Natafuta Military Academy for Private Military Training

Natafuta Military Academy for Private Military Training

Si Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda wala Burundi ambako kuna Private Military Academies kama utakavyo Wewe. Nchi nyingi za Kiafrika Usalama wake ni mdogo hivyo Viongozi wengi ( namaanisha ) Marais wake huwa hawaruhusu ' Private Training ' kama hiyo kuwepo kwa hofu kubwa tu kwamba huenda siku moja hizo ' Njemba ' zilizofunzwa privately ' Medani ' za Kivita wanaweza ' wakawapindua '. Kwa wenzetu nchi zilizoendelea ( namaanisha Ulaya ) ambazo zimeshakomaa sana ' Kidemokrasia ' wao wanavyo hivi Vyuo binafsi na Watu huenda ' kujifunza '

Kwa kukusaidia tu na kukurahishia Kazi Mkuu nakuomba jitahidi umpeleke Mwanao huyo JKT kisha huko atafunzwa na kupikwa vizuri sana na si ajabu huenda Mwanao akionekana yupo vizuri Jeshi la Wananchi wa Tanzania ( JWTZ ) linaweza kumchukua ili aweze pia kulitumikia na kuilinda nchi yake nzuri ya Tanzania.

Hata hivyo nikushauri tu kwamba usimpeleke Mwanao huko kwa kumlazimisha kwani hutopata unachotaka Yeye akipate na utakuwa unapoteza rasilimali zako na muda wake isipokuwa kama huyo Mwanao kweli unaona ana mapenzi ya mambo ya Kijeshi basi wahi haraka sana ' kamtupe ' huko JKT ' Wanamume ' wamemtengeneze ili hata akirudi Kwako uweze kumsahau kidogo kisha uanze kujivunia kuwa sasa una Jembe la ' Kutukuka ' katika Familia yako.

Kila la kheri.
Asante sana kwa ushauri, hakika nimepata kitu. lakini ningependa nimpeleke kwenye military academy ili apate mafunzo yatayomsaidia maishani mwake. nimeshamwandaa kisaikolojia and he seems ready for it! Dunia hii inazunguka kwa kasi sana, nahisi mgambo na JKT havitoshi...otherwise, natanguliza shukrani mkuu.
 
Asante sana kwa ushauri, hakika nimepata kitu. lakini ningependa nimpeleke kwenye military academy ili apate mafunzo yatayomsaidia maishani mwake. nimeshamwandaa kisaikolojia and he seems ready for it! Dunia hii inazunguka kwa kasi sana, nahisi mgambo na JKT havitoshi...otherwise, natanguliza shukrani mkuu.

Kauli ya kwamba Mgambo na JKT havitoshi unakosea sana na kwa kukusaidia tu basi hakuna mahala ambapo Wapiganaji hupewa Mafunzo ya nguvu na ya kufa Mtu kama hayo ya Mgambo na JKT na kama kuna Mtu hapo karibu yako ambayo anayajua ' Majeshi ' ya Tanzania na aina za Mafunzo yake muulize na atakuambia. Tena usije kushangaa huko Mgambo na JKT hao Vijana wanafunzwa ' Kimedani ' na ' Kiukakamavu ' zaidi kuliko hata huko Jeshini kwenyewe JWTZ na TMA.
 
Nje kuna vyuo Lakini itakuwa ni ujinga kumpeleka mtu akasomee kitu ambacho hakitumii kwa manufaa ya kitaifa au kimapata au kiajira

Pia unaweza kumpeleka kwenye mafunzo ya mapigano wa miguu na mikono (Karate) Upanga nadhani kuna sehemu wanafundisha kule
mkuu, huenda uko sahihi. Lakini hakuna kisichokuwa na faida ulimwengu huu. hata comedians huwa wanacheka tu na mwisho wa shoo wanavuna hundred/thousands of dollars. Let me think about it...once again, thank you
 
Ila ww mwenzetu duuh!! Umedhamiria, balaa!! But I hope ni kwania njema mkuu!!

Mm mwenyewe nimesoma enzi JKT imefutwa. Majuzi wameirudisha kwa lazima nikafurahi huenda na sisi wa makazini tutalazimishwa kwenda JKT hata mwezi 1.

Nakumbuka Walimu Grade A na Form Six leavers wakawa wanalazimishwa kwenda, au usipo enda ukimaliza chuo uende kambini kwako kwa zamani kumaliza zamu lasivyo ajira hakuna.

Majuzi tu CCM wamegundua JKT inaenda kuwatoa madaraka; vyombo vya ulinzi vingekuwa vinachezea kichapo toka kwa Raia wema balaaa; yaani ya siku hizi imekuwa mdebwendo siyo tena lazima, hadi uombe. Dogo mmoja kasema yale mafunzo magumu yamepunguzwa-mkienda kule mnafunzwa hasa kulima, kuvuna, na ukakamavu tu.

Nilitaka niende kule ili angalau niwe nawapa adabu Vibaka (Kujilinda) waliojaa Tz hii. Siyo wananikuta mikono laiiiini utadhani mtoto. Kujua kutumia silaha (iwapo nitakuja kuimiliki kihalali). Pia huwa sipendi uonevu (waonevu niwe nawapa vichapo).

Jameni hivi still naweza kwenda Jeshini kuomba kuungana na wale mgambo wao (wale wa jiji na wa kulinda taasisi) na wakanikubali kujifunza?
 
mkuu, huenda uko sahihi. Lakini hakuna kisichokuwa na faida ulimwengu huu. hata comedians huwa wanacheka tu na mwisho wa shoo wanavuna hundred/thousands of dollars. Let me think about it...once again, thank you
Africa ni sehemu tofauti sana na sehemu zingine Duniani Africa mwanafunzi anasoma kwa kujua kile anachosomea kitamfaidisha vipi tofauti na wenzetu wanasomea kitu kwa ajili ya kuongeza Maarifa na Ufahamu

Kama unataka vyuo vya nje kesho nikupe mawasiliano yao then utawasiliana nao kwa hapa Option pekee ni JKT na wenzie na huko ni Military Training mafunzo ya ukakamavu na matumizi ya Silaha za Moto na Baridi tu

Mengine ya Darasani ni mpaka vyuo vya kijeshi Arusha au Dar
 
Mnaandaa terrorist siyo,au Snipers, jitambulishe vizuri wewe nano na huyo ni nani je wewe siyo takibiiiiiiiir,vyuo vipo vingi nje ya nchi ila jitambulishe tatizo hizo ID zenu.
 
Ila ww mwenzetu duuh!! Umedhamiria, balaa!! But I hope ni kwania njema mkuu!!

Mm mwenyewe nimesoma enzi JKT imefutwa. Majuzi wameirudisha kwa lazima nikafurahi huenda na sisi wa makazini tutalazimishwa kwenda JKT hata mwezi 1.

Nakumbuka Walimu Grade A na Form Six leavers wakawa wanalazimishwa kwenda, au usipo enda ukimaliza chuo uende kambini kwako kwa zamani kumaliza zamu lasivyo ajira hakuna.

Majuzi tu CCM wamegundua JKT inaenda kuwatoa madaraka; vyombo vya ulinzi vingekuwa vinachezea kichapo toka kwa Raia wema balaaa; yaani ya siku hizi imekuwa mdebwendo siyo tena lazima, hadi uombe. Dogo mmoja kasema yale mafunzo magumu yamepunguzwa-mkienda kule mnafunzwa hasa kulima, kuvuna, na ukakamavu tu.

Nilitaka niende kule ili angalau niwe nawapa adabu Vibaka (Kujilinda) waliojaa Tz hii. Siyo wananikuta mikono laiiiini utadhani mtoto. Kujua kutumia silaha (iwapo nitakuja kuimiliki kihalali). Pia huwa sipendi uonevu (waonevu niwe nawapa vichapo).

Jameni hivi still naweza kwenda Jeshini kuomba kuungana na wale mgambo wao (wale wa jiji na wa kulinda taasisi) na wakanikubali kujifunza?
ni kweli mkuu, nimedhamiria haswa na ndo sababu nikaamua ku-share na wanazuoni wa JF. Binafsi naona mbali kidogo na ndiyo maana nikamzuia kutafuta kazi kwanza mpaka tutakapofika hatima ya hili. nimeishi na jamii ya watu mbalimbali na nimeona life style zao na wengi nchini mwao walienda jeshini or wana mafunzo ya kijeshi. kama mzazi, namwandaa ili naye aje kuwaandaa wadogo zake na watoto wake atakayewazaa...
 
ni kweli mkuu, nimedhamiria haswa na ndo sababu nikaamua ku-share na wanazuoni wa JF. Binafsi naona mbali kidogo na ndiyo maana nikamzuia kutafuta kazi kwanza mpaka tutakapofika hatima ya hili. nimeishi na jamii ya watu mbalimbali na nimeona life style zao na wengi nchini mwao walienda jeshini or wana mafunzo ya kijeshi. kama mzazi, namwandaa ili naye aje kuwaandaa wadogo zake na watoto wake atakayewazaa...
Imekaa vyema ndg, Pambana umpeleke JKT. Kuna kambi ya Kigoma huko ndio niliona wanafundishwa mazoezi magumu hadi kutembelea Tumbo wakiwa ndani ya wavu mrefuuuu kama m50 au m100 hivi.
 
Africa ni sehemu tofauti sana na sehemu zingine Duniani Africa mwanafunzi anasoma kwa kujua kile anachosomea kitamfaidisha vipi tofauti na wenzetu wanasomea kitu kwa ajili ya kuongeza Maarifa na Ufahamu

Kama unataka vyuo vya nje kesho nikupe mawasiliano yao then utawasiliana nao kwa hapa Option pekee ni JKT na wenzie na huko ni Military Training mafunzo ya ukakamavu na matumizi ya Silaha za Moto na Baridi tu

Mengine ya Darasani ni mpaka vyuo vya kijeshi Arusha au Dar
mkuu, nitashukuru ukinipa mawasiliano yao. respect bro
 
Imekaa vyema ndg, Pambana umpeleke JKT. Kuna kambi ya Kigoma huko ndio niliona wanafundishwa mazoezi magumu hadi kutembelea Tumbo wakiwa ndani ya wavu mrefuuuu kama m50 au m100 hivi.
huko wanasoma/ ku-train mafunzo kama Land warfare: force-on-force with the use of FX Simunition pamoja na Advanced Firearms Training - Live Fire contactt Drills? kama una taarifa kamili ya kozi wanazosoma JKT ninaziomba kama hutojali...bless up
 
huko wanasoma/ ku-train mafunzo kama Land warfare: force-on-force with the use of FX Simunition pamoja na Advanced Firearms Training - Live Fire contactt Drills? kama una taarifa kamili ya kozi wanazosoma JKT ninaziomba kama hutojali...bless up
Sina mkuu.
 
mkuu, ningependa yote kama ulivyoanisha hapo juu. bahati mbaya sisi wakati tupo vijana hatukupata fursa kama hizi na siwezi laumu sana...kwa kuwa dogo umri unaruhusu, akipata mafunzo kama, Threat assessment and risk analysis, Firearms Training - Single operative (Pistol & Carbine), Land warfare: force-on-force with the use of FX Simunition and Advanced Firearms Training - Live Fire contatct Drills with VI na nyingine nyingi itapendeza. na ni kwa nia njema tu.
Kwa maelezo yako kwann wewe mwenyewe usianzishe chuo chako cha kijeshi maana naona hadi curriculum unayo tayari...mzee wewe itakuwa commandoo unataka kumfundisha mwanao mbinu za kijeshi kuwa wawili muje kufanya mapinduzi....nahisi kina Fidel Castro wanaandaliwa kuja kufanya mapinduzi Tanzania. ...
 
Kwa maelezo yako kwann wewe mwenyewe usianzishe chuo chako cha kijeshi maana naona hadi curriculum unayo tayari...mzee wewe itakuwa commandoo unataka kumfundisha mwanao mbinu za kijeshi kuwa wawili muje kufanya mapinduzi....nahisi kina Fidel Castro wanaandaliwa kuja kufanya mapinduzi Tanzania. ...
mkuu, hilo la kuanzisha chuo cha kijeshi haliwezekani abadani. ila ni kwa nia njema tu nataka nimwandae dogo aje kuwa "something" kwenye jamii. najaribu kuona mbali kwa darubini kali...
 
Wana board, Heshima kwenu!
wakati taifa likiwa kwenye msiba mkubwa, nami naungana na ndugu na jamaa katika majonzi na masikitiko ya kuondokewa na vijana wetu, Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema awarehemu na kuwalaza mahala pema peponi. Amen!

Pia, kwa kuwa JF ni kisima cha fikra na maarifa ningependa kujuzwa kama kuna military academy nchini Tanzania or kwenye nchi jirani kwa ajili ya private military training. Natafuta chuo cha kijeshi kwa ajili ya first born wangu ambaye amemaliza chuo mwaka jana. sikutaka aanze kazi kwa sababu maalum...natanguliza shukrani.
jaribu KK security mkuu.
 
Back
Top Bottom