Napendekeza serikali ifunge projector madarasa yote shule za msingi badala ya kuajiri walimu, hii itasaidia kuokoa takriban trillion 3 Kwa mwaka

Hapo unakuta kuna watu wanakuita baba au mama
Kuleta dhihaka bila hoja yeyote ni kujiweka level moja na kenge, maana hata kenge angeweza kucomment hiki ulichopost bila hoja yeyote ndani yake.
 
Ukienda kwa mfumo huo serikali haitoajiri mtumishi yeyote siyo nurse,trafiki,askali na hata mahakimu itatumika projector kuamua kesi zilizo wasilishwa mahakamani,

Automatic mashine kufanya operation na kuzalisha wanawake.

Robot kukamata wezi na vibaka mtaani na kuzuia uharifu.

Robot kulinda mabenki.

🚦 kuongoza watu nchi nzima na mizani ya automatic, toch za kupima mwendokasi.

Kesho kutwa unakuja na msemo "Serikali haiwajali watoto wa masikini".

Hebu kua kwanza ndipo ufahamu umuhimu wa kuajiri na kuajiriwa
 
Ukiandika upumbavu tutakujibu upumbavu. Siwezi kuumiza akili kukujibu wewe mpuuzi uliyeandika kwa chuki kabisa dhidi ya waalimu.
Hapa unakuwa huna tofauti na mbwa, kama umekerwa kweli na hoja yangu, basi pangua hii hoja kwa hoja, vinginevyo utakuwa sawa na mbwa tu, maana hata mbwa anaweza kunijibu kwa kubweka tu, tayari nalo linakuwa ni jibu. Jitofautishe na mbwa, bweka mibweko yenye hoja ndani yake.
 
Acha upuuzi
 
Unapokuwa na tatizo, huna laxury ya kuchagua sana, unafanya kile kinachowezekana the best you can.
Hapo tatizo ni lipi na linatatuliwa vipi ? Au ni mwendelezo wa quantity (so called wasomi ni wengi) wakati quality (nothing to show for it) zaidi ya vilemmas (wanakariri)

Waanze kwanza kushusha bundle watu wajitafutie nondo, kwa sasa hata wenye uwezo na wangeweza kusoma online wanashindwa kutokana uroho wa serikali kukusanya Tozo
 
Kuleta dhihaka bila hoja yeyote ni kujiweka level moja na kenge, maana hata kenge angeweza kucomment hiki ulichopost bila hoja yeyote ndani yake.
Kwa matusi haya ndiyo unashauri serikali isiajili waalimu na madaktari?.🤔🤔🤔
 

Hiyo suruhu kwa tatizo lililopo nadhani sio sahihi. Labda nikuongezee wigo wa uwelewa labda kama wewe sio mtanzania

Incompetency kwenye kazi ni tatizo sio kwa walimu tu bali tatizo linalo ota mizizi sana kwenye kada mbalimbali za majukumu ya kazi.

Wahandisi, madaktari, polisi/trafiki, kilimo nk

Kuna wakati unakuta mtu kaajiriwa serikalini na mshahara mkubwa tu lakini ukipima reasoning yake tu kwa hicho kitengo chako unaweza kuzimia.

Kiufupi kuna vijana wengi tu wamesoma vyuoni na kupata gpa nzito lakini reasoning,performance ,creativity, endurance, vyote viko about 0.

Sidhani kama kweli walimu wote shule x wanaweza wakawa shallow kwenye knowlege.

Ninaimani wapo walimu maturusa na wapo walimu ni smart sana vichwani.

Si watoto wote wanauwezo wa kufuatilia vipind recorded labda kama ni katuni na muziki ama tamthilia.

Watoto wanahitaji mwalimu wa kuwa nao na kuwaelekeza nini cha kufanya na wao kumuliza maswali hapohapo na kubadilishana activity.
 
Watanzania wako milioni 60 walimu wako almost 200k

Na population growth inakuwa kubwa Kila mwaka.

Ratio ya mwalimu na mwanafunzi ni 1:45.

Still bado haijafikiwa kwa Sasa yawezekana ni 1:120 huko[emoji1]

Tufanye mwanao nae anasoma kati ya hao 120 ataelewa kweli!?. Si araishia kuwa kilaza halafu uje kuwananga WALIMU.

Serikali haiwezi avoid kuajiri walimu Kila mwaka ni takwa la population growth. Watoto wanaoandikishwa Kila mwana idla mwaka idadi yao inaongezeka maradufu.

Ndio maana serikali Kila uchwao wanajenga madaraja mapya kwa Kasi ila kuajiri walimu kwa mwendo wa Kobe.

Hatuwezi kuwa taifa lililoendela ikiwa tu elimu yetu tubaipeleka tu kwa mawazo ya kilevivile bila kuzingatia demand,supply, balance,ratios,na mengineyo

Nafikiri ulitoa hayo mawazo bila kufikiria.
 
Tena wanafunzi wa shule ya msingi kabisa unategemea waelewe kwa njia hiyo????
 
Watakuelewa Watu wachache sana katika hili. Mara nyingi hoja zako uko straight foward it means hutak blah blah wala kona kona. Kwa nature ya Waswahili watakuona hufai au mchawi lkn deepside ushauri wako kuna pahala unafanyakazi na unatija kwenye baadhi ya maeneo na tasnia
 
Anyway, tuache muda ukifika na wakatekeleza, as they always do, nitarudi kuweka update. Kwa sasa ngoja nifanye yangu tu.
 
Mkuu hii njia haiwezi kuwa rafiki kwa primary level na secondary level kwa nchi zetu za dunia ya 3.

Watoto wa Primary inabidi wakifunze chini ya uangalizi, shule sio masomo tu kuna vingi mtoto huandaliwa na kufundishwa.

Kwa watoto wa kiafrika ukiwaacha wenyewe hata hilo darasa watacheza tu na shule itakuwa kiwanda cha ujinga.

Hiyo idea itumike kwenye level za vyuo kuanzia cheti na kuendelea ambapo kuna watu wanajielewa
 
Ulikuwa na hoja ya msingi. Lakin kichwa chako mavi tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…