Napendekeza jaji Samatta au Tundu Lissu kwenye nafasi ya uspika wa Bunge la katiba kwa sababu...

Napendekeza jaji Samatta au Tundu Lissu kwenye nafasi ya uspika wa Bunge la katiba kwa sababu...

Wengine waliotajwa huko ni Samweli Sitta, Andrew Chenge, Juma Mwapachu na Pius Msekwa na Jaji Samatta mwenyewe.

waliotajwa wote ni weledi ukiondoa mzee wa vijisenti. hakuna mtanzania anayemwamini andrew, nionavyo mimi, bila kuchanganya siasa, juma ,pius au sitta wanaweza kuleta mezani kile watanzania tunataka. Lissu anafaa sana ila kwa hali ya woga tuliyonayo watz sidhani kama endapo mambo yataenda mrama kuna atakyehoji mambo...kwa maana iyo Lissu aachwe huru akiwa watchdog ukumbini. Akikaa mezani hatoweza kuleta mawazo yake ambayo kiukweli wengi tunayatemgemea yaboreshe. Lissu aachwe huru aweke mambo sawa endapo hali itakwama ktk ufafanuzi,miongozo na utaratibu... Ebu twende nje ya boksi, kwa kuwa tunatunga sheria mama ya nchi, kwa nini tusifikirie wale majaji wa mahaka kuu kusimamia iyo sheria?natambua ni muhimili mwingine ila ktk kuweka taifa mbele ebu tusijiminye kwenye mihimili wooote tushirikiane. ni mawazo yangu tu.
 
Lisu kwa sasa ni janga sugunla wazawa hafai msikitini wala kanisani.
 
Samatta anaweza lakini Lissu hafai hata kidogo. licha ya kuwa anaongozwa na uchadema lakini pia ataongoza bunge kwa misingi ya uongo, uzushi, uzandiki na husda


Kamanda Mikael,

Mimi natofautiana na wewe kuhusu tundu lisu kuwa SPIKA kwa sababu, spika si msemaji kwenye lile bunge kwa hiyo wananchi wengi watakosa mtu makini wa kuwawakilisha vizuri.

Tundu Lisu anatakiwa awe msemaji mkuu wa VYAMA vya Upinzani ili awakilishe vizuri na aweze kutoa ufafanuzi mzuri wa kisheria.

Badala yake Prof Safari au Mabere Marando anaweza Kuwa Spika wa Bunge la Katiba kuziba nafasi ya TL.
 
"Nafahamu ugumu wa ccm walio wengi kutomkubali Tundu Lissu ndani ya Bunge
la katiba kwa sababu za kisisa tu.
Hata hivyo, kuungana kwa NCCR MAGEUZI, CUF NA CHADEMA ambao wana
wabunge wengi kiasi, ukijumlisha na wajumbe 166 ambao tunategemea
hawatateuliwa na Rais na uwepo wa wabunge wanaccm wenye msimamo tofauti
na chama chao wakiwepo hawa waliopinga sheria hii inayolalamikiwa
kutoka bara, bila kusahau wabunge wa ccm wa zanzibar ambao wanaunga
mkono msimamo wa kambi ya upinzani kwa siri, kunampa Lissu uwezekano wa
kupata fursa hiyo hata kama ni kwa tabu sana"

Mkuu aweda hicho ulichokiandika hapo juu ndicho wasichokita ccm kukisikia,duniani wala mbinguni,thus why wanataka rais ateue wajumbe wa bunge la katiba ila wingi wa ccm na uhai wa ccm bungeni uendelee,

hizi tabia zetu za kutoa mbinu hadharani zitatucost sana,mara nyingi tumejikuta tukiwapa ccm majibu ya maswali magumu yanaowatatiza kila kukicha.

Mie napendekeza spika wa bunge atokane na wale wajumbe 166 ili asipendelee chama chochote
 
ni bora dr fastjet ajiuzulu kuliko akubali Lissu awe spika wa bunge la katiba.
 
Hilo la Lissu kuwa mwongo, mzushi, mzandiki na husda limeshajibiwa kama ifuatavyo,
Mosi, madai ya Lissu kwamba TEC, CCT na Shivyawata hawakuwakilishwa katika Tume ya warioba yalitolewa na taasisi hizo tatu, je, umewahi kusikia taasisi hizi tatu zikipinga kauli hiyo?
Pili,madai ya Lissu kwamba Zanzibar haikushirikishwa waziri Chikawe na hata Rais mwenyewe wameshakubali kuwa ni kweli.
Madai ya Lissu kuwa wajumbe 166 watatoka kwenye taasisi gani bado yako pale pale na kwamba chadema inapendekeza utaratibu tofauti ambao bado tunausimamia mpaka sasa.

NB; Kauli ya Lissu Bungeni siyo yake, ni kauli ya kambi ya upinzani kwa hiyo, kama Mnyika alivyosema, matusi hayo yasielekezwe kwake kwa sababu ule ni msimamo wa chama na siyo msimamo wa Lissu kwa kiutaratibu na kwa mujibu wa kanunu za Bunge.
Sawa mkuu?
Hiyo haiondoi ukweli kuwa Lissu ni muongo, mzushi mzandiki lakini bila kusahau kuwa ana kic.........
 
Kimsingi nakubaliana na hoja yako, lakini je, ni lazima spika asitoe maoni yake? Mimi nadhani itategemea kanuni watakazojiwekea itakavyokuwa. Ikumbukwe pale hakuna vyama au pande mbili zinazotofautiana. Watz wanaojenga mstakabali wa nchi yetu kwa faida ya vizazi vijavyo.

Nimefuatilia sana hoja zako mkuu. ila hapo penye redi mimi nakupinga kabisa. wabunge watakaopendekezwa na vyama watatetea maslai ya vyama vyao, navile vile asasi zingine zitakazotoa wabunge zitafanya vile vile. Tatizo kubwa hapa ni mfumo mzima walioutengeneza kupata wabunge wa bunge maalum la katiba. na ndio maana wengi walitaka kila chama kitoe idadi ya wabunge sawa bila kujali ukubwa wa chama na idadi ingine itoke kwenye asasi ziingine, na ikizingatiwa ilo nina imani uccm na uchadema utakua umekufa. Na upande mwingine tushukuru Mungu Chadema wamekuwa mstari wambele kutuwakilisha watanzania japo wanapata wakati mgumu kutokana idadi yao kuwa ndogo.
Tukija kwenye swala la Lisu kuwa speaker wa bunge la katiba sio mbaya kiutendaji kwa kwa asilimia 100 ataimudu vema hiyo kazi. Ila tatizo tutakosa mchango toka ccm kwasababu katika jambo ccm wanaloliogopa hapa duniani ni Tundu Lisu
 
Tundu Lissu kwenye uspika hapana,siyo kwamba hafai ila mchango wake utakua wa muhimu sana kama akiwa kitini kuliko mezani,nadhan mzee samatta anafaa tu.
 
Tuachane na hawa wazee ambao wamechoka na wengine wamechanganyikiwa Kimaisha. nampendekeza Wakili Edwin Simon Igenge kuongoza jahazi hilo. huyu jamaa ana uwezo mkubwa sana na ni mzalendo
Unamaanisha Jaji Samatta akachoka na kachanganikiwa? kweli magamba mnawatukana wazee nape alisema wazee wanasubili kufa leo wewe gamba mwingine unakuja kuwa wamechoka na kuchanganyikiwa>
 
Back
Top Bottom