Narudia tena, Usafiri wa daladala hapa Dar es Salaam ni kwa ajili ya watu masikini

Narudia tena, Usafiri wa daladala hapa Dar es Salaam ni kwa ajili ya watu masikini

Acha na hilo la kupanda daladala..mimi hawa watu wanaopanda daladala halafu wamevaa suti tena wamepanda daladala za mbagala k.koo huwa siwaelewi kabisa.

#MaendeleoHayanaChama
 
Habari wanajukwaa!

Natumaini hamjambo,

Hii sio kashfa bali ni ukweli mtupu.

Usafiri wa daladala hapa Dar ni kwaajili ya maskini.

Vijana tutafute pesa huku tukimwomba Mungu atuepushe na Usafiri huu uliojaa karaha na kadhia.

Haiwekani mtu una pesa zako usimame Kariakoo mpaka Mbagala, au usimame Kariakoo mpaka Tegeta.

Jioni ukitoka mjini kwenda pembezoni mwa jiji unavizia basi la kugeuka nalo ili upate siti, nako ukishangaa hupati.

Makonda jioni wanaringa kama wasichana mabikira.

Watu wananuka sigara mnapumuliana.

Mwendokasi nako niliwahi kupanda jioni nako hali ni ngumu. Kuna mfanyakazi mwenzangu alikatwa kidole na mlango wa mwendokasi asubuhi wakati anakuja kazini.
Hii picha chini haina uhusiano na mada bali iko hapo kuchangamsha mada.
Ni mimi mwanadaladala mwenzenu.
View attachment 1860695
Time kunangwa, na Matajiri washamba, waliokulia umaskini.!
 
Naunga Mkono Hoja! NAKAZIA kupanda Daladala ni Umasikini na hakuna anaye enjoy kupanda Daladala, tunapanda ili tufike tu! Haiwezekani eti Diamond apaki Rolls Royce aone usumbufu halafu apande Daladala [emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]wote mnaompinga mtoa mada ni Masikini.

Nauchukia Umasikini

Nauchukia Umasikini

Nauchukia Umasikini

Hata kutumia Tecno au Infinix Pia ni Umasikini.. Goodnight EVERI BADI

Sent from my SM-G531H using JamiiForums mobile app
Ushamba ndio uko hivyo.
Kutumia kitu ni preferences za mtu tu.
Kama wewe hapo unatumia simu ya 2014. Eti kisa tu sio Infinix. Wakati kuna infinix zenye bei kuzidi simu ako. .bora hata ungekuwa na s au note series ya Samsung ndio uwezo kunanga. Ishi kwa budget yako. Tangu uanze kuuchukia umasikini, umekuachia kweli..!
 
Mafuta ya elfu 50 yanatosha wiki mzima, sasa ukimwona mtu mpaka anapaki gari nyumbani kwasababu ya mafuta kukata huyo bado maskini
Hii ndio Jamii forum mkuu,kwa hiyo kwa kipasso chako cha million 2 unusu tena used ndio kimekupa kiburi kuja kutukana watu hapa jukwaani.

Kwa mantiki hiyo ya mafuta ya 50 elfu per week maana yake wewe ni mwalimu ni kwenda kazini na kurudi nyumbani kulala huna mitikasi yoyote wala ratiba za bata weekend.

Acha zarau za kishamba bwana mdogo maisha ni zaidi ya kupanda dala dala mji mzito huu.
 
Kwa taarifa yako huo ndio usafiri wa mjini kwa majiji yote duniani(Public transport)
Mabasi ya umma na Treni ndio hasa nyenzo ya kukuwahisha kwenye mishe zako hilo ni dunia nzima iko hivyo na usikae ukafikiria kutumia gari binafsi ndio utajiri,wote wapandao dala dala si eti kua hawana magari
Tatizo la wabongo wengi ni Hakuna Exposure wengi hawajatoka nchihii hata ke ya tu hapo mtuhajatia mguu wala passport huna!tembea ujionee!
 
Habari wanajukwaa!

Natumaini hamjambo,

Hii sio kashfa bali ni ukweli mtupu.

Usafiri wa daladala hapa Dar ni kwaajili ya maskini.

Vijana tutafute pesa huku tukimwomba Mungu atuepushe na Usafiri huu uliojaa karaha na kadhia.

Haiwekani mtu una pesa zako usimame Kariakoo mpaka Mbagala, au usimame Kariakoo mpaka Tegeta.

Jioni ukitoka mjini kwenda pembezoni mwa jiji unavizia basi la kugeuka nalo ili upate siti, nako ukishangaa hupati.

Makonda jioni wanaringa kama wasichana mabikira.

Watu wananuka sigara mnapumuliana.

Mwendokasi nako niliwahi kupanda jioni nako hali ni ngumu. Kuna mfanyakazi mwenzangu alikatwa kidole na mlango wa mwendokasi asubuhi wakati anakuja kazini.
Hii picha chini haina uhusiano na mada bali iko hapo kuchangamsha mada.
Ni mimi mwanadaladala mwenzenu.
View attachment 1860695
Wapo maskini wengi wenye magari binafsi na matajiri wanaopanda daladala
 
Kwenye eicher za tegeta nyuki to kivukoni asubuhi mnapangwa kama ndizi. Unashika bomba la kulia unakuta mama mwenye umri wa mama yako anakugeuzia tako naye kashika bomba la kushoto. Konda anapenya hapo hapo kuchukua nauli... Hakika huu usafiri ni wa kudhalilisha basi tu.
Eti kuna watu wanasema kuwa matajiri nao hupanda daladala ili wapate fikra tofauti. Kwani kwenye daladala kuna kupiga story?
Tajiri hapotezi muda kuongea na maskini . Ikitokea anaongea na maskini ujue yuko kwenye site zake au kwenye biashara zake. Lakini hawezi kupangwa kama mishikaki kirahisi.
 
Kwa taarifa yako huo ndio usafiri wa mjini kwa majiji yote duniani(Public transport)
Mabasi ya umma na Treni ndio hasa nyenzo ya kukuwahisha kwenye mishe zako hilo ni dunia nzima iko hivyo na usikae ukafikiria kutumia gari binafsi ndio utajiri,wote wapandao dala dala si eti kua hawana magari
Tatizo la wabongo wengi ni Hakuna Exposure wengi hawajatoka nchihii hata ke ya tu hapo mtuhajatia mguu wala passport huna!tembea ujionee!
Nadhani hujanielewa na umekurupuka kujibu.
Kwenye tittle nimeweka neno Daladala Dar es salaam.
Achana na miji ya wenye akili na uchumi wa kati na wa juu ulio halisi.
Wewe unaona ni sawa tu yale manyanyaso ya Makonda wa daladala hapa mjini?
Kupangwa kwenye mistari kamabahesabiwa rokoo jeshini sawa tu?
Usimame huku umebanwa Mbagara - Posta sawa tu?
 
Nyuzi kama hizi nazipenda sana yani zinanitoa stress na vile sina gari wala pikipiki mimi natembea na nauli tu.

Mtu 50 alfu anasema gharama ya mafuta ya wiki kwa gari ya usafiri.

Wakati huo kwa wiki gharama yangu mimi ya usafiri ni 10 alfu.

Wakuu sisi tiobarikiwa kumiliki nauli pia tumshukuru Mola pia.
Kwenye daladala kuna root nzuri aiaeee unakaa kwenye daladala unatamani usishuke haraka.Ila ukisimama ukabananishwa dah safari inakuwa ngumu.Ila kwenye mwendokasi hata ukisimama poa tu
 
Huo ndo ukweli.
Na ukiona eti una gari na umeshindwa kuweka mafuta ukaja kupanda daladala bado upo kundi lilelile tu. Mtu na pesa zako huwezi kubali kudhalilika na vurugu za daladala za dar aisee.

Mtu na ndambi yako na tai shingoni unapapambana kupata siti [emoji23][emoji23], daah aisee.

Umaskini mbaya jama, tuukatae.
Dar es Salaam Bora watu waendelee kuwa na kipato cha chini.Dar watu wengi wakiwa na kipato cha Kati au juu,mji utazidiwa kwa magari
 
Back
Top Bottom