Pre GE2025 Nape Nnauye: Nashangaa Watanzania wanaokwenda kusikiliza upuuzi wa Lissu. Tumkemee, tumtenge na tumlaani

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mbona ulimtukana magu nahakuna aliyeshughulika na wewe?!
 
Utamaduni wa hovyo kabisa huu kuheshimu Katiba ambayo yenyewe tu haina ueezo wa kujilinda pale inapikiukwa na viongozi na watu wao. Wala haina uwezo wa kuwawajibisha viongozi wanaoivunja.

Hiyo Katiba ilikuwepo wakati huyo Lissu anaikimbia nchi, Je ilifanya nini kumlinda? Nape wakati anatembezwa kwa miguu kutoka Mnazi Mmoja hadi Magogoni kwenda kuomba msamaha huku akichukuliwa picha hiyo Katiba si ndiyo hii lakini haikumlinda?
Ilikuwa wapi hiyo Katiba wakati watu wanatekwa huku wengine wakiuawa? Ilikuwa wapi hiyo Katiba wakati haki ya wananchi kupiga kura na kuchagua ikiporwa kwa uchaguzi kuvurugwa?

Hiyo Katiba si ilikuwepo kipindi kile na si ipo hata hivi sasa wakati wale walioivunja kipindi sasa hivi wanarudishwa madarakani huku wengine wakizidi kujiachia na kula maisha watakavyo?
Ndiyo Katiba hii ambayo Nape anataka iheshimiwe? Katiba ambayo inategemea utashi wa kiongozi?
 
Vipi vimeuzwa,Kwa bei gani? Kauziwa nani? Na Kwa muktadha huo Nchi haipati tena Mapato kutokana na vilivyouzwa?
 
Mishahara amepandisha lini?Mei mosi watumishi masikio yote kusubiri Nini tamko la serikali.
 
Katiba hulindwa na wananchi, yenyewe haiwezi kujilinda.
Wananchi wakiwa wa hovyo hawawezi kulinda na kutetea makubaliano waliyojiwekea.
 
Hivi huyu mpuuzi Nape anafahamu ni kwanini Wamasai wameporwa ardhi yao ya asili, anafahamu ni kwnini bandari ya bara pekee ndiyo iliyobinafsishwa kwa Waarabu? Anafahamu kuwa huyo anaemtetea aliwahi kutamka hadharani kuwa Katiba yetu ni kijitabu tu?? Je alilaaniwa??
Nape familia pamoja na wapendwa wa Marehemu Lowasa hawajasahau maneno yako machafu dhidi ya Lowasa 2015. Na Mungu hatokuwacha salama endelea kuweweseka.
 
Anajisafisha kumbe mama ameshamjua kama ni mnafiki
 
Juzi Mzanzibar alipodai Passport kwa Watanganyika, hawa akina Nape na Makala walikuwa kimyaa!

Kwamba Wazanzibar wana haki ya 'maneno ya kibaguzi;, Mtanganyika hana haki hiyo.
Kusema wabara waje znz kwa passport ni ubaguzi ? Pole sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…