Napinga hoja ya RC Makalla ya kulazimisha Mabasi yote ya Mikoani kupakia na kushusha abiria Stendi ya Magufuli pekee

"The patience of the bricklayer is assumed by the architect". Makala ndiyo architect hapa. Mipango yake haichukulii abiria watatesekaje. Kwani watamfanya nini? Ilitakiwa viongozi wa kisiasa wa mkoa wachaguliwe kwa kura za wananchi!

All these are consequences of a fundamental flaw. Katiba mbovu. Kwa katiba nzuri amri kama hii inakuwa ni kitu kinatokana na majadiliano ya madiwani na kupigiwa kura. Ikipita ndiyo inatangazwa. Kwa sasa ni Ayatollah Makala anasema apendacho na kinakuwa amri.
 
Samia bado anazungukwa na genge [SUKUMA GANG] , hawa watamtesa sana mpaka atakapo wa-phase out.
Huyu Makala siku moja atoke kwake kimanzichana kwa Daladala , aende Stendi mbezi kuwahi basi la saa 12 asubuhi, ndio ataelewa adha wapatazo wananchi.
Ukitoka kimanzichana saa nane usiku unafika saa 11 alfajiri mbezi, hapohujakata tiketi then uanze safari.
Hii nchi ina watu wa mihemko kuliko.
 
Hii nchi wanasikilizwa machinga na bodaboda tu,kundi hili Lina nguvu kubwa Sana ya ushawishi Kwa wanasiasa.
Hii yote imetokana na mwendazake kuwaona machinga, bodaboda na mama lishe ndiyo vipaumbele.

Sikuhizi ukipita mitaa ya Kariakoo na posta utakutana na mama lishe wanapika pembezoni mwa barabara yaani ni mwendo wa Moshi wa kuni city centre
 
Unafananisha Mwanza na Dar? Mtu wa Mbagala kwenda Mbezi Mwisho inabidi aamke saa 8 usiku ndipo atawahi basi
 
unajua kua pale stendi ya magufuli hakuna kampuni inaruhusiwa kupaki magari matano kwa wakati mmoja,na ilihimizwa wale wenye mabasi mengi kua na private places kuhifadhi mabasi.kunatofuati ya kupitia stendi kuu na kushusha abiria,pia hizi private stations nazo ni za kulipia sio bure.
 
Wewe umeongea point at least. Umetufungua akili zaidi
 
Nchi hi tuna viongoz ambao problem creators na sio solvers
 
usichanganye mada hakuna aliyepinga stendi kwenda mbezi kinachozungumzwa na suala la kulazimisha abiria kushushwa na kupakiwa ndani ya stendi ya mbezi.
 
huyu MAKALA atakuwa mkuu wa mkoa alietumikia muda mfupi sana Dar es Salaam.

yaani naishi Tabata kuna option ya kushushiwa Ubungo unanilazimisha nishushiwe huko porini Mbezi ili iweje?
Miaka 15 hapo mbezi patakua city,,ile stand imejengwa kwa kufocus miaka 20 mbele,,sio leo
 
Katika makosa makubwa Mama amefanya ni kumleta Makala Dar, alishindwa Mbeya akahamishiwa mkoa mdogo huko Rukwa/Katavi akashindwa, ataiwezaje Dar?

Badala ya kuja kutatua kero amekuja kuongeza kero, he is not for citizens
Mimi naona ni vizuri kila upande zinapoingia Barabara kuu kuwa na stendi kwa mfano kwa DSM upande wa kila road kuwe na stendi kubwa,barabara ya Nyerere(zamani Pugu road) na bagamoyo road hata katika miji mwingine tunaona Dodoma japo nao hawako vizuri sana halafu katikati kuwe na shuttle ya daladala
 
Wahakikishe basi za uda zinaoperate masaa 24 kutoka hiyo stand,,hiyo ndo simple solution..
 
Ila kuna miji imedumaa,,mfano shinyanga,,stand iko porini,na ukiachwa hapo usiku,unaweza hata kuliwa fisi..😂😂
 
Ni wazo zuri sana, hata hizo stand zingeungwa kwa mtandao wa trams za uhakika ingekuwa jambo la kipekee sana
 
Nilikutaga mamantilie anasukuma chapati kwenye veranda ya Mwanza Hotel,,ndo nikajua kumbe tuko choo cha kike..
 
Sasa hakutakuwa na maana ya stand watu wazoee tu hivyo hivyo daladal,bajaji,boda machinga wenye maduka yanayozunguka stand hiyo watakosa wateja
Mtu baada ya kununua maji ya kunywa stand anaenda kushushiwa huko shekilango mwisho stand inakuwa sio ishu watu watashindwa hata kufungua migahawa kwa kuhofia watakosa wateja
 
Kazi kubwa ya stendi ni mabasi kushusha na kupakiza abiria karibia na mahali wanapoenda au kuishi sio huo ugoro mwingine wa ziada unaouzungumizia wewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…