Narudia tena, Mafundi gereji msipojiongeza mtaishia kutengeneza gari za mwaka 90

Narudia tena, Mafundi gereji msipojiongeza mtaishia kutengeneza gari za mwaka 90

Tatizo la mafundi kukubali ukweli ni mgumu sana. Halafu wanapata pesa kwa kukadilra ndio maana wamelizika.

Mifumo ya magari sasa imebadilika ndio maana Nissan zinawashinda na kundandia kusema kimeo kumbe nyie ni vimeo.

Swala la vifaa ndio kabisa yani na mkuta fundi anatumia nyundo kuondoa kitu kwenye matairi mpaka unachoka.

Magari yanayo toka yanatumia electronic na umeme mwingi sana kuliko mlivozoea gari zenu 90.

Kila siku mnaunguza magari ya watu.
Unajuwa inatisha sana alafu ni ukweli mchungu
 
Uswahili upi we ndo mjinga watu msiomiliki magari mnashida sana, mfumo wa umeme uko tofauti sana na wa diesel/petrol
Ona sasa unavyo ropoka. We unadhani Wabongo wanauwezo wa kumiliki hayo magari unayo yaona kwenye muvi? We unamiliki aina gani ya gari kwanza?
 
Diagnostic mashine inadeal na management systems tu. Sensors, electrical actuators na modules(hii ni sehemu ndogo sana kwenye gari. Kuna vitu vingi sana bado havihitaji Diagnosis.

Mtu anakuja gari inagonga chini, anataka umfanyie diagnosis na mashine. Duh!
Uko sawa kabisa sijakataa kuna mifumo mingi tu bado haihitaji hiyo ila kwa mashine nyingi za sasa malfunction katika mifumo ya umeme inategemea sana kujua kupitia Diagnostic computer.

Mfano chuma hiko
IMG_20221217_203239_119.jpg
 
Acha Wahindi watoboe tu. Uaminifu unalipa. Wabongo wengi mi much know mno. Mteja akivaa kawaida wanaongeza bei, na wanakuwa serious balaa. Ila ukienda maduka ya Wahindi hata uvae kishamba utathaminiwa na utauziwa kwa bei halali.
Mswahili hawezi kutoboa kwa biashara kwa sababu ya kutokuwa waaminifu
Ana duka kubwa anaenda kuvamia na bunduki mji mwingine akiiba anakuja kumuachia mke auze vocha za mamilioni na vyakula

Ukimuuliza anakuambia mikopo babaaa
Ila wakiumbuka ndio unashangaa

Wengi ni matapeli kwa sababu biashara haipo kwenye damu na hajui nidhamu yake

Sasa wahindi, waarabu, na wasomali wamezaliwa wanaziona hela, wanaenda shule wakirudi wanauza duka
Nidhamu ya hela wanaijua tangu udogo na wanaiheshimu
Uaminifu wanauona kwa sababu ya chenji wanazorudisha na mzigo wanaotoa

Mswahili kaibuka tu na kuamua kuwa na biashara bila kujua baada ya miezi 6 atalipaje kodi
Hapo ndio anaanza utapeli na kuchukua mikopo

Kweli unafanya biashara unachukua mkopo wa kukuzidi mtaji?
 
Na yanakuja magari ya umeme kazi tunayo hawa mafundi wetu hawana idea na haya magari ya umeme kabisa hili ni janga lingine

Tatizo la watanzania sio watu wa kujiongeza
Mkuu kusema la haki bado tutatumia ya kizamani tu ingawa lazima tubadilike ila ndo hivyo tena

Magari ya sasa bila kuelekezwa mengine huwezi kuyaondoa mahali yalipo
Sasa sijui hao mafundi wanajifunza nini au wako tayari na nyundo zao?
 
Ukipeleka gari kwa mafundi wa chini ya muembe unabidi uwe makini. Nilipeleka gari kwa fundi mzoefu kabisa kinondoni ku overhaul engine. Matokeo yake akawapa madogo yeye akawa ana magari mengi kwa wakati mmoja. Nkamwambia hawa madogo unawapa unawaamini, kasema yes. Baada ya wiki naenda garage kutest gari nikagundua kabisa imekua nzito kuliko mwanzo. Vikombe wamegueza geuza. Nati hazijarudishishiwa. Nikamwambia fundi hii gari siitaki tena tafuta mteja wa milioni 4. Kisha ntakulipa gharama zako nusu. Alipopata mteja ndo alijua rangi zote.. nilichukua pesa yote hakupata hata thumun.
 
Uko sawa kabisa sijakataa kuna mifumo mingi tu bado haihitaji hiyo ila kwa mashine nyingi za sasa malfunction katika mifumo ya umeme inategemea sana kujua kupitia Diagnostic computer.

Mfano chuma hiko View attachment 2452405
Hii naona inahusiana na locomotives. Sina chochote ninachojua kuhusu hayo madude.

Suala la Diagnostic mashine, at least gari za ulaya ndio huwezi kufanya kazi bila mashine sababu karibu mifumo yote ya umeme wameintegrate ilink na diagnostic mashine.

Mfano gari za kijapani, mtu akiniambia anataka kufanya diagnosis ya engine, namuuliza km imewasha check engine. Kama haijawasha, namuandaa kabisa kisaikolojia kwamba tukipima tunaweza tukaona shida au tusione. Aamue yeye kupima au kuacha.
 
uliharibu nini mkuu.🤣🤣🤣🤣
Toyota Celica ilikua inatakiwa irudiwe rangi mi nilikua nyokaa kwa fundi hata kazi siijui vizuri akaniuliza naweza kuivua kioo Cha nyuma nikamwambia ndiyo nikafikiri ni vioo kama vya hiace, wakat natoa kioo nigangonga sehem flan ndogo tu aise kioo kikachanikachanika chote

tukatafuta kioo cha nyuma Cha Celica town hamna kila sehem alaf bei yake tukaambiwa ni ghali sana inazidi hata ghrama ya kurudia rangi, nikaona fundi wangu machozi yanamlenga huku ananiambia kmmae mtalipa na familia yako, tulivyorud gerej nikaona hii ni jela nikamvizia fundi kazubaa nikajidai naenda chooni nikaruka ukuta wa nyuma nikatoka nduki na mkoa nikahama kwa muda sijui kilitokea nini kwa fundi ila kazi ya gereji nikaacha
 
Tatizo wamiliki wengi wa magari wanapenda vitu vya mteremko, atengenezewe gari ikae vizuri kwa bei ndogo ndo kinacho waponza.

Kwanza unaendaje gereji bubu ambao wamezoea kutengeneza mabanzi ya kutoa spare kwa nyundo.
 
Toyota Celica ilikua inatakiwa irudiwe rangi mi nilikua nyokaa kwa fundi hata kazi siijui vizuri akaniuliza naweza kuivua kioo Cha nyuma nikamwambia ndiyo nikafikiri ni vioo kama vya hiace, wakat natoa kioo nigangonga sehem flan ndogo tu aise kioo kikachanikachanika chote

tukatafuta kioo cha nyuma Cha Celica town hamna kila sehem alaf bei yake tukaambiwa ni ghali sana inazidi hata ghrama ya kurudia rangi, nikaona fundi wangu machozi yanamlenga huku ananiambia kmmae mtalipa na familia yako, tulivyorud gerej nikaona hii ni jela nikamvizia fundi kazubaa nikajidai naenda chooni nikaruka ukuta wa nyuma nikatoka nduki na mkoa nikahama kwa muda sijui kilitokea nini kwa fundi ila kazi ya gereji nikaacha
🤣🤣🤣🤣pole mkuu. ubaya wakuio kikiwa nje ukigonga kidogotu kinamwagika Kama maji 😂kamabos mtata lazima ukimbie
 
Mafundi wa bongo ni miyeyusho Tena wote mfano mdogo ni IST compressor yake ni ya umeme na tangia huko imetumika na compressor hiyo hiyo ya umeme.Sasa ikishafika bongo wanakwambia compressor ya umeme ni jau boss inabidi tubadili tuweke ya kipumbu inayotumika kwenye VITZ ya kufanyia modify.Sasa unajiuliza huko ilipotoka mbona haijawahi sumbua?.
 
Back
Top Bottom