

~Nape Nnauye
Sasa ana mlilia nani huyo kipara
 
"Tulifungia vyombo vya habari, tumevifungulia bila masharti, je hawamuelewi mama?,
wafanyakazi wa Umma walikaa miaka mingapi bila kupandishiwa mshahara?,mama juzi kasema jambo lenu lipo, halafu anakuja mtu anasema mtaani watu hawamwelewi mama?"

~Nape Nnauye

Kusema na kutenda ni vitu viwili mbali mbali wewe chawa!! Kwani alipotoa ahadi hakujua kuwa wafanyakazi kwa kawaida hizo kauli za kuongezwa mishahara hutolewa tarehe moja Mei? Lipo mpaka lini wakati matatizo chungu nzima yamemuandama huku hajui afanye nini na UCHUMI unaelekea kwenye RECESSION! Nadhani hivi sasa atakuwa anapanga safari kukimbia kuwajibika!!
 
"Tulifungia vyombo vya habari, tumevifungulia bila masharti, je hawamuelewi mama?,
wafanyakazi wa Umma walikaa miaka mingapi bila kupandishiwa mshahara?,mama juzi kasema jambo lenu lipo, halafu anakuja mtu anasema mtaani watu hawamwelewi mama?"

~Nape Nnauye
Wanaolalamika wengi "A bunch of useless misukule, toxic people na wafuasi wa wanasiasa na wanaharakati"

Hakuna mtu mwenye akili timamu analalamika sana
 

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amezungumza kuhusu kauli ya ‘mama hatukuelewi’ ambayo anadai kuna watu wamekuwa wakiitumia wakimaanisha hawamuelewi Rais Samia Suluhu.

Huyu hapa Nape akizungumza katika Ufunguzi wa Kikao cha 17 cha Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano wa Serikali, Mei 9, 2022 Jijini Tanga katika Ukumbi wa Hoteli ya Regal Naivera:

“Mtu mmoja nimeona amerekodi video anasema ‘Mama huku mtaani watu hawakuelewi’, inawezekana wapo kweli ambao hawamuelewi, lakini nikajiuliza wale waliofukuzwa kwa vyeti feki wamerudishwa kazini.

“Watoto waliofukuzwa kwa ujauzito na walioacha shule kwa sababu mbalimbali wameruhusiwa kurudi shule.

“Kuna watu wamefunguliwa akaunti za biashara zilifungwa kwa sababu mbalimbali, bado unasema watu hawamuelewi, lakini kwa sababu hajibiwi inaonekana ni kama kweli watu hawamuelewi.

“Nilikuwa Karatu wakati nakagua mradi wa Anwani za makazi, wakaniambia kuna wakati ulikuwa ukitoka Karatu kwenda Arusha hukutani na magari ya watalii, lakini sasa hivi yanapishana tu magari ya utalii.

“Tumefungua vyombo vya habari bila masharti, wafanyakazi wa Serikalini walikaa miaka mingapi bia kupandishiwa mshahara, mama ameshasema jambo lenu lipo, hao nao hawamuelewi mama?

“Anaachwaje mtu kichaa mmoja hivi anasema ‘unajua huku hawakuelewi’, nawapa changamoto maofisa habari, unapokuwa afisa habari wewe ni katibu Mwenezi wa Serikali, wajibu wako ni kuwafanya wananchi waielewe Serikali.”

Chanzo: Maelezo
 
Maafisa habari wafanye kazi yao, Kuna YouTube channel ya manispaa ya kigamboni, Ina miaka haina taarifa mpya, wasifanye kazi kwa mazoea, waisemee serikali, na pia wawekewe vigezo vya kupimwa, ni mara ngapi wametoka makala YouTube? Instagram au Facebook kwa kuendana na malengo ya serikali
 
Halmashauri ya wilaya, mji mdogo, mji au manispaa na jiji hazina akaunti youtube, facebook pages au instagram pages hao maofisa habari updates za kazi za serikali wanawapaje wananchi wao au wapowapo tu
 
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amezungumza kuhusu kauli ya ‘mama hatukuelewi’ ambayo anadai kuna watu wamekuwa wakiitumia wakimaanisha hawamuelewi Rais Samia Suluhu...
Nape ukichaa upi? Unataka wampoteze? Nape....
 
Back
Top Bottom