Narudia tena, Usafiri wa daladala hapa Dar es Salaam ni kwa ajili ya watu masikini

Narudia tena, Usafiri wa daladala hapa Dar es Salaam ni kwa ajili ya watu masikini

Habari wanajukwaa!
Natumaini hamjambo,
Hii sio kashfa bali ni ukweli mtupu. Usafiri wa daladala hapa Dar ni kwaajili ya maskini.
Vijana tutafute pesa huku tukimwomba Mungu atuepushe na Usafiri huu uliojaa karaha na kadhia.
Haiwekani mtu una pesa zako usimame Kariakoo mpaka Mbagara, au usimame Kariakoo mpaka Tegeta.
Jioni ukitoka mjini kwenda pembezoni mwa jiji unavizia basi la kugeuka nalo ili upate siti, nako ukishangaa hupati.
Makonda jioni wanaringa kama wasichana mabikira.
Watu wananuka sigara mnapumuliana.
Mwendokasi nako niliwahi kupanda jioni nako hali ni ngumu. Kuna mfanyakazi mwenzangu alikatwa kidole na mlango wa mwendokasi asubuhi wakati anakuja kazini.
Hivi mkuu kumiliki gari la 4 millions ndy Tajiri?

Bado tuna safari ndefu sana ya kujitambuwa.
 
Habari wanajukwaa!
Natumaini hamjambo,
Hii sio kashfa bali ni ukweli mtupu. Usafiri wa daladala hapa Dar ni kwaajili ya maskini.
Vijana tutafute pesa huku tukimwomba Mungu atuepushe na Usafiri huu uliojaa karaha na kadhia.
Haiwekani mtu una pesa zako usimame Kariakoo mpaka Mbagara, au usimame Kariakoo mpaka Tegeta.
Jioni ukitoka mjini kwenda pembezoni mwa jiji unavizia basi la kugeuka nalo ili upate siti, nako ukishangaa hupati.
Makonda jioni wanaringa kama wasichana mabikira.
Watu wananuka sigara mnapumuliana.
Mwendokasi nako niliwahi kupanda jioni nako hali ni ngumu. Kuna mfanyakazi mwenzangu alikatwa kidole na mlango wa mwendokasi asubuhi wakati anakuja kazini.
Ukweli mchungu,daladala ni usafiri wa kifukara sana,na watu wanakuwa na hasira,msongo balaaa,ukimgusa mtu na begi,anaweza akakuporomoshea matusi hatari!
 
Nyumba nne za aina gani, ziko wapi, alijengaje?
Maana job kuna jamaa ana nyumba mbili hapa mjini ila kazini anakuja na baiskeli na manguo ya mtumba.
Kuna mtu anamiliki nyumba nne mjini lakini anatumia usafiri wa daladala, huyo tumweke kundi gani?
 
Teh kwa ninavyowajua wabongo watakuwa radhi wapande ya mia nne hayo ya buku yatakuwa yanazunguka matupu tu
Uko sahihi.
Siku moja wakati tuko M/complex tunasubiri daladala za Chanika akapita mjamaa na private car ile gari ina sehemu ya mizigo na sehemu ya watu (pick up).
Sasa akasema Gongolamboto 500 nyuma sehemu ya mizigo na kwenye siti 1000. Watu walijazana kwenye body nyuma huku siti zikikosa watu . Nilishangaa sana.
 
Sijawahi kufuatilia kujua rank ya umaskini kwa Tanzania unaanzia mtu awe/apate bei gani kwa siku au amiliki nini ili kumtofautisha na wale hohehae!

Mf;wapo watu a'cally kutokana na mazingira waliyoishi/kulia yaliwafanya kuwa tu social,uwezo wa kuhudumia gari wanao even kumiliki hizi baby walker zaidi ya moja wanao ila haiingii akilini eti mtu ujibane ili ununue gari kwa kuogopa kupanda daladala,maisha ni yako ninyi mnaoona aibu kupanda daladala mnaogopa macho ya watu hamjui kwamba mumiliki gari au musimiliki gari hamuwapunguzii wala kuwaongezea chochote wale mnaohisi wanawatazama.

Mimi nina Bajaj tatu mpya zinazunguka barabarani ila ukinikuta kwenye Mwendokasi kama siyo mimi vile yote ni kwa sababu naishi maisha yangu Tanzania hii ukiogopa ogopa vitu vidogo vidogo kama kupanda public buses kuna baadhi ya vitu vitaku-cost.
Point ya msingi sio kuogopa macho ya watu, ishu ni zile adha zinazopatikana kwenye usafiri wa daladala...zile habar za kushikilia bomba gari imeshona had mlangoni halafu mnakaa kwenye folen nusu saa nzima, kupambana mlangoni uwahi siti, au ukikaa ile siti ya katikati mtu anakuja na begi au mfuko wake anaushikilia hapo hapo karibia na kichwa chako...kuna baadhi ya maeneo ukiishi unawaza hata kuvaa baadhi ya nguo kwa sababu itarud haitamaniki,plus kupangwa kama nyanya na makonda na walivyo na mdomo mchafu ukizingua kidogo mnaharibiana siku ,..ni obvious ukiwa na uwezo mzur utawaza alternative ways za usafiri mjini ..iwe ni kutumia gari yako ,au ubber ili kuepuka habar za kupangana kwenye folen ndeefu pale gerezan kwenye mwendo kasi
 
Back
Top Bottom