Napendekeza bidhaa zipigwe kodi mara moja tu, njia ni hii

Napendekeza bidhaa zipigwe kodi mara moja tu, njia ni hii

Changamoto za multiple taxation
1. Lisiti moja ya EFD kutumika zaidi ya maramoja kwa bidhaa zenye bei ya kufanana
2. Unanua bidhaa za 1,000,000/= mfanya biashara ananegoshieti na mnunuzi anaandikiwa Lisiti ya 200,000/= .....anamtoa mnunuzi kiasi kidogo chini ya kodi aliyopaswa kulipa.
3. Mnunuzi na muuzaji kujilipua kuuziana biashara nje ya mfumo wa EFD
4. Kuwindana mtaani bila sababu eti una EFD au hauna
Changamoto hizi zitafutiwe suluhu
 
Tupunguziane milolongo katika ulipaji wa kodi, process zimekuwa nyingi
 
Tukifanya miamala inayohisisha bidhaa tunatakiwa kulipa tena kodi, 🤷🏽‍♂️
 
 
Tanzania tuna mfumo wa kodi ambao naweza kuuita ni 'Tax chain system'. Yaani ni kwamba bidhaa moja inaweza ikapigwa kodi hata mara kumi halafu wale watu walioilipia kodi mara ya 2 hadi ya 10 wanatakiwa wapeleke mahesabu TRA ili warudishiwe kodi yao;kivipi?

Mfano bidhaa imezalishwa kiwandani, mnunuzi wa kwanza atakayenunua atalipa 18% Vat, na hii tu ndio halali ya TRA kwa bidhaa hiyo, lakini kama huyu mnunuzi wa kwanza ataenda kuiuza itabidi atoe risiti ya EFD na atamlipisha tena mteja 18% Vat ambayo TRA itamdai, huyu nae akienda kuiuza itabidi atoe risiti ya EFD ambapo atamchaji tena mteja 18% VAT ambayo nayo itatakiwa kupelekwa TRA, and so on hata mara 10.

Ili kuepuka kulipa VAT mara mbili kila mfanyabiashara atapeleka mahesabu na risiti za VAT (kwa waliounganishwa na VAT) ili kujua kiwango cha ziada cha kile ambacho ameshalipa, na hicho tu ndicho atapaswa kulipa; hii process inaleta mlolongo mgumu na very complicated, yaani ni mfumo mgumu sana bila sababu, nadhani wote mnofuatilia haya masuala mtajua.

Lengo la TRA kung'ang'ania huu mfumo ni ili kupata 18% ya faida ya kila hatua ya uuzaji wa bidhaa, hata ikiuzwa mara 10 TRA hawajali, wanataka 18% ya ile faida (gross profit) ya kila mfanyabiashara katika kila chain link ya uuzaji wa bidhaa husika, hadi kwa final consumer, yule wa mwisho kabisa. (Wanakaba hadi penalti).

Hii inaweza kuonekana ni nzuri ukiitazama kwa juu juu, lakini in reality hii ni sawa na kutumia risasi kuwinda smaki baharini, unatumia 10shs. kukusanya shs.8, yeees, ukweli ndio huu. Badala ya kusababisha such an expensive practical complexity ni kwanini TRA isiwekeze instead kuhakikisha kodi yote ya kila bidhaa inalipwa palepale kiwandani bidhaa inapozalishwa au bandarini mzigo unapoingizwa, hata kama kodi ikiongezwa sio mbaya lakini ilipwe yote infull palepale kiwandani / bandarini.

Hebu fikiria tu harassment wanayopata wateja wanaposafirisha mizigo barabarani, watu husimamishwa hovyo hovyo na mapolisi 'Tigo' wale wenye silaha za kivita as if wanasimamisha jambazi, kumbe umebeba T.V tu ndio imekuwa nongwa, kwani hii T.V si imepitia bandarini??! Si mchukue kodi yenu yote huko huko muache wananchi waishi kwa amani?

Mateso kama haya walikuwa wanayapata wamiliki wa magari ambapo kila mwaka walipanga foleni TRA na office za MXMALIPO kulipia road license, tena barabarani TRA walipoteza nguvu kazi kubwa ya wasomi wenye madegree kusimamabarabarani eti kukagua sticker za road license, as if hizo gari hazitumii mafuta ambayo tayari yana kodi lukuki, binafsi nilianzisha uzi wa kupendekeza kodi hiyo nayo iunganishwe tu humo humo kwenye mafuta(Hivi ni kwanini road license isilipiwe kwenye mafuta?) watu waligoma goma ili mwishowe logic and common sense emerged victourious, serikali ikahamishia kodi hiyo kwenye mafuta na sasa hii kero imeisha

Muda mwingine umasikini tunajitafutia wenyewe kwa kukariri vitu vilivyopitwa na wakati, technolojia imekuwa, ni rahisi sana kukata kodi yote in full kwenye viwanda / bandarini, tubadilike bwana; nakaribisha maoni.

=================================
Update: 04/04/2021
Waziri wa Fedha na Mipango, Mwigulu Nchemba, amesema wanaangalia namna ya kutumia mfumo mpya wa ukusanyaji kodi
Andiko limeshiba sana
 
Andiko limeshiba sana
Mfumo huu ukitumika, naamini utachaguza sana ukuaji na ustawi wa biashara nchini, pamoja na kuongeza mapato kwa uhaki zaidi, kodi iongezwe ila ilipwe yote infull kwa mara moja pale pale kiwandani / Bandarini.
 
Haileti mantiki kodi ya shs. 10/= itumike gharama ya shs.7/= kuikusanya, hii haiingii akili!
 
Bandiko ni zuri, na Umefunguka kwa Mantiki.
But labda nikurekebishe tu kitu kimoja, sio mizigo yote ya TRA inapititia bandarini lakini pia ipo inayopitia bandarini lakini kwa sababu za umakini hazipigwi Kodi. Sasa tuache hizo zinazopitia Bandarini, Tuje kwenye hizi ambazo watu wasio wazalendo wanapitisha mizigo hiyo bila kufuata utaratibu(kwa kukwepa kodi). Sasa ni vizuri unapotoa hoja hiyo utoe pia na wazo ni namna gani TRA itapata kodi kwenye mizigo ambayo ilipitishwa kinyume na Utaratibu? Hapo utakuwa umewasaidia.

So far, Bandiko ni zuri, lina logoc ndani yake ni hayo tu.
Uzuri wa sheria ya mapato iko wazi kwa wakwepa kodi, atawajibishwa kwa mujibu wa sheria zetu za kodi
 
 
Mtoa hoja nakuunga mkono mtiririko wa kodi Tanzania unasababisha bei za bidhaa zetu kuwa kubwa sana na kuongeza gharama za maisha. Sijui kama wataalam wetu wamewahi kujiuliza jinsi gani hili jambo linatuletea hasara. Tanzania tumebarikiwa kuwa na bandari, bidhaa nyingi za nchi zinazotuzunguka zinapitia kwetu lakini bidhaa hizo hizo zikifika nchi za jirani zinapokwenda bei yake huwa rahisi kuliko hapa kwetu. Yaani wafanyabiashara wa kitanzania wanalazimika kwenda Uganda kuchukua mzigo na kuleta Tanzania, hivi hatuoni kuwa tunapoteza?

Kama tungekuwa tunafikiria vizuri tulipaswa kutengeneza mazingira wafanyabiashara wa nchi zinazotuzunguka Rwanda, Burundi, Zambia, Uganda & DRC wawe wanakuja kufunga mizigo hapa kwetu. Yaani ilitakiwa mtu akipiga hesabu kwa mzigo wa kawaida kwenda China, Dubai au Tanzania apate jibu bora niende Tanzania. Lengo hili hatuwezi kulifikia kwa aina ya kodi tulizokuwa nazo. Kwanza kodi zetu zinashawishi ukwepaji, yaani mfanyabiashara anashawishika kukwepa ili apate faida. Ni ukweli uliodhahiri mfanyabishara mdogo au wa kati akifuata masharti yooote na kodi zoooote za kibongo hawezi kutoboa. Hivyo, wanalazimika kukwepa kwa kutumia mbinu za kila aina.

Huwa najiuliza mfanyabiashara hata wa mtaani akifikia aina fulani ya mauzo anatakiwa kuandikishwa katika VAT kwahiyo bidhaa zake anatakiwa kuanza kuongeza 18%, wakati huo huo jirani zake ambao bado hawajafikia kiwango cha mauzo yake wanauza bidhaa ya aina hiyo bila 18%, kwa maana hii yeye hawezi kuuza tena akiendelea kuweka hiyo kodi. Sasa mfanyabiashara huyu unafikiri atakubali? Lazima atatafuta namna ya kuikwepa hii kodi ili aendelee ku-survive. Yaani kodi inamrudisha mtu nyuma hii sio sawa. Kodi ya VAT ilipaswa kuwekwa viwandani ili wanaokwenda kununua wakutane nayo hapo au kwa wafanyabiashara wakubwa wanaoagiza mizigo kutoka nje tu, na ipigwe pale mzigo unapoingia tu. Hawa wafanyabiashara wengine wapigwe kodi ya mapato pekee yake.
 
Tanzania tuna mfumo wa kodi ambao naweza kuuita ni 'Tax chain system'. Yaani ni kwamba bidhaa moja inaweza ikapigwa kodi hata mara kumi halafu wale watu walioilipia kodi mara ya 2 hadi ya 10 wanatakiwa wapeleke mahesabu TRA ili warudishiwe kodi yao;kivipi?

Mfano bidhaa imezalishwa kiwandani, mnunuzi wa kwanza atakayenunua atalipa 18% Vat, na hii tu ndio halali ya TRA kwa bidhaa hiyo, lakini kama huyu mnunuzi wa kwanza ataenda kuiuza itabidi atoe risiti ya EFD na atamlipisha tena mteja 18% Vat ambayo TRA itamdai, huyu nae akienda kuiuza itabidi atoe risiti ya EFD ambapo atamchaji tena mteja 18% VAT ambayo nayo itatakiwa kupelekwa TRA, and so on hata mara 10.

Ili kuepuka kulipa VAT mara mbili kila mfanyabiashara atapeleka mahesabu na risiti za VAT (kwa waliounganishwa na VAT) ili kujua kiwango cha ziada cha kile ambacho ameshalipa, na hicho tu ndicho atapaswa kulipa; hii process inaleta mlolongo mgumu na very complicated, yaani ni mfumo mgumu sana bila sababu, nadhani wote mnofuatilia haya masuala mtajua.

Lengo la TRA kung'ang'ania huu mfumo ni ili kupata 18% ya faida ya kila hatua ya uuzaji wa bidhaa, hata ikiuzwa mara 10 TRA hawajali, wanataka 18% ya ile faida (gross profit) ya kila mfanyabiashara katika kila chain link ya uuzaji wa bidhaa husika, hadi kwa final consumer, yule wa mwisho kabisa. (Wanakaba hadi penalti).

Hii inaweza kuonekana ni nzuri ukiitazama kwa juu juu, lakini in reality hii ni sawa na kutumia risasi kuwinda smaki baharini, unatumia 10shs. kukusanya shs.8, yeees, ukweli ndio huu. Badala ya kusababisha such an expensive practical complexity ni kwanini TRA isiwekeze instead kuhakikisha kodi yote ya kila bidhaa inalipwa palepale kiwandani bidhaa inapozalishwa au bandarini mzigo unapoingizwa, hata kama kodi ikiongezwa sio mbaya lakini ilipwe yote infull palepale kiwandani / bandarini.

Hebu fikiria tu harassment wanayopata wateja wanaposafirisha mizigo barabarani, watu husimamishwa hovyo hovyo na mapolisi 'Tigo' wale wenye silaha za kivita as if wanasimamisha jambazi, kumbe umebeba T.V tu ndio imekuwa nongwa, kwani hii T.V si imepitia bandarini??! Si mchukue kodi yenu yote huko huko muache wananchi waishi kwa amani?

Mateso kama haya walikuwa wanayapata wamiliki wa magari ambapo kila mwaka walipanga foleni TRA na office za MXMALIPO kulipia road license, tena barabarani TRA walipoteza nguvu kazi kubwa ya wasomi wenye madegree kusimamabarabarani eti kukagua sticker za road license, as if hizo gari hazitumii mafuta ambayo tayari yana kodi lukuki, binafsi nilianzisha uzi wa kupendekeza kodi hiyo nayo iunganishwe tu humo humo kwenye mafuta(Hivi ni kwanini road license isilipiwe kwenye mafuta?) watu waligoma goma ili mwishowe logic and common sense emerged victourious, serikali ikahamishia kodi hiyo kwenye mafuta na sasa hii kero imeisha

Muda mwingine umasikini tunajitafutia wenyewe kwa kukariri vitu vilivyopitwa na wakati, technolojia imekuwa, ni rahisi sana kukata kodi yote in full kwenye viwanda / bandarini, tubadilike bwana; nakaribisha maoni.

=================================
Update: 04/04/2021
Waziri wa Fedha na Mipango, Mwigulu Nchemba, amesema wanaangalia namna ya kutumia mfumo mpya wa ukusanyaji kodi

==========================
Update: 23/09/2022



===========================

V8 na matumizi ya hovyo ya wanasiasa yatatoka wapi wasipoendeleza mfumo wa kodi wa kiwizi na unyang'anyi?
 
Nilikua na haya mawazo toka siku nyingi mpaka nikasema uongozi unahitaji mtu ambaye ameshapitia kwenye biashara akapambana na marejesho ya benki, return n.k. Ila kama hujawahi kufanya biashara huwezi kuelewa kadhia.

Na pia anayepewa huu mzigo wa kodi ni yule mwananchi mtumiaji wa mwisho anayepokeaga khanga na kitenge wakati wa uchaguzi.
 
Mtoa hoja nakuunga mkono mtiririko wa kodi Tanzania unasababisha bei za bidhaa zetu kuwa kubwa sana na kuongeza gharama za maisha. Sijui kama wataalam wetu wamewahi kujiuliza jinsi gani hili jambo linatuletea hasara. Tanzania tumebarikiwa kuwa na bandari, bidhaa nyingi za nchi zinazotuzunguka zinapitia kwetu lakini bidhaa hizo hizo zikifika nchi za jirani zinapokwenda bei yake huwa rahisi kuliko hapa kwetu. Yaani wafanyabiashara wa kitanzania wanalazimika kwenda Uganda kuchukua mzigo na kuleta Tanzania, hivi hatuoni kuwa tunapoteza?

Kama tungekuwa tunafikiria vizuri tulipaswa kutengeneza mazingira wafanyabiashara wa nchi zinazotuzunguka Rwanda, Burundi, Zambia, Uganda & DRC wawe wanakuja kufunga mizigo hapa kwetu. Yaani ilitakiwa mtu akipiga hesabu kwa mzigo wa kawaida kwenda China, Dubai au Tanzania apate jibu bora niende Tanzania. Lengo hili hatuwezi kulifikia kwa aina ya kodi tulizokuwa nazo. Kwanza kodi zetu zinashawishi ukwepaji, yaani mfanyabiashara anashawishika kukwepa ili apate faida. Ni ukweli uliodhahiri mfanyabishara mdogo au wa kati akifuata masharti yooote na kodi zoooote za kibongo hawezi kutoboa. Hivyo, wanalazimika kukwepa kwa kutumia mbinu za kila aina.

Huwa najiuliza mfanyabiashara hata wa mtaani akifikia aina fulani ya mauzo anatakiwa kuandikishwa katika VAT kwahiyo bidhaa zake anatakiwa kuanza kuongeza 18%, wakati huo huo jirani zake ambao bado hawajafikia kiwango cha mauzo yake wanauza bidhaa ya aina hiyo bila 18%, kwa maana hii yeye hawezi kuuza tena akiendelea kuweka hiyo kodi. Sasa mfanyabiashara huyu unafikiri atakubali? Lazima atatafuta namna ya kuikwepa hii kodi ili aendelee ku-survive. Yaani kodi inamrudisha mtu nyuma hii sio sawa. Kodi ya VAT ilipaswa kuwekwa viwandani ili wanaokwenda kununua wakutane nayo hapo au kwa wafanyabiashara wakubwa wanaoagiza mizigo kutoka nje tu, na ipigwe pale mzigo unapoingia tu. Hawa wafanyabiashara wengine wapigwe kodi ya mapato pekee yake.
Hii ni moja ya comment bora nilizowahi kuziona JF toka nimejiunga 2013
 
Back
Top Bottom