Nataka kuachana na ualimu haraka. Nikimbilie wapi?

Nataka kuachana na ualimu haraka. Nikimbilie wapi?

Naongezea Mkuu, Kuna rafiki yangu somebody Felicia shimbewangoso alikuwa na ujuaji wa hapa na pale, aliingia Kama mwalimu wa krashi programu kwa enzi hizo miaka 2016/2017, Basi bwana kapiga kazi,muda ulipoenda akaenda kusomea bachelor ya mazingira sijui na Nini huko wlipohitimu alirudi kazini Kama kawaida,maana enzi hizo ufuatiliaji ulikuwa duni,hivyo aliendelea kupiga kazi Kama kawaida na bachelor yake hiyo.

Mwaka 2016 kwenye uhakiki wa watumishi hewa si akaombwa apeleke cheti Cha taaluma ,akitoe wapi ,maana bachelor yake alisoma vitu tofauti na ualimu,mwisho wa siku akapigwa chini ,Sasa hivi hata Mia Hana,kapauka sana ,anajutia uamuzi wake.

Mwisho wa siku kwako mtoa mada, usijifunze kwa walioshindwa, fanya kile moyo wako unakutuma kufanya, Mimi pia nampango wa kusoma mambo ya community development niachane na fani ya ualimu.

Kwanini asingefanyiwa RECATEGORIZATION?

#YNWA
 
Kinacho kufanya upigike siyo ualimu, ila ni uvivu wako na kutokufikiria nje ya box. Kama usipobadilika hata uwe na masters maisha yako yatakawa hivyo hivyo tu.

Usione watu wanaendesha vimagari vyao na wamejenga nyumba zao ukadhani ni vyeti vyao au kazi zao ndo zinawalipa. Siyo hivyo....ni uchakarikaji.

Popote ulipo pana fursa, ni wewe tu kuwa na jicho la tatu..na kuondoa uvivu.
Hii tunaita kujiongeza,wengi wanateseka kwa kukosa uwezo wa kujiongeza yaani wanakuwa rigid wanakosa flexibility.
Mtu anasoma halafu utakuta amerelax tu anangoja makaratasi yake ndio yamuokoe.
 
Mshikaji nilisoma naye Primary na sekondary, hakupata ufaulu mzuri akaenda Ualim Certificate alifanya kazi kama miaka mitano tu. Akaacha akaenda kusoma diploma ya medicine. Baba yake mzazi alikuwa mchungaji wa Kanisa. Walikuwa na maisha yakawaida sana kama unavyojua kijijini.
Kwenye maisha usiige mtu,kila mtu ana timing zake.
Hata kama kwao maisha ni ya kawaida huwezi kujua alifanya connection gani hadi akatoboa,siri ya mtu ni kichaka.
 
Bachelor of science in biology unarudi kuwa mwl . Kasome Bsc Aquaculture au Bsc fisheries Sua au udsm utakuja kunishukuru . Maafisa uvuvi ni wachache Sana. Tafuta wilaya yenye ziwa au baharu ufanyiwe recategirization utakuja kunishukuru. Au nenda kasome masuala ya Procurement and supplies. Watu wa procurement ni wachache walioajiriwa ufanyiwe recategirization uwe procurement officer pia utakuja kunishukuru. Kumbuka unavyoenda kusoma uwe na tricky Kuomba vyuo viwili unapeleka joining instructions ya kwamba unaenda kusoma education. Wewe unaenda kusoma chio kingine ili upewe ruhusa
Eti afisa uvuvi wachache [emoji1787]

Kabla ya kufanyiwa recategirization unajua mara ya mwisho ajira zao walitangaza lini ? Unaongea kana kwamba kuna uhitaji kwenye idara hiyo

Nimemaliza na wanangu wengi tu wa aquaculture hapo Sua bado ngoma ni bila bila


Mtoa mada siku hizi ajira ngumu baki huko huko ulipo ila tu ji upgrade ongeza elimu yako kwenye kada yako siku hizi ajira ni ngumu kila sehemu kila sekta
 
Niende kwenye mada moja kwa moja

Mimi ni mwalimu kiwango cha elimu ni diploma katika masomo ya PHYSICS na BIOLOGY.

Baada ya misukosuko ya ualimu ikiwa ni pamoja na kupigwa na maisha vizuri tu,
Nimekaa na kuamua kurudi shule kusoma/kujiendeleza kielimu.

Ndugu zangu naombeni ushauri wenu naweza soma course gani nje ya ualimu ambayo itakuwa na tija kidogo kwa taifa letu (ualimu siutaki tena Mimi nimechoka).

Sifa ni diploma ya ualimu wa sayansi katika masomo niliyo taja (PHYSICS na BIOLOGY).

Japo kuna watu wamenishauri kwa cheti changu hicho cha diploma nikasomee bachelor of science in PHYSICS or bachelor of science in BIOLOGY .

Naombeni ushauri jamani ualimu umenishinda nimeinua mikono juu....

NAWASILISHA.
Bachelor of science in Physics, Chemistry....Ili iwaje sasa?

Ni bora ujiendeleze Ualimu.

Au soma kozi za Afya.
 
Nenda kasome kozi za mazingira badae rahisi kukubalishia kwa sbb ya masomo yko na kuwa afisa mazingira 🙏
 
Eti afisa uvuvi wachache [emoji1787]

Kabla ya kufanyiwa recategirization unajua mara ya mwisho ajira zao walitangaza lini ? Unaongea kana kwamba kuna uhitaji kwenye idara hiyo

Nimemaliza na wanangu wengi tu wa aquaculture hapo Sua bado ngoma ni bila bila


Mtoa mada siku hizi ajira ngumu baki huko huko ulipo ila tu ji upgrade ongeza elimu yako kwenye kada yako siku hizi ajira ni ngumu kila sehemu kila sekta
Ajira za uvuvi zimetoka chache kipind cha hapo nyuma.
 
Akisoma CPA akiwa chuo itamlazimu kuanzia ATEC I mpaka aje kumaliza inawezekana na chuo chenyewe kikawa kimeisha na Bado asiipate hiyo CPA kwa sababu Hana msingi kwenye Uhasibu.

Bado hujamshauri
Na ikiwa mtu ana bachelor of science, say, education, then akaongezea na CPA. Akirudi halmashauri anaweza kufanyiwa recategorization kwa kwa cheti cha CPA?

Msaada mkuu kama una uelewa na hili.
 
Kinacho kufanya upigike siyo ualimu, ila ni uvivu wako na kutokufikiria nje ya box. Kama usipobadilika hata uwe na masters maisha yako yatakawa hivyo hivyo tu.

Usione watu wanaendesha vimagari vyao na wamejenga nyumba zao ukadhani ni vyeti vyao au kazi zao ndo zinawalipa. Siyo hivyo....ni uchakarikaji.

Popote ulipo pana fursa, ni wewe tu kuwa na jicho la tatu..na kuondoa uvivu.
Vocha ya elfu 10 hyo hapo,umejitahidi sana kuelezea ukweli
3457 467 345 2345
 
Eti afisa uvuvi wachache [emoji1787]

Kabla ya kufanyiwa recategirization unajua mara ya mwisho ajira zao walitangaza lini ? Unaongea kana kwamba kuna uhitaji kwenye idara hiyo

Nimemaliza na wanangu wengi tu wa aquaculture hapo Sua bado ngoma ni bila bila


Mtoa mada siku hizi ajira ngumu baki huko huko ulipo ila tu ji upgrade ongeza elimu yako kwenye kada yako siku hizi ajira ni ngumu kila sehemu kila sekta

Inawezekana kufanyiwa recategorization. Hakuna Idara yenye watumishi "waliotosha"
Unachotakiwa kufanya ni kutafuta halmashauri yenye upungufu halafu unahamia huko.

Usitake ufanyiwe recategorization hapohapo halmashauri yako.

Cha kufanya hapo ni kuhama halmashauri kwa kutafuta halmashauri yenye upungufu.

Mfano: Halmashauri yetu ilikuwa na Afisa tehama mmoja tu.

Juzi tulipokea mwana katokea halmashauri ya mjini na kuhamia kwetu.
Aliajiriwa huko mjini kama mwalimu ma diploma.
Kaenda kusoma IT.

Kurudi kakuta ma-IT wengii halmashauri kwao huko mjini.

Akaanza kutafuta Chaka, akalifumania halmashauri yetu.

Basi amehamia sasa, kwahiyo hapo tegemea bajeti ijayo anatoboa na kuwa full IT.

#YNWA
 
Na ikiwa mtu ana bachelor of science, say, education, then akaongezea na CPA. Akirudi halmashauri anaweza kufanyiwa recategorization kwa kwa cheti cha CPA?

Msaada mkuu kama una uelewa na hili.
Unaweza ila kuna maafisa utumishi wengi hawajui kusoma muundo pale unatakiwa ubadilishiwe kwa kutumia statement of result ya intermediate ndio wanaiterm kama degree au foundation wanaiterm kama certificate ila kuna baadhi ya maafisa utumishi hawajui muundo basi ni shida wanasumbua watu mno
 
Unaweza ila kuna maafisa utumishi wengi hawajui kusoma muundo pale unatakiwa ubadilishiwe kwa kutumia statement of result ya intermediate ndio wanaiterm kama degree au foundation wanaiterm kama certificate ila kuna baadhi ya maafisa utumishi hawajui muundo basi ni shida wanasumbua watu mno
Shukran sana tena sana mkuu mrsmau , huu mrejesho mzuri kwangu.
Hayo mengine tutaeleweshana tu kama mdogo mdogo.
 
Back
Top Bottom