Nijikite kwenye mada leo ktk pitapita zangu kariakoo nilikutana na mkutano wa mh Freeman Mbowe Raha/Muhonda Street nikasimama kitambo kidogo nikaendelea na mambo yangu. Baada ya masaa kadhaa TRA wakatuma vijana wadogo kukaa kila duka na kuanza kuwauliza wafanyabiashara maswali na kukaa...
Changamoto za multiple taxation
1. Lisiti moja ya EFD kutumika zaidi ya maramoja kwa bidhaa zenye bei ya kufanana
2. Unanua bidhaa za 1,000,000/= mfanya biashara ananegoshieti na mnunuzi anaandikiwa Lisiti ya 200,000/= .....anamtoa mnunuzi kiasi kidogo chini ya kodi aliyopaswa kulipa.
3. Mnunuzi na muuzaji kujilipua kuuziana biashara nje ya mfumo wa EFD
4. Kuwindana mtaani bila sababu eti una EFD au hauna
"Kila mtanzania mwenye umri wa zaidi ya miaka 18 na mwenye kipato anatakiwa kulipa kodi. Ili kutimiza amza hiyo, Serikali inakusudia kutoa namba ya utambulisho wa mlipakodi (TIN) kwa kila mtanzania mwenye umri wa kuanzia miaka 18 au zaidi" "Kwa kuwa utaratibu wa usajili wa namba ya utambulisho...
Waziri wa Fedha na Mipango amependekeza kugawa TIN kwa watu wa kuanzia miaka 18 na kuendelea, na taarifa hizi ziende sawa na NIDA ili kulipa kodi kwa usahihi. Baadhi ya watu wamehusianisha namna hii ya ukusanyaji kodi na Kodi ya kichwa, kitu ambacho naona ni kupotosha ukweli kuhusu kodi ya...
Tanzania tuna mfumo wa kodi ambao naweza kuuita ni 'Tax chain system'. Yaani ni kwamba bidhaa moja inaweza ikapigwa kodi hata mara kumi halafu wale watu walioilipia kodi mara ya 2 hadi ya 10 wanatakiwa wapeleke mahesabu TRA ili warudishiwe kodi yao;kivipi?
Mfano bidhaa imezalishwa kiwandani, mnunuzi wa kwanza atakayenunua atalipa 18% Vat, na hii tu ndio halali ya TRA kwa bidhaa hiyo, lakini kama huyu mnunuzi wa kwanza ataenda kuiuza itabidi atoe risiti ya EFD na atamlipisha tena mteja 18% Vat ambayo TRA itamdai, huyu nae akienda kuiuza itabidi atoe risiti ya EFD ambapo atamchaji tena mteja 18% VAT ambayo nayo itatakiwa kupelekwa TRA, and so on hata mara 10.
Ili kuepuka kulipa VAT mara mbili kila mfanyabiashara atapeleka mahesabu na risiti za VAT (kwa waliounganishwa na VAT) ili kujua kiwango cha ziada cha kile ambacho ameshalipa, na hicho tu ndicho atapaswa kulipa; hii process inaleta mlolongo mgumu na very complicated, yaani ni mfumo mgumu sana bila sababu, nadhani wote mnofuatilia haya masuala mtajua.
Lengo la TRA kung'ang'ania huu mfumo ni ili kupata 18% ya faida ya kila hatua ya uuzaji wa bidhaa, hata ikiuzwa mara 10 TRA hawajali, wanataka 18% ya ile faida (gross profit) ya kila mfanyabiashara katika kila chain link ya uuzaji wa bidhaa husika, hadi kwa final consumer, yule wa mwisho kabisa. (Wanakaba hadi penalti).
Hii inaweza kuonekana ni nzuri ukiitazama kwa juu juu, lakini in reality hii ni sawa na kutumia risasi kuwinda smaki baharini, unatumia 10shs. kukusanya shs.8, yeees, ukweli ndio huu. Badala ya kusababisha such an expensive practical complexity ni kwanini TRA isiwekeze instead kuhakikisha kodi yote ya kila bidhaa inalipwa palepale kiwandani bidhaa inapozalishwa au bandarini mzigo unapoingizwa, hata kama kodi ikiongezwa sio mbaya lakini ilipwe yote infull palepale kiwandani / bandarini.
Hebu fikiria tu harassment wanayopata wateja wanaposafirisha mizigo barabarani, watu husimamishwa hovyo hovyo na mapolisi 'Tigo' wale wenye silaha za kivita as if wanasimamisha jambazi, kumbe umebeba T.V tu ndio imekuwa nongwa, kwani hii T.V si imepitia bandarini??! Si mchukue kodi yenu yote huko huko muache wananchi waishi kwa amani?
Mateso kama haya walikuwa wanayapata wamiliki wa magari ambapo kila mwaka walipanga foleni TRA na office za MXMALIPO kulipia road license, tena barabarani TRA walipoteza nguvu kazi kubwa ya wasomi wenye madegree kusimamabarabarani eti kukagua sticker za road license, as if hizo gari hazitumii mafuta ambayo tayari yana kodi lukuki, binafsi nilianzisha uzi wa kupendekeza kodi hiyo nayo iunganishwe tu humo humo kwenye mafuta(Hivi ni kwanini road license isilipiwe kwenye mafuta?) watu waligoma goma ili mwishowe logic and common sense emerged victourious, serikali ikahamishia kodi hiyo kwenye mafuta na sasa hii kero imeisha
Muda mwingine umasikini tunajitafutia wenyewe kwa kukariri vitu vilivyopitwa na wakati, technolojia imekuwa, ni rahisi sana kukata kodi yote in full kwenye viwanda / bandarini, tubadilike bwana; nakaribisha maoni.
=================================
Update: 04/04/2021
Waziri wa Fedha na Mipango, Mwigulu Nchemba, amesema wanaangalia namna ya kutumia mfumo mpya wa ukusanyaji kodi
Mfumo huu ukitumika, naamini utachaguza sana ukuaji na ustawi wa biashara nchini, pamoja na kuongeza mapato kwa uhaki zaidi, kodi iongezwe ila ilipwe yote infull kwa mara moja pale pale kiwandani / Bandarini.
Bandiko ni zuri, na Umefunguka kwa Mantiki.
But labda nikurekebishe tu kitu kimoja, sio mizigo yote ya TRA inapititia bandarini lakini pia ipo inayopitia bandarini lakini kwa sababu za umakini hazipigwi Kodi. Sasa tuache hizo zinazopitia Bandarini, Tuje kwenye hizi ambazo watu wasio wazalendo wanapitisha mizigo hiyo bila kufuata utaratibu(kwa kukwepa kodi). Sasa ni vizuri unapotoa hoja hiyo utoe pia na wazo ni namna gani TRA itapata kodi kwenye mizigo ambayo ilipitishwa kinyume na Utaratibu? Hapo utakuwa umewasaidia.
So far, Bandiko ni zuri, lina logoc ndani yake ni hayo tu.
Mama Samiah ana lipi la kutuambia juu ya kauli yake kwamba akipata nafasi ya kukopa atakopa tena. Tumsikilize mwamba akiwafundisha wanafunzi wake, na endapo Rais wetu anaweza kuirudia ile kauli yake juu ya mikopo? ================================ Update: 15/02/2022...
Ukisafiri kutokea Dar kwenda mikoan utakutana sana na Magari tupu ya mizigo yakirudi Dar, haya yalipeleka mizigo kutokea Bandarini na sasa unakuta yanarudi tupu. Hii maana yake ni kwamba hakuna mizigo ya kubeba kutoka mikoani kupeleka Dar na hatimaye ioande meli? Kwa hio sisi ni wapokeaji wa...
Wakuu habari zenu.. Mwanamama mmoja mwenye Miaka 46 amefikishwa kizimbani kujibu tuhuma za kununua Bidhaa bila Kudai Risiti. Kwa Mujibu wa mshitaki ambae Ni TRA, walimtia mbaroni mteja huyo wakati wakiwa kwenye Doria zao za kawaida.. Haieleweki Mara moja kosa la Kununua Bidhaa bila Kudai...
Mtoa hoja nakuunga mkono mtiririko wa kodi Tanzania unasababisha bei za bidhaa zetu kuwa kubwa sana na kuongeza gharama za maisha. Sijui kama wataalam wetu wamewahi kujiuliza jinsi gani hili jambo linatuletea hasara. Tanzania tumebarikiwa kuwa na bandari, bidhaa nyingi za nchi zinazotuzunguka zinapitia kwetu lakini bidhaa hizo hizo zikifika nchi za jirani zinapokwenda bei yake huwa rahisi kuliko hapa kwetu. Yaani wafanyabiashara wa kitanzania wanalazimika kwenda Uganda kuchukua mzigo na kuleta Tanzania, hivi hatuoni kuwa tunapoteza?
Kama tungekuwa tunafikiria vizuri tulipaswa kutengeneza mazingira wafanyabiashara wa nchi zinazotuzunguka Rwanda, Burundi, Zambia, Uganda & DRC wawe wanakuja kufunga mizigo hapa kwetu. Yaani ilitakiwa mtu akipiga hesabu kwa mzigo wa kawaida kwenda China, Dubai au Tanzania apate jibu bora niende Tanzania. Lengo hili hatuwezi kulifikia kwa aina ya kodi tulizokuwa nazo. Kwanza kodi zetu zinashawishi ukwepaji, yaani mfanyabiashara anashawishika kukwepa ili apate faida. Ni ukweli uliodhahiri mfanyabishara mdogo au wa kati akifuata masharti yooote na kodi zoooote za kibongo hawezi kutoboa. Hivyo, wanalazimika kukwepa kwa kutumia mbinu za kila aina.
Huwa najiuliza mfanyabiashara hata wa mtaani akifikia aina fulani ya mauzo anatakiwa kuandikishwa katika VAT kwahiyo bidhaa zake anatakiwa kuanza kuongeza 18%, wakati huo huo jirani zake ambao bado hawajafikia kiwango cha mauzo yake wanauza bidhaa ya aina hiyo bila 18%, kwa maana hii yeye hawezi kuuza tena akiendelea kuweka hiyo kodi. Sasa mfanyabiashara huyu unafikiri atakubali? Lazima atatafuta namna ya kuikwepa hii kodi ili aendelee ku-survive. Yaani kodi inamrudisha mtu nyuma hii sio sawa. Kodi ya VAT ilipaswa kuwekwa viwandani ili wanaokwenda kununua wakutane nayo hapo au kwa wafanyabiashara wakubwa wanaoagiza mizigo kutoka nje tu, na ipigwe pale mzigo unapoingia tu. Hawa wafanyabiashara wengine wapigwe kodi ya mapato pekee yake.
Tanzania tuna mfumo wa kodi ambao naweza kuuita ni 'Tax chain system'. Yaani ni kwamba bidhaa moja inaweza ikapigwa kodi hata mara kumi halafu wale watu walioilipia kodi mara ya 2 hadi ya 10 wanatakiwa wapeleke mahesabu TRA ili warudishiwe kodi yao;kivipi?
Mfano bidhaa imezalishwa kiwandani, mnunuzi wa kwanza atakayenunua atalipa 18% Vat, na hii tu ndio halali ya TRA kwa bidhaa hiyo, lakini kama huyu mnunuzi wa kwanza ataenda kuiuza itabidi atoe risiti ya EFD na atamlipisha tena mteja 18% Vat ambayo TRA itamdai, huyu nae akienda kuiuza itabidi atoe risiti ya EFD ambapo atamchaji tena mteja 18% VAT ambayo nayo itatakiwa kupelekwa TRA, and so on hata mara 10.
Ili kuepuka kulipa VAT mara mbili kila mfanyabiashara atapeleka mahesabu na risiti za VAT (kwa waliounganishwa na VAT) ili kujua kiwango cha ziada cha kile ambacho ameshalipa, na hicho tu ndicho atapaswa kulipa; hii process inaleta mlolongo mgumu na very complicated, yaani ni mfumo mgumu sana bila sababu, nadhani wote mnofuatilia haya masuala mtajua.
Lengo la TRA kung'ang'ania huu mfumo ni ili kupata 18% ya faida ya kila hatua ya uuzaji wa bidhaa, hata ikiuzwa mara 10 TRA hawajali, wanataka 18% ya ile faida (gross profit) ya kila mfanyabiashara katika kila chain link ya uuzaji wa bidhaa husika, hadi kwa final consumer, yule wa mwisho kabisa. (Wanakaba hadi penalti).
Hii inaweza kuonekana ni nzuri ukiitazama kwa juu juu, lakini in reality hii ni sawa na kutumia risasi kuwinda smaki baharini, unatumia 10shs. kukusanya shs.8, yeees, ukweli ndio huu. Badala ya kusababisha such an expensive practical complexity ni kwanini TRA isiwekeze instead kuhakikisha kodi yote ya kila bidhaa inalipwa palepale kiwandani bidhaa inapozalishwa au bandarini mzigo unapoingizwa, hata kama kodi ikiongezwa sio mbaya lakini ilipwe yote infull palepale kiwandani / bandarini.
Hebu fikiria tu harassment wanayopata wateja wanaposafirisha mizigo barabarani, watu husimamishwa hovyo hovyo na mapolisi 'Tigo' wale wenye silaha za kivita as if wanasimamisha jambazi, kumbe umebeba T.V tu ndio imekuwa nongwa, kwani hii T.V si imepitia bandarini??! Si mchukue kodi yenu yote huko huko muache wananchi waishi kwa amani?
Mateso kama haya walikuwa wanayapata wamiliki wa magari ambapo kila mwaka walipanga foleni TRA na office za MXMALIPO kulipia road license, tena barabarani TRA walipoteza nguvu kazi kubwa ya wasomi wenye madegree kusimamabarabarani eti kukagua sticker za road license, as if hizo gari hazitumii mafuta ambayo tayari yana kodi lukuki, binafsi nilianzisha uzi wa kupendekeza kodi hiyo nayo iunganishwe tu humo humo kwenye mafuta(Hivi ni kwanini road license isilipiwe kwenye mafuta?) watu waligoma goma ili mwishowe logic and common sense emerged victourious, serikali ikahamishia kodi hiyo kwenye mafuta na sasa hii kero imeisha
Muda mwingine umasikini tunajitafutia wenyewe kwa kukariri vitu vilivyopitwa na wakati, technolojia imekuwa, ni rahisi sana kukata kodi yote in full kwenye viwanda / bandarini, tubadilike bwana; nakaribisha maoni.
=================================
Update: 04/04/2021
Waziri wa Fedha na Mipango, Mwigulu Nchemba, amesema wanaangalia namna ya kutumia mfumo mpya wa ukusanyaji kodi
Mama Samiah ana lipi la kutuambia juu ya kauli yake kwamba akipata nafasi ya kukopa atakopa tena. Tumsikilize mwamba akiwafundisha wanafunzi wake, na endapo Rais wetu anaweza kuirudia ile kauli yake juu ya mikopo? ================================ Update: 15/02/2022...
Nilikua na haya mawazo toka siku nyingi mpaka nikasema uongozi unahitaji mtu ambaye ameshapitia kwenye biashara akapambana na marejesho ya benki, return n.k. Ila kama hujawahi kufanya biashara huwezi kuelewa kadhia.
Na pia anayepewa huu mzigo wa kodi ni yule mwananchi mtumiaji wa mwisho anayepokeaga khanga na kitenge wakati wa uchaguzi.
Mtoa hoja nakuunga mkono mtiririko wa kodi Tanzania unasababisha bei za bidhaa zetu kuwa kubwa sana na kuongeza gharama za maisha. Sijui kama wataalam wetu wamewahi kujiuliza jinsi gani hili jambo linatuletea hasara. Tanzania tumebarikiwa kuwa na bandari, bidhaa nyingi za nchi zinazotuzunguka zinapitia kwetu lakini bidhaa hizo hizo zikifika nchi za jirani zinapokwenda bei yake huwa rahisi kuliko hapa kwetu. Yaani wafanyabiashara wa kitanzania wanalazimika kwenda Uganda kuchukua mzigo na kuleta Tanzania, hivi hatuoni kuwa tunapoteza?
Kama tungekuwa tunafikiria vizuri tulipaswa kutengeneza mazingira wafanyabiashara wa nchi zinazotuzunguka Rwanda, Burundi, Zambia, Uganda & DRC wawe wanakuja kufunga mizigo hapa kwetu. Yaani ilitakiwa mtu akipiga hesabu kwa mzigo wa kawaida kwenda China, Dubai au Tanzania apate jibu bora niende Tanzania. Lengo hili hatuwezi kulifikia kwa aina ya kodi tulizokuwa nazo. Kwanza kodi zetu zinashawishi ukwepaji, yaani mfanyabiashara anashawishika kukwepa ili apate faida. Ni ukweli uliodhahiri mfanyabishara mdogo au wa kati akifuata masharti yooote na kodi zoooote za kibongo hawezi kutoboa. Hivyo, wanalazimika kukwepa kwa kutumia mbinu za kila aina.
Huwa najiuliza mfanyabiashara hata wa mtaani akifikia aina fulani ya mauzo anatakiwa kuandikishwa katika VAT kwahiyo bidhaa zake anatakiwa kuanza kuongeza 18%, wakati huo huo jirani zake ambao bado hawajafikia kiwango cha mauzo yake wanauza bidhaa ya aina hiyo bila 18%, kwa maana hii yeye hawezi kuuza tena akiendelea kuweka hiyo kodi. Sasa mfanyabiashara huyu unafikiri atakubali? Lazima atatafuta namna ya kuikwepa hii kodi ili aendelee ku-survive. Yaani kodi inamrudisha mtu nyuma hii sio sawa. Kodi ya VAT ilipaswa kuwekwa viwandani ili wanaokwenda kununua wakutane nayo hapo au kwa wafanyabiashara wakubwa wanaoagiza mizigo kutoka nje tu, na ipigwe pale mzigo unapoingia tu. Hawa wafanyabiashara wengine wapigwe kodi ya mapato pekee yake.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.