Inaitwa " a stepping stone business" yaani wafanyabiashara wengi kabla ya kuingia kwenye biashara nyingine walizonazo walianza kwenye hiyo biashara. Vitu vya msingi kuvijua kwenye biashara hiyo
1. Uaminifu na Weledi wa Kijana ni kitu cha kwanza ili ufanikiwe ktk biashara hii tumeshuhudia wafanyabiashara wengi wakianguka na wengine wakiamka tokana na Wasaidizi ktk biashara hizo
2. Faida ni ya uhakika ingawa ni ndogo inayokuwa kwa muda mrefu inabidi uwe mvumilivu sana ili duka likae sawa na mwanzoni uwe na ufuatiliaji wa karibu sana
3. Uchaguzi wa eneo la kufanya biashara nalo ni muhimu. Kwa mfano kuna eneo ambalo hakuna Muajiriwa hata mmoja, sehemu nyingine unakuta Waajiriwa wa kumwaga
4. Ukaguzi, Uchunguzi na Utunzaji kumbukumbu wa mara kwa mara ni muhimu sana itakusaidia kujua maendeleo ya biashara, itakusaidia kubaini mbinu za kibiashara, ville vile itasaidia kujua kama msaidizi ana mapungufu au laa
Unaweza mchunguza hata huyo kijana wako kama ana kauli njema kwa wateja au laa, yuko aggressive au laa kwa kutumia watu wengine ambao wataenda dukani kama wateja
5. Mahusiano mazuri toka kwa Suppliers na upande mwingine Customers ni kitu cha muhimu sana ili ufanikiwe bila kusahau mahusiano na taasisi za fedha Ukiwa na mahusiano mazuri na Suppliers ni rahisi kupata bidhaa nyingi kwa mali kauli upande wa Customers utajua mahitaji halisi ya wateja na wachache utaowakopesha watakulipa timely
6. Teknolojia ni muhimu katika utunzaji kumbukumbu vile vile hivi sasa kuna App maalum za kufanya Manunuzi directly kutoka kwa Manufacturer au Dealer na Software saidizi ktk Stock Traxking na Sales Tracking
7. Mahitaji ya Kisheria, hakikisha huna ugomvi na Serikali na Mamlaka zake kwa kulipa kodi na tozo zote zinazohitaji
8. Wekeza ktk kujifunza na kutaka ushauri. Tafuta Business Consultant akupe ushauri at least kila baada ya miezi 3 fanya nae kikao. Wekeza ktk kujifunza toka kwa wafanyabiashara wenzio. Nilishaona mtu anadaiwa kodi na TRA Tshs 60m lakini baada ya kutafuta Tax Consultant na kuziweka report zake vizuri alilipa Tshs 2.5m
9. Jitofautishe wewe na biashara yako, sio kwa sababu biashara ni yako basi kuwe hakuna mpangilio Baba, Mama, Watoto, Mjomba wanaingia na kutoka dukani kadri watakavyo. Kukiwa na hali kama hiyo wasaidizi dukani hufurahia sana kwani chochote kitakachotokea dukani hawatawajibika. Uhusiano.wako wewe na duka ni faida tuu, hivyo basi chochote utachochukua dukani lazima kiorodheshwe hatimae kilipwe au kikatwe kwenye faida