Pre GE2025 Nape Nnauye: Nashangaa Watanzania wanaokwenda kusikiliza upuuzi wa Lissu. Tumkemee, tumtenge na tumlaani

Pre GE2025 Nape Nnauye: Nashangaa Watanzania wanaokwenda kusikiliza upuuzi wa Lissu. Tumkemee, tumtenge na tumlaani

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Tanzania, Nape Nnauye amelaani vikali kauli iliyotolewa na Makamu mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu kuhusu madai ya Rais Samia kuwaondoa Wamasai wa Ngorongoro kisa yeye ni Mzanzibari.

Waziri Nape amesema kauli hii inapaswa kupingwa na kila mwenye akili timamu kwani ni hoja za watu waliofilisika kisiasa.

"Watanzania tusikubali upuuzi huu, na mimi nitawashangaa watanzania waliozaliwa wakati wa Muungano hata wanaokwenda kumsikiliza mpuuzi huyu, tumkemee, tumtenge, tumlaani" amesema Nape.

Amebainisha ikiwa watanzania wataendelea kuangalia vitendo hivi vya ukosoaji kwa Rais kwa kutumia jinsia, kabila au sehemu anakotoka watakuwa hawaitendei haki nchi.

Ameongeza, "Ni Rais huyu ndiye amesema andamaneni, polisi kawalindeni, na leo walikuwa wanaandamana hapa. Wamelindwa na Polisi, wamesindikizwa walipoenda, wamesababisha foleni dodoma hapa, magari yamesimamishwa ili wao waandamane, kwa uungwana wa huyu mama anayemtukana"


View: https://www.youtube.com/live/2FZwDIHGIYE?si=sJH-YKoIJDyvB8rQ

Mbona ulimtukana magu nahakuna aliyeshughulika na wewe?!
 
Zanzibar ina beach nzuri sana na vivutio vingine vya utalii, Samia hajavigusa ameuza vya Tanganyika.

Unatetea ujinga kwa vile unafaidika na utawala wake na kusahau kuwa watoto wako na uzao wako ni wa Tanganyika!

Watu wanaweka kumbukumbu, kama si wewe adhabu hizo watabeba uzao wako za kutetea kuuzwa tanganyika!
Utamaduni wa hovyo kabisa huu kuheshimu Katiba ambayo yenyewe tu haina ueezo wa kujilinda pale inapikiukwa na viongozi na watu wao. Wala haina uwezo wa kuwawajibisha viongozi wanaoivunja.

Hiyo Katiba ilikuwepo wakati huyo Lissu anaikimbia nchi, Je ilifanya nini kumlinda? Nape wakati anatembezwa kwa miguu kutoka Mnazi Mmoja hadi Magogoni kwenda kuomba msamaha huku akichukuliwa picha hiyo Katiba si ndiyo hii lakini haikumlinda?
Ilikuwa wapi hiyo Katiba wakati watu wanatekwa huku wengine wakiuawa? Ilikuwa wapi hiyo Katiba wakati haki ya wananchi kupiga kura na kuchagua ikiporwa kwa uchaguzi kuvurugwa?

Hiyo Katiba si ilikuwepo kipindi kile na si ipo hata hivi sasa wakati wale walioivunja kipindi sasa hivi wanarudishwa madarakani huku wengine wakizidi kujiachia na kula maisha watakavyo?
Ndiyo Katiba hii ambayo Nape anataka iheshimiwe? Katiba ambayo inategemea utashi wa kiongozi?
 
Zanzibar ina beach nzuri sana na vivutio vingine vya utalii, Samia hajavigusa ameuza vya Tanganyika.

Unatetea ujinga kwa vile unafaidika na utawala wake na kusahau kuwa watoto wako na uzao wako ni wa Tanganyika!

Watu wanaweka kumbukumbu, kama si wewe adhabu hizo watabeba uzao wako za kutetea kuuzwa tanganyika!
Vipi vimeuzwa,Kwa bei gani? Kauziwa nani? Na Kwa muktadha huo Nchi haipati tena Mapato kutokana na vilivyouzwa?
 
Mishahara amepandisha lini?Mei mosi watumishi masikio yote kusubiri Nini tamko la serikali.
 
Utamaduni wa hovyo kabisa huu kuheshimu Katiba ambayo yenyewe tu haina ueezo wa kujilinda pale inapikiukwa na viongozi na watu wao. Wala haina uwezo wa kuwawajibisha viongozi wanaoivunja.

Hiyo Katiba ilikuwepo wakati huyo Lissu anaikimbia nchi, Je ilifanya nini kumlinda? Nape wakati anatembezwa kwa miguu kutoka Mnazi Mmoja hadi Magogoni kwenda kuomba msamaha huku akichukuliwa picha hiyo Katiba si ndiyo hii lakini haikumlinda?
Ilikuwa wapi hiyo Katiba wakati watu wanatekwa huku wengine wakiuawa? Ilikuwa wapi hiyo Katiba wakati haki ya wananchi kupiga kura na kuchagua ikiporwa kwa uchaguzi kuvurugwa?

Hiyo Katiba si ilikuwepo kipindi kile na si ipo hata hivi sasa wakati wale walioivunja kipindi sasa hivi wanarudishwa madarakani huku wengine wakizidi kujiachia na kula maisha watakavyo?
Ndiyo Katiba hii ambayo Nape anataka iheshimiwe? Katiba ambayo inategemea utashi wa kiongozi?
Katiba hulindwa na wananchi, yenyewe haiwezi kujilinda.
Wananchi wakiwa wa hovyo hawawezi kulinda na kutetea makubaliano waliyojiwekea.
 
Hivi huyu mpuuzi Nape anafahamu ni kwanini Wamasai wameporwa ardhi yao ya asili, anafahamu ni kwnini bandari ya bara pekee ndiyo iliyobinafsishwa kwa Waarabu? Anafahamu kuwa huyo anaemtetea aliwahi kutamka hadharani kuwa Katiba yetu ni kijitabu tu?? Je alilaaniwa??
Nape familia pamoja na wapendwa wa Marehemu Lowasa hawajasahau maneno yako machafu dhidi ya Lowasa 2015. Na Mungu hatokuwacha salama endelea kuweweseka.
 
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Tanzania, Nape Nnauye amelaani vikali kauli iliyotolewa na Makamu mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu kuhusu madai ya Rais Samia kuwaondoa Wamasai wa Ngorongoro kisa yeye ni Mzanzibari.

Waziri Nape amesema kauli hii inapaswa kupingwa na kila mwenye akili timamu kwani ni hoja za watu waliofilisika kisiasa.

"Watanzania tusikubali upuuzi huu, na mimi nitawashangaa watanzania waliozaliwa wakati wa Muungano hata wanaokwenda kumsikiliza mpuuzi huyu, tumkemee, tumtenge, tumlaani" amesema Nape.

Amebainisha ikiwa watanzania wataendelea kuangalia vitendo hivi vya ukosoaji kwa Rais kwa kutumia jinsia, kabila au sehemu anakotoka watakuwa hawaitendei haki nchi.

Ameongeza, "Ni Rais huyu ndiye amesema andamaneni, polisi kawalindeni, na leo walikuwa wanaandamana hapa. Wamelindwa na Polisi, wamesindikizwa walipoenda, wamesababisha foleni dodoma hapa, magari yamesimamishwa ili wao waandamane, kwa uungwana wa huyu mama anayemtukana"


View: https://www.youtube.com/live/2FZwDIHGIYE?si=sJH-YKoIJDyvB8rQ

Anajisafisha kumbe mama ameshamjua kama ni mnafiki
 
Juzi Mzanzibar alipodai Passport kwa Watanganyika, hawa akina Nape na Makala walikuwa kimyaa!

Kwamba Wazanzibar wana haki ya 'maneno ya kibaguzi;, Mtanganyika hana haki hiyo.
Kusema wabara waje znz kwa passport ni ubaguzi ? Pole sana
 
Back
Top Bottom