Nataka kuiona nguvu ya milioni 2 kwenye biashara mpya

Shukrani sana mkuu
 
Asante sana mkuu, nimeanzia kujifunza hapahapa kwenye hii comment yako
 
Hilo ni kweli kabisa kama haijazoeleweka na wateja na ni mpya ina changamoto kidogo ila kama unaweza kuweka hata mbili kwa kubebana ni vizuri zaidi
La kujiuliza je hiyo kilo 50 itakulipa kwa kodi na ushuru pamoja na mishahara?
Itanilipa iwapo kilo moja itanipa faida ya 1000,na kuhakikisha kilo zote 50 zinaisha kwa siku; kwa sababu fremu nitalipia 200,000/=,kijana muuzaji 200,000/=,usafirishaji 100,000/=
 
Kama upo sehemu changamfu biashara ya pay point imekaa vyema. Usiogope kama wapo wengine hilo eneo wanafanya biashara hiyo, cha muhimu ni kuwa na salio muda wote baada ya muda wa miezi kadhaa watakuzoea tu.
Kila la kheri ndugu.
Hii inakuwaje mkuu?
 
Biashara pekee itakayo inua mtaj wako ni MANG SHOP. Yani duka la bithaa ndogo ndogo za nyumbani
 
Asante mkuu
Kama upo sehemu changamfu biashara ya pay point imekaa vyema. Usiogope kama wapo wengine hilo eneo wanafanya biashara hiyo, cha muhimu ni kuwa na salio muda wote baada ya muda wa miezi kadhaa watakuzoea tu.
Kila la kheri ndugu.
 
Biashara hii ni nzuri changamoto ni kwenye eneo kwa ajili ya hiyo biashara....kama umekodi kwa mswahili akiona unapata...unashangaa timbwilitimbwili linaanza
Ni kweli kabisa mkuu,nakumbuka nilikuwa nalipa kodi laki 5 Mara gafla nikaambiwa laki 8,sijakaa sawa 1milioni,kabla sijamaliza kushangaa nikaambiwa nihame
 
Tafuta vijana 20 nunua Katanga watembeze na kuleta salio kila siku elfu 10 Fanya hesabu mwenyewe hapo
 
Fanya unaloona kwako linafaa,usituchoshe,hela yako wewe,matumizi tukupangie sisi.

Nimesoma huku kichwa kikiwaza namna ya kumshauri jamaa ambaye anataka kuanzisha Biashara ili atengeneze kipato Chake binafsi bila mgongo wa mwajiriwa.Ila hii reply yako imenitia hasira sana yani bora ungenyamaza ungeonekana una busara.
Nitakuja kwa ajili ya kukushauri
 
Kama alivyosema mchangiaji mmoja hapo juu Cc chasha farming.
Kabla ya kuangalia ni Biashara gani unakusudia kuifanya ni lazima ufanye utafiti kwanza Katika Maeneo unayoishi,jamii inayokuzunguka ina changamoto zipi,Je Kama mjasiriamali unaweza kutatua zipi Kati ya hizo.

Pesa huwa ni matokeo baada ya kutatua changamoto/matatizo ya watu wanaotuzunguka Katika maisha yetu.Hizo huduma/Biashara hapo juu ni hatua ya mwisho kabisa baada ya kufanya uchunguzi na kugundua changamoto na kupata suluhishao lake.
Ebu achana na hizo Biashara kwanza,ingia mtaani fanya uchunguzi alafu huko utapata wazo la Biashara ipi ni sahihi kwa watu sahihi kwa wakati huu.
Service should stand as an input and profit should stand as an output.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…