Nape Nnauye kama January Makamba, maji ya shingo yamfika. Amuangukia Rais Magufuli baada ya kumnanga

Nape Nnauye kama January Makamba, maji ya shingo yamfika. Amuangukia Rais Magufuli baada ya kumnanga

Hwkima nzuri,hwshima nzuri.Rais wangu mungu akutunze Sana.
 
Hongera sana kwa MH. Rais Magufuli, nampongeza sana yeye kwa huruma yake, angeweza mpuuzia lkn amemridhia na kumsamehe.
 
Ndogo ndogo za kitaa zinadai Bugiri ndiye aliyemualika Nape Ikulu.

Magu anamuhitaji Nape kwasababu anahitaji kura za watu wa kusini, na Nape nae anamuhitaji Magu ili ajiweke katika nafasi nzuri ya jina lake kupita kama mgombea 2020.

In short,kila mtu hapo anamuhitaji mwingine kuelekea 2020.

Ni kweli tunajua CCM hawategemei sanduku la kura kushinda, ila ni ukweli pia wangependa zaidi washinde kupitia sanduku la kura.
 
Mbunge wa Mtama Nape Nnauye amefika Ikulu jijini Dar Es Salaam kwa ajili ya kuomba msamaha. Ameomba msamaha na kusamehewa kosa aliliofanya miezi michache iliyopita.


Akizungumza akiwa nje ya Ikulu baada ya kuzungumza na Rais Magufuli, Nape Nnauye amesema "Kwanza nimekuja kumuona baba yangu lakini Mwenyekiti wa Chama changu, Rais wangu kwasababu wote mnajua mambo yaliyopita au kutokea hapo katikati na mimi kama mtoto wa CCM, kama mwanae, nimeona ni vizuri nije niongee na Baba yangu.

Nashukuru kwamba amenipa fursa ya kuja kumuona na ameniambia amenisamehe na amenipa ushauri na kwakweli kwa dhati ya moyo wangu nishukuru sana amenipa fursa kubwa sana."



Mbunge Nape anaendelea kusema "Kwa kweli Muheshimiwa Rais kama Baba yangu, kama mzazi wangu nashukuru sana kwa fursa uliyonipa kwa kunisikiliza, kwa kunisamehe, kunishauri, kunielekeza nifanye nini huko mbele ninapokenda."

Rais Magufuli amesma "Mimi nimeshamsamehe kwa dhati Nape, amekuwa akiandika 'message' nyingi sana za kuomba msamaha hata saa nane za usiku nimemuona huyu mtu akiomba msamaha'"

"Leo ameniomba hapa aje anione na kabla, amejaribu sana, ameenda kwa Mzee Mangula amefika hadi kwa Mzee Opson na Mama Nyerere, amehangaika kweli. Na kwamba sisi tumeumbwa kusamehe, na wewe umemuona asubuhi amekuja hapa nikasema siwezi kumzuia kumuona ngoja nimuone kwanza japo nilikuwa na kikao kingine na kikubwa"
ameongeza Rais Magufuli

"Anachozungumza ni kwamba naomba Baba unisamehe, najua kusamehe kunaumiza lakini nasema kwa dhati kabisa nimemsamehe kabisa na anaeleza yaliyokuwa yanamsibu na baadhi ya watu waliokuwa wanamrubuni. Wengine wapo kwenye chama lakini nasema yote tumesamehe kwa sababu bado ni kijana mdogo na ana 'future' nzuri kwenye maisha yake."

"Nikiendelea kumshikilia kwenye moyo wangu, kwanza ni dhambi kubwa kwa mwenyezi Mungu na imeandikwa tusamehe saba mara sabini na Mungu amtangulie katika shughuli zake, akalee mke wake na familia yake, akakitumikie chama na akawatumikie wananchi wa jimbo lake."
Amemalizia Rais Magufuli

Wakimalizia katika maongezi yao nje ya Ikulu, Rais Magufuli alimuuliza Nape "Kwa hiyo ulikuwa huna amani?"

Nape: Sana

Rais Magufuli: Uwe na amani na Mungu akusaidie

Pia soma;
Eti kuna watu ndani ya JF walishabikia misimamo ya watu hawa. Uzembe wao ukageuzwa kuwa ushujaa. wakawa ni kigezo cha ubora wa rais. Kwa ujumla kama kawaida yangu, nawakumbusha, kuweni makini na wanasiasa wetu ambao wengi ubora wao uko chini.

Baada ya kuwa na viwango duni vya wanasiasa kwa miaka zaidi ya 20, tunashindwa kuvumilia au kuelewa uwezo mkubwa wa rais. Hawa watu hawana pa kwenda nje ya siasa. Bado wale wapiga kelele wa upinzani ambao nao ni kama vijana wa foolish age.
 
Ndogo ndogo za kitaa zinadai Bugiri ndiye aliyemualika Nape Ikulu.
Boss, hebu rudia kusoma msg zako juu ya sifa ulizomwaga kwa Nape ukiamini ni shujaa. Hata kama kaitwa je, yuko kiwango cha chini kiasi cha kuambiwa maneno ya kubembeleza? Kama wasemavyo waingereza, ukitaka kujua wewe ni nani, angalia unaowaunga mkono walivyo.
 
Magu anamuhitaji Nape kwasababu anahitaji kura za watu wa kusini, na Nape nae anamuhitaji Magu ili ajiweke katika nafasi nzuri ya jina lake kupita kama mgombea 2020.

In short,kila mtu hapo anamuhitaji mwingine kuelekea 2020.

Ni kweli tunajua CCM hawategemei sanduku la kura kushinda, ila ni ukweli pia wangependa zaidi washinde kupitia sanduku la kura.
Ukishasema sanduku la kura, Nape alibebwa! Nape siyo mbunge wa mikoa ya kusini, ni mbunge wa jimbo moja tu! Sifa za Nape unazozitoa ni zile za toilet paper.
 
Magu anamuhitaji Nape kwasababu anahitaji kura za watu wa kusini, na Nape nae anamuhitaji Magu ili ajiweke katika nafasi nzuri ya jina lake kupita kama mgombea 2020.

In short,kila mtu hapo anamuhitaji mwingine kuelekea 2020.

Ni kweli tunajua CCM hawategemei sanduku la kura kushinda, ila ni ukweli pia wangependa zaidi washinde kupitia sanduku la kura.

makufuli hamuhitaji nape kabisa . kaa ukijua makufuli ana wananchi wengi wanaompenda wanaomchukia ni wale waliobanwa na pili hata kama tanzania nzima usimpigie kura lakini atashinda
 
Magufur Anauwezo wa kuwaengua kwenye mchakato wa kura za maoni 2020 na akampitisha mgombea namba2 na 2025 wakigombea tena kwenye kupitishwa na ccm ili wawe wagombea ubunge magufur ana wahengua tena , kwaiyo January na Nap wameliona ilo wangejifanya manunda ubunge wageusikia kwe Redio tu, ingebid wasubili mbaka 2030 magufur atakuwa ana nguvu tena, Maana 2025 kipind cha uchaguz magufur anakuwa bado Raisi na mwenyekiti wa chama.
mkuu mpaka leo unafatilia katiba ya Tz, huyo haondoki hapo ikulu labda akipenda au afe mwenyewe akipenda pia.

usijidanganye kuwa ataachia madaraka. kamwee
 
January alikua hajamwambia Nape kama yeye kashaomba msamaha[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Nape baada ya kusikia kumbe wenzie wameomba msamaha ikabidi na yeye ajiongeze. Kujifanya kichwa nazi halafu ukose ubunge 2020
 
Hahahha awamu hii tumepatikana...."yani amehangaika kweli ameenda kwa mzee Mangula, mama Maria...." huu ni msamaha au kuaibishana
 
Kila goti litapigwa
tapatalk_1567708054798.jpeg
 
Mie kumsifia Nape? 😳😳😳😳😳
Eti ni shujaa? Ushujaa kwenye lipi? Hebu weka ushahidi wa kuthibitisha kauli yako.

Alichokifanya nape baada ya Clouds kuvamiwa ni wajibu wake ili kufanya uchunguzi kabla ya kuchukua hatua.

Nasubiri ushahidi wa niliyoyaandika.

Boss, hebu rudia kusoma msg zako juu ya sifa ulizomwaga kwa Nape ukiamini ni shujaa. Hata kama kaitwa je, yuko kiwango cha chini kiasi cha kuambiwa maneno ya kubembeleza? Kama wasemavyo waingereza, ukitaka kujua wewe ni nani, angalia unaowaunga mkono walivyo.
 
Kitendo cha mbunge wa jimbo la Mtama mh Nape Nnauye leo kwenda kuungama dhambi zake zote kwa Rais Magufuli kumeacha dilema na maswali yasiyojibika vichwani mwa wafuatiliaji wa siasa za chama tawala na za upinzani nchini.

Je, maungamo na kukiri toka moyoni alikokufanya leo Nape ni majuto kweli ya makosa na fedheha alizomfanyia Rais Magufuli au ni kujikosha tu baada ya kubaini wenzake kina Makamba na Ngeleja walienda kuomba msamaha na wakasamehewa?

Je, kambi ya upinzani iliyokuwa ikiwatetea Nape na wenzake, hivi sasa inasemaje baada ya kuona baba na mwana wamepatana?

Tujadili kwa pamoja.

001E4C28-8E4D-43A7-A628-E2B7C136BB7D.jpeg
 
Issue ya wana CCM waomba 'msamaha' 1 yr kabla ya uchaguzi inafikirisha sana.....

Mtu akifikiria kujiajiri anapoteza usingizi saa 8 usiku.. duh
 
Sisi wakristo ungamo letu linalazimisha kutaja dhambi zote unazozikumbuka na mwisho tunasema ".....kwa dhambi hizi na nyingine zote nisizozifahamu ..." Kisha Padre anakutangazia msamaha na kukutaka usitende dhambi tena.

Kwenye kutaja dhambi unaweza kulazimika kuwataja na wengine mlioshirikiana kutenda dhambi hizo na hapo ndio napata wasiwasi kwamba huenda kukawa na foleni endelevu ya watakaomba msamaha.

Chukulia mfano kama William alikuwa wa kwanza kukiri kosa na kuomba msamaha atashindwa kuwataja aliokuwa anaongea nao kweli?!

Mbarikiwe sana.
Maendeleo hayana vyama!
 
Back
Top Bottom