Nash MC, kwanini asipewe tuzo kwa darasa hili?

Nyie akili kubwa si mnasemaga hamsikilizi redio, media house ni biashara hivyo wengi wape!
media inawanafki wengi at least saizi wamepunguza

hip hop ni wanamziki wasio shoboka na promo (hapa simzungumzii lunya)

kuna kipindi nikki aliwachana wale majamaa walikua wanajiita wakali wa media yani wao ndio wanao request ngoma za wasanii, tena kunawatu mpaka waliajiriwa hadi kwenye kitengo cha wakali wa media yani zile meseji za request zilikua zinapitia kwao

yaani hao ndio walikua wanachagua ngoma gani ipigwe ipi iachwe, kuna ngoma hata kama imeombwa mara nyingi ila kwasababu zao binafsi hawaipigi

kunawatu walikua wana request ngoma za kina nikki mbish, nash na wasanii wengine wa tamaduni

kuna jamaa mmoja alishawahi kupewa makavu na nikki anaitwa evans chua, huyu mwamba alikua ana request kazi za nikki mbishi sana. Sasa kuna siku jamaa akamuibukia nikki kwamba ampe mtonyo ili aendelee kugonga nyimbo zake

Nikki akamchana akamuuliza "hizi ngoma una request kwa mapenzi tu au mimi nilishawahi kukuomba uwe unazi request" jamaa akasema "hamna bro mbona wakina madee wanafanya hivyo mbona fresh"

Kumbe machizi wakitoa ngoma wanatenga kibunda kwamba huyu anashikishwa buku 10 ya vocha ili kuhakikisha ndani ya week ngoma ishakua hit na baada ya wiki mbili ngoma inakua ishakua hit inajitegemea yenyewe hapo haina haja ya ku request ishaingia kwenye rotation
 
Sikia dogo, mimi nime-battle na Ramadhan Mponjika role model wenu masela washamba. Google him
Battle hata wakina msaga sumu na manifongo wanashiriki

Kushiriki battle sio icon ya kuijua hip hop
 
Battle hata wakina msaga sumu na manifongo wanashiriki

Kushiriki battle sio icon ya kuijua hip hop
Naijua hiphop kuliko hao watoto washamba kina nash sijui niki mbishi.

Najua one and two.

Najua sixteen bars.

Najua freestyle.

Wakati nafanya hayo hao watoto walikuwa wananyonya nafikiri.
 
Naijua hiphop kuliko hao watoto washamba kina nash sijui niki mbishi.

Najua one and two.

Najua sixteen bars.

Najua freestyle.

Wakati nafanya hayo hao watoto walikuwa wananyonya nafikiri.
Onyesha uwezo wako wa freestyle hapa kwa kunichana mimi

Ukishindwa hapo maneno yako yote yataonekana ni uzushi
 
Track adimu hii...
Madini tupu humo...

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
 
Upuz mtupu yaani

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
 

Alisema Ibra Da Hasla " system ipo corrupt" hip hop ina vitu vingi sana.

Nash anakwambia "walimu someni kitabu cha Makaveli, mjiulize mpo kwenye system au victim"
 
"Kaka Suma umesomeshwa kwa kodi za wanyonge, tunadai haki yetu unataka tuiombe, hio haiwezekani hata kwa makonde,"

Nyimbo nzima alimsema JK. Free Africa wakaipiga hewani wakapewa onyo kali kwa uchochezi na TCRA, Nash akajiita A.K.A MCHOCHEZI

Mchochezi a.k.a Maalim Ponda. 😁

-Kaveli-
 
Nimemsikiliza pia humo akizungumzia zao la kusini, pia nimefurahi sana kitu inaitwa ADUI..[emoji16][emoji16]

Sent from my TECNO LC6a using JamiiForums mobile app

Anamtuma 'Beti' akaziangalie korosho kule Masasi, baada ya kudhulumiwa na 'mzazi namba moko'. πŸ˜€πŸ˜€

Beti anaahidi ataandika na kitabu cha anguko la kusini.

-Kaveli-
 
Amenikosha, huyu Nash ndio yuleyule niliyemjua enzi zangu za ujana.Whats wrong with hawa 'watamaduni' wengine, naona kama wamepoteza taste na focus
 
Amenikosha, huyu Nash ndio yuleyule niliyemjua enzi zangu za ujana.Whats wrong with hawa 'watamaduni' wengine, naona kama wamepoteza taste na focus

Mkuu hii ngoma 'Ongea na Mwanao' inakosha sana. Ni Maalim haswaa katika ubora wake.

Nash hajabadilisha taste ya mziki wake. Na hatobadilika kamwe!

-Kaveli-
 
Onyesha uwezo wako wa freestyle hapa kwa kunichana mimi

Ukishindwa hapo maneno yako yote yataonekana ni uzushi

Hana uwezo huo. Ni mpiga kelele tu huyo.

-Kaveli-
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…