Nape Nnauye atishishiwa Bastola na kusukumizwa kwenye gari

Nape Nnauye atishishiwa Bastola na kusukumizwa kwenye gari

Mwalim KASHASHA hii red card ya NAPE unaizungumziaje?

Asante JESE JOHN hii card ya nape ni kama ya kujitakia mwenyewe na pia naweza kusema ni ya kizembe na ameigharimu timu yake.

Mwanzoni ilionekana nape ni mchezaji msumbufu alikuwa anashambulia sana na amekosa nafasi nyingi za wazi za kumfunga makonda.tatizo kubwa alilonalo nape alikuwa anashambulia alaf anasahau kurudi nyuma haraka kuzuia.
Alaf kuna muda kama alikuwa anacheza na jukwaa na pia kama alitaka kuwafurahisha wapinzan badala ya kocha wake.alikuwa hafuati maelezo ya kocha kwasababu alijiona ni profeshno.

Sasa makonda alivyoona kuwa nape anashambulia sana lango lake akawa anacheza kwa timing kwanza akawa anatuliza mashambulizi ya nape nakuanzisha long pass ambazo zilifanikiwa japo sio sana.
Akaamua kuanzisha kazi moja tu nayo nikucheza eneo la nape na kumkera kera tu kwa vile alijua nape ni mtu wa hasira kwa hiyo akimchokoza lazma nape atapaniki na akipaniki refa tafanya kazi yake.
ndipo makonda akaamua kumchokoza chokoza nape kama vile materaz kwa zidane.

Nape alishindwa kuvumilia ndipo akarusha teke ambalo limemgharimu na refa amempa kadi ya moja kwa moja.huu ni uzembe wa wachezaji wetu alishindwa kujifunza kwa mwakyembe.

Mm nasema hii ni kadi ya kizembe sana.
Na ile timu itabaki kuwa teja kwa ccm kwasababu hata 2015 yule kocha wao alisema tusipoitoa ccm madarakani mwaka huu hatutaitoa tena milele.
Kwa hyo hapo sion njia yoyote ya kuwatoa hawa ccm kwenye michuano hii.

Kwako jese john
 
Hakuna pa kuhemea, ukiingia huku ni Bunduki, ukitokea huku ni Bunduki. Yan ni mabunduki tu daahhh.. Juzi tu bunduki zimeingia studio, Leo zimeingia mkutanoni. Yan daaahh
 
Wangeliabgushia mvua ya mawe tu na kupondaponda kichwa chake ndio angekoma kuringa na kipisto uchwaara chake. Ma....ina zake
 
Hao wachache kama wakifahamika kwa majina ni vyema kuwaanika hadharani ili wachukuliwe hatua za kinidhamu kuinusuru taasisi hiyo nyeti
 
..hii ni ndani ya wiki sasa watu wanatishiwa na bunduki na vyombo vya usalama.....hapa ndipo tumefika kama nchi....yani imefikia hata waziri anatolewa bastola!...je mlalahoi wa mtaani inakuwaje?....kama mtu wa usalama anaweza kutumia silaha yake namna hii je ni askari kiasi gani wanawafanyizia ubaya raia huko mitaani??
...tukio hili likiachwa lipite nitasngaa sana sana....
 
Yaani hii mijitu ni ya hovyo kishenzi. Majambazi, wezi wa kutumia silaha matapeli ni hayahaya. Ht aibu hayana
Sidhani kama ameambiwa nenda kamvute kwa kutumia nguvu.
Maaskari wengi bongo badala ya kuanza na diplomacy wakakwambia vizuri tu uende, wanaanza na nguvu kwanza, ambaye halijui hili basi hajawahi kukamatwa.
 
Kitendo cha kutishia kuua kwa bastola kilichotaka kufanywa na kijana mmoja ambaye mimi siamini kama ni sehemu ya usalana wa Taifa ni muendelezo wa matumizi ya nguvu bila kutumia sheria ulioasisiwa na Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam Paulo Makonda. Pamoja na ufinyu wangu juu ya uelewa wa sheria hicho kitendo ni kinyume cha sheria na hakikubaliki katika jamii ya kitanzania.

Baada ya kuona Video za matumizi ya nguvu za Paulo Makonda dhidi ya Clouds Media, tupo tuliosema kuwa kuachwa kwa kitendo hicho ni kitu cha hatari sana kwa Taifa kwani kitaset precedence kwa mamlaka zetu kuanza kawaida ya kutumia nguvu kama tulivyoona kwenye tukio la Nape. Ni matumaini yetu watanzania huyo kijana atakamatwa na kupelekwa mahakamani na apewe haki yake ili kutoa fundisho kwa wengine. Kama kijana huyo ataachwa, basi tujiandae na taifa la matumizi ya vyombo vya moto na solaha nyingine.

Aidha, kitendo hicho (kama aliyekifanya ni sehemu ya usalama wa Taifa) pia kinatoa taswira nyingine kwamba kumbe tatizo la nchi lipo kwenye Idara hii. Wengi tuko matarajio kwamba Idara hii ipo imara, haiyumbi na miongoni mwa najukumu yake ni kuhakikisha taifa linakuwa salama kwa kuweza kufanya forecasting ya mambo yote yatakayoondoa amani na usalama wa nchi yetu. Kwa kifupi kama nchi tuko katika kizaizai kikubwa sana kwani tumaini pekee sasa ni kwa ndugu zetu wa "mabakamabaka".

Tanzania ni kubwa kuliko yeyote, Tanzania ni kubwa kuliko Rais. Tungependa kuona Katiba inafuatwa, inalindwa na inatekelezwa. Haki na Ulinzi wa anaoupata Rais unatokana na Katiba, hivyo iwapo katiba haiheshimiwi, hakuna maana kwa vyombo vyetu kuwalinda wenye kuhatarisha umoja wa Taifa letu ambalo limekuwa kisiwa cha amani katika eneo hili la maziwa makuu.

Nimalizie kwa kutoa rai kwa bunge letu tukufu. Bunge ndio mamlaka pekee inayosimamia serikali. Yatosha kujifunza kwamba mbaya hana rafiki. Fanyeni kazi yenu ya kuisimamia na kuiwajibisha serikali. Sababu mnayo, Uwezo mnao, nguvu mnayo, watanzania wapo nyuma yenu, kilichobaki ni nia thabiti kwenu. Hakuna mtanzania mjinga atakayekataa "kuwarudisha tena mjengoni" iwapo mtafanya maamuzi yenye kulinda hadhi ya Tanzania. Msije kusema watanzania hatukuwaambia.

Mungu Ibariki Tanzania.
 
Mtambo Wa kuzalisha hofu! Aibu! Aibu! Aibu! Kuingia na bunduku kwa watu ambao hawana hata kirungu!! Huo ni woga!! Tena ni woga Wa kukimbia kivuli chako mwenyewe!
 
  • Thanks
Reactions: MTK
maulidi kitenge alijitahidi..kusema askari yule atumie busara
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Km waziri na mwanasiasa mkubwa kafanyiwa hivi je sisi tuonashinda kwenye keyboard za computer na smartphone???

Nilidhani movie Ile silaha alivyoonyeshwa dah..
 
hivi bwana yule anawadudu gani bichwani!!!!!huu woga umepitiliza sasa,utafikiri harmorapa
 
Back
Top Bottom