Napinga Daladala kuingizwa kwenye BRT

Napinga Daladala kuingizwa kwenye BRT

Hiyo mwendo kasi ni sikio la kufa. Gari inaweza toka Kimara mpaka Jangwani ipo tupu inarudi yard. Kwa akili za kawaida kibiashara inategemewa ibebe walau abiria wanaoshukia njiani mpaka Jangwani lakini inawapita abiria vituo vyote mpaka inafika Jangwani. Watu wameshatoa sana maoni ya maana hapa JF na mpaka wao wenyewe walikuja wakafungua uzi wao hapa lakini hakuna hata ushauri moja waliotekeleza kwa nini kampuni isife?

Serikali iruhusu wafanya biashara wenye uwezo na uzoefu kwenye sekta ya usafiri kama Bakheresa, Abood, Shabiby na wengineo wapewe baadhi ya ruti kwa mfano Bakharesa unampa ruti ya Mbezi - Kariakoo na Abood unampa ruti ya Mbezi - Feri tu hakuna kusimama mahali. Hapa kati anabaki mwendokasi na mabasi yake mabovu ndio akili za kibiashara zitawakaa.

Serikali kama ina nia kweli ya kuondoa tatizo la usafiri kwa watu wa Dar iruhusu usafiri walau coaster chache zenye AC level seat ila waruhusiwe kuongeza nauli kidogo kwa mfano Kimara - Posta nauli iwe 1,500. Mwenye uwezo wa kupanda dala dala apande, mwenye uwezo wa kupanda coaster apande na hata mwenye uwezo wa kupanda mwendokasi apande. Ikumbukwe kuwa sasa hivi coaster nyingi zile zilizokuwa zinasafiri kwenda mikoani usiku maarufu kama hakuna kulala hazina kazi baada ya mabasi makubwa kuruhusiwa kusafiri usiku.

Ni mtizamo tu.
Kwa msisitizo hizo coaster ziruhsiwe chache kila ruti na zibebe level seat tu watu wanne wanne tu bila kusimamisha abiria ili zisije kuua biashara ya daladala za kawaida ambazo ni msaada mkubwa sana kwa watu wa kipato cha chini.
 
Hapa wakisoma lazma wacheke kwa nguvu 😁😁

Umaskini uliopo ni reflection tosha ya uoga wetu na labda tusubiri hiki kizazi kiburi, jeuri na chenye mawazo huru "2000 kids" Maana wanaonesha matumaini ya uthubutu ila hiki kilichopiga kura kati ya mgombea na kimvuli. Sahau mkuu 😁
Wewe unataka ufike kazini kwako au unataka mradi WA brt!? Zingatia Zaidi Mambo Yako acha wivu
 
Ni wazo zuri hasa kwa watumiaji wa huo usafiri angalau wapate usafiri kwa wakati kuliko huu usumbufu unaoendelea, changamoto ni usalama kupanda na kushuka kwa abiria pamoja hasa kwa muundo wa vile vituo vya mwendokasi BRT na mlango wa hizo daladala
 
Hii ndio serikali ya mama na anaupiga mwingi ila **** watu wanamuhujumu mama ili 2025 aonekane kituko. Washajua wapo na uongozi dhaifu kwanini wasiwafanyie madudu
 
Wewe unataka ufike kazini kwako au unataka mradi WA brt!? Zingatia Zaidi Mambo Yako acha wivu
Mkuu hiyo kazi sina ndio maana kila jioni ikifika huwa naenda posta ya zamani kucheki view bora kabisa ya BRT. Sasa wakiweka na daladala wataharibu
 
Hii ndio serikali ya mama na anaupiga mwingi ila **** watu wanamuhujumu mama ili 2025 aonekane kituko. Washajua wapo na uongozi dhaifu kwanini wasiwafanyie madudu
Anajihujumu mwenyewe
 
Ndio maana sipendi kufuatilia siasa za tz maana zinaniumiza kichwa tu

Wanasiasa wanawategemea sana watanzania wenye kufikiri Kama wewe kuhusiana na siasa, ndio mtaji wao mkuu.


Lakini kumbuka tu ni mambo mabaya pekee ndio yanayoumiza kichwa, mazuri yanatuliza akili na kuruhusu kichwa kufanya kazi.

Na mambo hayo mabaya hayajiondoi, kadiri uhisivyo maumivu ndivyo ari ya kuyaondoa inavyopanda na njia kuzidi kufunguka.

Siasa ndio Mfumo wa binaadam wa kulinda maslahi yake hapa duniani.
 
Ule mradi wao wanaungangania kuendesha wakati wao kuendesha
Hawawezi na hawatokuja kuweza kuendesha...wampe tu mwekezaji/mtu binafsi tu
wao wanachoweza ni kuchota mijihela na kula basi

Ova


Nionyeshe Mradi mkubwa aliowahi kupewa mwekezaji hapa Tanzania na ukafanikiwa kwa asilimia angalau 95 na wananchi wakafaidi kwa 100%??

Vinginevyo unazungumzia kubinafsisha?

Watanzania tuna kasumba chafu. Watu wanahujumu miradi ya kitaifa makusudi ili wapewe wao hiyo miradi ama wapewe udalali wa kutafuta wawekezaji ili wapate uhakika wa 10% kila Mwaka wa mavuno!

Kibaya zaidi tunalindana na kuitana Miamba vichochoroni huku nchi ikizidi kurudi nyuma badala ya kusonga mbele!

Kibaya zaidi hao wawekezaji wanaoletwa kila mara nao ni wapigaji Sawa na hao madalali wao!!

Facken kabisa!
 
Mkuu hiyo kazi sina ndio maana kila jioni ikifika huwa naenda posta ya zamani kucheki view bora kabisa ya BRT. Sasa wakiweka na daladala wataharibu
Hope watatumia mixed Lane na Sio special Lane za brt
 
Halafu kuna wapumbavu wanadai tuendeshe wenyewe bandari? DP World ije tu kwasababu hata mradi wa mabasi umetushinda.
 
Back
Top Bottom