Narudia tena, Mafundi gereji msipojiongeza mtaishia kutengeneza gari za mwaka 90

Narudia tena, Mafundi gereji msipojiongeza mtaishia kutengeneza gari za mwaka 90

kwasababu sahivi huumwi siyo? Ngozi nyeusi iskie tu. Ngoja upatwe na chochote mbio kwa madaktari haohao unaowakebehi sasa hivi.
Ngozi nyeusi imekukosea nini, yani watu washindwe kusema uchafu wanaokutana nao huko mahospitalini kwakua ni ngozi nyeusi?

Hosptali za maana hapa Tz zinajulikana, huko kwingine ni ujinga tu.
 
Siyo mafundi tu; binafsi hapa Tanzania naona Kada zote hufanya kazi zao kwa kubahatisha..

Hata hawa Madaktari wetu, wengi wanabahatisha kwenye kutibu wagonjwa..

Wanasiasa ndiyo usiseme, na Uchawi wanatumia ili kufanikisha siasa zao Uchwara..

Tanzania ni maeneo machache sana wanazingatia Professionalism kwa asilimia 100%..

Nadiriki kusema Ikulu yetu pamoja na Wizara na Ofisi zote za Umma ndiyo Vinara wa kufanya mambo Kikanjanja kanjanja..
Ahsante, ahsante!
Umemaliza
 
Nyundo haikwepeki..
Hata mimi ningekuwa fundi ukija na Toyota lazima niipige nyundo ili nijue tatizo..Gari ngumu kila mahali..Haina sensors za kugundua tatizo.. Hainyumbuliki.. Lazima uilegeze na nyundo..!
Ila Mjerumani nitasita kidogo..!

Ishu ni aina ya nyundo inayotumika..
Kuna wooden mallet.. rubber mallet..!
 
Siyo mafundi tu; binafsi hapa Tanzania naona Kada zote hufanya kazi zao kwa kubahatisha..

Hata hawa Madaktari wetu, wengi wanabahatisha kwenye kutibu wagonjwa..

Wanasiasa ndiyo usiseme, na Uchawi wanatumia ili kufanikisha siasa zao Uchwara..

Tanzania ni maeneo machache sana wanazingatia Professionalism kwa asilimia 100%.
Mkuu umenena vema sana.
 
Nyundo haikwepeki..
Hata mimi ningekuwa fundi ukija na Toyota lazima niipige nyundo ili nijue tatizo..Gari ngumu kila mahali..Haina sensors za kugundua tatizo.. Hainyumbuliki.. Lazima uilegeze na nyundo..!
Ila Mjerumani nitasita kidogo..!

Ishu ni aina ya nyundo inayotumika..
Kuna wooden mallet.. rubber mallet..!
Kwa nini utasita kidogo kwa Mjerumani?
 
Nunueni magari ya manual, ya diesel yasiyotumia umeme mwingi
Nadhani unazungumzia engine za diezel za miaka ya 90's and before kama vile 1HZ.

Engine za diesel zina umeme mwingi afadhali ukutane na engine ya petrol.

Mfano tu 1KD, injector pump ina sunction control valve na temperature sensor. Common rail yake in pressure sensor na pressure regulator. Nozzle zote ni za umeme na zina control yake. Huo ni mfumo tu wa kuinject mafuta kwenye engine, hujagusa turbo, hujagusa air intake.

Mind you ,hiyo ni engine ya mwaka 2000 halafu ni toyota. Hapo hujakutana na engine ya mercedes.
 
Back
Top Bottom