Nape Nnauye atishishiwa Bastola na kusukumizwa kwenye gari

Nape Nnauye atishishiwa Bastola na kusukumizwa kwenye gari

Dah!

Mimi si mpenzi wa CCM na si shabiki wa Nape ila hicho nilichokiona kwenye hiyo video sijakifurahia.

Kwangu haki ni haki tu.

Ni nini hasa kilipelekea yote hayo?

Kuna anayejua humu anieleweshe zaidi?
Ni kweli ulichokisema.

Lakini mwanausalama alikuwa 'calm' tena aliongea kwa upole 'Mheshimiwa rudi kwenye gari..', Wakati huo Mh. Nape akiwa amevaa shati bila kuchomekea na ameweka mikono yote mifukoni (kulia na kushoto); baadaye anasikika (Nape) akimwambia mwana usalama " ....usinishike hivyo Bwana, ondoka" wakati huo anamsukuma mwanausalama kwa mkono wa kushoto lakini mkono wake wa kulia ukiwa bado humo mfukoni; kwa akili za kawaida...askari lazima ajihami maana huo mkono wakulia wa Nape ambao umo mfukoni hajui umeshika nini. Na hata Nape alivyosukumwa sukumwa hakutoa mkono huo wa kulia mpaka (labda) alipohakikisha kuwa sasa mfuko wa kulia wa suruali lake umezibwa na gari ndipo alipotoa mkono mfukoni. Na watu wakaongezeka pale...!

Naliona hivyo tukio hili. Lakini maelezo mazuri anaweza kuyatoa mwanausalama mwenyewe kwa nini alifanya vile.
 
Tunapotaka Jeshi la Polisi liboreshwe na liachane na kasumba za mkoloni tunataka kuepukana na ubabaishaji kama huu wa kuamrisha kufanya kitu hata kama hakina msingi wa kisheria. Kuna wapuuzi wanadhani hili jeshi ni poa tu maana linashughulikia zaidi wapinzani(Lissu na Lema), lakini upuuzi huu unajengeka ndani ya jeshi na matokeo yake watakaoumia zaidi ni wanyonge ambao hata elfu tano ya kumhonga askari amuachie hana.

Haya mambo hayana mwenyewe. Hata rais anaweza kuwa victim wa jeshi kama hili-maana kuna kustaafu. Kuna ndugu na jamaa ambao wanaweza wakaangukia ktk mikono ya jeshi hili babaishaji. Hata askari wenyewe hawako salama ndani ya jeshi hili. Fikiria mtu anakutuma wewe askari ukaue wakati yeye amekaa na mke wake nyumbani. Kumbuka unaua mtu-sio kuku na hivyo damu ya mtu huyo inakuandama maisha yako yote. Mshahara mnaopata enyi askari hautoshi kuua raia wema wanaotumia haki yao ya kikatiba kuwa na mawazo tofauti na watawala.
Soma post # 423 ya uzi huu.
 
Hili genge lote ni waandishi wa habari? au na vibaka walikuwemo? kweli ipo haja ya kuifanyia mabadiliko taaluma ya uandishi wa habari imekuwa ya kihuni mno.
 
Ni kweli ulichokisema.

Lakini mwanausalama alikuwa 'calm' tena aliongea kwa upole 'Mheshimiwa rudi kwenye gari..', Wakati huo Mh. Nape akiwa amevaa shati bila kuchomekea na ameweka mikono yote mifukoni (kulia na kushoto); baadaye anasikika (Nape) akimwambia mwana usalama " ....usinishike hivyo Bwana, ondoka" wakati huo anamsukuma mwanausalama kwa mkono wa kushoto lakini mkono wake wa kulia ukiwa bado humo mfukoni; kwa akili za kawaida...askari lazima ajihami maana huo mkono wakulia wa Nape ambao umo mfukoni hajui umeshika nini. Na hata Nape alivyosukumwa sukumwa hakutoa mkono huo wa kulia mpaka (labda) alipohakikisha kuwa sasa mfuko wa kulia wa suruali lake umezibwa na gari ndipo alipotoa mkono mfukoni. Na watu wakaongezeka pale...!

Naliona hivyo tukio hili. Lakini maelezo mazuri anaweza kuyatoa mwanausalama mwenyewe kwa nini alifanaya vile.

Kwa kweli sidhani kama macho na masikio yangu yamenidanganya hapo.

Nape hakuwa belligerent hata kidogo.

Na huyo jamaa, whatever he is, hakuwa kabisa na sababu kutoa silaha yake na kumtishia Nape.

Halafu, hivi kosa la Nape hapo lilikuwa ni lipi hasa?

Kuongea na watu/ waandishi wa habari imekuwa kosa siku hizi?

Utadhani tupo North Korea!
 
Habar za usiku wazee.
Tukiunganisha matukio yanayoendelea kutokea nchini kwetu na ukiyatafakari kwa kina unashindwa kupata majibu yakukufanya uone mambo yapo sawa.
Sijui kuna nini
Ila lazima kutakua na kitu ambacho tunatakiwa kujua jama raia.
Tuvute subra tuone kesho Mh.Rais atazungumza nini kuweka sawa hii hali iliyopo
 
ameitia aibu tasinia husika

hasira za nini bila kutumia akili? anataka kuua mbele ya kamera? it was suppose to be professional

duh kumbe wahuni vile..........

ninaimani hawajatoka nyumba nyeupe wale jamaa (Nyumba nyeupe takatifu)

mungu mbaliki raisi wetu
 

Attachments

Wapuuzi fulani wale waliomtetea bashite kwenda kwenye kituo fulani na armed gang watakuambia hakutolewa bastola [emoji849][emoji849][emoji849]
 
Ha ha ha
ni muendelezo wa kauli za kibabe tu.
Kingine ni kusisitiza makondo piga kazi
 
Ni aibu kwa taaluma nzima ya usalama,kwa mwanausalama kumvamia kiongozi bila ya kujitambulisha na kuonyesha kitambulisho na kuanza kumtisha kwa bastola ili atii amri yako.
Nakushauri kamanda Sirro umrudishe uyu kijana akasome vizuri sheria za usalama kuliko kulitia aibu jeshi la polisi.

😀😀😀

nimefurahi sana maake harmorapa haya ndiyo magape yake
 
ee76cfe2e6aa97ef8027c12102bbbf3b.jpg

Onyo na hatua kali za kinidhamu na za kisheria zichukuliwe dhidi ya askari aliyemtishia Nape kwa bastola.
Onyo la nini?.....unadhani huwa wanabeba kama mapambo...kwa taarifa yako hakuna silaha inayotengenezwa kwa ajili ya mnyama huwa ni kwa ajili ya binadamu!
 
Ni kweli ulichokisema.

Lakini mwanausalama alikuwa 'calm' tena aliongea kwa upole 'Mheshimiwa rudi kwenye gari..', Wakati huo Mh. Nape akiwa amevaa shati bila kuchomekea na ameweka mikono yote mifukoni (kulia na kushoto); baadaye anasikika (Nape) akimwambia mwana usalama " ....usinishike hivyo Bwana, ondoka" wakati huo anamsukuma mwanausalama kwa mkono wa kushoto lakini mkono wake wa kulia ukiwa bado humo mfukoni; kwa akili za kawaida...askari lazima ajihami maana huo mkono wakulia wa Nape ambao umo mfukoni hajui umeshika nini. Na hata Nape alivyosukumwa sukumwa hakutoa mkono huo wa kulia mpaka (labda) alipohakikisha kuwa sasa mfuko wa kulia wa suruali lake umezibwa na gari ndipo alipotoa mkono mfukoni. Na watu wakaongezeka pale...!

Naliona hivyo tukio hili. Lakini maelezo mazuri anaweza kuyatoa mwanausalama mwenyewe kwa nini alifanya vile.[/Q

Kwa akili ya kawaida waziri aliyesimamishwa kazi masaa 24 yaliyopita ameitisha press atoe bastola ampige mtu/mwana usalama?never Nape hawezi kufanya hivyo,kiongozi wa serikali akishampiga risasi na yeye maarufu unadhani ujinga huo anaweza kuufanya ,pale mwana usalama anajua kabisa hawezi kudhuriwa hata na kiwembe na nape ,mwana usalama alipoona nape mbishi na yeye kapewa kazi nape asizungumze akaamua atumie nguvu na vitisho ili kiongozi huyo a-surrende

Nape alivyoshikwa alimuuliza kitambulisho kipo wapi ndipo yule mwana usalama akatoa bastola ,

Maneno ya usinishike toka bwana ni pale alipokuwa amesukumizwa hatua chache kwenda kwenye gari..mkuu umechakachua Maelezo ya tukio

Mwana usalama hakuwa threatened na nape na hata wenzake hawakuwa na wasiwasi wowote ule waliokuwa wakimshinikiza nape aingie kwenye gari
 
.....

Maneno ya usinishike toka bwana ni pale alipokuwa amesukumizwa hatua chache kwenda kwenye gari..mkuu umechakachua Maelezo ya tukio

....
Nimeitaza iyo clip mara ishirini na saba....ndiyo nikatoa maelezo hayo hapo juu. ebu angalia vizuri hiyo clip mwanzoni mwana usalama anaamfuata Nape mpaka hatua ya askari kuamua kujihami.
 
Hawa maaskari tumesoma nao vichwani hamna kitu eti ndo wanapewa silaha watulinde duuuh fafafafaa tu hawa
 
Back
Top Bottom