Napenda wanawake wanaojisitiri kimavazi kuliko wa vimini na mawigi

Napenda wanawake wanaojisitiri kimavazi kuliko wa vimini na mawigi

ukweli ni kwamba hayo ni maono au matakwa yako.... japo siku hizi mambo yamebadilika sana unaweza kuniona navaa ushungi 24/7 kumbe ni mchafu wa matendo kupindukia sifai afadhali yule avaae hizo nguo zisizojistiri ila lile vazi limenifanya kuonekana ni mwema na maovu yangu yamejificha nyuma yake.




hijab isn't just what you are wearing but its also what you do and say. its who you are
Hilo la tabia mada nyingine mkuu.
 
Najua wengine watasema naishi enzi za ujima lakini kiukweli nikimwona binti kajisitiri nguo iliyofunika mwili vizuri, kichwani ana mtandio au kilemba huwa najihisi faraja kubwa sana moyoni.

Shida nikiona wale wa visuruali vya kuchanika, vimini na mawigi ya kichina huwa najihisi kutapika.
Sasa sijui ni ushamba wangu au kuna wanaume wengine hali kama hii huwakuta.

Nawakilisha.
Ni wa dini ile!
 
Najua wengine watasema naishi enzi za ujima lakini kiukweli nikimwona binti kajisitiri nguo iliyofunika mwili vizuri, kichwani ana mtandio au kilemba huwa najihisi faraja kubwa sana moyoni.

Shida nikiona wale wa visuruali vya kuchanika, vimini na mawigi ya kichina huwa najihisi kutapika.
Sasa sijui ni ushamba wangu au kuna wanaume wengine hali kama hii huwakuta.

Nawakilisha.
mwanamke anaejifunika huwa wamoto sbb anahifadh joto ila anaejiachia vimin huw wabarid
 
Aise nilifikil ni mimi tu maana huwa nawaangaliaga sana wadada wa Kizenj wanavyovutia na hijab zao kwa kweli nawapenda na ukitaka kuwaona nenda kigambonino
 
Busara za baba.

Msichana alinunua simu smartphone ambayo ni ghali mno. Baba yake alipoiona alimuuliza "Binti yangu uliponunua hiyo simu yako ya gharama cha kwanza kufanya kilikua ni nini?"

"Niliweka screen protector kuzuia michubuko ya kioo na nikanunua cover kwa ajili ya kuzuia ikianguka isichubuke" binti alijibu.

"kuna mtu alikusukuma kufanya hivyo?" baba alimuuliza bintie

"Hapana" binti alijibu

"Unafikiri huko si kuwatukana waliotengeneza simu kwamba hawakukamilisha kazi yao? Baba aliendelea kuuliza.

"Hapana baba" ni kwamba hata wanaotengeneza wanawakumbusha watu kuweka cover katika simu zao kuzuia kuharibika kwa urahisi"

"Je uliiwekea cover kwa vile simu ni bei rahisi na inamuonekano mbaya?" Baba aliendelea kusaili

"ukweli nimeiwekea cover sitaki iharibike mapema na ipoteze uthamani wake" binti aliendelea kumjibu baba yake.

"ulipoiwekea cover, imepunguza uzuri wa simu yako?"

"Hapana baba nafikiri ndio imeonekana nzuri zaidi tofauti na mwanzo, na imeipa simu yangu ulinzi ili isiharibike"

Baba akamwangalia binti yake kwa upendo na akamwambia, " Je kama nikikuomba ukave mwili wako ambao unathamani kubwa kuliko hata hiyo simu yako kwa nguo ndefu zisizo onyesha maungo yako kwa watu hovyo hovyo utafanya hivyo?"

Binti alibaki kimya!

Uvaaji wa nguo fupi na zisizo na staha ambazo zinaweka wazi maungo yenu obvious zinapunguza thamani yenu na heshima kwa jamii. Watakaokutamani ni wanaume wakware tu wale wahuni wahuni! Ila mwanaume mwenye heshima zake hawezi akavutiwa nawe kwake atakuona kama msichana fulani wa kileo unayefaa kwa usiku mmoja tu na sio kwa maisha.
Ni kwel the most valuable things in this word are covered and protected kwa mfano tunapata wap madini ya diamond ,gold chini ya ardhi yamefichwa na miamba mikubwa
 
Back
Top Bottom