Nataka kuanzisha Kabila jipya na la kisasa

Nataka kuanzisha Kabila jipya na la kisasa

yeah ni rahisi, lakini muanzisha kabila kasema tutakua hatupo chini ya taifa lolote…ndo nikahoji itawezekanaje
Hapo atujuze😀😀
Mimi siko sana kwenye utambulisho kwa maana hakuna faida zozote tukitambulika sasa. Cha msingi ni taratibu kujenga misingi imara ya kabila letu.

Utambulisho utakuwa na maana kwetu sisi ndani kwa ndani kujuana lakini si watu wa nje 😎
 
Ukiweza kuepusha kabila lako na uchawi, 50% ya mafanikio itakuwa mbeleni mwako
 
Ukiweza kuepusha kabila lako na uchawi, 50% ya mafanikio itakuwa mbeleni mwako
Hizo ndiyo moja ya sababu zinazonisukuma kufanya jambo hili. Hatutakuwa na makandokando kama hayo. Kitakuwa kizazi pure 😎
 
naomba niwe mmojawapo mkuu....jina langu liwe mojawapo ya koo za kabila letu jipya
 
Hii nchi kuendelea itakuwa ni ngum sana,yaani unawaza kujenga vitu kama kabila tena? Haya...sasa hilo kabila litaanza lini kujijenga mkuu?
 
Kuna faida kubwa kwenye umoja. Makabila mengi yalianza bila vision. Mazingira tu yalipelekea watu kukutana sehemu moja na baada ya muda muingiliano, mfanano wa lugha, mila na desturi zilizojengeka ukawaunganisha. Imagine sasa haya yote uyafanye kwa makusudi na kwa kufuata vision mliyojiwekea.

Imagine kundi dogo la watu wakae chini wajenge vision moja ya aina ya watu wanaotaka kuwa halafu kwa umakini mkubwa waanze kujijenga kwa vizazi kadhaa.

Baada ya muda fulani wawe na elimu na maarifa ya hali ya juu, wawe na mila na desturi ambazo ni mpya na tofauti lakini ambazo ni modern kama siyo futuristic. Imagine uunde kabila ambalo limetapakaa dunia nzima, wawe watu wenye mamlaka katika serikali kubwa duniani, katika majeshi, taasisi za media, fedha na zingine zenye ushawishi kabla hata hilo kabila halijajulikana au kutambulika rasmi.

Hilo ndiyo nakusudia kufanya na najua kwa uvumilivu linawezekana. Sitakuwepo wakati hilo limestawi ila nitajivunia kupanda mbegu hiyo.

Napokea ushauri, ukosoaji na pia wale wanaotaka kushiriki katika mwanzo huu mpya mnakaribishwa. 😎


Kabila halianzishwi na mtu bali linaanzishwa na Mungu mwenyewe na tayari makabila yalishaanzishwa na kamwe huwezi pata kabila jipya nje ya makabila yaliyokuwepo. kuanzisha kabila jipya ni sawa na mtu kuanzisha bahari mpya mbali na bahari hizi zilizokwishakuwepo.
 
Wewe hauna tofauti na Nimrod wa mnara wa Babeli, muulize kilichompata.

Nguvu iliyo nyuma ya wazo lako sio nzuri. Utapotea
 
Nipo tayari kua mmoja wa kabila jipya,
Kikubwa tu;
Kusiwe na mambo ya ushirikina,
Tusichanganye Kabila na Dini,
Kuwe na Usawa kwa kila Mtu,
Kuwe na demokrasia ya kweli,
Kabila liendane na mfumo wa Dunia wa Sasa kwa maana Sayansi na Teknolojia.
 
Kuna faida kubwa kwenye umoja. Makabila mengi yalianza bila vision. Mazingira tu yalipelekea watu kukutana sehemu moja na baada ya muda muingiliano, mfanano wa lugha, mila na desturi zilizojengeka ukawaunganisha. Imagine sasa haya yote uyafanye kwa makusudi na kwa kufuata vision mliyojiwekea.

Imagine kundi dogo la watu wakae chini wajenge vision moja ya aina ya watu wanaotaka kuwa halafu kwa umakini mkubwa waanze kujijenga kwa vizazi kadhaa.

Baada ya muda fulani wawe na elimu na maarifa ya hali ya juu, wawe na mila na desturi ambazo ni mpya na tofauti lakini ambazo ni modern kama siyo futuristic. Imagine uunde kabila ambalo limetapakaa dunia nzima, wawe watu wenye mamlaka katika serikali kubwa duniani, katika majeshi, taasisi za media, fedha na zingine zenye ushawishi kabla hata hilo kabila halijajulikana au kutambulika rasmi.

Hilo ndiyo nakusudia kufanya na najua kwa uvumilivu linawezekana. Sitakuwepo wakati hilo limestawi ila nitajivunia kupanda mbegu hiyo.

Napokea ushauri, ukosoaji na pia wale wanaotaka kushiriki katika mwanzo huu mpya mnakaribishwa. 😎
Zipo jumuiya (societies) zenye mrengo mmoja na utaratibu wa pekee pamoja na itikadi yao ya kipekee. Zipo brotherhoods mbalimbali kama Freemasonry, Illuminati, Sculls and Bones, Knight Templers, mashirika ya kitawa ndani ya Kanisa Katoliki yanayoishi kama familia ndogo ndogo na kubwa kubwa, n.k.

Kwa ujumla halitakuwa jambo nje ya hayo niliyotaja hapo. Kuliita kabila utaita hivyo lakini utaishia na mifumo kama niliyotaja hapo juu.
 
Back
Top Bottom