Natafuta binti wa kazi kwa ajili ya Mama Ntilie. Mshahara Tsh. 3,000/- kwa siku

Acha lawama za kipuuzi tafuta hela,hiyo mshahara ni uonevu na hampati mfanyakazi kwahiyo senti bakini nayo tu.
 
Hata mimi naitamani sema nipo mbali. Bonge la kazi kwa masaa 6
Njoo tuvutane tuishi Dilek.
Utanisaidia sana mana nahitaji mwanamke jasiri wa kuwa mama watoto.

Mwanamke mwenye uthubutu wa biashara hata kwa mtaji wa laki
 
Umebadili ID mkuu,300 anapika na chapati??akianza kuumwa kifua hyo 3000 itamtibu??acheni kunyanyasa watoto wa wenzenu kukanda ngano na kucjoma chapati kunaumiza kifua sana.
Ndio nimebadili mama
Hii ajira sio forced labour jamani
Mbona viwanda vya nondo ambako moto ni zaidi ya degree 300 ba zaidi kuna watu wanalipwa kidogo na ham wahurumii?
 
Ndio maana nmejiajiri mimi haya mambo yae kumuvujia jasho mtu hapana
Natafuta namna niboreshe welfare ya wafanyakazi wangu

Biashara yangu bado iko katika kiwango duni sana mkuu kuanzia mtaji, vifaa vya kazi, enei wanalokaa wateja na kipindi hiki cha mvua ndio hali inakuwa tete sana

Msinilalamikie sana kuhusu mshahara, ndio kwanza najikakamua na hii kitu
 
Sijalalamika naelewa unacho maanisha hata mimi nme ajiri vijana almost kumi nawalipa elf 5 per day ila jasho wanalovuja wangejifanyia kazi zao ingewalipa zaidi
 
Njoo tuvutane tuishi Dilek.
Utanisaidia sana mana nahitaji mwanamke jasiri wa kuwa mama watoto.

Mwanamke mwenye uthubutu wa biashara hata kwa mtaji wa laki
Mie bibi yako, nipo na babu yako hapa
 
Sijalalamika naelewa unacho maanisha hata mimi nme ajiri vijana almost kumi nawalipa elf 5 per day ila jasho wanalovuja wangejifanyia kazi zao ingewalipa zaidi
Tuko pamoja mkuu
Tupambane nchi yetu ipige hatua katika kujikomboa kiuchumi
 
Saa moja mpaka sa 7 buku3
Kwa viwandan sa moja mpaka 12 buku 4 au 3

Baadhi buku 6 na hawa wanapiga kazi mpaka saa tatu usiku au sa nne



Kipindi bora?


Huyu binti naona hapa atakuwa na muda wake wa ziada akijipanga vizur

Biashara za mama ntilie sio za kulipana 10000 kwa siku Mbona selikali tu inalipa watumishi wake mpaka 6000 kwa siku ambayo kwa mwezi 180

Na kazi kibao tu
 
Shida hao wote wanaolalamika hawajawahi kufanya biashara hata ya pipi hawajui changamoto yoyote ya biashara..mshahara wa mama Ntilie kwa siku ni elfu 3-4 japo maeneo machache wanalipa elfu 5(kama mimi) hadi 6 mwisho na hapo uwe unauza kweli kweli vinginevyo utafunga asubuhi tu.
Jf ina vijana wa ajabu sana, mbona hamsemei mishahara ya viwandani huko watu wanafanya kazi masaa 12 kwa elfu 4? Chakula juu yao!

Nendeni hapo ubungo external mkaone nyomi ile ndo mje hapa kukashifu ajira nyingine..
 
Mkuu tuvumiliane tu

Wana Jf si kwamba wanaishi USA na UK.

Tuko nao bongo hapa hapa tunakula makande ya buku, supu za mapupu na chapati 2 na wengine wanapiga pasi ndefu.

Sasa tukikutana humu kwenye thread tofauti kila mtu anajimbwambafai kivyake

Siri za PM naziacha huko huko
 
Pale Mbagala kuna kiwanda cha rasta wanalipwa elfu 45 kwa wiki mbili,nauli na chakula juu yako.Kazi unaingia saa 2 mpaka 11 jioni na sio poa kazi za humo ni hatari.
Wanalipwa 4000?
 
30 per day. 30*30,000 = 900,000 kwa mwezi. Ukiwa kama mama ntilie unao uwezo wa kuajiri msichana msaidizi kwa pesa hiyo?
Tena anafanya kwa masaa 6 kwa siku. Kama kuna sehemu wanalipa hivyo naomba uniunganishie tafadhali.
Nicheki PM nikuunganishe Bi Dada.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…