Nape Nnauye: Tuhangaike kujenga mifumo imara na siyo kutumainia mtu mmoja

Nape Nnauye: Tuhangaike kujenga mifumo imara na siyo kutumainia mtu mmoja

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Ndugu Nape alipohojiwa kuhusu vuguvugu la kumuongezea Rais Magufuli muda wa utawala wake amesema haya yafuatayo.

1. Kwanza anashangazwa na kwamba ndiyo kwanza miaka mitano ya muhula wa pili wa utawala wa Rais Magufuli umeanza halafu watu wanaanza kuzungumza ya baadae, wakati haya waliyoomba kura kwayo hawajayamaliza.

2. Pili anashangazwa na watu wanaowaza utadhani wana ahadi na Mwenyezi Mungu kuhusu kujua nani atakuwepo kesho na nani hatakuwepo.

3. Anasema, Kilicho cha msingi ni kujenga mifumo imara ili hiyo mifumo iweze kulinda mafanikio yaliyopatikana na tusigeuze mtu kuwa ndo mafanikio yenyewe maana watu huja na kuondoka na Mungu ndo anapanga uhai wa watu.

MY TAKE
Msimamo wa Nape ni msimamo mzuri, wanaotaka Magufuli abaki madarakani kinyume cha katiba ya sasa hao wanajali maslahi yao binafsi na si ya nchi yetu. hawana tofauti na wale ambao Nyerere alisema kila alipotaka kung'atuka walimwambia Mzee endelea bila wewe nchi itayumba kumbe ikaja kugundulika walikuwa wanajali matumbo yao binafsi, walikuwa hawana uhakika kuwa akitoka madarakani basi Rais ajaye atawalindia nyadhifa zao!

Msikilize wewe mwenyewe hapa:




MSIMAMO WA RAIS MAGUFULI KUHUSU KUONGEZA MUDA NI HUU HAPA CHINI

 
Hahahaa Nape kwisha habari yake. Angekuwa Waziri na yeye angekuwa anasema apewe 5+2+7. Wote hawa ni hopeless bunch of losers.

Magufuli kawakata korodani. Hakuna rangi wataacha kuona. Magufuli wanaye mpaka Israel amchukue. Kinyago chao wenyewe kinawatesa.
 
Labda bunge la India.
Umemjibu vizuri sana. Bunge hili hili letu? Haya mambo yalishapangwa na ndiyo maana safari hii wamepitishwa wabunge wa hovyo hovyo. Nasema kupitishwa kwa sababu hakukuwa na uchaguzi. Atakachokifanya Magufuli ni kuwaambia (kwa kutumia wapiga debe wa kisiri) ''kubalini hoja ipite na nitahakikisha mnakuwa wabunge wangu muda wote nitakaokuwa madarakani ili tusaidiane kupiga kazi''.
 
Umemjibu vizuri sana. Bunge hili hili letu? Haya mambo yalishapangwa na ndiyo maana safari hii wamepitishwa wabunge wa hovyo hovyo. Nasema kupitishwa kwa sababu hakukuwa na uchaguzi. Atakachokifanya Magufuli ni kuwaambia (kwa njia kutumia wapiga debe) kubalini hoja ipite na nitahakikisha mnakuwa wabunge wangu muda wote nitakaokuwa madarakani ili tusaidia kupiga kazi.
Inaogopesha sana kuona mtu anaetaka kubakia madarakani ndo type hizo za Magufuli tutaumia sana kwa kweli
 
Kazungumza mambo ya maana sana,tatizo umeamua kuacha akili zako nyumbani ndio maana badala ya kujadili hoja unakimbilia kumshambulia mtu.
Huyo lazima ni wale wale wachumia tumbo. Toka kanda pendwa
 
Hoja namba 2 na 3 nimeshaziandika sana hapa.
 
Ameongea ukweli sio sahihi kumtegemea mtu mmoja, tatizo lenyewe tunaenda mwaka wa sita culture ya ufanyaji kazi serikalini aijabadilika pamoja na kwamba amejaribu kuwaacha wakurugenzi na wakuu wa wilaya/mikoa wale wale ulitegemea by now wawe na experience ndio kwanza ata kusimamia miradi yao shida.

Wizarani wataalamu pia awajabadilishwa ovyo lakini bado hakuna consitent serikalini matatizo aliyoyakuta mpaka leo yapo kwa percent kubwa inabidi aanze trouble shooting kila mara anaposimama kukutana na wananchi mpaka yeye mwenyewe anajiuliza kazi za watu wengine serikalini ni nini kama kila anapofika ni yeye ndio atupiwe shida.

Mtu pekee anaelekea kuweza kuendesha wizara aliyokabidhiwa ni Dr Gwajima ila apunguze mapepe. Huyo mrithi wa Magufuli given the social contexts za jamii yetu aonekani.

Hao mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya; raisi akinyuti na wao uwaoni tena kwenye camera mpaka aibuke.

Let’s face it ignorance is another major issue watanzania bado awajajua ku deal na consequences of their action ppl take life so easy in Tanzania; ningekuwa naishi mjini nikapata ata wenyekiti wa mtaa watu ndio wangeelewa I do not tolerate stupidity ukitupa taka mtaani unakula fine hapo hapo au nakupa fagio ufagie mtaa mzima.

In short serikali imejaza mapambo kwa majina ya wasimamizi wasio na managerial skills husika za kuendesha wizara yaani wewe waziri mpaka ufike site ndio ujue mradi upo 40% badala ya 90% kama ulivyoambiwa huna supervision matrix ya kila mradi na communication zako za watu chini je.

Akiondoka Magufuli tunarudi square 1 jumlisha na hizi pressure za wafanyakazi wa serikali atakaefuata akiendekeza kelele za hawa watu atakuta mapato yote anawapa wao kama mishahara na marupurupu; hana kinachobaki kwa ajili ya miradi ya kimkakati ya maendeleo.
 
Ameongea vyema! Mifumo imara ni muhimu kwa maendeleo endelevu na sio kumtegemea mtu mmoja.
 
Back
Top Bottom