Nataka kuachana na ualimu haraka. Nikimbilie wapi?

Nataka kuachana na ualimu haraka. Nikimbilie wapi?

Mshikaji wangu alikuwa mwalimu shule ya msingi. Akaupiga chini akaenda kusoma diploma medicine akamaliza akapiga degree medicine sasa hivi ni doctor.
Wakati aliacha kazi ilikuwa kama masihara. Mwisho alitoboa.
Sio kila njia aliyopita mtu na mwingine anaweza kupita.

Tungepata na background ya huyo Dokta aliyepiga chini Ualimu ili tuweze kumshawishi na huyu vizuri
 
Sio kila njia aliyopita mtu na mwingine anaweza kupita.

Tungepata na background ya huyo Dokta aliyepiga chini Ualimu ili tuweze kumshawishi na huyu vizuri
Mshikaji nilisoma naye Primary na sekondary, hakupata ufaulu mzuri akaenda Ualim Certificate alifanya kazi kama miaka mitano tu. Akaacha akaenda kusoma diploma ya medicine. Baba yake mzazi alikuwa mchungaji wa Kanisa. Walikuwa na maisha yakawaida sana kama unavyojua kijijini.
 
Ahsante kaka na nitaubeba ushauri wako...pia naomba niulize swali , ni vp endapo nitaenda kusoma bachelor ya biology ama physics pasipo ualimu ? Inaweza niletea shida kwa mwajiri?
Naungana na jamaa aliyekushauri kuwa ukasome Bachelor ya Ualimu tena halafu baadae ukasome Master ya kitu kingine e.g Master of Business Administration then utaweza kupata wigo wa kuhamia taasisi zingine.

NB: Usisahau pia umri unakimbia, kwa bongo umri ukikimbia halafu huna msingi wa uchumi ni risk sana.
 
Upo sahihi .... mshahara umetoka jana lakin leo sina kitu na gas inaelekea ukingoni , na ndugu na wadogo zangu wanaomba chochote, wanaamini nnakaz nna pesa kumbe taabu tupu
Halafu enzi nasoma primary Walimu nilikuwa nawaona maisha mazuri sana.

Kuna Mwl alikuwa amezaa watoto wengi(7+) huku akiendelea kuzaa, halafu hana source nyingine ya income isipokuwa mshahara tu.

Mke ni mama wa nyumbani, watoto wake wakubwa wa kwanza na wa pili alikuwa anawasomesha sekondari shule za private, halafu maisha yalikuwa yanaenda vizuri tu. Sijui siku hizi kwanini haya mambo yanashindikana hata kama mambo yanabadilika.
 
Mshikaji nilisoma naye Primary na sekondary, hakupata ufaulu mzuri akaenda Ualim Certificate alifanya kazi kama miaka mitano tu. Akaacha akaenda kusoma diploma ya medicine. Baba yake mzazi alikuwa mchungaji wa Kanisa. Walikuwa na maisha yakawaida sana kama unavyojua kijijini.
Kwa ufupi alikuwa na support wakati anasoma Diploma ya Medicine.

Kwa mtu ambaye hana support ni vigumu, isipokuwa kama anajiweza mwenyewe kujihudumia
 
Kinacho kufanya upigike siyo ualimu, ila ni uvivu wako na kutokufikiria nje ya box. Kama usipobadilika hata uwe na masters maisha yako yatakawa hivyo hivyo tu.

Usione watu wanaendesha vimagari vyao na wamejenga nyumba zao ukadhani ni vyeti vyao au kazi zao ndo zinawalipa. Siyo hivyo....ni uchakarikaji.

Popote ulipo pana fursa, ni wewe tu kuwa na jicho la tatu..na kuondoa uvivu.
Bro maeneo niliyopo hayan support kabisa npo Tanga ndan ndan
 
Uamuzi wa kuacha kazi ni sawa na uwamuzi wa mtu kutaka jinyonga hashirikishwi mtu so jilipue mwanangu acha kazi uwalimu kitu gani bwana ila mwalimu mbona tunaoma walimu wanamiliki nyumba za kisasa, magari mazuri ,.watoto zao wanasoma shule nzuri hawa walimu wa serikali gani au Wana majini ndani
Hao wapo ndio lakin utakuta unapata 1 kwa 100 au labda walio mjin ....Mimi hapa kituon kwangu hamna kitu ata kula wanakula vibaya tena chakula cha watoto wa hostel
 
Acha kujidhalilisha mwalimu acha dhalilisha walimu kama shida zako ni wewe usiwapake matokeo walimu nyie ndio mnatakiwa kufukuzwa kazi maanq hamjitambui
Bro kua mtulivu kaka, hamna anaeweza nifukuza kazi kisa nimesema ukweli kua maisha ni magumu, najua ata wew unatambua lkn nashangaa kwanini unakua mkali
 
Naungana na jamaa aliyekushauri kuwa ukasome Bachelor ya Ualimu tena halafu baadae ukasome Master ya kitu kingine e.g Master of Business Administration then utaweza kupata wigo wa kuhamia taasisi zingine.

NB: Usisahau pia umri unakimbia, kwa bongo umri ukikimbia halafu huna msingi wa uchumi ni risk sana.
Shukran kaka
 
Niende kwenye mada moja kwa moja

Mimi ni mwalimu kiwango cha elimu ni diploma katika masomo ya PHYSICS na BIOLOGY,,,

Baada ya misuko suko ya ualimu ikiwa ni pamoja na kupigwa na maisha vizuri tu,
Nimekaa na kuamua kurudi shule kusoma / kujiendeleza kielimu.

Ndugu zangu naombeni ushauri wenu naweza soma course gani nje ya ualimu ambayo itakua na tija kidogo kwa taifa letu (ualimu siutaki tena Mimi nimechoka),

Sifa ni diploma ya ualimu wa sayansi katika masomo niliyo taja (PHYSICS na BIOLOGY).

Japo kuna watu wamenishauli kwa chet changu hicho cha diploma nikasomee bacherol of science in PHYSICS or bacherol of science in BIOLOGY .

Naombeni ushauri jamani ualimu umenishinda nimeinua mikono juu....

NAWASILISHA.
Badala ukawe MC unarudi tena kupoteza hela?
 
Halafu enzi nasoma primary Walimu nilikuwa nawaona maisha mazuri sana.

Kuna Mwl alikuwa amezaa watoto wengi(7+) huku akiendelea kuzaa, halafu hana source nyingine ya income isipokuwa mshahara tu.

Mke ni mama wa nyumbani, watoto wake wakubwa wa kwanza na wa pili alikuwa anawasomesha sekondari shule za private, halafu maisha yalikuwa yanaenda vizuri tu. Sijui siku hizi kwanini haya mambo yanashindikana hata kama mambo yanabadilika.
Bro alaf waalimu wa msingi nimefuatilia nimegundua Wana maisha mazuri kuliko sisi wa secondary, sijui mchawi wetu nani
 
Late 2009 kuna Mwl mmoja alifanya uamuzi kama huu unaoutaka wewe, yeye alisoma kozi fupi ya Ualimu wa Sekondari mwaka 2006 kipindi Shule za kata zimeanzishwa. Sasa alimua kwenda kusoma Degree ila aliamua kubadili kozi ya kwenda kusoma chuo, alichagua Accountancy na alifanikiwa kudahiliwa UDOM.

Wakati anaomba ruhusa kwa mwajiri wake(DED) alidanganya kuwa anaenda kusoma Ualimu akapewa ruhusa.

Baada ya kumaliza Chuo akiwa na Degree ya Accountancy akashindwa kurejea kwa mwajiri ili aendelee na kazi maana alidanganya tangu mwanzo. Akaamua kuingia mtaani ili atafute kazi. Aisee mambo yakawa magumu sana akafanya Application nyingi za kazi bila kuitwa hata Interview moja, stress si ikapiga hodi akakondeana hatari maana mwanzoni alikuwa bonge. Wenzio ambao hawakudanganya wakarejea kazini(Ualimu) bila usumbufu wowote tena wengine waliopata GPA kubwa walipangiwa Vyuo vya Ualimu kwenda kufundisha, yeye akaanza kujutia uamuzi wake.

Sasa hivi sijui yuko wapi maana mara ya mwisho nilikutana naye mwaka 2015.

Kwa hiyo binafsi nashauri kama hauna chanzo kingine cha ugali, usiache ualimu ukakimbilia kusoma kozi nyingine tofauti na hiyo Ualimu, imagine walimu wamejaa mtaani wenye degree na wanatamani wakafundishe hata Primary angalau wapate hela ya kusogeza siku
Maneno makavu kabisa haya bila kumuwazia mtaji atapata wapi

Niliajiriwa nikiwa Afisa kata wa fani X
Baada ya kufanya Kazi mwaka nikarudi chuo kusoma fani Y (Nilidanganya kwa DED naenda kusoma X ila nikaenda kusoma Y).

Na kibaya/kizuri zaidi nikaunga kabisaa mpaka masters ya Y.

Kurudi kazini (baada ya kutoka chuo) nikawasilisha cheti.
Baada ya miezi kadhaa nikafayiwa recategorization na kwenda kwenye hiyo Idara ya Y, nikafanya Kazi miezi 8 nikapata shavu la KUKAIMU MKUU WA IDARA.

The point is Amoc thefdon unaweza kusoma chochote na kufanya Kazi yoyote.

Ukirudi kazini ukakuta HR anazingua Kuna fursa kibaoo...
1. Kuhamia ofisi nyengine ya serikali (transfer)
2. Kuomba Kazi upya kupitia Ajira.go.tz

#YNWA
 
Late 2009 kuna Mwl mmoja alifanya uamuzi kama huu unaoutaka wewe, yeye alisoma kozi fupi ya Ualimu wa Sekondari mwaka 2006 kipindi Shule za kata zimeanzishwa. Sasa alimua kwenda kusoma Degree ila aliamua kubadili kozi ya kwenda kusoma chuo, alichagua Accountancy na alifanikiwa kudahiliwa UDOM.

Wakati anaomba ruhusa kwa mwajiri wake(DED) alidanganya kuwa anaenda kusoma Ualimu akapewa ruhusa.

Baada ya kumaliza Chuo akiwa na Degree ya Accountancy akashindwa kurejea kwa mwajiri ili aendelee na kazi maana alidanganya tangu mwanzo. Akaamua kuingia mtaani ili atafute kazi. Aisee mambo yakawa magumu sana akafanya Application nyingi za kazi bila kuitwa hata Interview moja, stress si ikapiga hodi akakondeana hatari maana mwanzoni alikuwa bonge. Wenzio ambao hawakudanganya wakarejea kazini(Ualimu) bila usumbufu wowote tena wengine waliopata GPA kubwa walipangiwa Vyuo vya Ualimu kwenda kufundisha, yeye akaanza kujutia uamuzi wake.

Sasa hivi sijui yuko wapi maana mara ya mwisho nilikutana naye mwaka 2015.

Kwa hiyo binafsi nashauri kama hauna chanzo kingine cha ugali, usiache ualimu ukakimbilia kusoma kozi nyingine tofauti na hiyo Ualimu, imagine walimu wamejaa mtaani wenye degree na wanatamani wakafundishe hata Primary angalau wapate hela ya kusogeza siku
Naongezea Mkuu, Kuna rafiki yangu somebody Felicia shimbewangoso alikuwa na ujuaji wa hapa na pale, aliingia Kama mwalimu wa krashi programu kwa enzi hizo miaka 2016/2017, Basi bwana kapiga kazi,muda ulipoenda akaenda kusomea bachelor ya mazingira sijui na Nini huko wlipohitimu alirudi kazini Kama kawaida,maana enzi hizo ufuatiliaji ulikuwa duni,hivyo aliendelea kupiga kazi Kama kawaida na bachelor yake hiyo.

Mwaka 2016 kwenye uhakiki wa watumishi hewa si akaombwa apeleke cheti Cha taaluma ,akitoe wapi ,maana bachelor yake alisoma vitu tofauti na ualimu,mwisho wa siku akapigwa chini ,Sasa hivi hata Mia Hana,kapauka sana ,anajutia uamuzi wake.

Mwisho wa siku kwako mtoa mada, usijifunze kwa walioshindwa, fanya kile moyo wako unakutuma kufanya, Mimi pia nampango wa kusoma mambo ya community development niachane na fani ya ualimu.
 
Back
Top Bottom