Napendekeza kwenu kuwa Ridhiwani Kikwete atatufaa sana Urais baada ya Magufuli

Napendekeza kwenu kuwa Ridhiwani Kikwete atatufaa sana Urais baada ya Magufuli

KooZito

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2020
Posts
397
Reaction score
1,377
1610083847217.png

Wanabodi,

Miaka mitano ya Rais John Pombe Magufuli si mingi. Itaisha muda si mrefu.

Ninajua 2015 vijana wengi wa CCM walijitokeza kuutaka Urais wakiwemo January Makamba, Mwigulu Nchemba hata Hamisi Kigwangala lakini wote waliangukia pua baada ya kuachwa kwenye mchujo.

Kwa mwaka 2025 kwa mtazamo na maoni yangu twende na kijana Ridhiwan Kikwete. Kijana huyu ni mnyenyekevu, hodari, mchapakazi, msomi, muumini wa haki za binadamu na haiba ya kiuongozi.

Riz amezaliwa na kukulia familia ya utawala na hivyo kuwa na uzoefu na si wa kuokota dodo chini ya mwembe. Anatufaa maana hana tamaa ya madaraka.

#RK2025
 
Mambo mengine kabla ya kupost uwe unashaurisha watu wanaokuzunguka.

Umeandika pumba tu hapa, Huyu hata ukatibu wa wizara hafai.
Endelea kumfuatilia kijana huyu. Ni kiongozi makini sana.
#RK2025
 
Baada ya hapo afuate Jesca Magufuli.
Kama atakuwa na sifa mujarabu kama za mwenzie hakuna shida
Unataka wote humu tuuze madawa ya kulevya
"madawa ya kulevya" ndio nini au ulitaka kusema "dawa za kulevya?" Kama la pili ni sahihi basi unakosea. Hata baba yake akitaka Urais 2005 tuliimbiwa sana ni mgonjwa wa Ukimwi lakini ametuongoza kwa salama sana.
 
Madawa ya kulevya kila kona

Majenereta ya umeme kila duka

Kuunda makampuni ya kuiuzia umeme TANESCO

Ufaulu sekondari mpaka division six

Wake zetu kwenda kusuka nywere Marekani

Kuondoa machinga kwa kuwa ni uchafu

Aisee naunga mkono hoja.
 
Ni maoni yako na ni lazima na wala siyo hiari ya heshimiwe.

Bila shaka umekuwa ukiona Mh Rais akiteuwa viongozi waliotokea upinzani kuwa mawaziri ma RC, ma DC, Mabalozi nk..nk... na wamekuwa wakifanya vizuri to the satisfaction ya Mh. Rais, kwangu mimi hii inaonesha upande ule kwa sasa hakuna leadership material,hivyo basi tujaribu upande mwingine.
 
Madawa ya kulevya kila kona

Majenereta ya umeme kila duka

Kuunda makampuni ya kuiuzia umeme TANESCO

Ufaulu sekondari mpaka division six

Wake zetu kwenda kusuka nywere marekani

Kuondoa machinga kwa kuwa ni uchafu

Aisee naunga mkono hoja.
Kwani amewahi kuongoza lini hayo yakitokea? Tazama Zanzibar chini ya Hussein itakavyopaa. Kiongozi huandaliwa. Mtazame Kenyatta.
 
Hii nchi ni ya ukoo mmoja tu hamna watu wengine, majina mengine
 
Kwahiyo wewe uliyeandika hufai kuwa Rais kwa kuwa tu baba yako hajawahi kua Rais?

Mbona Magufuli amekua Rais na hajakulia kwenye familia ya wanasiasa?

Mimi ninadhani labda hoja iwe uzoefu, elimu, namna ya kutatua changamoto za wapiga kura wake nk
 
Sema umekataa wewe usiwasemee wengine. Sioni kijana wa kushindana na Ridhiwani katika medani ya uongozi. #RK2025
Amefanya kitu gani cha maana.

Kwenye Urais huko mbali hebu tumkague kwenye nafasi yake ya Ubunge tu amefanya nini cha maana, kuna ushujaa gani wa maana alioufanya hadi wewe ushawishike kwamba anafaa Urais.

Ina maana wewe hutaki kwenye ukoo wenu atokee Rais hadi unashabikia familia ya wenzako waendelee kurithishana vyeo halafu wewe unafaidika nini? Kujikomba kwingine mpunguze jamani, jifunze kubalance shobo hata kidogo.

Katika pumba zote zilizowahi kutokea Jf hii imezidi.

Ni bora hata ungesema Paul Makonda kidogo inaingia akilini kwa sababu uchapakazi wake ulikuwa unaonekana kuliko kumpendekeza huyo mla bata aje kuwa Rais.
 
Back
Top Bottom