Napendekeza jaji Samatta au Tundu Lissu kwenye nafasi ya uspika wa Bunge la katiba kwa sababu...

Napendekeza jaji Samatta au Tundu Lissu kwenye nafasi ya uspika wa Bunge la katiba kwa sababu...

Ningependa spika asiwe aliegemea upande wowote wa chama cha siasa. Hii itaongeza impartiality katika maamuzi. Hivyo kwa maoni yangu, Samatta sawa (naamini hajaegemea chama chochote!), Lissu hapana (ni gwanda).

Hata hivyo naheshimu mchango mkubwa wa Lissu na naamini anao uwezo mkubwa tu.


Nashukuru kwa mchango wako.
Nakubaliana na hoja yako kimsingi. Sasa fikiria kwamba samatta na mwapachu, hawatapata fursa ya kuwa wajumbe kwenye Bunge la katiba (mpka sasa siyo wajumbe) kati ya Mwapachu, Sitta, Chenge na Lissu ambao tayari ni wajumbe by virtue of Being wabunge wewe utampendekeza nani maana wote ni wanasiasa.
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Gazeti la Rai wiki hii limekuja na majina mengi lakini kati ya hayo mimi naona mwenye sifa ya kuongozi Bunge hilo la katiba kama tutaweka itikadi za kisiasa pembeni Jaji mkuu mstaafu Barnabas Samatta au Wakili Tundu Lissu kwa sababu;

Wote ni wanasheria makini wenye uwezo mkubwa sana wa kuchambua sheria ambyo ndo jambo litakalokuwa linahitajika sana ndani ya Bunge hilo.

Pili, Jaji Samatta na Tundu Lissu ni watu wasio na kashfa yo yote. Samatta mwenyewe aliwahi kusema wakati akiwa jaji mkuu kuwa ni heri hakimu mwadilifu mwenye uwezo mdogo kisheria kuliko hakimu mwenye uwezo mkubwa lakini fisadi. Kwa hiyo, yeye mwenyewe na Tundu Lissu ni wanayo sifa zote mbili -- uadilifu usiotiliwa shaka na uwezo mkubwa wa kuchambua mambo. Akina Chenge watatuchafulia mchakato wetu, wakae mbali na nafasi hii.

Nafahamu ugumu wa ccm walio wengi kutomkubali Tundu Lissu ndani ya Bunge la katiba kwa sababu za kisisa tu.
Hata hivyo, kuungana kwa NCCR MAGEUZI, CUF NA CHADEMA ambao wana wabunge wengi kiasi, ukijumlisha na wajumbe 166 ambao tunategemea hawatateuliwa na Rais na uwepo wa wabunge wanaccm wenye msimamo tofauti na chama chao wakiwepo hawa waliopinga sheria hii inayolalamikiwa kutoka bara, bila kusahau wabunge wa ccm wa zanzibar ambao wanaunga mkono msimamo wa kambi ya upinzani kwa siri, kunampa Lissu uwezekano wa kupata fursa hiyo hata kama ni kwa tabu sana.

Ikumbukwe kuwa, jambo la msingi ni kuptakiana kwa spika bora awe Jaji mkuu mstaafu samatta, Wakili Tundu Lissu au mtu mwingine ye yote kutoka po pote. Maombi yetu ni kuwa tusiwapate akina makinda na Ndugai kwenye jambo hili nyeti sana linaloshikilia mustakabali wa nchi yetu kwa miaka zaidi ya 100 ijayo.
Siku njema.
Nawasilisha.
Aweda.

Katiba ya Tanzania si jambo la kulifanyia mzaha kwamba hata punguani kama Tundu Lissu kutajwa kuisimamia.
 
Wengine waliotajwa huko ni Samweli Sitta, Andrew Chenge, Juma Mwapachu na Pius Msekwa na Jaji Samatta mwenyewe.

Jamani tuache ushabiki wa vyama. Katiba tunayotengeneza ni ya watanzania wote sio ya wana-CCM, CDM, CUF, NCCR etc na pia ni katiba ya vizazi vijavyo. Hao wote waliotajwa hapo juu including Tundu Lissu ni MAKADA WA VYAMA. Tunataka Spika ambaye atakuwa IMPARTIAL. Hayuko BIASED towards any political party. Mimi ningependelea kabisa kwa dhati ya MOYO wangu SPIKA wa BUNGE LA KATIBA awe Judge BARNABAS SAMATTA.

But again this is my wishful thinking, I bet my neck, kwakuwa mchakato wa katiba tayari umehodhiwa na CCM believe me Spika wa Bunge la Katiba atakuwa kada wa CCM! Hutakiwa kuwa a ROCKET SCIENTIST kutambua hilo. The writing is already on the wall.
 
Nashukuru kwa mchango wako.
Nakubaliana na hoja yako kimsingi. Sasa fikiria kwamba samatta na mwapachu, hawatapata fursa ya kuwa wajumbe kwenye Bunge la katiba (mpka sasa siyo wajumbe) kati ya Mwapachu, Sitta, Chenge na Lissu ambao tayari ni wajumbe by virtue of Being wabunge wewe utampendekeza nani maana wote ni wanasiasa.
Sitta (pamoja na matatizo yake) angeweza kufaa zaidi kwa sababu angalau ni mtu ambaye pande zote "mbili" za kisiasa zinaweza "kuishi" naye. Lissu hawezi kukubalika na upande ule mwingine, ni mwiba mkali kwao.
 
kama mtakataa Tundu lisu asiwe spika wa mbunge maalumu tutaitisha maandamano nchi nzima.

Dah, Maandamano hayo mngeitisha mwaka 2010 wakati Lisu alivyomwagwa na Mwanamama ANNA SEMAMBA MAKINDA
 
hata mimi napendekeza awe ni mzee samatta coz ni mtu makini sana.
 
Katiba ya Tanzania si jambo la kulifanyia mzaha kwamba hata punguani kama Tundu Lissu kutajwa kuisimamia.

Mkuu,
Mingoi, hata kama humpendi ni Lissu lakini nadhani kwa heshima aliyopewa na wananchi wake waliomchagua ni vizuri ukuapunguza ukali wa maneno. Kumbuka ukisema Lissu ni Punguani ina maana na sisi tunaomuunga mkono hapa JF umetutukana, Chadema wote anaowaongoza Bungeni kama mnadhimu umewatukana na kubwa zaidi watz wa Singida Mashariki waliomchagua nao umewatukana. Fikiria hilo unapochagua aina ya maneno ya kutumia kwenye jukwaa letu hili pendwa ili liendelee kuheshimika pia. siku njema.
 
Sitta (pamoja na matatizo yake) angeweza kufaa zaidi kwa sababu angalau ni mtu ambaye pande zote "mbili" za kisiasa zinaweza "kuishi" naye. Lissu hawezi kukubalika na upande ule mwingine, ni mwiba mkali kwao.

I get your point.
 
Katiba ya Tanzania si jambo la kulifanyia mzaha kwamba hata punguani kama Tundu Lissu kutajwa kuisimamia.

MKUU, Kuna kipindi CHADEMA walianzisha hoja ambayo niliiona ya msingi kuwa Spika wa Bunge asiwe Mbunge au kiongozi wa CHAMA CHA SIASA. Sasa nasikitika kuona Michael Aweda ambaye ana wadhifa ndani ya chama hichohicho anapendekeza Lisu ambaye ni mwanasheria wa chama chao kuwa Spika wa Bunge la Katiba. Hii maana yake ni nini, ni kuwa wanachotamka CHADEMA sicho wanachokimaanisha. Ukiongezea na hiyo sifa ya upunguani aliyonayo Lisu ndo kabisa CHADEMA wana mkakati wa kuliharibu bunge la Katiba
 
Mkuu,
Mingoi, hata kama humpendi ni Lissu lakini nadhani kwa heshima aliyopewa na wananchi wake waliomchagua ni vizuri ukuapunguza ukali wa maneno. Kumbuka ukisema Lissu ni Punguani ina maana na sisi tunaomuunga mkono hapa JF umetutukana, Chadema wote anaowaongoza Bungeni kama mnadhimu umewatukana na kubwa zaidi watz wa Singida Mashariki waliomchagua nao umewatukana. Fikiria hilo unapochagua aina ya maneno ya kutumia kwenye jukwaa letu hili pendwa ili liendelee kuheshimika pia. siku njema.

Mkuu, kuchaguliwa na wananchi si hoja kwani katika majimbo mengine, wananchi wamechagua mpaka wavuta bangi. wananchi wakati mwingine wanapiga kura za kukomoana kutokana na CCM kutosikiliza na kuzingatia machaguo ya wananchi. hayo yametokea katika majimbo ya Ubungo, Kawe, Iringa Mjini, Mbeya Mjini, Nyamagana, Arusha Mjini, Singida kwa Lisu na kwingineko
 
Mkuu,
Mingoi, hata kama humpendi ni Lissu lakini nadhani kwa heshima aliyopewa na wananchi wake waliomchagua ni vizuri ukuapunguza ukali wa maneno. Kumbuka ukisema Lissu ni Punguani ina maana na sisi tunaomuunga mkono hapa JF umetutukana, Chadema wote anaowaongoza Bungeni kama mnadhimu umewatukana na kubwa zaidi watz wa Singida Mashariki waliomchagua nao umewatukana. Fikiria hilo unapochagua aina ya maneno ya kutumia kwenye jukwaa letu hili pendwa ili liendelee kuheshimika pia. siku njema.

Wewe binafsi unadhani Lissu ni mtu mwenye akili timamu?
 
Mkuu,
Mingoi, hata kama humpendi ni Lissu lakini nadhani kwa heshima aliyopewa na wananchi wake waliomchagua ni vizuri ukuapunguza ukali wa maneno. Kumbuka ukisema Lissu ni Punguani ina maana na sisi tunaomuunga mkono hapa JF umetutukana, Chadema wote anaowaongoza Bungeni kama mnadhimu umewatukana na kubwa zaidi watz wa Singida Mashariki waliomchagua nao umewatukana. Fikiria hilo unapochagua aina ya maneno ya kutumia kwenye jukwaa letu hili pendwa ili liendelee kuheshimika pia. siku njema.
Punguani sio tusi bali ni sifa anayoibeba binadamu na kumbuka kuwa kiongozi si sifa wala kigezo cha kuwa una akili kupita wengine au uko timamu yanaweza pia kuwa makosa ya wananchi kuchagua na ndio demokrasia.
 
Mkuu, kuchaguliwa na wananchi si hoja kwani katika majimbo mengine, wananchi wamechagua mpaka wavuta bangi. wananchi wakati mwingine wanapiga kura za kukomoana kutokana na CCM kutosikiliza na kuzingatia machaguo ya wananchi. hayo yametokea katika majimbo ya Ubungo, Kawe, Iringa Mjini, Mbeya Mjini, Nyamagana, Arusha Mjini, Singida kwa Lisu na kwingineko
Hata Kilwa kusini kuna jamaa anajiita -----
 
HIvi mkuu Aweda wajumbe wa hilo bunge hata akina
LUSINDE
PROFESSOR MAJI
LA KAIRO
NCHEMBA
NKAMIA
SERUKAMBA .......
hawa nao watakuwa wajumbe?
naomba ufafanuzi
 
Hata Kilwa kusini kuna jamaa anajiita -----

Huyu ndio chizi kabisa, wabunge hasa wa upinzani hawana utaratibu wa kuchujwa na vyama vyao. Huko ukiwa mpigaji kelele za kutosha unapata kuwa mbunge. Orodha ya wabunge machizi ni ndefu mno ukimuongeza na Machali pia.
 
Huyu ndio chizi kabisa, wabunge hasa wa upinzani hawana utaratibu wa kuchujwa na vyama vyao. Huko ukiwa mpigaji kelele za kutosha unapata kuwa mbunge. Orodha ya wabunge machizi ni ndefu mno ukimuongeza na Machali pia.

Nakushukuru Mkuu. Tuendelee kuorodhesha majina ya wabunge wao ambao wanajipa sifa kumbe akili zao si timamu hata kidogo. hapo hatujaweka wale wasagaji
 
HIvi mkuu Aweda wajumbe wa hilo bunge hata akina
LUSINDE
PROFESSOR MAJI
LA KAIRO
NCHEMBA
NKAMIA
SERUKAMBA .......
hawa nao watakuwa wajumbe?
naomba ufafanuzi

Mkuu, hao hawakosekani na ndo watakaofanya siku Lisu akipendekezwa na akina AWEDA apandishe ukichaa wake mara moja. Umemsahau na Dk Hamisi Kigwangallah
 
HIvi mkuu Aweda wajumbe wa hilo bunge hata akina
LUSINDE
PROFESSOR MAJI
LA KAIRO
NCHEMBA
NKAMIA
SERUKAMBA .......
hawa nao watakuwa wajumbe?
naomba ufafanuzi
Z
1237039_558673150836333_73024561_n.jpg


Huyu naye mwenye suti ya kijivu ni mjumbe tena ni msaidizi wa karibu na Tundu Lissu

 
Back
Top Bottom