Nataka kughairi kufunga ndoa, zimebaki week 3. Nifanye nini kutimiza azma yangu?

NDOA sio lelemama na si kwa wenye roho nyepesi; NDOA ni tamu lakini pia sio rahisi

Binafsi naamini kigezo cha kwanza cha kufunga ndoa ni kuwa tayari kiakili hii itakusaidia sana kwenye vipindi vigumu vijavyo ambavyo siku zote na kwenye NDOA zote huwa vipo, kama moyo wako unakataa kabisa usikilize kwani majuto ni mjukuu. NDOA sio ya jamii yote kwa ujumla, NDOA ni yako wao yao ni harusi tu.

Nahisi pengine hali yako inasababishwa na kiburi cha mwezako, usiende nalo hilo kwenye NDOA ni hatari.

Ujinasueje?

  • Ongea na mwenzako kwamba unataka ''kujinasua''
  • Ongea na wazazi wako, wao ni watu wazima na wanaweza kukusaidia on the way forward

Kila la kheri
 
Mkuu hebu eleza huyo binti unampenda sana na je yeye kwako upendo wake ukoje?... Na kingine ni kwamba Je huyo Binti unahisi ana tabia ambazo kipindi cha mpito hiki umeona kabisa hamuwezi kuendana nae?...Kuwa muwazi....
Kingine je umewahi sex nae au labda pia ulishawahi chepuka kwenye hayo mahusiano na labda ulikochepukia umeona kutamu zaidi ya Hapo unapotarajia kuweka ndani?
 
Kuoa si dawa ya kuacha kumtumikia shetani maana hata waliopo ndoani wanamtumikia
Kuna ndoa nyingine ukiingia tu inakuwa kama ndio umedahiliwa na shetani, unakuwa mteja mteja kweli! Kuna watu nawajua walianza tabia za ugomvi na ulevi baada ya ndoa, kabla ya hapo walikuwa wapole mno! Wapo waliofunga ndoa zikawageuza kuwa vicheche, wanatafuna kila kinachopita mbele yao. Wengine ndoa zimewafanya kuwa washirikina, wachawi hasa! Na wengine wamegeuka wauaji, wako jela, wengine wamejiua.
Kwa waliokatazwa talaka, ndoa ni uamuzi unaoweza kumjenga mtu au kumsambaratisha kabisa!
Think before you leap. Ukiona hapa hakuna maisha sepa tu, usiogope, lakini tafakari kwanza.
Na kwa kutambua umuhimu wa uamuzi na hiyari katika ndoa, sisi wakristo huulizwa mara nyingi, hata wakati wa kuingia lango la kanisa Padri huwauliza mmojammoja "Umekuja kufunga ndoa bila shuruti na kwa moyo radhi?" Hapo una fursa ya kujibu ndiyo au hapana, ukisema hapana utageukia hapohapo mlangoni urudi ulikotoka! Na pale altareni utaulizwa tena. Hii yote ni kwa nia ya kuhakikisha wahusika wamejitafakari vema katika hatua zote hadi itakapotamkwa "alichokiunganisha Mungu mwanadamu asikitenganishe"
 
Umesema vyema mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…